MWILI WANGU AFYA YANGU.
All about nutrient and supliments
01/03/2020
*UJUE UGONJWA WA P.I.D*
Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa kifupi PID, ni moja ya matatizo ambayo huwaathiri sana wanawake. Kwa kawaida maambukizi haya huusisha shingo ya uzazi (cervix) hali ambayo hujulikana k**a cervicitis, nyama ya mfuko wa uzazi (endometrium) ambayo kitaalamu huitwa endometritis, na mirija ya uzazi (fallopian tubes) hali ijulikanayo kitabibu k**a salpingitis.
1⃣ *_PID husababishwa na nini?_*
Pamoja na aina kadhaa za vimelea kuhusishwa na PID, vimelea vya jamii ya Neisseria Gonorrhoeae pamoja na Chlamydia trachomatis ndivyo vinavyoongoza kwa umaarufu zaidi katika kusababisha PID kwa akina mama.
2⃣ *Je mwanamke huambukizwaje PID?* Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na ✅Kufanya ngono isiyo salama. ✅Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara baada ya kujifungua (au postpartum period) ✅Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post abortion) au mara baada ya mimba kutoka (miscarriage) ✅Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi (IUCD) k**a njia mojawapo ya uzazi wa mpango. ✅Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya PID.
3⃣ *Dalili za PID ni zipi?* Zipo dalili kadhaa za ugonjwa huu wa PID. Miongoni mwa dalili hizi ni :- ✅Mwanamke kuhisi maumivu ya tumbo hasa maeneo ya chini ya kitovu ✅Kupata maumivu ya mgongo. ✅Mwanamke kupata utoko mchafu sehemu za siri. Utoko huu huambatana na harufu mbaya. ✅Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa. ✅Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa. ✅Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi. ✅Kupata homa. ✅Wakati fulani kuh canisi kichefuchefu na
Pia kutapika.
Karibuni sana upate tiba na msaada kwa kupiga 0622291850 share na wadada wenzio
01/03/2020
JIPATIE TIBA SAHIHI YA BAWASILI (HEMORRHOIDS)
Bawasili ni hali ya kuvimba au kutanuka kwa mishipa ya vena{varicose viens} iliopo ndani ya njia ya haja kubwa. Katika ile misuli imara inayozungunguka na kutengeneza muundo wa njia ya haja kubwa pamoja na puru{rectum}ambapo sasa ugawanywa katika aina mbili ya ndani na ya nje.
Bawasili ni mojawapo ya tatizo ambalo mara nyingi linapotokea humfanya mtu kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba sahihi.
Kuna aina mbili za Bawasiri
Bawasil Ya Nje: Aina hii ya bawasili hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa, na huweza kuambatana na maumivu, pamoja na kuwashwa kwa ngozi katika eneo hilo. Hali hii huwa na maumivu makali sana na ngoziyake ugeuka kuwa ya blue au zambarau. Mara nyingine mishipa hiyo ya damu (vena) hupasuka na damu huganda na kusababisha aina fulan ambalo kitaalamu linaitwa Thrombosed hemorrhoid.
Bawasili Ya Ndani: Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa. Na huwa haimbatani na maumivu na wengi huwa hawatambui kuwa wanatatizo hili.
Aina hii imegawanyika katika mainisho yafuatayo:
Daraja I- Bawasiri kutotoka katika mahali pake pa kawaida
Daraja II- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe baada ya tukio hilo.
Daraja III- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kuirudisha mwenyewe baada ya tukio hilo.
Daraja IV- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na vigumu mtu kuirudisha baada ya tukio hilo.
JE BAWASILI HUSABABISHWA NA NINI?
• Tatizo sugu la kuharisha
• Kupata kinyesi kigumu
• Uzito kupita kiasi (obesity)
• Kupenda kufanya ngono ya njia ya haja kubwa (a**l s*x)
• Kwa ujumla mambo yanayo ongeza shiniko katika tumbo.kunyanyua vitu vizito, kikohozi cha muda mrefu nk
• Umri mkubwa,
• Vyakula vya kukoboa,
• Kufanya kazi ukiwa umekaa kwa muda mrefu.
• Kuchuchumaa kwa muda mrefu wakati wa kujisaidia.
• Mtu mwenye tatizo la ini
•
DALILI ZA BAWASILI
• Damu kwenye kinyesi wakati wa kujisaidia (hematochezia)
• Maumivu au usumbufu njia ya haja kubwa
• Kinyesi kuvuja.
• Kijiuvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa
• Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa
• Kujitokeza kwa kinyama (bawasili) wakati wa haja kubwa
MATATIZO YANAYOWEZA KUTOKANA NA BAWASILI
• Upungufu wa damu mwilini (Anemia)
• Strangulated hemorrhoids
• Kushindwa kujisaidia kwa amani
NJIA ZA KUZUIA BAWASILI
• High fibre diet {makapi lishe}, kula mboga za majani, matunda, na nafaka kwa wingi.
• Kunywa maji mengi kiasi cha kutosha.
• Punguza kukaa kwa muda mrefu sana hasa ukiwa chooni, kwa sababu unaweza kuongeza shinikizo katika mfereji wa haja kubwa.
• Fanya mazoezi
Utofauti wa hemorrhoids na re**al fissures
• Bawasili ni hali ya kuvimba kwa mishipa ya vena iliopo ndani ya haja kubwa. Re**al fissures ikiwa ni hali ya kuchanika au kuwa na vidonda kwenye njia ya haja kubwa. Na ikiwa ni tatizo ambali hutokana na kupata kiasi kikubwa kupita uwezo wa njia yenyewe. Hivyo basi k**a kutaingia bacteria basi hili huwa ni tatizo la kudumu eneo husika.
KWA USHAURI NA TIBA WASILIANA NASI KWA NAMBA
0622291850/sms/call/whatsaap
21/02/2020
Watu wengi wanapata changamoto ya vidonda vya tumbo (ULCERS). na wametumia dawa mbalimbali bila mafanikio.
JE, UNATAKA SULUHISHO?
Tumia bidhaa za forever living products ambazo ni ALOE VERA GEL na FIELDS OF GREEN kutatua tatizo la vidonda vya tumbo.
JIBU K**A NDIO! ILI KUPATA ODA YAKO LEO
WASILIANA NASI KUPITIA 0622291850 AU whatsapp 0622291850
21/02/2020
JE, MENO YAKO YANAUMA,KUFA GANZI, YAMETOBOKA, KINYWA KINATOA HARUFU MBAYA NA UNA VIDONDA MDOMONI?
TUMIA DAWA YETU YA MENO ILIYO BORA KABISA KUONDOA MATATIZO YAKO NA KUNG'ARISHA MENO.
DAWA YETU HAINA FLOURIDE. NA UKIIANGALIA IMEANDIKWA NO FLOURIDE. HAWAJAWEKA FLOURIDE KWASABABU FLOURIDE INA MADHARA KWA AFYA YA MENO. NDIO MAANA KWENYE DAWA ZINGINE WAMEANDIKA USIMEZE NA KWA MTOTO MDOGO UMSIMAMIE. LAKINI NI MARA CHACHE SANA MTOYO KUACHA KUMEZA.
DAWA YETU HATA UKIMEZA HAINA MADHARA.
ZA
KUONDOA HARUFU MBAYA KINYWANI.
MAUMIVU KWENYE MENO KWA KUUA BAKTERIA WANASABABISHA MENO KUOZA.
MADONDA KINYWANI
K**A HUDUMA YA KWANZA K**A UMENG'ATWA NA MDUDU, UMEUNGUA NA TUMBO KUJAA GESI. KWAHIYO PIA ITAKUSAIDIA KUONDOA HAYO MATATIZO.
KWA MAHITAJI NA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI KWA 0622291850 AU WHATSAPP MOJA KWA MOJA.+255622291850
21/02/2020
TUMIA NEW FOREVER KIDS KUMREJESHEA MTOTO WAKO HAMU YA KULA.
Watoto wengi wanakosa lishe bora kwasababu wanashindwa kupata virutubisho vya kutosha kutoka kwenye chakula. Hii inasababibishwa na watoto kutopenda kula mboga za majani. Vilevile ukosefu wa vitamini unaweza ukawapelekea watoto kukosa hamu ya kula na hivyo kuwapelekea kudhoofika kwa afya zao.
FOREVER KIDS NI NINI?
Ni kirutubisho ambacho kina mchanganyiko wa vitamini na madini mbalimbali ambayo yatoka kwenye matunda na mboga mbalimbali k**a vile karoti,spinach, cabbage, apples cranberries na nyanya.
Forever kids iko katika mfumo wa vidonge au tembe vitamu k**a p**i ambavyo hupelekea watoto kuvipenda kuvitafuna.
kids ina vitamini A,C, D na B12 pamoja na madini ya calcium,chuma na zinc.
