Dr Lyimo

Dr Lyimo

Share

Tunatoa ushauri na kutatua changamoto za kiafya kwa kutumia tiba lishe zisizo na kemikali

19/09/2022

Taua changamoto za mfumo wa.mmeng'enyo wa.chakula kwa kutumoa dawa za tiba lishe zisizo na kemikali.

19/09/2022

Kiungulia (heartburn) ni hali ya kuhisi mchomo (maumivu k**a moto) unaotokea nyuma ya mfupa wa kidari. Kwa kawaida maumivu haya huanzia kwenye umio (oesophagus) na kupanda kifuani na yanaweza kuenea mpaka kwenye shingo au koo.

Ni nini husababisha kiungulia?
Karibu kila mtu hupatwa na kiungulia kwa wakati fulani katika maisha yake. K**a unapata kiungulia mara kwa mara, unaweza kuwa na ugonjwa unaosababishwa na kucheua mara kwa mara unaoitwa gastroesophageal reflux disease. Katika hali ya kawaida, chakula kinapoingia tumboni, ukanda wa misuli ulio mwishoni mwa umio hukaza na kukifungia chakula tumboni. Ukanda huu huitwa lower esophageal sphincter. K**a ukanda huu hautafunga vyema au kulegea, asidi zinazosaidia kumeng’enya chakula zilizo tumboni, zinaweza kurudi juu kwenye umio na kusababisha hisia ya mchomo.

Nani yuko katika hatari zaidi ya kupata kiungulia?
Ujauzito na dawa nyingi zinaweza kusababisha kiungulia.
Kiungulia hutokea kwa sababu mtoto anayekua hujaza fumbatio la mama na kusukuma tumbo juu zaidi kuliko kawaida. Asidi zilizo kwenye tumbo la mama zinazosaidia katika umeng’enyajiwa chakula husukumwa juu kwenye umio lake na kusababisha hisia ya mchomo. Ni muhimu kumhakikishia mama mjamzito kuwa tatizo hili litakwisha baada ya kujifungua.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address

Ilala
Dar Es Salaam