Kibu walugari

Kibu walugari

Compartir

Music band

25/05/2022
15/05/2022

SIMULIZI; SITAKUFA MPAKA NITAJIRIKE
SEHEMU; YA 04
MTUNZI; NERIRAH EVA

Tulipoishia,,,,,,

Ukileta ujinga tu hapa unakufa cha muhimu apa ni kufanya kazi tulio tumwa basi...kisha deleva aliwasha gari na kuanza safari uku nikiwa natetemeka sana na kuloa jasho mwili mzima.

Songa nayo........

"Tulifika eneo husika kulikuwa na gari nyeusi nzuri mno kiukweli nilitamani ata mimi nije nimiliki gari k**a lile"

Oya unashangaa nini mda wa kazi...ilikua sauti iliyonitoa kwenye dibwi la mawazo

Sasa tunafanyaje apa!

Ok wewe kaa kwenye gari me nitaenda kumalizana nao kisha Hamisi akashuka kwenye gari

"Mda wote nilikua nachungulia dilishani nilishangaa kuona watu tulio tumwa kuwapelekea mzigo wapo serious sana hawacheki wala kukwepesha macho Mungu alisaidia dili lilienda vizuri tukarudi kwa boss"

Mda mwingine uache kushangaa shangaa fanya kilicho kupeleka vinginevyo utakuja ufe

Ilikua ni sauti ya boss iliyo nish*tua na kuhisi wenda atakua mchawi kisha vijana wake walisogea na kututoa vitu walivyotubandika apo awali

"Siku tatu mbele boss alituagiza kupeleka mzigo sehemu nyingine safari hii tuliongezewa bausa mmoja hii kazi nilikua siipendi kabisa ila ilibidi tu nijikaze"
.Tulipoenda palikua na umbali kuliko awali tulifika lakini kabla hatujabadilishana mzigo ulitokea uvamizi wa ghafra yule bausa alitutupia mzigo na kutuamuru turudi kwenye gari kisha akaanza kupambana na wale watu alifanikiwa kuwauwa wote, kwa mala ya kwanza nilishuhudia watu wakifa mbele yangu,

Hiki kitendo kilizidi kunitia uoga wa kuendelea kubaki pale nilitamani ata niondoke lakini nikakumbuka yale maneno ukitaka kutoka pale lazima utoke maiti hii ilinitia uoga zaidi

"Hii hali ya kushuhudia vifo vya watu mbele yangu iliendelea kunifanya nishindwe kuvumilia kuwepo pale iliendelea hadi mwaka ukakatika na kikweili boss alikua na umri mdogo lakini kuua kwake ilikua kawaida sana k**a anachinja kuku vile, nikaona siwezi baki hapa lazima nitafte njia ya kujikomboa nitoroke pale"

Mungu si Athumani kuna siku kulikua na sherehe yake ya kuzaliwa pale nyumbani kwa boss alialika watu wengi walikuja watu tofauti wenye pesa zao nikajisemea moyoni leo watu ni wengi sana lazima nijichanganye nitoroke hapa

Ilipofika mida ya usiku wageni wanavotawanyika nami nikajichanganya niliwahi kwenye gari moja nikajificha nyuma ya buti

"Gali lilitembea umbali mrefu kidogo kisha likasimama nikawasikia wakisema tununue vitu dukani kwanza walikua ni mke na mume, walipo shuka tu nikapata nafasi ya kuchungulia palikua sehemu iliyochangamka nikaona apa patakua ndo chunya mjini acha nishuke apa kabla hawajarud ilibidi nishuke pale taratibu nisishutukiwe"

Pembeni palikua na mgahawa kwa kua nilikua na pesa tulizo kua tukipewa na boss nikaona sio mbaya nikipata chakula uku nikifkiria wapi pa kwenda,

Nilipo kua mgahawani alikuja mrembo mwenye sura ya upole mno na mnyenyekevu mno kwa mala ya kwanza nikajikuta nimempenda sana yule binti

Karibu nikuhudumie nini?

Aaaaahhhh! naweza pata wali samaki

Samaki wameisha tumebakiwa na wali nyama

Ok niletee!

Baada ya mda akaleta....samahani naitwa Deo je wew mwenzangu

Alitabasamu kisha akanijibu naitwa Irene

Wow! Jina zuri

Asante...

