WpCo Updates

WpCo Updates

Share

WpCo Football Update

18/07/2026

Tetesi za usajili Yanga___
______Zimefika Ngapi Uko
*Uko wapo wachezaji 99+ Wanatajwa kusajiliwa___

17/07/2026

Simba SC Tanzania rasmi imetangaza kuachana na mshambuliaji Jonathan Sowah ambaye Kutokana sababu mbalimbali hakufanikiwa kuonyesha kile alicho nacho ndani ya Msimbazi.

Wakati huo huo_________????

Klabu ya Singida Black Stars imeendelea kuonyesha dhamira yake ya kujenga kikosi imara kitakachoshindana kwa nguvu katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2026/27 baada ya kuingia katika hatua za mwisho za mazungumzo ya kumrejesha nchini mshambuliaji raia wa Ghana, Jonathan Sowah.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na mwandishi wa habari za usajili, Hans Rafael, viongozi wa Singida Black Stars wamefikia hatua kubwa katika mazungumzo hayo huku pande zote zikionekana kuwa na mwafaka mzuri kuhusu masharti ya mkataba.

Iwapo dili hilo litakamilika k**a inavyotarajiwa, Sowah atakuwa mmoja wa usajili mkubwa zaidi wa dirisha hili la usajili nchini Tanzania na kuongeza nguvu kubwa katika safu ya ushambuliaji ya Singida Black Stars.
WpCo Updates

17/07/2026

Ladack Chasambi
Chasambi ni miongoni mwa vijana wenye kipaji kikubwa ambao wamekuwa wakifuatiliwa kwa karibu na mashabiki wa Simba. Licha ya kuonyesha uwezo mzuri katika baadhi ya mechi alizopata nafasi, bado hajawa chaguo la kudumu ndani ya kikosi cha kwanza.

Taarifa zinaeleza kuwa tayari klabu ishaamua kuachana naye ili kutengeneza nafasi kwa usajili mpya au kumpa fursa ya kucheza zaidi katika mazingira tofauti.

Ni mwendo wa fyekeo 😂😂😂 kusafisha uchafu wote Unyamani🦁🦁🦁

17/07/2026

TETESI ZA USAJILI YANGA DIRISHA KUBWA 2026/2027

📌📝James Akaminko Aondoka Rasmi Azam FC Baada ya Mkataba Wake Kumalizika
Kiungo mkabaji raia wa Ghana, James Akaminko, ameondoka rasmi ndani ya kikosi cha Azam FC baada ya mkataba wake kufikia tamati, hatua inayohitimisha safari yake ya takribani misimu minne akiwa na timu hiyo ya Chamazi.

Kuondoka kwa Akaminko kumezua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka nchini, hasa baada ya taarifa mbalimbali kuhusisha jina lake na Young Africans (Yanga SC), inayodaiwa kuwa miongoni mwa klabu zinazofuatilia kwa karibu huduma zake katika dirisha kubwa la usajili la msimu wa 2026/2027.

Sasa akiwa mchezaji huru (Free Agent), Akaminko anaweza kufanya mazungumzo na klabu yoyote bila kuwepo kwa ada ya usajili, jambo linalomfanya kuwa mmoja wa wachezaji wanaovutia zaidi katika dirisha hili.

💬💬💬💬 Akaminko Anaweza Kuchukua Nafasi ya Mohamed Damaro?

Moja ya maeneo ambayo Yanga inaweza kuhitaji kuimarisha ni nafasi ya kiungo mkabaji baada ya Mohamed Damaro kurejea Singida Black Stars kufuatia kumalizika kwa muda wake wa mkopo.

Kuondoka kwa Damaro kumeacha pengo ambalo linahitaji kujazwa na mchezaji mwenye uwezo wa kucheza katika eneo la kati kwa ufanisi.

James Akaminko ana sifa zinazoweza kuendana na mahitaji hayo kutokana na uwezo wake wa:

✅Kuvunja mashambulizi ya wapinzani.
✅✅Kushinda mipira ya pili.
✅✅✅Kusaidia safu ya ulinzi.
✅✅✅✅Kusambaza mipira kwa wachezaji wa mbele.
✅✅✅✅✅Kucheza chini ya presha katika mechi kubwa.

Kwa uzoefu wake wa misimu kadhaa katika Ligi Kuu Tanzania Bara, anaweza kuhitaji muda mfupi kuzoea mfumo wa timu mpya endapo atatua Yanga SC.

