Aggy Afya center
Aggy Afya center tunatoa huduma za Afya kwa kutumia virutubisho lishe.
04/07/2023
(FIBROIDS)
LIJUE TATIZO LA UVIMBE KWENYE KIZAZI KWA MWANAMKE
Uvimbe kwenye kizazi ni Uvimbe ambao hutokea katika misuli laini ya mfuko wa uzazi wa mwanamke (Uterus). Tatizo la uvimbe kwenye kizazi hujulikana kwa kitaalamu k**a “uterine fibroids/leiomyoma/uterine myoma”.
Uvimbe huu husababisha kubadilika kwa umbo na ukubwa wa kizazi. Mara nyingi Wanawake wengi huanza kupata maumivu makali wakati wa hedhi kutokana na tatizo hili. Wakati mwingine mwanamke anaweza kupata tatizo hili akiwa kwenye ujauzito, hali hii inaweza kusababisha shida wakati wa kujifungua na kupelekea mwanamke kujifungua kwa upasuaji.
Tatizo hili huweza kuongezeka ukubwa wakati wa ujauzito kutokana na kiasi kikubwa cha homoni ya estrogen. Kuvuja damu na maumivu ya tumbo pia huweza kutokea kutokana na uvimbe kupoteza damu yake. Kwahiyo madaktari wa wanawake hupendekeza mgonjwa kufanyiwa ultrasound mara kwa mara ili kufatilia maendeleo ya uvimbe.
Tatizo la uvimbe kwenye kizazi ni kubwa na linawatokea wanawake wengi sana. Inakadiriwa kwamba 75% ya wanawake hupata tatizo hili katika kipindi fulani cha maisha yao. Kwa mujibu wa jarida la New England Journal of Medicine, kila mwaka zaidi ya wanawake 200,000 wanafanyiwa upasuaji wa kuondoa kizazi chote (hysterectomy) kutokana na tatizo hili.
Soma pia hii makala: Ujue Ugonjwa Wa Ge***al Warts (Kuota Vinyama Sehemu Za Siri) na Tiba Yake.
○● Aina Za Uvimbe Kwenye Kizazi:
Kuna aina kuu nne (4) za uvimbe kwenye kizazi kulingana na sehemu unapotokea kwenye mfuko wa uzazi ambao ni pamoja na;
(1) Intramural Fibroids.
Hii ni aina ya uvimbe ambayo uwapata sana wanawake. Aina hii ya uvimbe hukua na kumea kwenye misuli ya ukuta wa mfuko wa mimba (uterus). Kadri uvimbe huu unavokua basi husababisha kupanuka au kuvutika kwa kizazi na kusababisha dalili k**a hedhi.
(2) Subserosal Fibroids.
Aina hii ya uvimbe hukua nje ya ukuta wa mfuko wa mimba, wakati mwingine kuelekea kwenye kibofu cha mkojo. Aina hii ya uvimbe huweza kusababisha maumivu ya chini ya mgongo kutokana na kwamba uvimbe huu unasukuma neva za uti wa mgongo na kusababisha presha kubwa kwenye eneo la chini ya mgongo.
(3) Submucosal Fibroids.
Aina hii ya uvimbe hukua karibu na ukuta wa kizazi. Hii inaweza kusababisha kutokwa na damu kwa muda mrefu wakati wa hedhi na shida kwenye kushika ujauzito.
(4) Cervical Fibroids.
Huu uvimbe hukua kwenye tishu za mlango wa kizazi ambao huitwa cervix. Uvimbe hutokea mara chache sana ukilinganisha na aina zingine za uvimbe kwenye kizazi.
Uvimbe Kwenye Kizazi Husababishwa Na Nini?
Uvimbe kwenye kizazi husababishwa na wingi wa vichocheo mwilini, homoni ya estrogen ambayo hupelekea mwanamke kupata hedhi, ambapo matumizi ya njia za uzazi wa mpango pia ni vichocheo ambavyo huchangia kuongezeka kwa homoni ya estrogen.
○● Sababu Za Uvimbe Kwenye Kizazi:
Mambo yafuatayo yanaongeza uwezekano kwa mwanamke kupata uvimbe kwenye kizazi;
(1) Kurithi.
k**a mama au dada yako aliwahi kuugua tatizo la uvimbe kwenye kizazi basi wewe pia utakuwa kwenye hatari zaidi ya kupata uvimbe huu.
