CK AFYA & TIBA
"AFYA & TIBA" Mtangulize Mungu, jiongoze, linda afya yako na pata ushauri na tiba kwa ajili ya afya yako. Karibuni sana na Mungu akulinde.
Tunapatikana Posta azikiwe street ips building floor no. 3.
Tufahamu kuhusu viongo na mifupa. Bones and joints.
Viungo ni sehemu katika mwili wako ambapo mifupa miwili huungana, k**a vile vifundo vya mikono, viwiko, mabega, nyonga, magoti na vifundo vya miguu.
Viungo pia vinapatikana sehemu ambazo huenda usifikirie, k**a vile katikati ya mifupa mingi iliyo kwenye miguu, mikono, fupanyonga, na uti.
Maumivu makali kwa zaidi ya kiungo kimoja (aghalabu zaidi ya viungo 5) kwa kawaida yanasababishwa na tatizo la muda mrefu la viungo
Baadhi ya magonjwa yanayosababisha maumivu ya viungo yanaweza pia kusababisha upele, homa, maumivu ya macho, au vidonda mdomoni
Visababishi vya maumivu kwenye viungo vingi kwa kawaida ni tofauti na vile vya maumivu kwenye kiungo kimoja.
Maumivu kwenye viungo vingi husababishwa na:
Ugonjwa wa baridi yabisi
Ugonjwa wa baridi yabisi ni mwako wa viungo unaosababisha kuvimba, maumivu, na kukak**aa kwa viungo. Visababishi vya ugonjwa wa baridi yabisi ni tofauti kulingana na iwapo viungo vilianza kuumia ghafla (kwa muda mfupi) au umekuwa na maumivu kwa muda mrefu (ya kudumu).
Ugonjwa wa baridi yabisi unaotokea ghafla (kwa muda mfupi) katika zaidi ya kiungo kimoja mara nyingi husababishwa na:
Maambukizi kutokana na virusi
Kuanza kwa tatizo la viungo au kulipuka kwa tatizo la viungo lililokuwepo kwa muda mrefu (k**a vile ugonjwa wa baridi yabisi ya rumatoidi)
Sababu zisizotokea sana ni pamoja na:
Ugonjwa wa Lyme
Kisonono
Maambukizi ya Streptococcal
Ugonjwa wa baridi yabisi uliosababishwa na maambukizi katika sehemu nyingine ya mwili
Ugonjwa wa Jongo
Ugonjwa wa baridi yabisi unaodumu kwa muda mrefu katika zaidi ya kiungo kimoja husababishwa na:
Sababu zisizotokea sana ni pamoja na:
Ugonjwa wa Lyme
Kisonono
Maambukizi ya Streptococcal
Ugonjwa wa baridi yabisi uliosababishwa na maambukizi katika sehemu nyingine ya mwili
Ugonjwa wa Jongo
Ugonjwa wa baridi yabisi unaodumu kwa muda mrefu katika zaidi ya kiungo kimoja husababishwa na:
24/12/2024
Madhara 9 ya vidonda vya tumbo mwilini
Vidonda vya tumbo ni majeraha au vidonda ndani ya kuta za tumbo.
Majeraha au vidonda hivyo huleta maumivu yanayokera na hutokea mara nyingi tumboni na yanaweza kutibika lakini k**a hutachukuwa hatua mapema za kutibu yanaweza kukuletea majanga mengine mengi kiafya.
Tumbo na utumbo mdogo vina kuta maalumu yenye ute ute wa ulinzi ambao hulilinda tumbo lako dhidi ya maadui wanaoleta shida tumboni mwako yaani bakteria wabaya, virusi na vijidudu nyemelezi vingine.
Wakati kuna vitu vingi vinavyoweza kukusababishia vidonda vya tumbo ikiwemo kutumia dawa za kupunguza maumivu kwa muda mrefu bila ushauri wa kitaalamu, kuvuta sana sigara au kunywa pombe kupita kiasi; kuna bakteria ambaye anaweza kulaumiwa k**a mhusika mkuu wa vidonda vya tumbo.
Tatizo la vidonda vya tumbo linalosababishwa na huyu bakteria ni kuwa anachelewa sana kukuonyesha dalili kwamba una vidonda vya tumbo.