16/07/2026

🆕AZAM FC wameleta ukuta kutoka Ulaya! Henri Stanic ametua Chamazi rasmi. Je, huyu ndiye beki atakayewasaidia Azam kuvunja utawala wa Simba na Yanga msimu huu, au ni usajili mwingine wa kawaida? Maoni yako ni yapi? 👇💙💛⚽

Henri Stanic ni beki wa kati wa kimataifa kutoka Ubelgiji mwenye umri wa miaka 23 ambaye Azam FC wamemtambulisha rasmi k**a mchezaji mpya.

Stanic amekulia katika akademi za RSC Anderlecht, moja ya klabu kubwa nchini Ubelgiji, kabla ya kujiunga na OH Leuven.

Baadaye alianza soka la kulipwa akiwa FK Liepāja ya Latvia mwaka 2023, kisha akahamia Jerv ya Norway mwaka 2024, kabla ya kujiunga na Balzan FC ya Malta mwaka huohuo.

Mwaka 2025 alisajiliwa na Stellenbosch FC ya Afrika Kusini ambako alipata nafasi ya kucheza Ligi Kuu ya Afrika Kusini na mashindano ya CAF. Sasa ametua Azam FC akiwa na uzoefu wa kucheza katika nchi nne tofauti za Ulaya pamoja na Afrika Kusini.

✅Akiwa na kimo cha takribani mita 1.94, Stanic anatajwa kuwa beki mwenye nguvu kwenye mipira ya juu, utulivu wa kumiliki mpira na uwezo wa kuanzisha mashambulizi kutoka nyuma.

💬Wachambuzi wengi wanaona Azam wamepata beki mwenye wasifu wa kimataifa ambaye anaweza kuwa nguzo muhimu ya safu ya ulinzi msimu ujao.

16/07/2026

🆕Simba SC imetangaza rasmi kuachana na wachezaji hawa saba:

Chamou Karaboue
Naby Camara
Edwin Balua
Joshua Mutale
Awesu Awesu
Omari Omari
Moussa Camara

🆕📰Kuhusu Moussa Camara, wachambuzi wengi na mashabiki tayari wameonyesha mshangao kwa sababu alikuwa mmoja wa makipa walioonekana kuwa na mchango mkubwa katika mechi za Simba kitaifa na kimataifa

Wapo wanaoona huu ni uamuzi wa kuanza upya kikosi na kupunguza baadhi ya nafasi za wachezaji wa kigeni ili kusajili nyota wapya, huku wengine wakiamini kuondoka kwake ni hasara kwa uzoefu wake alikuwa nao kikosini kabla ya kuuumia msimu uliopita.

Hata hivyo, sababu rasmi za kila mchezaji kuondolewa bado hazijaelezwa kwa kina kwenye tangazo la "Asanteni Sana."

Kwa upande wa mashabiki, jina la kutokana na mchango wake katika vipindi tofauti vya msimu aliocheza.

16/07/2026

Unavyomchukia Lionel Messi ndiyo anavyozidi kufanya maajabu! 🐐🔥

Waliosema hawezi kubeba Kombe la Dunia, alilibeba. Waliosema zama zake zimeisha, ameendelea kuandika historia. Na jana dhidi ya England, akiwa na miaka 39, hakufunga lakini alitoa pasi mbili za mabao na kuiongoza Argentina kutinga fainali ya Kombe la Dunia kwa ushindi wa 2-1.

Messi amethibitisha mara nyingi kuwa ukubwa wa mchezaji haupimwi kwa maneno ya wanaomchukia, bali kwa kile anachofanya uwanjani. Kila wanaposema amekwisha, yeye anarudi na sura mpya ya maajabu. 🏆🇦🇷

Swali langu ni moja tu: Baada ya yote haya, bado una sababu ya kusema Messi si GOAT? 🤔👇

16/07/2026

🔵⚪ KARIBU TENA NYUMBANI, KIPRE JUNIOR! 🔥

Baada ya kipindi cha kusubiriwa kwa hamu na mashabiki, hatimaye Kipre Junior amerejea rasmi Azam FC. Ni kurejea kwa mmoja wa viungo wenye ubunifu mkubwa, uwezo wa kutengeneza nafasi na kufunga mabao muhimu.

Je, ujio wake utaiwezesha Azam FC kuvunja ukame wa ubingwa na kufanya makubwa zaidi msimu huu? Mashabiki wa Wanalambalamba wana kila sababu ya kuwa na matumaini makubwa.

Karibu tena nyumbani, Kipre Junior! 💙

15/07/2026

Argentina 2-1 England

Messiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii two assists 😅😅😅🫡🫡🫡🙌🙌

15/07/2026

Msimu Huu
Usajili ni Mwendo Wa Kush*tukiza Tu😅

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Website

Address

Dar Es Salaam