(2) Umri.
Wanawake wenye umri zaidi ya miaka 30 wapo katika hatari ya kupata tatizo hili.
(3) Lishe.
Matumizi ya vyakula vya wanga na sukari kupita kiasi huongeza hatari ya kupata tatizo hili.
(4) Uzito Mkubwa Na Kitambi.
Wanawake wenye uzito mkubwa na kitambi wako kwenye hatari zaidi ya kupata tatizo hili.
(5) Matumizi Ya Njia Za Kupanga Uzazi.
Matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango huongeza ukuaji wa fibroids kwani vidonge hivi huweza kupandisha homoni ya estrogen kwa wingi.
(6) Kubalehe Mapema.
Wanawake wanaobalehe mapema na kuanza kupata hedhi chini ya miaka 10 wako kwenye hatari zaidi ya kupata tatizo hili.
(7) Wanawake Wenye Shinikizo Kubwa La Damu.
○● Dalili Za Uvimbe Kwenye Kizazi:
Zifuatazo ni dalili zinazojitokeza kwa wanawake wengi zaidi wenye uvimbe kwenye kizazi;
(1) Kupata hedhi inayochukua siku nyingi kuanzia siku 7 na zaidi (Prolonged menstrual bleeding).
(2) Kupata hedhi nzito (Heavy menstrual bleeding).
(3) Kujiskia umeshiba muda mwingi (Abdominal fullness).
(4) Maumivu ya nyonga.
(5) Kupata mkojo mara kwa mara na kushindwa kutoa mkojo wote kwenye kibofu.
(6) Kukosa choo kwa muda mrefu au kupata choo kigumu.
(7) Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa.
(8) Maumivu chini ya mgongo na kwenye miguu.
(9) Madhara mbalimbali ya uzazi k**a ugumba na mimba kutoka.
○● Matibabu Ya Uvimbe Kwenye Kizazi:
Matibabu ya uvimbe kwenye kizazi yanaweza kugawinyika katika sehemu tatu (3) ambazo ni pamoja na;
(1) Upasuaji (Myomectomy).
Tiba hii hutumika endapo Uvimbe ni mmoja na sio kubwa sana. Matibabu haya hutoa Uvimbe na kubakiza kizazi.
(2) Hysterectomy.
Haya matibabu yanahusisha kutoa sehemu ya Uvimbe yote iliyo katika kizazi maana yake kutoa kizazi chote endapo Uvimbe utakuwa mkubwa sana au vivimbe vikiwa vingi vikiwa katika kizazi.
(3) Dawa Za Kutuliza Maumivu.
○● Madhara Ya Uvimbe Kwenye Kizazi:
Yafuatayo ni baadhi ya madhara ya uvimbe kwenye kizazi kwa wanawake ambayo ni pamoja na;
■Ugumba (infertility).
■Kukosa choo (constipation).
■Figo kushindwa kufanya kazi (kidney failure).
■Tumbo kuvimba (abdominal distention).🙏
HITIMISHO:
Uvimbe unaweza kujirudia tena endapo vichocheo vinavyosababisha Uvimbe havita sawazishwa. Hivyo tumekuandalia program maalumu itakayokusaidia kuondokana kabisa na tatizo la uvimbe kwenye kizazi, program hii inahusisha matumizi ya virutubisho vilivyotokana na mimea na matunda.
Call: 0657187144
30/06/2023
🪵UGONJWA WA PID🪵
(Pelvic Inflammatory Disease)
au Maambukizi Katika Mfumo wa Uzazi wa
Mwanamke.
Magonjwa ya zinaa ndio sababu kuu ya
wanawake kupata maambukizi katika mfumo wa
uzazi yani (PID). Mwanamke 1 kati ya wanawake 8 walipota PID katika wakati wowote ndani ya maisha yao hupata tabu kushika mimba
*(PID) NI NINI?*
PID ni maambukizi katika mfumo wa uzazi wa
mwanamke na mara nyingi husababishwa na
magonjwa ya zinaa k**a gonorrhea na
chlamydia ila kuna aina ya maambukizi mbali na
magonjwa ya zinaa yanaweza kusababisha
maambukizi ya PID.
