MTAfrica Wellness

MTAfrica Wellness

Share

π—ͺπ—²π—Ήπ—Ήπ—»π—²π˜€π˜€ | π—₯𝗲𝗳𝗢𝗻𝗢𝗻𝗴 π—¦π˜π˜†π—Ήπ—² | π—œπ—»π˜€π—½π—Άπ—Ώπ—Άπ—»π—΄ π—Ÿπ—Άπ˜ƒπ—Άπ—»π—΄
πŸ“© DM for consultations & curated essentials

14/10/2025

OCTOBER, 14TH 2025
HAPPY NYERERE DAY

Today we honor the Father of our Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere πŸ‡ΉπŸ‡Ώ
A visionary leader whose wisdom, humility and patriotism continue to guide us.

MTAfrica Health & Wellness stands for that same spirit - building a stronger, healthier and more conscious Africa. 🌍πŸ’ͺ🏽

27/09/2025

Kisukari ni moja ya sababu kuu za magonjwa ya figo.

Sukari ikiwa nyingi mwilini huathiri mishipa midogo ya damu kwenye figo, jambo linalopunguza uwezo wa mishipa hii kuchuja uchafu na maji ya ziada mwilini.

Kadiri uharibifu unavyoongezeka, figo hushindwa kufanya kazi ipasavyo kwa sababu hazipati damu ya kutosha hali inayopelekea matatizo mengine makubwa k**a shinikizo la damu, kuvimba kwa mwili, magonjwa au shida za figo na hatimaye figo kushindwa kabisa kufanya kazi (kidney failure).

Jinsi ya kulinda figo zako:

βœ… Dhibiti kiwango cha sukari mwilini, k**a unatumia dawa za sukari zingatia utaratibu wa dawa na usiache kutumia dawa na usibadili dawa bila maelekezo ya daktari.
βœ… Kunywa maji ya kutosha
βœ… Punguza chumvi kupita kiasi
βœ… Epuka matumizi ya dawa bila ushauri wa daktari
βœ… Fanya uchunguzi wa figo

0767 536 986 MTAfrica Wellness

16/08/2025

Afya ya nywele inategemea sana lishe bora yenye virutubisho muhimu. Mayai ni chanzo kizuri cha protini na biotini, virutubisho vinavyosaidia ukuaji wa nywele na kuzuia nywele kukatika. Vilevile, Yogurt ina vitamini B5 na protini, ambavyo huimarisha nywele na kuzuia upotevu wake. Parachichi kwa upande wake lina vitamini E na mafuta ya asili yanayosaidia kulinda nywele dhidi ya uharibifu na kuzifanya zibaki na unyevu wa kutosha.

Mafuta ya samaki ni chanzo bora cha asidi ya mafuta ya Omega-3, ambayo huchochea ukuaji wa nywele na kuboresha afya ya ngozi ya kichwa, hivyo kuzuia ukavu na mba. Pia, vyakula vya jamii ya karanga k**a lozi na korosho vina biotini, zinki na mafuta mazuri yanayosaidia kuimarisha nywele na kuzifanya zionekane zenye afya na kung'aa.

Kwa kula vyakula hivi mara kwa mara, mtu anaweza kuimarisha afya ya nywele zake, kuzuia kukatika, na kuhakikisha kuwa ngozi ya kichwa inabaki yenye unyevu na afya bora.
0767 536 986

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address

Dar Es Salaam