Kinga ni bora kuliko tiba

Kinga ni bora kuliko tiba

Share

KUTOA ELIMU NA TIBA KWA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

13/03/2022

*Siku ya FIGO duniani ➡️ *

Siku ya Figo Duniani huadhimishwa duniani kote kila Alhamisi ya pili ya mwezi Machi tangu mwaka 2006.

📔Mwaka huu inaadhimishwa leo tarehe 10/3/2022.

Soma u*i huu kuelewa kuhusu Afya ya figo👇

Ugonjwa wa kudumu wa figo ni huathiri utendaji wa figo.

Kazi hizi huathirika na ugonjwa wa figo:

1️⃣kutengeneza kemikali inayochochea utengenezaji wa chembe nyekundu za damu.

2️⃣kusaidia upatikanaji wa madini yanayoimarisha mifupa.

3️⃣kusaidia upatikanaji wa vitamin D mwilini.

4️⃣kurekebisha shinikizo la damu

5️⃣Kurekebisha kiwango cha maji

6️⃣ Kuondoka takamwili itokanao na utendaji wa mwili na sumu mwilini.

*Magonjwa ya figo hutokana na sababu mbalimbali kulingana na umri wa waathirika.*

*Magonjwa haya kwa watoto husababishwa na:*

➡️ Magonjwa yanayotokana na matatizo ya mfumo wa mkojo ambayo watoto huzaliwa nayo.

➡️magonjwa mengine k**a malaria,kuhara, kisukari,maambukizi ya bakteria.

*Kwa watu wazima chanzo kikubwa cha magonjwa ya figo ni: *

1️⃣ugonjwa wa kisukari
2️⃣shinikizo la damu.

⚠️Pia utumiaji wa dawa, mitishamba na magonjwa ya kuambukiza k**a ilivyo kwa watoto yanaweza kuathiri figo kwa watu wazima.

➡️ Yapo pia magonjwa mengi ambayo huathiri figo moja kwa moja mfano mawe ya figo na njia ya mkojo.

❌Zipo sumu na dawa za mbalimbali zinazoathiri figo ikiwa ni pamoja na dawa za maumivu k**a diclofenac hasa zinapotumika kiholela.

‼️ Matumizi ya mitishamba yameripotiwa kuathiri utendaji wa figo.

☑️ Tafiti za ugonjwa wa figo zinaonyesha kuwa kati ya mwezi Agosti 2014 na Februari 2015 kati ya watoto 513 waliopimwa magonjwa ya figo katika Hospitali za Bugando na Sekou Toure asilimia 16.2% walikuwa na matatizo ya figo.

➡️Utafiti mwingine uliofanyika Kilimanjaro 2014, uliohusisha watu 481, watu 7% walionekana kuwa na matatizo ya figo.

➡️Utafiti huu ulionyesha uhusiano wa karibu kati ya uwepo wa tatizo la figo na ugonjwa wa kisukari, shinikizo la damu na matumizi ya mitishamba.

*Mambo yanayochochea uwezekano

13/03/2022

UFAHAMU UGONJWA WA NGIRI NA SULUHISHO LAKE

Ngiri hujulikana pia k**a “Hernia” kwa Kiingereza. Ugonjwa wa ngiri ni matokeo anayopata mtu kutokana na misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikilia au kubeba viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi na kupelekea viungo hivyo kutoshikiliwa vizuri katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Tunaweza kuufahamu zaidi ugonjwa wa ngiri k**a hali inayotokea katika mwili ambapo sehemu fulani ya nyama ya viungo mbalimbali vya mwili hujipenyeza kupitia sehemu iliyo dhaifu ya mwili na kutokeza upande wa pili. Sehemu inayoathiriwa mara nyingi ni maeneo ya tumbo, kokwa, pumbu na kadhalika ambapo baadhi ya viungo vya mwili vilivyomo tumboni hujipenyeza kupitia vitundu vinavyopitisha mishipa ya fahamu inayohudumia kokwa (Spesmatic Cord), hivyo baada ya kujipenyeza huteremka hadi ndani ya korodani hali ambayo hukamilisha kuwepo kwa ugonjwa wa mshipa wa ngiri.

Sehemu ambazo Ngiri inaweza kutokea ni pamoja na maeneo ya:👇🏽🤏🏾💥

👉Tumboni
👉Eneo la kinena
👉Eneo la paja kwa juu
👉Eneo ambalo mtu amewahi kufanyiwa upasuaji siku za nyuma
👉Kifuani nk

Ugonjwa huu wa ngiri unawapata watu wa jinsia zote na wa umri wowote.

AINA ZA NGIRI

Ugonjwa wa mshipa wa ngiri unaweza kujitokeza maeneo mbalimbali ya mwili na aina ya ngiri hutegemea na sehemu ngiri ilipojitokeza.

