Afya-njema

Afya-njema

Share

TUNAWASAIDIA WAGONJWA KWA KUTUMIA MIMEA DAWA ASILI.

01/06/2026

Majibu mawili sahihi yatapokea zawadi

🌱

30/05/2026

MAAJABU MAKUBWA YA ALOE VERA JUICE
__________________________________________________________

🔘 Aloe vera ni mmea mmoja wa ajabu sana katika upande wa matibabu (Medicinal plant) na kwa upande pia wa Virutubisho Lishe (Nutrition).

🔘 Ukiachana na Matumizi yake MAKUBWA kwa upande wa Vipodozi vya Ngozi na Cream au Lotion.

👇👇

🔘 ALOE VERA JUICE, Ni Moja ya Dawa nzuri sana kwa mfumo wa mmeng'enyo wa chakula kiujumla hasa ikitumiwa na kuandaliwa kwa utaratibu nzuri.

🔘Kuna JAMII Zaidi ya 300 za mimea hii ya Aloe vera, Ila zinazoweza kutumika katika Juice ni JAMII mbili hivi au Tatu tu zinazojulikana.

1️⃣ Tafuta JAMII ya Aloe vera Barbadensis

2️⃣ Tafuta JAMII ya Aloe vera Chinensis

✅Tumia nyama nyeupe ya ndani ya Jani la Aloe vera kuandaa juice yako.

Hakikisha unaosha Vizuri kutoa vumbi, tope, na Uchafu mwingine wa nje. Kisha kata juu na chini na pembeni mwa Jani lako Ili litoe maji maji ya NJANO (Aloin/Anthraquinone): Hii ni Chungu sana ukiinywa pamoja na juice yako, Utaharisha vibaya haitakiwi.

⛔ANGALIZO: ALoe vera: Hakikisha una ondoa Ile njano kwa Kuosha hata mara Tatu au nje Jeli yako kabla hujaisaga isije ikakusababishia kuharisha na kupoteza maji mengi.

🔘SAGA JUICE YAKO: Changanya na Tangawizi kidogo, Asali pia kidogo, na Limao kwa mbaliiiii Ili upate Ladha tu.

🔘 TUMIA: Asubuhi na jioni (50mls
Jioni pia unywe (50mls

Tumia ukiwa tumbo lako lipo wazi haujala chakula kigumu.

🔘FAIDA KUBWA: ALoe vera juice inaweza kukuponya kabisa matatizo ya Tumbo ikitumiwa Sawasawa.

✅ ACID REFLUX IPO Vizuri sana
✅HUPATI CHOO IPO Vizuri sana
✅KULINDA UKUTA WA TUMBO IPO Vizuri sana
✅ KUSAIDIA KINGA YA MWILI IPO Vizuri sana
✅ Kuondoa uvimbe uvimbe ndani ya Tumbo Safi
✅ITAKUPA NGUVU ZA MWILI IPO Vizuri sana.

👇👇👇 SOMA ZAIDI Kuhusu ALOE VERA JUICE

29/05/2026

Na Dr Ken
Tiba Asili Tanzania

HIVI UNAFAHAMU KIUNGULIA KUJIRUDIA TAFSIRI YAKE NI NINI KATIKA MFUMO WA CHAKULA??
____________________________________________________________

 KIUNGULIA: Ni hali ya kukera inayoweza kumtokea mtu yoyote na husababisha maumivu makali kwenye kifua na upande wa juu wa tumbo. 

Hali hii inaendana kwa ukaribu na tatizo la kupanda kwa tindikali (acid reflux). 
Lakini pia Kuna utofauti kati ya acid reflux na kiungulia( heartburn.)

Kama nilivyoeleza hapo juu kuwa acid reflux ni kitendo cha kupanda kwa tindikali kutoka tumboni kurudi juu kwenye koo la chakula na kusababisha maumivu ya kifua ambayo tunaita ni kiungulia (Heartburn)
Kwahiyo acid reflux ndio inayoweza kusababisha Kiungulia (HEARTBURN)

Hali ya kiungulia ni kitendo cha kawaiada kutokea kwa watu wengi na inatokea kwa kila mtu, lakini k**a tu haiambatani na maumivu makali ya kifua, k**a maumivu yakizidi kuwa makali na yanatokea mara kwa mara hapo ndipo tatizo huanza.

Kama tatizo likiendelea zaidi basi hufikia hatua ya tatu na kuitwa gastroesophageal reflux disease(GERD), kwa hiyo kadiri kiungulia kinachukua muda mrefu mpaka kuathiri tishu za umio (GERD) ni hatari zaidi kwasababu inaweza kupelekea uwezekano wa kupata Saratani ya Koo. 

SULUHISHO LAKE KABISA
____________________________________

✅Andaa juice Asili ya Majani ya Aloe vera gel (Nyama nyeupe ya ndani ya Jani).

Kisha, osha Vizuri kabisa kwa maji safi hata mara Tatu Ili kuondoa uchungu wote.