FAIDA ZA FOREVER KIDS.
hamu ya kula kwa mtoto. Ambapo inampatia virutubisho zaidi na kuboresha afya yake.
kuumpa mtoto vitamini na madini muhimi kwa afya njema na kuboresha mfumo wa kinga na hivyo kuuwezesha mwili wake kipambana na magonjwa.
Ina ladha nzuri ambayo inampelekea mtoto aipende kuitumia.
Pia watu wazima wanaruhusiwa kutumia k**a unapata changamoto ya kutopata hamu ya kula.
NB: INA TEMBE 120 AMBAZO ZINAWEZA KUTUMIKA KWA MIEZI MIWILI.
NAMNA YA KUTUMIA FOREVER KIDS.
Kwa mtoto wa miaka miwili mpaka miaka minne atumie tembe(vidonge) mbili kwa siku chini ya usimamizi wa mzazi.
Kwa mtoto ambae ana miaka zaidi ya minne na watu wazima watumie vidonge vinne kwa siku.
KWA MAELEZO ZAIDI NA KUPATA ORDER YAKO WASILIANA NASI KWA KUTUMA NENO KWENDA 0622291850 AU WHATSAPP 0622291850
21/02/2020
PUNGUZA UZITO KIAFYA
Je Uzito mkubwa, tumbo kubwa ni kero kwako?
Watu wengi wamekuwa wakihangaika sana kutaka kupunguza uzito nakujikuta wakitumia njia mbali mbali ambazo si salama kabisa kwa afya sababu wamekuwa wakichukizwa na uzito walio nao.
ili uweze kupunguza uzito kuna vitu vikubwa Viwili vya msingi sana kuvijua, uzito mkubwa husababishwa na SUMU nyingi pamoja na MAFUTA yaliyozid mwilini hivyo hupelekea watu kudhani kujinyima kula au kwenda Gym pekee huwafanya wapunguze uzito laa hasha, tambua mafuta mengi kuzid mwilini ni matokeo wakati chanzo cha kuongezeka uzito ni sumu nyingi ambazo hupelekea ini kuzalisha mafuta mengi ili kukabiliana na sumu nyingi zilizopo mwili.
unapojinyima kula unaunyima mwili virutubisho ambavyo unahitaji kila siku na unapoenda gym kufanya mazoezi hukusaidia kupunguza mafuta lakin huondoa mafuta mengi zaid hata ambayo mwili unahitaji hivyo kupelekea ini kujihami tena kuzalisha mafuta mengine tena ili kukabiliana na sumu zinazozidi kuzalishwa na matokeo yake utapunguza calories kadhaa naukitoka hapo ham ya kula itakuw kubwa zaid na kujikuta unaongeza carolies nyingine nyingi zaid na uzito kurudi pale pale au kuongezeka zaidi.
Ili uweze kupunguza uzito yatakiwa upate program maalum na mazoezi maalum kabisa zitakazo kusaidia kuondoa sumu ili uandae mwili kupunguza uzito kiafya kabisa kabisa bila kujinyima sana kula na kufanya mwili uendelee kupata virutubisho unavyohitaji kila siku.
KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI KUPITIA 0622291850 AU TUMA NENO KWA WHATSAPP NO. 255622291850
21/02/2020
UHUSIANO KATI YA DAMU NA TABIA YA MTU
Je unajua kuwa tabia ulizonazo ni kutokana na kundi lako la damu?
Kwa kawaida kila binadamu yuko kwenye kundi mojawapo la damu kati ya makundi manne A,B,AB na O.
Makundi haya yanaweza kutumika kufahamu tabia za binadamu na jinsi hii yaweza kuwa rahisi na ya karibu zaidi kuliko kutumia nyota “astrology” k**a ambavyo wengi wanafanya, na wataalamu wanasema tabia kwa
uhusiano na kundi la damu ina uhakika zaidi kuliko wenye vyanzo vingine. Mbali na tabia, ukweli ni kwamba makundi yetu ya damu yanaweza kutuonyesha pia vile mtu anavyopendelea na asivyopendelea,
kazi anazopendelea, watu anaowapendelea na hata vyakula. Baadhi ya watafiti nchini korea wamebainisha kuwa hata namna tunavyopendelea kuketi hutegemea sana na makundi yetu ya damu, sasa tuangalie uhusiano huu
Damu kundi “A”
Hawa watu maranyingi huwa mifano ya kuigwa na wengi kwasababu ya kiu zao na upiganaji wao kwenye mafanikio, ni watu wema,wapole na wenye tabia njema.