Wakati unaweza kuishi na vidonda vya tumbo kwa muda fulani bila kukuletea shida kubwa, kuviacha kwa muda mrefu bila kupata matibabu kunaweza kukuletea madhara yafuatayo;
Madhara 9 ya Vidonda vya tumbo mwilini
💥Kuvuja damu ndani ya mwili (Internal bleeding and serious blood loss)
💥Upungufu wa damu (Anemia)
💥Kutapika damu
💥Kupata kinyesi cheusi k**a cha mbuzi
💥Kuvurugika kwa mfumo wa mmeng’enyo wa chakula (Obstructed digestion)
💥Shida katika kupumua
💥Saratani ya tumbo (Stomach cancer)
💥Msongo wa mawazo (stress)
💥Kupungua kwa nguvu za kiume
Ni muhimu kupata vipimo na uchunguzi zaidi wa daktari mapema tu unapohisi unaweza kuwa na vidonda vya tumbo ili kuzuia usipatwe na madhara haya yatokanayo na vidonda vya tumbo.
Vidonda vya tumbo huwa ni rahisi kutibika unapowahi kuanza matibabu kuliko ukisubiri mpaka viwe sugu.
Vyakula usivyotaliwa kula k**a unaumwa vidonda vya tumbo. Kuna maelezo mengi juu ya vyakula kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.
Kuna wanaosema hiki hakifai wengine hiki kinafaa lakini kwa ujumla vyakula vifuatavyo vinakubalika na wengi kwamba havifai kwa mtu mwenye vidonda vya tumbo, navyo ni;
✳PiliPili Manga nyeusi na nyeupe
✳PiliPili kichaa
✳Vinywaji vyenye Kaffeine
✳Kahawa
✳Pombe
✳Chai ya rangi
✳Chokoleti na cocoa
✳Soda zote
✳Juisi zote za dukani
✳Sukari na viongeza utamu vingine vya kutengenezwa
✳Wali na ugali wa sembe
✳Vyakula vinavyopikwa katikati ya mafuta mengi k**a vile maandazi nk (Fried foods)
✳Nyanya
✳Mnanaa (Peppermint)
✳Mbegu mbegu zenye Omega – 6
✳Maziwa fresh na bidhaa nyingine zinazotokana na maziwa
Kuepuka vyakula hivi ni hatua moja kuelekea kwenye uponyaji wako hata hivyo unahitaji kubadili tabia zako zingine ikiwemo kuachana na msongo wa mawazo (stress) kwa gharama yoyote.
Iwe ni mtu ambaye una kawaida ya kuugua vidonda vya tumbo mara kwa mara au huumwi vidonda vya tumbo kwa sasa, kuviepuka vidonda hivi ni pamoja na kuhakikisha mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula unafanya kazi vizuri kwa kiwango chake cha juu kabisa.
Pia unaweza kuimarisha afya ya mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula kwa kufanya yafuatayo:
♨Kunywa maji glasi 2 (nusu lita) mara tu uamkapo kutoka kitandani kila siku. Kunywa tena kiasi hiki cha maji kila nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi, mchana na cha jioni kila siku.
♨Kula chakula kichache milo mingi. Kula hata mara 5 kwa siku lakini chakula kidogo kidogo siyo kingi kwa wakati mmoja.
♨Kula pole pole ulapo chakula
♨Hakikisha unapokula chakula huna mawazo mawazo (stress) yoyote.
♨Kula zaidi vyakula vyenye nyuzi nyuzi
♨Kula vyakula vyenye bakteria wazuri (probiotics) k**a vile mtindi na uji wa unga wa ndizi
♨Punguza kukaa chini au kwenye kiti masaa mengi
Hata k**a utampata huyu bakteria (H. pylori) k**a unao bakteria wengine wazuri tumboni ni rahisi kwako kumdhibiti huyu anayeleta vidonda vya tumbo.
Kuimarisha afya ya mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula ni jambo zuri kiafya siyo kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo tu bali kwa mtu yoyote asiyependa kuugua mara kwa mara kwani tumboni ndiko kuliko na injini ya mwili wote kwa ujumla.
