msema kweli
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from msema kweli, Ifakara.
26/08/2026
Laurian Kulwa Deusdedith (@lauriankulwadeusdedith) USISAHAU KUWA WEWE NI WEWE NA UNAYO SABABU YA KUWA WEWE Kuna sababu kwa nini wewe si mtu mwingine. Katika maisha, moja ya vita vikubwa ambavyo mtu anaweza kupigana si vita dhidi ya watu wengine, bali ni vita vya kujikubali mwenyewe. Tunapoangalia mafanikio ya wengine, wakati mwingine tunaanza kujiul...
26/08/2026
Makala hii inahimiza mtu kujitambua, kujikubali na kuthamini upekee wake. Mwandishi anaeleza kuwa kujilinganisha sana na wengine kunaweza kumfanya mtu asione thamani yake na kuishi maisha ya kujaribu kuwafurahisha watu.
Dhumuni kuu la Laurian Kulwa Deusdedith ni kumsaidia msomaji kuelewa kwamba ana thamani kwa kuwa yeye mwenyewe, bila kulazimika kuwa nakala ya mtu mwingine ili akubalike. Mtu anaweza kujifunza kutoka kwa waliofanikiwa, kubadilika na kujiboresha, lakini hatakiwi kupoteza utambulisho wake.
Makala pia inasisitiza kwamba kujipokea si kukubali udhaifu, bali ni kutambua ulipo, kutumia uwezo ulio nao na kujenga toleo bora zaidi la nafsi yako.
Kwa ujumla, mwandishi anatukumbusha kuwa kila mtu ana safari, uwezo na upekee wake. Hivyo, usiishi maisha ya mtu mwingine; jifunze, kua na boresha maisha yako, lakini usisahau kuwa wewe ni wewe.
— Laurian Deusdedith | Msemakweli Official
Soma makala yote kupitia kiunganishi hiki hapa chini>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
Laurian Kulwa Deusdedith (@lauriankulwadeusdedith) USISAHAU KUWA WEWE NI WEWE NA UNAYO SABABU YA KUWA WEWE Kuna sababu kwa nini wewe si mtu mwingine. Katika maisha, moja ya vita vikubwa ambavyo mtu anaweza kupigana si vita dhidi ya watu wengine, bali ni vita vya kujikubali mwenyewe. Tunapoangalia mafanikio ya wengine, wakati mwingine tunaanza kujiul...
Usiseme utamjua rafiki wa kweli kwenye shida, wapo marafiki wa kweli ambao hawawezi kuhimili kila aina ya mateso unayopitia maishani.
Petro alikuwa mwanafunzi mwaminifu wa Bwana Yesu, alipambana sana ikafika wakati akamtoa mtu sikio, ila kuna saa alimkana Yesu.
Nafikiri aliogopa kuingizwa kwenye mateso ya Yesu. Tuishi na wapendwa wetu vile maisha yanataka kuna changamoto zinakuja ni mwenyewe pekee yako unatakiwa kupambana.
18/08/2026
HAJARISHI UMEPOTEZA NINI, IMARISHA KILICHOBAKIA
Mara nyingi tunapoteza nguvu nyingi tukijutia kile TULICHOPOTEZA na wale ambao hawapo tena katika maisha yetu.
Lakini maisha hayasimami kwa sababu umeachwa na mtu, umepoteza nafasi, muda, mali, kazi au fursa uliyoiota MAISHANI MWAKO.
Katika Biblia takatifu kitabu cha 2 Wafalme 4:1–7, Elisha hakumwuliza mjane, “Umepoteza nini?” Bali alimuuliza: “Una nini nyumbani?”
Hili ni somo muhimu;
.......usiruhusu kile ulichopoteza kikufanye usione thamani ya kile ambacho bado ukonacho ndani yako.
Tambua kilichobaki.
Kithamini.
Kikuze.
Kitumie kwa hekima.
........na kifanye kuwa ile fursa ya maisha yako uliyoita kila siku ukiwa na MATUMAINI ya kuifanya kuwa kweli.
Huenda kile ulicho nacho leo ni kidogo, lakini kinaweza kuwa mwanzo wa jambo kubwa UNALOLIOTA ndani ya kesho yako.
Haijalishi umepoteza nini; swali ni, umebaki na nini, na utakitumia kufanya nini?
Usitumie maisha yako yote kuomboleza yaliyopita. Imarisha kilichobakia, kwa sababu huenda humo ndimo ulipojificha mwanzo wa maisha mapya.