Pamoja na hayo ni rahisi sana watu hawa kupata msongo wa mawazo “stress” na kufikiria sana vitu. Wakiamua kujitoa kwa ajili ya kumsaidia mtu basi wanazama kabisa na wanaweza hata kujisahau wao.
Mazuri yao
Ni watu wanaopenda vitu vikamilike katika hali ya juu “perfectionists”, wanapenda mpangilio maalumu, wanapenda na wanaweza kuchambua mambo sawia, wanawajibika na kubeba majukumu yao,wana huruma na wako tayari kusaidia, waaminifu, ni wagunduzi, wanamaanisha, wavumilivu, na wenye tabia njema.
Mapungufu yao
Wasumbufu,wana hisia kali hata kwenye vitu vya kawaida, wakitaka kitu wametaka, wengine wana aibu,wengine wakimya zaidi na wanaopenda kujichanganya.
Kwenye maisha ya kijamii
Ni mtu ambaye unaweza kumwamini na kumtegemea
Anajali na kumaanisha
Wakati wote huepuka shari,misuguano na magomvi
Maranyingi hawapendezwi wala kufurahia sherehe zenye makelele na shangwe za ajabu ajabu,wanapendelea ukimya na utulivu.
Kazini
Unaweza kumwamini na kumtegemea katika majukumu
Wanapenda ufanisi wa kiwango cha juu kwahiyo kazi zao mara nyingi ni bora sana.
Bahati mbaya wanajali sana hata vitu vilivyo vidogo nahii huwafanya kuwa na msongo wa mawazo kirahisi.
Wasio waelewa vema watu wa kundi hili wanaweza kupata shida kufanya nao kazi
Kwenye mahusiano na mapenzi
Ni ngumu kidogo wao kufunguka na kushirikisha mambo yao.
Wanaweza kuonekana wenye aibu, au waoga.
Ukitaka kumchumbia au kuchumbiwa na mtu wa kundi ‘A’ unahitaji uvumilivu.
Wakiamua kupenda utawafahamu wakati wote na ingawa watakuruhusu ufahamu tu yale maeneoa ya maishani mwao ambayo wanajua unahusika, hawawi wazi katika kila eneo.
Ukweli mwingine kuhusu watu wa kundi ‘A’
Ni watu wabunifu na wenye ujuzi wa usanii “artists”
Wa**lewa kirahisi sana, kilevi kidogo tu kitampelekesha sana
Wengi wao hupendelea kula mboga mboga “vegetarians”
Damu kundi “B”
Watu wa kundi hili maranyingi ni wenye tabia za kuasi na ni ngumu kuwazuia au kuwatuliza. Wanandoto na maono makubwa,wanasukumwa kwa kasi na kiu zao ingawa wanaweza kuwa wakali na wasumbufu na mara
nyingine ngumu kukaa na kuzoeana nao. Wanakisimamia sana kile wanachokiamini hata k**a ulimwengu mzima usimame kinyume nao.
Mazuri yao
Wanasukumwa katika kufikia malengo yao, wako kasi kiutendaji,wanapenda raha,wana hisia nzito , wanayatazama maisha katika mtazamo chanya , wanaweza kujisimamia na kujitegemea na hawahitaji ushirika au kukubaliwa na wengine.
Mapungufu yao
Wabinafsi sana,mara nyingine wanakwepa majukumu yao,wagumu sana kusamehe,wasumbufu,wanaweza kuwa wakatitili na wenye hasira za haraka.
Maisha yao kijamii
Maranyingine ni ngumu kushirikiana nao au kuwa nao maana wanapenda kufanya mambo yao wenyewe.
Kazini
Ingawa wanaweza kuwa na malengo mengi na maono pia lakini wanaweza kuwa wasumbufu na wagumu katika kushirikiana nao kazini. Ni ngumu kufanya nao kazi maana wanataka kufanya pekeyao.
Mahusiano na mapenzi
Unaweza kufurahi nao sana kwenye mapenzi lakini uwe tayari kuvumilia hasira zao kali na za ghafla. Vumilia hali yao ya kukwepa majukumu pia,fahamu kuwa wanaweza kuwa wakali, wakatili na wasio maanisha kile wanachokisema.