H. pylori ni bakteria anayesababisha vidonda vya tumbo kwa karibu ya zaidi ya nusu ya watu wote duniani hivyo uwezekano wa kumpata au kuugua ugonjwa huu ni mkubwa sana kwa mtu yoyote.
Pia kuna dawa za kutumia ili kukusaidia kutibu vidonda vya tumbo kwa asilimia kubwa.
Ofisi zetu zipo Posta azikiwike ips buliding street floor no 3.
24/12/2024
FAHAMU DALILI 20 ZA VIDONDA VYA TUMBO
1. Kichefuchefu hasa wakat wa kula au baada ya kula
2. Kupoteza hamu ya kula na kubagua vyakula
3. TUMBO kuwaka moto
4. TUMBO kuunguruma
5. Gesi nyingi tumboni
6. Kiungulia
7. Tumbo kuuma ukichelewa kula au baada ya kula na hasa ukila vyakula vya mafuta, kukaanga na fast food zote au vyenye viungo sana
8. Kiungulia mara kwa mara
9. Kucheua sana hasa vitu vichachu au vichungu
10. Kukaukiwa sana maji kwenye koo
11. Kuishiwa nguvu unapokosana na vitu flan
12. Kupoteza fahamu
13. Kuumwa kichwa mara kwa mara
14. Macho kuuma na kupoteza uono
15. Vichomi kifuani na kuumwa kifua
16. Kubanwa pumzi
17. KUKOSA choo na kupata choo kigumu au kidogo sana
18. Kumwa mgongo upande wa kushoto na mbavu
19. Moyo kulipuka, kuchoma, na mapigo ya moyo kwenda mbio
20. Kupata hofu isiyo na sababu yoyote hasa usiku
21. KUKOSA hamu ya tendo la ndoa na kushindwa kuhimil vizuri tendo kwa jinsia zote
22/12/2024
Dalili za vidonda vya tumbo
Dalili za vidonda vya tumbo ni pamoja na:
maumivu ya sehemu ya juu ya tumbo,kiungulia,kubeua,tumbo kujaa gesi nakichefuchefu. 1
Ikiwa kidonda kinatoa damu, unaweza kuona damu nyekundu au damu ilyovilia (damu nyeusi) kwenye kinyesi. Kutokwa damu kunaweza kuambatanishwa na uchovu na kukosa nguvu. K**a kidonda cha tumbo kinasababisha shimo kwenye utumbo, hii inaweza kusababisha maumivu ya ghafla ya tumbo, homa, kichefuchefu na kuzimia.
22/12/2024
IJUE PEPTIC ULCER yaani vidonda vya tumbo.
21/12/2024
Bawasiri inatibika ni kumuamini Mungu na kuamini tiba zetu baada ya hapo kufuata kanuni na masharti utakayo pewa na madakatar wetu.
AFYA NI MTAJI.
21/12/2024
Karibu upate ushaur na tiba kutoka kwa madakar wetu. Pia dawa zinapatikana
21/12/2024
Hemorrhoids kwa kiswahili bawasiri
Utambuzi wa Bawasiri
Utambuzi hufanywa na daktari kwa kuchukua maelezo ya mgonjwa na kuchunguza njia ya haja kubwa. Uchunguzi wa njia ya haja kubwa hujumuisha kuangalia eneo hili na kuingiza kidole taratibu kuchunguza sehemu ya ndani ya njia ya haja kubwa. Ikiwa bawasiri hazionekani kirahisi, au sababu ya kutoka damu haijaeleweka vizuri, uchunguzi wa ziada huweza kufanywa ili kuhakikisha hamna sababu nyingine ya dalili hizi.
Matibabu ya Bawasiri
Bawasiri inatibika na kuna njia mbalimbali za kutibu bawasiri. Tiba halisi ya bawasiri ni kuhakikisha kupata choo kilaini na kuepuka kufunga choo, ili kuepuka hali kuwa mbaya zaidi. Krimu za kupaka na dawa za kuingiza katika njia ya haja kubwa (suppositories) zinaweza kusaidia kupunguza uvimbe, mwasho na maumivu. Dawa hizi hupatikana katika maduka ya dawa. Kuna matibabu mengine ambapo sindano au kamba maalum hutumika ili kupunguza ukubwa wa mishipa ya damu. Dawa ya bawasiri sugu ni upasuaji
Kinga ya Bawasiri
Kuhakikisha unapata choo kilaini husaidia kuzuia bawasiri na kupunguza kujirudia kwa dalili za bawasiri. Hii huwezekana kwa kula vyakula vyenye nyuzinyuzi (fiber),kunywa maji ya kutosha, kuwa na uzito unaofaa, kuepuka kukaa kwa muda mrefu, kuepuka kujikamua wakati wa haja kubwa na kuepuka kubeba vitu vizito mara kwa mara.