*JE! MWANAMKE HUAMBUKIZWAJE PID?*
Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza
kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na:
- K**a una ugonjwa wa zinaa na haijatibiwa
- Kufanya ngono zembe isiyo salama (yani kulala
na wanaume tafauti tafauti)
- Kuwa na mpenzi ambaye ana wanawake wengi
nnje
- K**a umekuwepo na historia ya PID hapo
nyuma
- Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara
baada ya kujifungua (au postpartum period)
- Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya
kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post
abortion) au mara baada ya mimba kutoka
(miscarriage)
- Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa
uzazi (IUCD) k**a njia mojawapo ya uzazi wa
mpango
- Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya
PID
- Kutumia (Vaginal Dauche)
*UTAJUAJE UKO NA (PID)?*
Zipo dalili kadhaa za ugonjwa huu wa PID.
Miongoni mwa dalili hizi ni:
- Mwanamke kuhisi maumivu ya tumbo hasa
maeneo ya chini ya kitovu
- Kupata maumivu ya mgongo
- Mwanamke kupata utoko mchafu sehemu za
siri. Utoko huu huambatana na harufu mbaya.
- Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
- Kupata maumivu au kutokwa na damu wakati
wa tendo la ndoa
- Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi
- Kupata homa
- Kupata damu innje ya siku zako zako za-
kawaida kupata damu ya hedhi
- Wakati fulani kuhisi kichefuchefu k**a
mwanamke mja mzito na kutapika
*VIPIMO VYA PID*
Hakuna vipimo maalum kudhibitisha mwanamke
ameathirika ila Dactari hujua mwanamke
ameathirika baada ya kuchukua historia ya
muhusika na kufanya vipimo vingine k**a:
- Kuchunguza mkojo ili kufahamu k**a mgonjwa
ana mimba. Kipimo hiki ni muhimu hasa kwa
mwanamke aliye katika umri wa kuzaa au
mwenye uwezo wa kubeba mimba
- Uchunguzi wa mkojo kwenye darubini ili
kutambua aina za vimelea vinavyomletea
mgonjwa uambukizi. Aidha mkojo huweza
kuoteshwa katika maabara kwa ajili ya kutambua
aina nyingine za vimelea viletavyo uambukizi huo.
- Kupima damu kwa ajili ya kuchunguza jinsi aina
mbalimbali za chembe za damu zilivyoathiriwa na
uambukizi huo au k**a kuna mwingiliano na
magonjwa mengine yaliyojificha. Kipimo hiki kwa
kitaalamu huitwa (Full Blood Picture).
- Kuchukua utando unaozunguka shingo ya uzazi
na kuuotesha kwa ajili ya utambuzi wa aina za
vimelea viletavyo maambukizi hayo. Kipimo hiki
huitwa (Cervical culture)
- Aidha ni muhimu pia kufanya vipimo vingine kwa
ajili ya utambuzi wa magonjwa yaambukizwayo
kwa njia ya kujamiiana, k**a vile virusi vya
ukimwi na kisonono.
- Mgonjwa pia anaweza kufanyiwa ultrasound ya
nyonga ili kuangalia k**a kuna athari yeyote
katika mfumo wake wa uzazi.
*JE PID INAWEZA KUTIBIWA?*
Jibu ni ndio k**a itagunduliwa mapema inawezakana.
Pia kwa kutumia virutubisho lishe vya kampuni yetu.
*MADHARA YAKUTO-FWATA MATIBABU*
- Maumivu ya mfuko wa uzazi wakudumu
- Utapata ugumu wa kushika mimba
- Ectopic pregnancy (mtoto kuwa innje ya mfuko
wa uzazi)
- Kuziba kwa njia ya uzazi
*JINSI YA KUZUIA MAAMBUKIZI*
Kuna njia kadhaa za kuzuia maambukizi katika
mfumo wa uzazi. Njia hizi ni pamoja na:
- Njia hakiki ya kujizuia na maambukizi haya ni
kuwacha ngono zembe na kufanya ngono salama
- Kuwahi kuwaona wataalamu wa afya mara dalili
za ugonjwa huu zinapoanza kujitokeza au pindi tu
unapogundua kuwa mwenzi wako ana dalili za
magonjwa ya zinaa au anatembea na wanawake
wengine
- Kufanya vipimo mara kwa mara hasa vya
mfumo wa uzazi, pamoja na vipimo vya
maambukizi ya magonjwa yanayosambazwa kwa
njia ya ngono (STI) khususan ugonjwa wa
chlamydia ufanyie vipimo kila mwaka mara 1
- Kutofanya ngono mara baada ya kujifungua,
mimba kutoka au mara baada ya kutoa mimba ili
kuhakikisha njia ya shingo ya uzazi imefunga
vema.