Baadhi ya ukweli wa kitafiti kuhusu watu wa kundi B.
Wanatabia ya utukutu.
Pamoja na baadhi ya mazuri yao bado wanaweza wasiwe watu wazuri kwenye kuwa mume, au kuwa wapenzi wazuri kwa wasichana wao. Hii ni kutokana na urahisi
wa tabia za kukosa uaminifu kimapenzi na urahisi wa kuumiza mioyo ya wengine.
Wanatabia ya kupenda wanyama “they love pets”
Wana kinga kubwa na imara ya mwili katika kujikinga na magonjwa.
Wanafurahia zaidi vyakula vitokanavyo na wanyama k**a vile maziwa “dairy products” n.k
Damu kundi “AB”
Kundi hili ni watu wenye haiba mchanganyiko, hawa huwa na tabia tofauti kuanzia kuwa waoga na wenye aibu hadi wengine ni wapenda mitoko na wacheshi,wako
wanafanya mambo kwa kuongozwa na mawazo na wengine hawawazi kabisa kile wanacho taka kukifanya,hii inafanya watu wa kundi hili kuwa watu wa kushangaza sana mara unapokuwa nao.
Mazuri yao
Ni rahisi sana kuwa rafiki nao.
Wanachukuliana na mazingira haraka na kwa urahisi.
Wenye kufurahisha unapokuwa nao ingawa ni watu wasiotabirika.
Wana mawazo,wana akili sana,hupenda kuweka mambo yao kwa vitendo na pia huongozwa na misimamo ya kifikra.
Mapungufu yao
Wagumu katika kufanya maamuzi.
Wanasahau sana
Ni wenye hisia za kayumba “mood swing”, mara wana furaha mara wamekasirika.
Sio waaminifu.
Ni wapinzani,wabishi na wakosaji.
Ni watu wabinafsi.
Maisha ya kijamii
Wanaweza kuwa marafiki wazuri na wenye kufurahisha.
Maongezi yao ni yenye kuhamasisha nayenye akili na kufikiria kwa hali ya juu.
Kwa kutokuwa wenye kutabirika, wengine huhofia
kuumizwa kihisia au kukatishwa tamaa au kuumizwa moyo na watu hawa, hususani pale wanapokuwa sio waaminifu.
Kazini
Wanaweza kuwafurahisha na kuwapa burudani mnapofanya kazi nao lakini sio watu wa kuwategemea sana,wanaweza kukuangusha kirahisi.
Mahusiano ya mapenzi
Kuwa katika mahusiano na mtu wa kundi la damu la AB kunaweza kuwa kwenye kufurahisha,unaweza usiwena nyakati nyingi za upweke. Pamoja na haya fahamu kwamba watu hawa wanaweza kuwa wabishi na
wakosoaji na maranyingine maneno yao yanaumiza. Mpenzi wa mtu au watu wa hivi lazima aelewe jinsi hisia zao zilivyo na zinavyobadilika mara kwa mara,na pale inapobidi basi uwetayari kuwapa nafasi wanayostahili ili usijiumize sana.
Baadhi ya ukweli wa kiutafiti kuhusu watu wa kundi hili.
Ni watu wazuri kwenye mambo yahusuyo fedha.
Maranyingi wanajihusisha na wanaopendendelea shughuli za kisanaa au mambo yenye sanaa ‘arts’
Ni watu wanaoaminika kuwa wabinafsi zaidi hata katika uchangiaji wa damu,watu hawa wanaweza kupewa damu na mtu mwingine yeyote ila wao hawawezi kumpa damu yeyote isipokuwa mwenzao wa AB.
K**a walivyo watu wa kundi ‘A’ na kundi ‘B’,watu wa kundi la damu ‘AB’ hupendelea vyakula vya mboga mboga “vegetables” na pia vyakula vitokanavyo na wanyama “dairy products”
Kundi la damu aina ya O.
Hawa mara nyingi wanajitahidi kuwa mahodari na mashujaa katika mambo tofauti. Mara zote kiu yao ni kuwafurahisha na kuwapendeza watu wengine ni wenye moyo wa uongozi wenye kiu ya kuwaona rafiki zao
wakiwa wenye furaha wakati wote. Sio wagumu wa mabadiliko, wako tayari kubadilika, ni wenye mawazo mapana naya wazi, sio wagumu kifikra na ni marafiki wazuri.
