bago health consultant
Natoa huduma kwa magonjwa mbalimbali k**a vile magonjwa ya mifupa, changamoto za uzazi kwa kina mama
21/12/2025
FAHAMU KUHUSU PID
🩺 PID ni nini?
PID (Pelvic Inflammatory Disease) ni maambukizi ya njia ya uzazi ya ndani ya mwanamke, yanayoshambulia:
1. mfuko wa uzazi (uterus),
2. mirija ya uzazi (fallopian tubes),
3. na ovari.
Ni ugonjwa unaotokana na kuenea kwa bakteria kutoka ukeni au shingo ya kizazi kwenda ndani ya mfumo wa uzazi wa juu.
⚠️ Sababu kuu za PID
PID husababishwa zaidi na maambukizi ya magonjwa ya zinaa (STIs) — hasa:
1. Chlamydia trachomatis
2. Neisseria gonorrhoeae (Gonorrhea)
Lakini pia inaweza kusababishwa na:
1. Bakteria wengine wa kawaida waliopo ukeni wanaoingia ndani kwa sababu ya:
2. kujisafisha kwa kutumia vifaa vya ndani ya uke (douching),
3. upasuaji au uchunguzi unaohusisha kizazi,
4. mimba ya nje kuharibika au kutoa mimba bila usafi,
5. tendo la ndoa bila kinga (condom),
6. kuwa na wapenzi wengi.
🔍 *Dalili za PID*
Dalili zinaweza kuwa nyepesi au kali, na wakati mwingine mwanamke hana dalili kabisa.
Zile zinazoonekana zaidi ni:
1. Maumivu ya tumbo la chini (lower abdomen)
2. Homa au joto mwilini
3. Kutokwa na uchafu ukeni wenye harufu mbaya
4. Maumivu wakati wa tendo la ndoa
5. Maumivu wakati wa kukojoa
6. Hedhi zisizo za kawaida (nzito au zenye maumivu makali)
7. Kutokwa damu nje ya kipindi cha hedhi
8. Uchovu na kichefuchefu
⚠️ *Madhara ya PID isipotibiwa*
1. K**a haitatibiwa mapema, PID inaweza kusababisha:
2. Kushikana kwa mirija ya uzazi (blockage) → ugumba
3. Mimba kutunga nje ya kizazi (ectopic pregnancy)
4. Maumivu ya kudumu ya tumbo la chini
5. Kuvurugika kwa hedhi na homoni
Kwa maoni,ushauri na tiba wasiliana nasi kupitia WhatsApp namba; 0718499414
WhatsApp 0718499414
16/12/2025
Kiboko ya miwasho ukeni,U.T.I sugu, PID na fangus ukeni
Hakuna kuteseka tena na matatizo ya uzazi njoo ujipatie suluhu ya kudumu💪
WhatsApp 0718499414
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Dar Es Salaam
255