⚡Ngiri maji
– Hii ni aina ya ngiri ijulikanayo pia kwa kitaalamu k**a (hydrocele)

⚡Ngiri kavu (Hernia)
– hujulikana pia k**a ‘fermoral hernia’ kwa wanawake na huitwa ‘scrotal hernia’ kwa wanaume

⚡Ngiri ya kwenye kifua
– hujulikana pia kitaalamu k**a ‘hiatus hernia’

⚡Ngiri ya tumbo
– hujulikana pia k**a ‘Abdominal Hernia’

⚡Ngiri ya kwenye kitovu
– hujulikana pia k**a ‘Umbilical Hernia”

⚡Ngiri ya sehemu ya haja kubwa
– hujulikana pia k**a ‘Anal Hernia’ ?

DALILI ZA UGONJWA WA NGIRI CHANGA(isiyo komaa)

Dalili za ugonjwa huu wa ngiri ziko nyingi sana kwa hiyo hapa nitataja dalili chache tu.

Nazo ndizo hizi zifuatazo 👇
1. Kubana tumbo khasa chini ya kitovu

14/02/2022

Magonjwa Haya ni Hatari Sana Kuliko UKIMWI. Ukizembea Kupata Tiba, Mwisho Wake ni Mbaya

➡️Homa ya Ini (Hepatitis 😎 na Uvimbe wa Ini
➡️Kufeli kwa Ini (Cirrhosis) na Magonjwa mengine ya Ini
➡️Ugonjwa wa Figo
➡️Kisukari
➡️Shinikizo la Juu la Damu (BP)
➡️Magonjwa ya Moyo
➡️Stroke
➡️Kifua Kikuu na Magonjwa ya Mapafu
➡️Saratani ya Ubongo na Saratani nyingine
➡️Magonjwa ya Bandama

Haya magonjwa yakigundulika kwa kwako, fanya uwezavyo kukinga ueneaji wake na kuti maana yanazuia Kinga kufanya Kazi na kuanzisha matatizo mengine.

Wasiliana nasi
0768114257
Natural suppliments

10/01/2022

ANGALIZO;

Mwanaume ukigudua mkeo/mwenza wako ana maambukizi sugu ya PID, Chlamydia au zinaa, msaidie haraka kupata Tiba na CHUKUA TAHADHARI kwa kutumia Kinga.

Madhara Yake ni makubwa kwa mwanaume;
➡️Husababisha Maambukizi hatari ambayo husababisha maumivu makali na makovu yasiyopona kwa mwanaume
➡️ Huathiri mirija ya Uzazi wa mwanaume
➡️ Maambukizi haya hujionesha ndani ya siku kuanzia 2 nahchka Mua kupona
➡️ Husababisha Ugumba

Kuwa makini. wasiliana nasi kwa msaada zaid

10/01/2022

Madhara Hatari Anayoyapata Mwanamke Asipotibu Maambukizi Katika Via vya Uzazi (PID)

✍🏻Maambukizi katika via vya uzazi kwa kawaida hujulikana k**a PID, kitaalamu kirefu chake ni Pelvic Inflammatory Disease, kwa Kiswahili maana yake ni maambukizi ya magonjwa katika via vya uzazi.

✍🏻PID, ni maambuki yanayoathiri viungo vya uzazi vya mwanamke na hutokana na mchanganyiko mbalimbali wa magonjwa ya zinaa, hasa yaliyosababishwa na bakteria wa Pangusa (Chlamydia-ugonjwa huu tutaujadili siku zijazo) au kisonono.

✍🏻Ugonjwa wa PID unapokaa muda mrefu bila kutibiwa, unaweza kusababisha uharibifu mkubwa usiobadilika katika mfumo wa uzazi wa mwanamke, hasa;
👉Katika mfuko wa kizazi (uterus),
👉Vifuko vya mayai (Ovaries) na
👉Mirija ya mayai (Fallopian Tubes).

✍🏻Ugonjwa huu unapokaa muda mrefu mwilini bila kutibiwa humfanya mwanamke;

👉Kupatwa na Ugumba Wanawake wengi wamekuwa wakisumbuka na ugonjwa huu.
👉Ugonjwa wa kisonono pamoja na pangusa (Chlamydia) ndio vyanzo vikuu vya maambukizi katika via vya uzazi wa mwanamke.
👉Mwili wa mawanamke unapokuwa na afya kamili, mlango wa kizazi huwa na nguvu ya kuzuia bakteria wasiweze kuingia katika viungo vya ndani vya uzazi kutoka ukeni.
👉Hata hivyo, wakati mlango wa kizazi unapokuwa wazi na kuruhusu magonjwa ya zinaa kuingia, hasa kisonono na pangusa, mlango wa kizazi hupata maambukizi na kisha hupoteza uwezo wake, hivyo kuruhusu maambukizi na bakteria kuingia na kufika juu kwenye viungo vya uzazi.
👉Hapa kuna mambo ambayo huwafanya wanawake kupatwa na tatizo hili kwa urahisi, mambo hayo ni:
1️⃣kuwa na wapenzi wengi ama kutoka nje ya ndoa,
2️⃣kuanza mambo ya mapenzi mapema hasa chini ya miaka 20,
3️⃣kupiga bomba ukeni kwaweza kusaidia vimelea kuingia ndani na kusababisha maambukizi katika viungo vya uzazi.