Faida zao
Ni wenye ujasiri, wanashindana katika mambo mengi mfano mambo ya maendeleo, hufanya kazi sana na kwa bidii, ni waaminifu, wanaweza kujieleza, ni marafiki wazuri, wanasamehe, mitazamo yao ni chanya, huweza kuhisi au kuonamambo hata kabla hayajatokea,wanakiu ya kufahamu na kudadisi na pia niwatu wema na watoaji.
Mapungufu yao
Maranyingine wanaweza kuwa wenye fujo, wanaopenda sifa, wanavutia vitu upande wao, wanaepuka au kukwepa majukumu,unaweza kuona hawa wanaigiza mambo, wakitaka wametaka hadi wapate na nirahisi kuwaondoa kwenye kile wanachokifanya “easy to be distracted”.
Maisha ya kijamii
Ni marafiki wazuri na unaoweza kuwategemea, ni waaminifu, ni wawazi,ingawa mara nyingine wanaweza kukuudhi, pia wakati mwingine wanatamani kusikilizwa wao tu.
Kazini
Wana kiu ya mafanikio, hufanya kazi kwa bidii ingawa kukatishwa tamaa na kupoteza hamasa ya kazi kirahisi sana. Mara nyingine ili wafikie malengo ni vema wakisimamiwa kwenye kazi wanayo fanya badala ya kuachwa wafanye wenyewe..
Mahusiano ya mapenzi
Ni watu wenye mvuto wa kimahaba pia watu hawa wana hisia Kali za kimapenzi wanaweza kuonyesha mapenzi kwa wale wanaowapenda ila ni vema ukafahamu kuwa watu hawa hutarajia upendo wa jinsi ile ile wao wanavyoonyesha upendo kwako bila hivyo utakosana nao.
Ukweli wa kitafiti kuhusu watu hawa
HAWAPATI MARADHI KIRAHISI
Kwanza ifahamike kuwa watu wenye damu kundi hili wamegawanyika mara mbili ambazo ni damu kundi “O” chanya (O positive) na kundi “O” hasi (“O” negative) mgawanyo huu umetokana na mgawanyo wa kitaalamu
ambao huitwa “rhesus factors” ambao ndio unaotumika kugawanya makundi ya damu.
Kwa ujumla kundi hili la damu liwe hasi au chanya halina proteins maalumu zilizomo ndani ya damu ambazo huitwa “antigens” ambazo ndizo mara nyingi ni rahisi
kushika magonjwa isipokuwa lina “antibody” ambazo ndizo kinga mwili zinazopambana na maradhi ndiyo maana damu kundi “O” linaitwa “Universal Donor” damu kundi lolote linapokea.
Na kwa wakati fulani maradhi yanayowasumbua watu wenye damu kundi hili ni malaria, kichwa na mafua na wengine husumbuliwa sana na ugonjwa wa kutoka damu za pua (Rhinits) au wengine huita kambaku ambao
husababishwa na kula nyama yenye lehemu nyingi (cholestrolel) ambazo ni nyama ya ng’ombe, kondoo, samaki aina ya dagaa, uwono na mboga ya majani inayoitwa kisamvu na wakati mwingine maziwa ya ng’ombe au kutembea kwenye jua kali sana au kutumia manukato yenye harufu kali.
NI WAPENDA NGONO
Watu wenye damu kundi hili wana hisia kali sana za mapenzi hii ni kutokana wana homoni nyingi, hali hii inawapelekea kupenda sana ngono na vile vile huwa
wakizaa wanafanana sana na watoto wao iwe sura, tabia au mwendo iwe mwanamke au mwanaume
Watu hawa Mara nyingi huwashwa masikio yao kwa ndani hivyo Mara nyingi wanajikuna masikio
Wanaaminika huwa na tabia za kijeshi.
Wengi wao kwa asili ni watu wa kupenda michezo.
Wanaaminika kuwa watu wema na waliotayari kusaidia mtu yeyote, hata katika uchangiaji wa damu ‘watu wa kundi ‘O’, wanaweza kumpa damu mtu mwingine yeyote.
Wanapendelea na kujisikia raha wanapokula nyama “meet lovers”.
Like and share
21/02/2020
Baada ya kupata watoto wanawake wengi wanaongezeka uzito na wanaweza kujikuta wameangukia kwenye uzito uliopitiliza na kuingia kwenye hatari ya magonjwa yanayosababishwa na uzito uliozidi k**a kuumwa miguu, mgongo, Presha na Sukari.