✅Baada ya Hapo, saga kwenye Blenda yako, na uweke kidogo Tangawizi na Asali mbichi Ili kupata ladha.

MATUMIZI YAKE
______________________

✅Kunywa juice yako kutwa mara mbili (1x2/siku)

Kwa mfululizo wa siku 14,21, 28, au 30.

Asubuhi kabla hujala chakula kizito tumboni, na jioni kabla ya mlo wa jioni.

HUTAONA MATATIZO YA TUMBO KIUJUMLA.

12/05/2026

Wapendwa wateja wetu wa 🌱 ,ona kiasili.

✅Ni muda sasa umefikia wa kuwaletea kitu mkipendacho wengi, na chenye msaada mkubwa Sana kwa afya ya:

1: Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula
(Vidonda vya tumbo
(Acid reflux
(Gastritis

2: Mambo ya Urembo wa ngozi na Uponyaji wake.

TUNAKULETEA, ALOVERA GEL JUICEEEEEEE🥤

Hii ni Tiba, Kinywaji, na Kirutubisho kamili kabisaaaaaaaa 🤝😘🥤

Endelea kukaa karibu nasi, kwa ajili ya taarifa Zaidi.

Photos from Afya-njema's post 11/05/2026

Na Dr Ken
Tiba Asili Tanzania
Ilala -Dar es salaam.

JE, UMEWAHI KUJIULIZA KUWA UKIWA SAFI NDANI YA MWILI UTAKUWA NA NGOZI BORA ?
______________________________________________

💧Kama Unataka kuwa na Afya nzuri ya ngozi safi yenye kung'ara, isiyokuwa na madoadoa, Chunusi kubwa zinazoacha alama ukizitoboa, Ngozi yenye rangi moja tulivu pamoja na kupunguza michaniko, Basi hauna budi kujihudumia kuanzia ndani ya mwili wako, Kisha nje ndiyo kunafuata.

UMUHIMU WA JUICE HII BORA
________________________________

💧Huongeza Kinga na kuzuia Seli kuharibika: Amla ina Vitamini C nyingi, ambayo, pamoja na curcumin ya manjano, hutoa ulinzi mkali wa antioxidant dhidi ya sumu za vyakula ndani ya mwili.

💧Huboresha Afya ya Mmeng'enyo wa Chakula: Aloe vera hufanya kazi k**a wakala wa kutuliza utumbo, huku mchanganyiko huo ukisaidia kuboresha mmeng'enyo wa chakula na unyonyaji wa virutubisho.

💧Huondoa Sumu Mwilini: Mchanganyiko huu mara nyingi hutumika kuondoa sumu kutoka kwenye ini na kusaidia afya yake kwa ujumla.

💧✅Huboresha Ngozi na Nywele: Kiwango cha juu cha vitamini na antioxidant husaidia kupunguza chunusi, kuboresha umbile la ngozi, na kukuza ukuaji wa nywele.

💧Hupunguza Uvimbe na Maumivu: Manjano na aloe vera vinajulikana kwa sifa zao za kuzuia uchochezi, ambazo zinaweza kusaidia kudhibiti maumivu ya viungo.

💧Husaidia Kudhibiti Uzito: Mchanganyiko huu unaweza kusaidia kudumisha viwango vya sukari kwenye damu vyenye afya na kuweka mwili ukiwa na maji mwilini, na kusaidia kimetaboliki.

JINSI YA KUTUMIA
___________________

Muda Bora:
Kunywa mililita 15–30mls, za mchanganyiko huu kwenye tumbo tupu asubuhi na jioni kabla ya kula. Hii huchukuliwa kuwa bora kwa kufyinzwaji mwilini

🌱 , pona kiasili.

Ilala sokoni Dar es salaam.

Photos from Afya-njema's post 03/05/2026

✅Kiuhalisia, Miili yetu hii inaundwa na chembechembe Ndogo Ndogo sana zinazotokana na vyakula pamoja na matunda tunayokula Kila siku.

✅Unachokula ndiyo kinachokujengea mwili wako. Kukupatia Nguvu, na kukupa Uwezo wa kujikinga dhidi ya maambukizi ya magonjwa mbalimbali.

✅Je, Unakula kinachotakiwa na Mwili? Au una unakula Ili mradi njaa isikusumbue.

Lishe Bora, afya Bora, Maisha Bora.

Kula chakula k**a Dawa, na siyo kunywa Dawa k**a chakula.

Karibu sana , pona kiasili.

Tumeendelea kuwa msaada kamili kwa Wengi.

◾Ilala sokoni -Dar es salaam.

02/05/2026

⬛Tumeendelea kuwa msaada Zaidi kwa Akina mama wengi hapa Tanzania pamoja na Mabinti walio katika Umri wa kuzaa.

K**A UNA CHANGAMOTO HIZI:
_________________________________

✅UTI Komavu
✅ Fangasi SUGU ukeni
✅ Uvimbe maji (Ovarian cyst)
✅ Uvimbe kwenye kizazi (Fibroids)
✅ Mvurugiko wa Homoni za Uzazi
✅ Presha na Sukari aina ya pili.
✅Kutokushika ujauzito
✅ Matatizo ya Arthritis na Gout
✅ Tatizo la Asidi kuzidi tumboni pamoja na Vidonda vya tumbo.

👍 Karibu sana upate Ushauri na Tiba.

📱0783170528.

🌱, pona kiasili .

ILALA SOKONI DAR ES SALAAM.

02/05/2026

Na Dr Ken
Tiba Asilia Tanzania

JE, UNAUJUA MFUMO WA FAHAMU UNAORATIBU KAZI ZA TUMBO.
_____________________________________

▪️ Mwili kiujumla unaendeshwa na mfumo wa Fahamu unaoanzia kwenye ubongo. Mfumo wa Neva aina ya VAGUS NERVE, ndiyo huratibu shughuli zote za tumbo lako. Mfano:

1️⃣Kuruhusu Msuli wa kubana na kuachia katika Eneo la chini la umio, (Lowe esophageal muscle). Hii ndiyo valve inayozuia chakula kikiingia tumboni kisirudi kooni.

2️⃣ Mishipa ya VAGUS, Huratibu Namna tumbo linavyoweza kusaga na kuchanganya chakula, Kisha kukiruhusu kianze kutoka kwenda kwenye utumbo mwembamba

3️⃣Inaratibu Zoezi Zima la Uzalishaji wa Chachu ya Tumbo. (Asidi). Kuamsha neva ya vagus, haswa kupitia njia zisizo za uvamizi.

NINI HUATHIRI MFUMO WA FAHAMU UNAORATIBU KAZI ZA TUMBO?
______________________________________

Sababu KUU ni hizi Tatu:
✅Msongo wa mawazo sana.

✅ Matumizi ya Pombe Kali pamoja na Sigara

✅ Kunywa vitu vyenye uchachu sana pamoja na Matumizi makubwa ya Sukari huathiri upelekaji wa taarifa kwenye ubongo na kusababisha msisimko mkubwa wa kuta za tumbo.

UFANYE NINI ?
________________

✅ Mazoezi mepesi na Lishe.

Mfano:

▪️Massage ya shingo taratibu, Tumbo, na kuchua kwa maji ya Moto.

▪️ Vyakula vinavyochochea msisimko mkubwa wa kuta za tumbo kuacha.

▪️Pumzika vya kutosha, na ulale kichwa kikiwa na sapoti ya mto Ili kifua kiinuke juu.

✅ Pata Tiba sahihi na Ushauri wa kitaalam.

, pona kiasili.

Ilala sokoni Dar es salaam.

28/04/2026

🌱 , pona

28/04/2026

Na Dr Ken
Tiba Asili Tanzania
📱0783170528

MATOKEO MABAYA YA KONGOSHO KUVIMBA
_____________________________________________

⬛Kama inavyofahamika kuwa Kongosho huhusika moja kwa moja katika suala zima la usagaji wa chakula kwa kuzalisha vimeng'enya (Enzymes) kupitia seli tofauti tofauti zake.

Inapotokea Kuna changamoto ya Athari kwake hasa kutokana pengine na:

✅ Kuziba kwa mrija wa kumwaga vimeng'enya

✅ Matumizi makubwa ya pombe kali

✅ Maambukizi komavu ya Bakteria pamoja na virus.

Basi yafuatayo ni matokeo yanayojidhihirisha kwenye mwili wako k**a Dalili KUU za Kongosho kushindwa kufanya KAZI zake.

1️⃣Maumivu ya Tumbo na Kuvimbiwa sana: Maumivu makali, kwa kawaida kwenye tumbo la juu, mara nyingi hutoka mgongoni na huongezeka sana baada ya kula, hasa vyakula vyenye mafuta mengi. Kuvimba na hisia ya kushiba ni jambo la kawaida.

2️⃣Kichefuchefu na Kutapika: Kichefuchefu na kutapika mara kwa mara hutokea mara kwa mara, mara nyingi husababishwa na kutoweza kusaga chakula, jambo ambalo husababisha usumbufu mkubwa na linaweza kusababisha upungufu mkubwa wa maji mwilini.

3️⃣ Kinyesi chenye Mafuta. (Steatorrhea). Kutokana na ukosefu wa vimeng'enya vya mmeng'enyo wa chakula (kutojitosheleza ) chakula hakisagwi ipasavyo, na kusababisha kinyesi chepesi, kikubwa, chenye mafuta ambacho ni vigumu kukisafisha, hali inayojulikana k**a steatorrhea.

4️⃣Kupunguza Uzito na Utapiamlo: Pancreatitis sugu husababisha kupungua uzito na utapiamlo kwa sababu mwili hauwezi kunyonya virutubisho, licha ya hamu ya kula ya kawaida au iliyopungua.

5️⃣Kupoteza Hamu ya Kula: Wagonjwa wengi hupata ukosefu wa hamu ya kula, na kusababisha kupungua uzito zaidi na udhaifu unaowezekana.

🌱 , pona kiasili.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Address

SHEKILANGO
Dar Es Salaam