PENGO Sports news

PENGO Sports news

Share

02/09/2025

🎙HEMED SELEMAN 'MOROCO'

"Najisikia vibaya na waandishi wa habari wa kwetu wameshindwa kuwa wazalendo na timu ya Taifa, tunaona waandishi wa nchi nyingine walivyo wazalendo na nchi zao, Waandishi wanapaswa kuisapoti timu yao, wanapaswa kuja kwenye interview."

Mimi k**a Kocha wa Taifa Stars nawaomba sana waandishi waisapoti timu yao maana hata wakitusema sisi tutachukulia k**a changamoto ya kutusukuma ila mueneshe tu uzalendo kwa timu ya taifa kwa kijitokeza kwa wingi, mfano k**a hapa mmekuja wachache ila mlipaswa kuwa wengi kuonesha tu kuwa mnaisapoti timu ya taifa lenu.

Sisi tunasafiri sana huko tunaona namna waandishi wanajitokeza kwenye mahojiano ama press za timu zao zinapocheza wao wanaenda kwa wingi ishara ya Uzalendo ila kwetu waandishi wamekosa uzalendo kabisa, kwa nyie wachache mliokuja nawaomba sana muhahimize waandishi wengine waje sisi hata wakitukosoa tunachukulia k**a changamoto ila uwepo wao ni muhimu sana k**a uzalendo kwa taifa lao."

- Hemed Morocco
Kocha Mkuu wa Taifa Stars.

Usiache kulike comment and share Kwa wingi

02/09/2025

Alexander Isak Aweka Historia mpya kwa kujiunga na Liverpool FC
Klabu ya Liverpool imeandika ukurasa mpya wa historia kwa kumsajili mshambuliaji hatari wa Sweden, Alexander Isak, akitokea Newcastle United. Usajili huu umegharimu £125 milioni, ada ambayo ni rekodi mpya ya ligi kuu ya Uingereza, na inaweza kufikia hadi £150 milioni kutokana na vipengele vya nyongeza.

Isak amesaini mkataba wa miaka sita, ishara ya imani kubwa ambayo Liverpool wameweka juu ya uwezo wake wa kusaidia timu kurejea kileleni barani Ulaya na ndani ya EPL.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 tayari ametambulishwa rasmi Anfield, na atavaa jezi namba 9 – namba ambayo imewahi kuvaliwa na magwiji wa klabu akiwemo Robbie Fowler, Fernando Torres, na hivi karibuni Roberto Firmino.

Kwa upande wake, Isak amesema ana furaha kubwa kujiunga na moja ya vilabu vikubwa zaidi duniani na kuahidi kutoa kiwango cha juu ili kuisaidia Liverpool kufanikisha malengo yake makubwa msimu huu.

Usajili huu si tu unazidisha kasi ya mashambulizi ya Liverpool, bali pia ni ujumbe wazi kwa wapinzani wao: Liverpool bado ipo tayari kupigania mataji makubwa ndani na nje ya Uingereza.

Usiache kutembelea page yetu Kila siku Kwa habari motomoto za kimichezo

01/09/2025
03/08/2025

Klabu ya Simba Sc imemtambulisha kiungo mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’ Mohamed Bajaber kutoka klabu ya Kenya Police FC

Bajaber (22) amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia Simba Sc mpaka Juni 2027.

02/08/2025

Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars imeanza vyema mashindano ya kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN2024 baada ya kuilaza Burkina Faso 2-0 katika dimba la Benjamin Mkapa.

Tanzania ipo Kundi B la michuano hiyo sambamba na Mauritania, Madagascar, Jamhuri ya Afrika ya kati na Burkina Faso.

FT: Tanzania 🇹🇿 2-0 🇧🇫 Burkina Faso
⚽ 45+3’ Sopu
⚽ 71’ Zimbwe Jr

PATA habari motomoto za kimichezo kupitia page yetu ya sports news

01/08/2025

Mtanzania Kelvin John mbape wa bongo anayecheza soka la kulipwa nchini Denmark katika Klabu ya Aalborg inayoshiriki Ligi daraja la kwanza, amefanikiwa kuwa Mchezaji bora wa mwezi July wa Klabu .

Congrats keep it up Kelvin .p.john

01/08/2025

Klabu ya Simba SC imemtambulisha mshambuliaji hatari Jonathan Sowah kutoka Singida Black Stars

Mshambuliaji Jonathan Sowah amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Simba SC na alipokuwa Singida BS alifunga magoli 15 katika mechi 15

Usiache kufatilia taarifa mbalimbali za kimichezo kupigia page yetu

30/07/2025

Simba SC yamsajili kiungo fundi kutoka Senegal! 🇸🇳

Klabu ya Simba SC imekamilisha usajili wa kiungo mahiri Alassane Kanté kutoka klabu ya CA Bizertin ya Tunisia. Kiungo huyo wa kimataifa kutoka Senegal amejiunga na Wekundu wa Msimbazi kwa mkataba wa miaka 2, ukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

Kanté anajulikana kwa uwezo mkubwa wa kutuliza mchezo, pasi za uhakika, stamina ya hali ya juu, na uwezo wa kusoma mechi – ni mchezaji wa aina ya kiungo anayechanganya nguvu na akili, akiongeza chaguo la kiufundi katika eneo la kati.

Akiwa amepitia klabu kadhaa barani Afrika Kanté analeta uzoefu mkubwa unaoendana na malengo ya Simba SC katika kutafuta mafanikio ya ndani na kimataifa!

@ Msimbazi, Alassane Kanté – mashabiki wa Simba wapo tayari kushuhudia moto wako!

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Morogoro?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address

Ifakara
Morogoro
0672882601