Naomba nikuhakikishie jambo,unaweza kupunguza uzito,unaweza kurudia Shepu yako ya Kabla ya Kuwa na watoto.Haijalishi umejifungua kwa njia gani.
Je na wewe unataka kupunguza uzito nipigie
Whatsap 0622291850
Kwa mawasiliano namba; 062229185
17/02/2020
WEWE DADA ULIE KUWA NA TUMBO KITAMBI hii inakuhusu Wewe dada, mama,shangaz k**a unatumbo linalo kufanya usiwe na muenokano mzuri sasa limefkia mwisho. Pata virutubisho vitokavyo kusaidia kuondoa kitambi au tumbo lililo kaa vibaya.Pia tuna kupa ushauri jinsi ya kula vizuri na aina gani ya vyakula uvitumie iliusipate tena tumbo au kambi.... Kwa maelezo zaidi piga/sms/whatsapp:0622291850
10/02/2020
Mwanzo 2:16
Mungu akamwamuru huyo Mwanaume "Waweza kula MATUNDA yeyote katika bustani"
Tafiti zinaonyesha asilimia 60 hadi 80 za magonjwa mengi siku hizi yanaanzia tumboni.
Je, Unakula na kunywa nini?
Tujitahidi kutumia Chakula bora k**a dawa ili tusije tumia dawa k**a chakula!!!
Milo yetu isikose matunda na mbogamboga kwa wingi na maji mengi. Pia tuzingatie mazoezi/kuushughulisha mwili utoe jasho.
Mawasiliano ni 0622291850
10/02/2020
JIFAHAMU HUENDA UNATATIZO LA PRESHA YA KUPANDA AMA YA KUSHUKA. 0622291850
PRESHA YA KUPANDA.
Hii hutokea pale nguvu ya msukumo wa damu inayosukumwa na moyo kwenda kwenye mishipa ya damu(Arteri) kuwa kubwa kuliko njia ya mishipa hiyo hivyo kushindwa kuhimili nguvu au mgandamizo huo wa damu,unaweza kuwa na tatizo hili la mgandamizo mkubwa wa damu(Hypertension) kwa mda mrefu bila kuhisi dalili zozote na kupelekea uharibifu wa mishipa ya damu kuzid kuendelea hadi kusababisha Shinikizo la damu(Heart Attack).
presha ya kupanda ni 140mmHg juu yaani pale mgandamizo wa damu unapozid wakati 90mmHg ni pale moyo unapojilegeza na kujaza damu k**a visemavyo vipimo ya tatizo hii..Kwamba
~Presha ya kawaida(Normal) ni 120/80mmHg
~Presha ya kupanda(Hypertension)
Stage 1) 140/90mmHg
Stage 2) 160/100mmHg
Stage 3) 180/110mmHg
Presha kubwa zaidi(Hypertensive Crisis) 240/120mmHg.
SABABU ZA PRESHA YA KUPANDA
A) STAILI YA MAISHA
i) Kutojishughulisha/Uvivu.
ii) Chumvi nyingi kwenye chakula cha kusindikwa na chenye mafuta.
iii) Pombe na uvutaji wa Sigara.
iv) Chakula kisicho na madini ya Pottasium ya kutosha.
B) UMRI
i) Umri unapozidi kuwa mkubwa kuanzia miaka 60 kunauwezekano wa kupata tatizo hili.
C) JINSIA
-Wanaume wapo hatarini kupata kwenye umri mdogo wakati Wanawake hupatwa zaidi wanapokuwa na umri mkubwa.
D)KURITHI.
E)UZITO MKUBWA.
F)MSONGO WA MAWAZO.
DALILI ZA PRESHA YA KUPANDA
i) Kizunguzungu.
ii) Kichwa kuuma.
iii) Kutoona vizuri.
iv) Kichefuchefu.
v) Kubanwa na Pumzi.
MADHARA YA MGANDAMIZO MKUBWA WA DAMU.
i) Uvimbe mkubwa kwenye kuta za arteri(Aneurysm).
ii) kupanuka au kudhoofika kwa moyo hadi kufikia kishindwa kusukuma damu ya kutosha(Heart Failure).
iii) Kusinyaa kwa mishipa ya damu kwenye figo na moyo kusababisha vishindwe kufanya kazi,ubongo na miguu pia.
iv) kupasuka kwa mishipa ya damu na kusababisha macho kutoona Vizuri au Upofu kabisa.