Baada ya hapo nilitafta gest nikalala hapo hadi asubuhi lengo langu lilikua ni kutafta iyo sehemu ya kalasha nikawa kila siku naenda kula pale mgahawani hadi nikajenga mazoea na binti mrembo Irene

Nilipo ona kaanza kuniamini ilibidi nimweleze shida yangu

Ooooh kuna mtu ambae namjua nae ana kalasha anaitwa mzee Zumba ila sijui utamwingiaje maana sio mtu lahisi

Nashukuru kwa vile nipo karibu nawew naamini itawezekana ...Irene akatabasamu

"Siku zilienda mpaka wiki mbili, nacho shukuru yule boss alikua akitupa pesa nyingi ko ziliweza kunisitili kila nikienda kumtafta mzee Zumba nikawa namkosa hadi nikaanza kukata tamaa nikiwa nimepumzika kwenye chumba changu nilisikia mlango unagogwa nilipofungua alikua ni Irene coz nilimwelekeza chumba nilichochukua"

Yaan wew si ununue simu hadi naanza kukutafta kwa mguu jamani!

Pole kunanini mbona unahema ivyo ????

Zumba kapita pale kaelekea kalashani kwake nenda haraka saizi na hawezi kukuamini kwasababu hakujui, kaka angu anajuana nae nimemwomba amdanganye wew ni ndugu yake kakubari anakusubir mgahawani twende haraka basi
..Kweli tulienda pale mgahawani kaka ake alinipeleka adi kwa Zumba kweli Mungu ni mwema nilikua na bahati nikakubaliwa na kuambiwa wiki ijayo nianze kazi nilishukuru sana na kumshukuru kaka ake Irene sana,

"Nilifanya kazi kwa bidii k**a hakuna kesho kila nikipata pesa tulikua tukishauliana na Irene tunafungua biashara ilifika mda nilifungua biashara nyingi na kubwa kusema ukweli maisha ya umasikini yalikua yameisha nilijenga nyumba yangu kubwa ya kuishi nikajenga na kijijini pia kwa wazazi wangu"

Lakini sikuishia hapo miaka ilipozidi kwenda nilifanikiwa kujenga hoteli kubwa nilimshukuru sana Mungu biashara zangu Nyingi alikua akisimamia Irene kwasababu nilikua nikimwamini sana na yeye ndo sababu ya mimi kupata mali zote izo

Kwa kua tulidumu kwenye mahusiano miaka mitano nikaona sio mbaya niweze kumuoa awe mke wangu wa ndoa nikaenda kwao nikatoa posa tukapanga nimpeleke nyumbani kabla ya kutoa mahari wamjue

"Na mda huo nilikua nikimiliki gari ya ndoto yangu kweli maisha yalikua ya furaha tukaanza safari ya kurudi makete na nikaona sio mbaya nipitie kumlipa fadhila kaka alie nisaidia pindi nilipo fika mbeya kwa mala ya kwanza wakati tupo mbeya tulipita mtaa mmoja tukakuta kuna mzee anatolewa vitu nje kuna watu walikua wakitoa kila kitu ndani huruma ikanishika nikasimamisha gari niliposhuka na kuuliza kulikoni, vijana walinijibu kwa hasira tunamdai laki tatu huyu mjinga hataki kutulipa"
.Ile namwangalia mtu anae daiwa alikua ni mjomba nilishtuka sana na kuita Mjomba????

"Ndipo nae akainua kichwa kuniangalia alivyo niona alilia kwa uchungu na kuniomba msamaha kwa kunitelekeza stendi nilimwangalia sana nilitaka kuondoka Irene akanigusa nisiondoke tumsaidie kwanza sikua na namna niliingia kwenye gari nikachukua pesa nikawapa wanao mda laki tatu nae nikamwachia laki mbili alinishukuru kwa kupiga magoti lakini sikumjibu kitu nikaondoka zangu"

_Tulifika kwa kaka tuliongea mengi sana kisha nae nilimpa zawadi nilizobeba tukaanza safari ya kurudi kijijini...kweli siku ya pili yake tulifika kijijini kwa sababu tulilala njiani, wazazi wangu walifurahi sana kumwona Irene wakatoa baraka zao baada ya hapo tukaondoka tukaanza mipango ya harusi.

"Mwezi mmoja baadae ndoa ilifungwa na kila kitu kilienda k**a ilivyo pangwa Namshukuru Mungu nikatimiza lengo langu la kua SITOKUFA MPAKA NITAJIRIKE, nimetoa simulizi hii kwa wewe kijana mwenzangu mtaftaji mwenye ndoto na malengo makubwa hakikisha una fanya ibada muombe Sana Mungu kila jambo mtangulize Mungu na uamini kwamba Mungu hakuna jambo asilo liweza tena yeye hachelewi wala hawai, baada ya hapo fanya kazi kwa bidii na kwa kujituma sana na kwa malengo na hakikisha unatafta hela ya halali naamini utafanikiwa asante na kwakheri.

Mwisho.....................................................................

15/05/2022

Happy Sunday

¿Quieres que tu empresa sea el Salón De Belleza mas cotizado en Barcelona?
Haga clic aquí para reclamar su Entrada Patrocinada.

Teléfono

Página web

Dirección

123
Barcelona