Remember that
" Your focus should be in what you have remained with and not what you have lost."
Na Mungu Atabless
Laurian Kulwa Deusdedith
05/08/2026
Wasiwasi huiba sehemu kubwa ya maisha yetu kuliko MATATIZO yenyewe.
Wengi wetu hutumia muda mwingi kuhangaika kuhusu mambo ambayo hata HAYAJATOKEA.
......tunajikuta tukirudia mazungumzo yaliyopita akilini, tukiwaza matokeo mabaya zaidi, na kubeba mizigo ambayo ipo katika fikra zetu pekee.
Mchoro huu rahisi unatukumbusha jambo muhimu sana: Ikiwa huna tatizo, basi huna sababu ya kuwa na WASIWASI.
Na ikiwa una tatizo, jiulize swali moja tu:
Je, kuna jambo ninaweza kufanya kulihusu?
Ikiwa jibu ni ndiyo,
.....acha kuwa na wasiwasi na anza kuchukua hatua. Hata hatua ndogo inaweza kukusogeza karibu zaidi na SULUHISHO. Hatua huipa akili mwelekeo, ilhali wasiwasi huifanya izunguke bila kupata jibu.
Ikiwa jibu ni hapana,
......basi wasiwasi hautabadilisha chochote. Hautafanya kesho iwe rahisi zaidi, hautatatua tatizo, wala hautakupa utulivu wa moyo.
Badala yake, utaendelea kukupokonya nguvu na utulivu wa leo.
Amani ya kweli haitokani na kuwa na maisha yasiyo na changamoto. Inatokana na kutambua tofauti kati ya yale unayoweza kuyadhibiti na yale usiyoweza KUYADHIBITI.
Follow msema kweli kwa maudhui zaidi, yanayokujenga na kukuhamasisha.
02/08/2026
Si Vyema Kujisemea Vibaya Pale Unapopitia Magumu maishani mwao.
Watu wengi huanza kujisemea vibaya baada ya kupitia maumivu, kushindwa au kukataliwa, wakiamini kuwa matatizo yao ndiyo YANAYOWAFAFANUA.
.......kadiri yanavyojirudia maneno hasi k**a "Mimi siwezi" au "Sina thamani," ndivyo akili inavyoanza KUYAAMINI k**a ukweli.
Hali hii huongezeka pale UNAPOZUNGUKWA
na watu wanaokosoa kila hatua yako badala ya KUKUTIA moyo.
Je, unaweza kutarajia maisha yako yabadilike ikiwa sauti unayoisikia kila siku ni ile ya kujidharau?
Tafiti za American Psychological Association (2024) zinaonyesha kuwa mazungumzo hasi ya ndani (negative self-talk) yanahusishwa na kuongezeka kwa msongo wa mawazo, wasiwasi na kupungua kwa KUJIAMINI.
.......ndiyo maana mtu huanza kuona kila changamoto k**a UTHIBITISHO wa kushindwa badala ya fursa ya KUJIFUNZA.
Ukombozi wa fikra huanza pale unapoachana mzunguko wa maneno hasi na kuanza kujisemea ukweli unaojenga MATUMAINI.
Chagua kukaa karibu na watu WANAOKUINUA, wanaokukumbusha uwezo wako na wanaokutia moyo hata UNAPOKOSEA.
Badili kauli zako kutoka "Nimeshindwa" kwenda "Nimejifunza, na nitaendelea kupambana," kwa sababu maneno huongoza mtazamo na matendo yako.
Kumbuka jambo moja kuwa,
Ushindi wa kwanza katika maisha haupatikani kwa kubadilisha mazingira, bali kwa kubadilisha mazungumzo unayofanya na nafsi yako kila siku(Intrapersonal communication).
Usisahau kushare na marafiki zako ili nao wapatae kuelewa.Na Mungu Atabless
Laurian Kulwa Deusdedith
29/07/2026
Laurian Kulwa Deusdedith (@lauriankulwadeusdedith) USISUBIRI WAKATI SAHIHI "Usisubiri upepo ubadilike; jifunze kutumia upepo uliopo kusafiri." Maisha HAYAWAZAWADII wanaosubiri. Yanawazawadia wale wanaothubutu kuchukua hatua. Usisubiri wakati sahihi kwa sababu ukweli ni huu: wakati sahihi hauji, unatengenezwa na maamuzi UNAYOYAFANYA leo. Wathamini wa...
Click here to claim your Sponsored Listing.