Mwajuma na afya

Mwajuma na afya

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mwajuma na afya, Health/Beauty, Dar es Salaam.

08/12/2022

nini husababisha kiungulia?
Karibu kila mtu hupatwa na kiungulia kwa wakati fulani katika maisha yake. K**a unapata kiungulia mara kwa mara, unaweza kuwa na ugonjwa unaosababishwa na kucheua mara kwa mara unaoitwa gastroesophageal reflux disease. Katika hali ya kawaida, chakula kinapoingia tumboni, ukanda wa misuli ulio mwishoni mwa umio hukaza na kukifungia chakula tumboni. Ukanda huu huitwa lower esophageal sphincter. K**a ukanda huu hautafunga vyema au kulegea, asidi zinazosaidia kumeng’enya chakula zilizo tumboni, zinaweza kurudi juu kwenye umio na kusababisha hisia ya mchomo.


@+255625900937

08/12/2022

Kiungulia ni tatizo katika mfumo wa chakula ambalo husababishwa na kucheuliwa kwa mchanganyiko wa tindikali na chakula kutoka tumboni kuelekea katika koo la chakula(eneo kati ya umio na tumbo) mchanganyiko huu wenye tindikali huunguza maeneo haya na kusababisha maumivu makali katika koo la chakula.

Nyongo huzalisha tindikali iitwayo Hydrogen Chloride(HCl), tindikali hii ni kali sana na ina uwezo wa kumengenya hata chuma. tindikali hii huzalishwa na kusafirishwa tumboni ambako hutumika kumeng'enya chakula na kuangamiza vimelea ambavyo huweza kuwa hatari mwilini.

Kati ya tumbo na koo la chakula kuna mlango ambao hurekebisha upitaji wa vyakula kati ya tumbo na koo la chakula, hivyo kuathiriwa kwa mlango huu ndio hasa sababu kubwa ya kiungulia, mlango huu huweza kuathiriwa kwa namna nyingi ikiwemo msukumo mkubwa chakula kutoka tumboni au kusinyaa na kutanuka kwa misuli inayorekebisha ufungukaji wa mlango huo.

@0625900937

08/12/2022

Ni moja ya changamoto zinazotokana na mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula na limekuwa likiwatesa watu wengi Sana , kibaya zaidi Ni kwamba watu wengi hawajui wafnyr Nini kuweza kuepukana na changamoto hii au vihatarishi vinavyoweza kumfanya MTU akapata tatizo hili na tiba sahihi ya tatizo hili.

Leo katika makala hii ningependa tuangalie kwa undani zaidi nini Chanzo Cha Tatizo hili, dalili , Madhara na tutaenda mbali zaidi kwa kugusia kundi linaloathirika zaidi ambalo Ni wajawazito na Namna ya kuweza kukabiliana na tatizo hili la kiungulia .
Nakusihi ufatilie kwa ukaribu makala hizi ujifunze zaidi.

Kwa masiliano zaidi piga/whatsup
+255625900937

05/12/2022

YA BAWASIRI/MGORO BILA KUFANYIWA UPASUAJI
+255625900937

👉BAWASIRI ni ile hali ya kutokwa na kinyama kwenye njia ya haja kubwa au uvimbe kwenye tundu la haja kubwa

ZA UGONJWA WA BAWASIRI

Ishara na dalili za bawasiri kawaida hutegemea aina ya Bawasiri

BAWASIRI YA NJE
Hizi ziko chini na nje ya ngozi karibu na sehemu ya kutolea haja kubwa. Ishara na dalili zinaweza kujumuisha:

1. Kuwasha katika maeneo yaliyozunguka sehemu ya haja kubwa
2. Maumivu au usumbufu
3. Kuvimba kuzunguka sehemu ya kutolea haja kubwa
4. Mara nyingine yaweza Kuvujadamu au k**a michubuko
5. Kutokwa na kinyama baada ya kwenda haja.

BAWASIRI YA NDANI
Bawasiri ya ndani iko ndani ya sehemu ya kutolea haja. Kawaida huwezi kuziona au kuzihisi, na mara chache husababisha usumbufu. Lakini kukaza au kuwasha wakati wa kupitisha kinyesi kunaweza kusababisha:

1. Kutoa haja/kinyesi chenye damu na maumivu yasiyo makali. Unaweza kuona kiasi kidogo cha damu nyekundu kwenye haja yako.
2. Maumivu na muwasho sehemu ya haja

UTAKAYO PATA ENDAPO USIPOCHUKUA HATUA MAPEMA
⚡Saratani ya utumbo mpana

⚡Kutokuhimiri choo

⚡Upungufu wa nguvu za kiume

⚡Kutokupata hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke

⚡Kuvurugika kwa homoni

⚡Kukosa molali ya kufanya kazi na kuathirika kisaikolojia

MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA BAWASIRI.