*PRESHA YA KUSHUKA(HYPOTENSION)*
Hii hutokea pale mgandamizo wa damu usukumwao na moyo kupitia kwenye njia au kuta za mishipa ya damu(Arteri) kuwa mdogo kuliko upana wa mishipa yenyewe hivyo kupelekea damu chache kufika kwenye ubongo,figo na sehem nyingine za viungo mwilini.
Mfano wa Viwango Vyake ni:
* 90/60mmHg.
* 115/60mmHg.
* 115/50mmHg.
DALILI ZA PRESHA YA KUSHUKA.
i)Kizunguzungu na kuanguka.
-Hii hutokana na damu kufika kidogo kwenye ubongo hasa pale unapokuwa na tatizo la kiafya.
ii) Mapigo ya moyo kuongezeka.
-Hii ni hasa pale unapokuwa umeketi na kuinuka ghafla kiwango cha damu yako kinakuwa kimebaki sehem ya chini Miguuni na endapo hakutakuwa na hatua yoyote kuchukuliwa na mwili wako husababisha presha yako kushuka na ikiwezekana kudondoka ghafla na hata kuzimia pia.
iii) kushindwa kuzingatia vzuri jambo
-kutokuwa makini eitha na taarifa muhimu upewayo au jambo muhimu la kulifanyia kazi.
iv) Kujihisi kuchoka choka sana na kutapika.
v)Kuvuta pumzi kwa taabu.
AINA ZA PRESHA YA KUSHUKA.
I)ORTHOSTATIC HYPOTENSION.
-Hutokana na kubadili mazingira uliyonayo kwa ghafla mfano.kusimama ghafla kutoka ulipokaa au ulipo lala na huwa haichukui mda mrefu ni sekunde kadhaa mpaka dakika moja.
II)NEURALLY MEDIATED HYPOTENSION(NMH).
Huwapata zaidi vijana na watoto kutokana na÷
-Utumiaji wa pombe.
-Utumiaji mkubwa wa dawa za presha ya juu(ya kupanda).
-Utumiaji wa dawa za nusu kaputi wakati wa kufanyiwa Oparesheni.
III) SEVERE HYPOTENSION.
Hutokana hasa hasa na kupoteza fahamu.
HALI INAYOSABABISHA PRESHA HII
i) Kuwa na mimba.
ii) Matatizo ya hormoni mwilini(Hormone imbalance).
iii) Maradhi ya Kisukari.
iv) Utumiaji mkubwa wa dawa za hospitali zikiwamo za presha ya kupanda.
v) Maradhi ya Moyo
KWA USHAURI ZAIDI JUU YA UTATUZI WA TATIZO HILI LA PRESHA NA MENGINEYO TUWASILIANE KWA. 0622291850
08/02/2020
Suala la kupunguza uzito linakuwa rahisi sana pale tu unapopata njia sahihi na salama kiafya ambayo imefanyiwa utafiti kwa miaka mingi na wataalamu waliobobea kwenye Masuala ya Afya na Lishe bora.
Hata hivyo watu wengi kwa kukosa ufahamu juu ya njia ipi ni salama na ipi siyo, wamejikuta wakiumiza miili yao na Afya wakitumia njia hizo ambazo zinafahamika, huku wakijikuta wanakonda badala ya kupungua na hata baadae kuongezeka zaidi ya walivyokuwa mwanzo.
Unapokuwa na uzito mkubwa kwanza unaonekana mzee wakati umri bado mdogo, unapoteza muonekano wako mzuri(michepuko huanzia hapa) ,unakuwa hatarini kupata maradhi k**a presha, Kisukari,hormonal imbalance, kuziba kwa mirija ya uzazi kwa mwanamke, miguu kuuma, uchovu n. k.
*IPO NJIA SALAMA KIAFYA*
Kumbuka safari ya kupunguza uzito inahitaji kuwa na nia ya dhati. Hivyo ipo Program ya C9 ambayo itakusaidia kuondoa sumu mwilini na kupunguza uzito kiafya kwa siku tisa na hii itakufanya ujisikie mwepesi, mwenye nguvu, Ngozi yako pia itang'aa zaidi na zaidi ya hayo, *YOU WILL FEEL BETTER AND LOOK BETTER*
Kwa maelezo zaidi na ushauri piga/WhatsApp 0622291850 andika neno *UZITO *
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam