sikaf_natural_products
tunatoa huduma ya ushauri bure juu ya kuboresha afya kiasili.Pia tunatoa huduma ya bidhaa za asili k
26/04/2023
Je, unahitaji kuboresha Afya na muonekano wa Ngozi yako kwa bidhaa asili za urembo?...
SIKAF tunakuletea bidhaa asili kwa 100%, Mafuta asili ya Ganda la Chungwa, sabuni ya ganda la Chungwa, scrub ya unga wa ganda la Chungwa, lotion asili nk.
🔸Kwa mwenye chunusi,ngozi ngumu na Ngozi isiyo na nuru bidhaa hizi zitakusaidia sana.
🔸Pia kwa wale walioharibika ngozi kutokana na vipodozi vya kemikali ipo suluhisho maalum.
🔸Matokeo ni kuanzia wiki tatu za matumizi.
Gharama ni k**a ifuatavyo:
Orange Serum:15,000
Recovery Serum:15,000
Aqua Serum:25,000
Sabuni ya Ganda la Chungwa:7,000
Sabuni ya Maziwa ya Mbuzi:7,000
Mafuta asili ya lotion:15,000
Scrub ya Ganda la Chungwa:15,000
Si lazima uchukue vyote bali package maalum kutokana na changamoto ya ngozi na aina ya ngozi yako. Package kamili inakuwa katika punguzo la 7%.
Tunapatikana Kariakoo Gerezani mataa ya Kamata. Kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0713 434 180.
08/12/2020
Je, unafahamu kuwa Unga wa Mchele ni moja ya bidhaa ya asili muhimu sana kwa ajili ya Kung'arisha Ngozi? 🧚♂️
◽Changanya Unga laini wa mchele na maziwa ya mtindi kisha paka usoni na uache kwa lisaa limoja na uoshe.
◽Fanya hvyo kwa wiki mara nne💖
Sponsored by@sikaf_group_of_companies
04/12/2020
🔹Watu wengi wamekuwa wakiamini kula kidogo ama kushinda Njaa hupunguza unene.. Kuamini hivi haitoshi kwani Diet si kushinda njaa ama kula kidogo bali ni Chakula gani unakula, kwa muda gani na kwa kiasi Gani.
🔹Mfano asubuhi hauli,mchana unakula andazi moja na saa saba usiku unakula chapati moja... Hapo unajitafutia madonda ya tumbo tu na kujidhoofisha Afya yako.
🔹Post zijazo tutakuelekeza vyakula vipi ule, kwa kiasi gani, kwa muda gani na kipi cha ziada kufanya ili upungue ukiwa bado na Afya😉
04/12/2020
🔹Wengi wanahisi kushinda njaa ama kula kidogo ndio kupunguza uzito, si hivyo kwani unaweza kula kidogo ila hicho kidogo unachokula kipo katika kundi la vyakula vinavyoongeza uzito mfano usile asubuhi halafu mchana ule chipsi moja na usiku wa saa saba ule andazi moja... Hapo hujafanya kitu zaidi ya kushinda Njaa na kujiweka kwenye hatari ya baadhi ya magonjwa.
🔹Post zijazo tutakuelekeza vyakula vipi ule, kwa namna gani na kwa muda gani.
Usisahau ku turn on notifications 😉
20/11/2020
Chuki,Hasira, Vinyongo, mawazo na huzuni huvuruga mfumo wa homoni zinazo husika na kuleta Nuru ya Ngozi.
1:Huchochea wingi wa homoni ya Cortisol ambayo huchelewesha ngozi kutengeneza seli mpya hvyo kufubaa, hupunguza collagen na kufanya ngozi iwe ngumu pia hupunguza maji kwenye Ngozi na kufanya Ngozi iwe kavu sana.
2:Stress huchochea kemikali ya histamine inayosababisha kupata vipele vya kuwasha na huongeza uzalishwaji wa mafuta hvyo kupelekea Ngozi kupata Chunusi.
3:Ngozi huwahi kuzeeka kutokana na mzunguko wa damu kuegemea kwenye Moyo na Mapafu hivyo Ngozi hukosa virutubisho muhimu na kusinyaa.
Punguza Hasira,mawazo, huzuni na vinyongo ili Ngozi yako iwe na Nuru na utavutia wengi😊
19/11/2020
14/10/2020
🔸Ngozi kuwa na mafuta mengi ni matokeo ya uzalishwaji mwingi wa Mafuta asili ya Ngozi(Sebum) kwenye tezi za mafuta ndani ya Ngozi.