Dalili Za PID

✍🏻Dalili za PID zinatofautiana kwa mtu mmoja hadi mwingine. Kwa baadhi ya wanawake dalili huwa mbaya na kwa wengine dalili huwa za kawaida. Wakati mwingine wanawake hukaa na ugonjwa kwa muda mrefu bila k

03/01/2022

http://2.pr/

17/12/2021

FAIDA ZA KUTUMIA MAFUTA YA SAMAKI (omega 3)

🦈Husaidia kuimarisha uwezo wa macho kuona
🦈Husaidia kuimarisha mifupa na kuongeza uteute kwenye joint .
🦈Husaidia kuondoa mafuta mabaya mwilini(bad cholesterol).
🦈Husaidia kuimarisha Afya ya ubongo na kurudisha kumbukumbu (kwa watoto na watu wazima).
🦈Husaidia katika Afya ya uzazi kwa wanawake, husaidia ukuaji wa mimba na mtoto tumboni.
🦈Husaidia kuondokana na tatizo la mimba kuharibika na kujifunga kabla ya wakati (miscarriage).
🦈Husaidia kuimarisha Afya ya ngozi.
🦈Husaidia wenye matatizo ya moyo na Presha.

Matumizi ya mafuta ya samaki hayana mipaka katika kundi au umri wa mtumiaji, watu wa rika zote kulingana na mahitaji ya kiafya wanashauriwa kutumia mafuta ya samaki ili kuweza kuimarisha afya zao.

Kwa wanaohitaji kuyapata au ushauri zaidi wasiliana nasi

13/12/2021

🔘VIDONDA VYA TUMBO🔘

Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda, hii hutokea ni baada ya kuharibika kwa ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaoitwa mucus. Kemikali ambayo ni acidi inayozalishwa mwilini kiasili husaidia kuyeyusha chakula na kuua wadudu tumboni, k**a ukuta wenye ute ukiharibiwa na kushindwa kufanya kazi basi kemikali (acid) itaathiri tumbo au utumbo na kuruhusu bakteria kuendelea kusababisha vidonda vya tumbo.

Vidonda vya tumbo vinatibika kirahisi ila vikicheleweshwa bila kutibiwa huweza kusababisha tatizo kubwa. Ni tatizo linalotesa sana na kuwanyima raha watu wengi, linahitaji umakini na pia husababisha magonjwa mengine k**a kansa, amoeba (amiba), homa, kupungua u*ito.

🔵AINA YA VIDONDA VYA TUMBO 🔵
Kuna aina zipatazo mbili za Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers)

1.Vidonda vya tumbo kubwa
(Gastric ulcers)

▶️Hivi ni vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani kwenye tumbo kubwa

2.Vidonda vya utumbo mdogo
(Duodenal ulcers)

▶️Hivi ni vidonda ambavyo hutokea kwenye utumbo mdogo (hasa juu)

Bakteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori)

🔘CHANZO CHA VIDONDA VYA TUMBO 🔘

1.Matumizi ya dawa za kupunguza maumivu k**a asprin, (NSAIDs), (Advil, Aleve, na zingine)

2.Kuwa na mawazo mengi

3. Kula vyakula vinavyozalisha acid kwa wingi

4.Kunywa pombe na vinywaji vikali

5.Uvutaji wa sigara

6.Kuto kula mlo kwa mpangilio

🔘DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO 🔘

1.Kupata maumivu ya tumbo yanayokuwa k**a ya moto (kuunguza) baada na kabla ya kula

2.Kupatwa na kiungulia karibu na chembe ya moyo

3.Tumbo kujaa gesi na kuvimbiwa

4.Kichefuchefu na kutapika tena yawezekana kutapika damu

5.Kupata haja kubwa ya rangi kahawia au nyeusi yenye harufu mbaya sana, pia haja yaweza kuchanganyikana na damu.

6.Kupoteza hamu ya kula na kupungua u*ito

7.Kushindwa kupumua vizuri

🔴MATIBABU YAKE🔴
Tatizo la Vidonda vya tumbo linatibika so k**a una tatizo hilo karibu tiba ipo ambayo utaw

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Morogoro?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address

Kibandani
Morogoro