🩺 ya Bawasiri hutegemeana na aina ya Bawasiri, Mara nyingi Wagonjwa wa Bawasiri hupatiwa Tiba ya kukutwa kinyama na kushauriwa kuendelea na tiba ya vyakula lakini Tiba huwa haina matokeo mazuri kwa sababu BAADA ya muda TATIZO hujirudia kutokana na kwamba , hawajatibu Chanzo Cha TATIZO.Hivyo Tiba nzuri ya Bawasiri Ni kutumia Dawa itakayotibu Chanzo Cha TATIZO huku ukiendelea na tiba ya chakula.

🥝ZINGATIA KANUNI YA CHAKULA BORA KWA KUENDELEA KULA MBOGAMBOGA ZA MAJANI , MATUNDA NA NAFAKA ZILIZOKOBOLEWA.

🥝KUNYWA MAJI MENGI ANGALAU GLASI SITA HADI 12 KWA SIKU.

🥝EPUKA KUTUMIA MUDA MREFU CHOONI.

🩺KWA USHAURI NA TIBA
PIGA/WHATSUPP +255625900937
-na-afya

28/11/2022

Fahamu kuhusu Bawasiri.
👉Je! Bawasiri Ni nini?
👉Nini kinasababisha Bawasiri?
👉Chanzo Cha Bawasiri Ni Nini?
👉Dalili za Bawasiri Ni nini?
👉Je! Madhara ya Bawasiri Ni zipi?
👉Je! Bawasiri inatibika?

Kifahamu kwa undani kuhusiana na changamoto ya Bawasiri
Usiache kufatilia madarasa yangu la afya kila siku au piga simu au tuma ujumbe wa whatsup kwenda 👉+255625900937

24/11/2022

Chanzo cha tatizo

Watoto wadogo, hasa wale ambao bado wananyonya na ndio kwanza wamenzishwa vyakula vigumu zaidi ya maziwa ya mama, mara nyingi hupatwa na choo kigumu au kukosa choo kabisa, hii hali tunaiita constipation au kuvimbiwa. K**a mama anasumbuliwa na tatizo la kukosa choo huenda mwanae pia akasumbuliwa na tatizo hilo.
Mwajuma na afya

24/11/2022

wa choo kwa mtoto husababishwa na mambo mengi, kubwa katika hayo ni mlo mbaya usiozingatia afya. Mlo mbaya unajumuisha kuacha kula matunda na mboga za majani. na staili mbaya ya maisha ikiwa ni pamoja na kutokunywa maji ya kutosha kwa siku. Iwapo mtoto wako mchanga au mdogo ana tatizo la kukosa choo fanya yafuatayo:

1. Massage tumbo la mtoto. Kufanya hivi hufanya misuli ya tumbo kulegea na kuweza kumfanya mtoto apate choo kirahisi.

2. Mfanyishe mazoezi – mlaze mtoto kwa mgongo, shika miguu kisha anza kuzungusha k**a mtu ana nyonga baiskeli. Hii inasaidia misuli ya tumbo kutanuka na kusogea hivyo kuufanya utumbo upate pressure na kusaidia choo kutoka kirahisi.

3. K**a mtoto anakunywa maziwa ya kopo (formula) badilisha umpe maziwa yenye nembo (brand) tofauti. Maziwa huweza kuwa chanzo cha kumfanya mtoto avimbiwe. Kubadilisha huweza kuondoa tatizo.

4. Pendelea kumpa mtoto mlo wenye virutubisho vya nyuzi nyuzi (fibre). Vyakula hivi ni k**a mboga za majani na zile jamii ya kunde – maharage pamoja na matunda – apple n.k.

5. Hakikisha mtoto anakunywa maji ya kutosha. Maji ni muhimu sana, hasa kwa mtoto anayezidi umri wa miezi 6. Hakikisha anapata maji ya kutosha ili kuupa mwili wake uwezo wa kujisafisha na kutoa uchafu kirahisi. Kutokuwa na maji mengi huweza kumletea matatizo makubwa zaidi ya kukosa choo. Hivyo kuwa makini.

6. Usikoboe chakula cha mtoto

7. Usimpe vyakula vyenye sukari

8. Mpe juisi mara 2 au 3 kwa siku. Hakikisha juisi anayopewa mtoto inatengenezwa na matunda, siyo juisi ya kununua. Afya ya mwanao ni kitu muhimu, hivyo hakikisha usalama na ubora wa chakula anachokula.

9. Mpake mafuta ya n**i sehemu ya kutolea choo. Hii husaidia kulainisha vizuri misuli na kuwezesha kupata choo kirahisi.

10. Muogeshe maji ya uvuguvugu

11. Mpe matunda k**a apples, machungwa, plums, appricot, prunes haya yanasaidia kinyesi kutokua kigumu na kikavu.

12. Hakikisha haumpi mtoto chini ya mwaka mmoja maziwa ya ng’ombe. Maziwa ya ng’ombe hayashauriwi kwa mtoto chini ya umri wa mwaka mmoja kutokana na kutokuwa na uwiano bora wa virutubisho kwa mahitaji ya mtoto. Unaweza kusoma vizuri kwenye makala nyingine hapa.

13. Yote haya yakishindikana, tafadhali muone daktari wa watoto ili apate kumuangalia ziadi na kumpa tiba mbadala.

Mwajuma na afya
+25525900937

24/11/2022

mzazi utakumbana na mambo mengi. Hakuna kitu kinamuumiza mzazi k**a kumuona mwanae anapata maumivu. Vitu vingi hutokea, pengine kutokana na makosa yetu au katika hali ya kawaida katika kukua kwa mtoto. Na kipindi kigumu sana katika malezi ni pale unapoanza kulea mtoto wa kwanza mwaka wa kwanza wa maisha yake.

Leo napenda kuongelea swala muhimu sana ambalo huwapata watoto wengi na k**a mzazi anakuwa siyo mzoefu anaweza kupata wasiwasi. Hili ni tatizo la mtoto kukosa choo. Nimejifunza mengi katika kulea, hivyo napenda kukushirikisha kwenye mbinu tofauti za kutatua matatizo madogo madogo kabla ya kukimbilia hospitali.
Tatizo la kukosa choo watoto wadogo au kuwa na choo kigumu na jinsi ya kulitatua
Watoto wadogo hasa wale ambao bado wananyonya na ndio kwanza wamenzishwa vyakula vinginevyo zaidi ya maziwa, mara nyingi hupatwa na choo kigumu au kukosa choo kabisa hali tunayoiita kimombo, constipation.

Hali hiyo huanza pale mtoto anapoachishwa maziwa ya mama na kuanza kunyweshwa maziwa ya kopo au mengineyo au pia anapoanzishwa kula vyakula vingine zaidi ya maziwa. Mara nyingi watoto wanaonyonya maziwa ya mama huwa hawasumbuliwa na tatizo hilo, bali tatizo hilo huanza kujitokeza pale wanapoanza kulishwa vyakula vingine zaidi ya maziwa ya mama. Pia mama ambaye tayari mwenyewe anasumbuliwa na tatizo la kukosa choo, huenda mwanae pia akasumbuliwa na tatizo hilo.

Iwapo mtoto wako mchanga au mdogo ana tatizo la kukosa choo au kupata choo kigumu kwanza wasiliana na daktari au mpeleke hospitalini ili upate ushari wa daktari. Pia unashauriwa kujaribu njia zifuatazo:
Mwajuma na afya
@+255625900937

24/11/2022

Tatizo la kukosa choo watoto wadogo au kuwa na choo kigumu na jinsi ya kulitatua
Watoto wadogo hasa wale ambao bado wananyonya na ndio kwanza wamenzishwa vyakula vinginevyo zaidi ya maziwa, mara nyingi hupatwa na choo kigumu au kukosa choo kabisa hali tunayoiita kimombo, constipation.

Hali hiyo huanza pale mtoto anapoachishwa maziwa ya mama na kuanza kunyweshwa maziwa ya kopo au mengineyo au pia anapoanzishwa kula vyakula vingine zaidi ya maziwa. Mara nyingi watoto wanaonyonya maziwa ya mama huwa hawasumbuliwi na tatizo hilo, bali tatizo hilo huanza kujitokeza pale wanapoanza kulishwa vyakula vingine zaidi ya maziwa ya mama. Pia mama ambaye tayari mwenyewe anasumbuliwa na tatizo la kukosa choo, huenda mwanae pia akasumbuliwa na tatizo hilo.

Mtoto mwenye tatizo la kukosa choo huwa anapata choo kwa shida huku akisumbuliwa na tumbo na kupata choo kigumu. Wakati mwingine hulia wakati akipata choo huku akijiminya na kukunja uso.
Muone daktari iwapo mtoto ana umri wa chini ya mwezi mmoja na hajapata choo kwa siku 4.

@+25525900937
#.

23/11/2022

mwili: Mazoezi yanasaidia kuimarisha mzunguko wa damu kwenye mfumo wa chakula na kuimarisha misuli na hivo kurahisisha utolewaji wa kinyesi. Utafiti unasema watu wanaotumia mda mwingi wakiwa wamekaa hasa maofsini wanaongoza kwa kuapata matatizo ya kukosa choo kwa mda mrefu.
@+255625900937

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address

Dar Es Salaam