🔸Mafuta ya Sebum husaidia kuleta unyevu kwenye Ngozi,kung’arisha na kulainisha ila yakizidi sana husababisha tundu za Ngozi kuziba,kuhifadhi bakteria na kuleta Chunusi za muda mrefu😖.
🔸Bidhaa Nzuri za Asili ambazo huondoa tatizo hili na kuacha Ngozi yako ikinawiri ni Mdalasini aina ya Ceylon na Ganda la Chungwa.
🔸SIKAF Natural Products tumekuchanganyia bidhaa hizi mbili na kuongezea Unga wa mchele ambao huongeza ufanisi na kuacha Ngozi yako laini, inang'ara na yenye kuvutia😊.
🔸Tumia unga huu wa Confidence Secret kwa ajili ya Afya ya Ngozi yako na matokeo mazuri ya Ngozi yako💚
28/08/2020
🔸Ngozi kuwa na mafuta mengi ni matokeo ya uzalishwaji mwingi wa Mafuta asili ya Ngozi(Sebum) kwenye tezi za mafuta ndani ya Ngozi.
🔸Mafuta ya Sebum husaidia kuleta unyevu kwenye Ngozi,kung’arisha na kulainisha ila yakizidi sana husababisha tundu za Ngozi kuziba,kuhifadhi bakteria na kuleta Chunusi za muda mrefu😖.
🔸Ngozi kuwa na Mafuta mengi na Chunusi ni vitu ambayo ni Changamoto kuvitibu ila k**a unaipenda Ngozi yako, ili ipendeze yakupasa kuwa mvumilivu kwani yahitaji muda,juhudi na Gharama kiasi.
1:OSHA USO
🔹Osha uso angalau mara mbili kwa siku ili kuzibua matundu yaliyoziba.
2:TUMIA VIPODOZI SAHIHI
🔹Usitumie lotion zilizoandikwa for dry skin au kuchanganya vipodozi tofautitofauti kwa muda mfupi(unaichanganya Ngozi😇).
3:PUNGUZA MATUMIZI YA MAKEUP
🔹Makeup ikikutana na Ngozi yenye mafuta mengi huziba tundu za Ngozi hivyo ukifanya make up mfano zaidi ya mara nne kwa wiki Ngozi itakua haipumui na kuchochea Chunusi za muda mrefu ⌚ 🤯.
4:TUMIA MAFUTA ASILI YA NGOZI.
🔹Mafuta ya Jojoba ni mafuta ambayo virutubisho vyake vinafanana na mafuta yanayozalishwa na Ngozi. Endapo ukitumia mafuta haya,Ngozi inapunguza uzalishwaji wa mafuta yake na kuanza kutegemea unayopaka.
5:PAKA MASK ASILIA ANGALAU MARA MBILI KWA WIKI.
🔹Mask asilia zipo za aina nyingi mfano Unga wa Ganda la Chungwa,Manjano,Liwa,Nyanya,Aloevera, Mdalasini nk.
23/08/2020
Ngozi yako huashiria k**a ni ya mafuta endapo
🔸 usipopaka Mafuta baada ya muda mchache uso unakuwa umejaa Mafuta,
🔸ukipaka poda bila foundation baada ya muda mchache inakua imepotea,
🔸rahisi kupata chunusi,
🔸ukitembea juani unasweat sana usoni.
🔸Pia ukijifuta kwa karatasi nyeupe au au karatasi ya kupimia Ngozi hutoka na matone mengi ya Mafuta.
Sababu za Ngozi kuwa na mafuta mengi ni
🔹Kurithi
🔹Umri(Kadri umri unavyoongezeka mafuta hupungua usoni ndio maana wazee wengi wana ngozi kavu)
🔹Kuongezeka ukubwa wa tundu za Ngozi
🔹Kutumia vipodozi visivyo endana na Ngozi yako.
Post ijayo tutakuelekeza namna ya kuweka sasa kiwango cha mafuta cha Ngozi yako😊
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Address
Dar Es Salaam
SIKAFNATURALPRODUCTSMAHIWADARESSALAAMTZ,11106
Opening Hours
| Monday | 09:00 - 17:00 |
| Tuesday | 09:00 - 17:00 |
| Wednesday | 09:00 - 17:00 |
| Thursday | 09:00 - 17:00 |
| Friday | 09:00 - 17:00 |
| Saturday | 09:00 - 12:00 |