Kwa msaada zaidi kuondokana na tatizo hili wasiana nasi kwa tiba bora za Asili toka marekani🏅
Kwa maelezo Zaid piga 0657187144
30/06/2023
TATIZO LA GANZI YA MIGUU NA MIKONO(MIGUU KUWAKA MOTO NA TIBA YAKE)
Ganzi ni moja ya tatizo/ugonjwa unaowakumba watu wengine sana na ni tatizo ambalo linakera sana kwa sababu hata unapoenda hospitali Mara nyingi utapimwa lakini awaoni tatizo tatizo lolote
NINI HASWA CHANZO CHA TATIZO HILI
1:UMRI
Kawaida mtu anapokua umri umeenda, mwili mzima uzeeka pamoja na mfumo mzima wa damu, hii husababisha mishipa midogo midogo ya damu kufa, au kuziba hii husababisha chakula na hewa ya oksijeni kutofika kwa ufasaha maeneo ya mbali k**a miguuni na vidoleni hali hii hupeleekea mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa safi hivyo ganzi hutokea
2:KISUKARI
Sukari inapokua nyingi kwenye mzunguuko wa damu hupelekea kuunguza mishipa ya damu halo hii husababisha mishipa kusinyaa ambalo hupelekea hewa ya oksijeni na chakula kutofika kwa ufadsaha maeneo ya mbali sana k**a miguuni na mikononi hali hii husababisha mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa hivyo husababisha ganzi
3:DAMU NZITO
Damu inapokua nzito pia hupelekea MTU kupata tatizo LA ganzi kwa ni husababisha kutofika kwa damu kwenye mishipa midogo midogo ya damu hii hupelekea ganzi pia
4 UZITO MKUBWA
Uzito mkubwa unaweza kupeleka kupata changamoto ya ganzi Kwa baadhi ya viungo katika mwili kutokana na damu kuwa nzito na kushindwa kusafiri vizuri katika mishipa midogo midogo kutokana na kiasi kikubwa cha mafuta kwenye njia za damu
5 KUKAA MDA MREFU
Watu wengi hupata changamoto yakupata tatizo la ganzi kutokana na kukaa sehemu moja mda mrefu bila kufanya mazoezi kutokana labda na kazi unayoifanya au sabb nyingine yoyote inayokulazimu kukaa sehemu moja mda mrefu
TIBA YA GANZI
Tuna virutubisho asilia kabisa na iliyodhibitishwa na mamlaka ya chakula na dawa
-Hii ni dawa asili ya kupambana na tatizo hili bila madhara
-Imetengenezwa na mitishamba mitatu yenye uwezo mkubwa sana wa kufungua mishipa midogo midogo ya damu ambayo inapoziba au inapokua ndio chazo cha tatizo hili
-Huzuia damu isivilie kwenye mishipa hivyo huondoa hatari ya kiharusi
-Huiuisha mishipa midogo midogo ya damu na kuruhusu damu kupita
Pia tuna kirutubisho chenye madini aina tano ambayo ni muhimu kwa afya ya kila mmoja
-Inafaa sana Kwa afya ya mifupa na kusaidia kwenye changamoto ya maumivu au uchakavu wa viungo husaidia kuondoa tatizo la ganzi ikiambatana na bidhaa nyingine
Pia kwa changamoto zifuatazo
*Homon imbalance
**Tezi Dume
***Pressure
****Sukari
*****Bawasiri
******Mfumo wa uzaz wa mwanaume/nguvu za kiume
Kwa ushauri na tiba wasiliana na Muhudumu wetu
Whatsapp na kupiga
Kwa malezo zaidi karibu.
Afya bora kwa vitu asilia
0657187144
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Telephone
Website
Address
Arusha