Hitimisho
Bawasiri ni hali inayoweza kukera lakini mara nyingi hazina madhara mabaya kwa afya ya binadamu. Ugonjwa huu unaweza kuisha wenyewe ndani ya wiki. Bawasiri mara nyingi hujirudia, na hali huzidi kuwa mbaya kadiri muda unavyosonga mbele. Bawasiri ni tatizo la kawaida ambalo linaweza kuathiri watu wengi wakati fulani maishani mwao. Kwa bahati nzuri, kuna hatua ambazo mtu anaweza kuchukua kuboresha hali hii au kuzuia kujirudia. Kwa mfano, kuhakikisha ulaji wa chakula chenye ufumwele (fiber) mwingi na kunywa maji ya kutosha kunaweza kusaidia kuzuia tatizo la bawasiri.
Endelea....
kupunguza dalili za bawasiri, unaweza kujaribu matibabu ya nyumbani k**a vile ku
21/12/2024
*Vitu vingine vinavyoongeza hatari ya kupata bawasiri ni pamoja na:*
1. Kuwa na uzito wa mwili kupita kiasi, ujauzito, na kula vyakula visivyo na nyuzinyuzi (fibre) za kutosha.
2. Kubeba vitu vizito mara kwa mara.
3. Kuhara kwa muda mrefu na kufunga choo (constipation).
4. Kujamiiana kinyume na maumbile.
5. Historia ya uwepo wa ugonjwa wa bawasiri katika familia.
6. Magonjwa yanayoathiri njia ya haja kubwa
7. Kuketi kwa muda mrefu
8.Uzee na matatizo ya kutopata choo.
21/12/2024
Ugonjwa huu unaweza kusababisha mwasho, maumivu na damu au k**asi kutoka wakati wa kujisaidia haja kubwa ingawa wakati mwingine hauna dalili. 1 Madhara ya bawasiri ya ndani ni pamoja na damu kutoka wakati wa kujisaidia, damu kuganda ndani ya mishipa ya damu na maumivu. Kutokea kwa bawasiri kunaweza kuhusishwa na hali k**a uzee, ujauzito, kuharisha au choo kufunga (constipation), saratani kwenye nyonga au kuketi kwa muda mrefu. Tiba ya bawasiri inategemea aina ya bawasiri na ukubwa wa tatizo. Matibabu ya bawasiri yanaweza kuhusisha matumizi ya dawa au upasuaji mdogo.
IJUE BAWASIRI NA CHANGAMOTO YAKE..
Kwanza tunatikiwa kujua bawasiri ni nini???
Bawasiri ni kuvimba kwa mishipa ya damu iliyopo ndani ya au katika eneo linalozunguka njia ya haja kubwa. Ni hali ambayo inaweza kusababisha nyama kujitokeza nje. Hivyo bawasiri inaweza kuwa bawasiri ya ndani au bawasiri ya nje.
21/12/2024
MATUNDA na FAIDA zake kwenye miili yetu.
Matunda yana vitamini muhimu, madini na kemikali za mimea. Pia zina nyuzinyuzi. Kuna aina nyingi za matunda zinazopatikana na njia nyingi za kuzitayarisha, kupika na kuzitumikia. Lishe yenye matunda mengi yanaweza kukusaidia kukulinda dhidi ya saratani, kisukari na magonjwa ya moyo.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam
000
Opening Hours
| Monday | 08:00 - 21:00 |
| Tuesday | 08:00 - 21:00 |
| Wednesday | 08:00 - 21:00 |
| Thursday | 08:00 - 21:00 |
| Friday | 08:00 - 21:00 |
| Saturday | 09:00 - 16:00 |