Witty Afya
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Witty Afya, Morogoro.
03/04/2025
Kwa baadhi ya watoto vyakula tajwa hapo juu vinaweza chochea aleji / mzio
Hivyo k**a mwanao ana asili ya aleji, epuka vyakula hivi
Muhimu, angalia virutubishi anavyokosa kwenye vyakula tajwa
Na mpe chakula mbadala
Kwa mfano
Mtoto mwenye aleji ya mayai anakosa protein ...anakosa vitamini A & E, anakosa madini chuma, anakosa Biotin
Lakini virutubishi hivyo hivyo anavyokosa anaweza kuvipata kwenye vyakula vingine ambavyo havimpi aleji
Kwa mfano iyo protein ataipata kwenye nyama, maharage & njegere n.k
Madini chuma atayapata kwenye nyama, mboga za majani, n.k
Jambo la msingi la wewe mzazi kufanya
Ni kuangalia chanzo mbadala cha virutubishi anavyokosa
Na pindi utakapo amua kumpa ivyo vyakula vilivyo na asili ya aleji, tumia sheria ya siku 4
Tag & share na mama mwenzio aje ajifunze
Afya
25/03/2025
MATEGE (rickets) ni nini
Matege ni kupinda miguu kwa watoto wadogo kutokana na uwepesi au ulegevu wa mifupa.
SABABU
☑️Ukosefu na upungufu wa Calcium na vitamini D uliokithiri na wa mda mrefu.
Vitamini D huusaidia mwili wa mtoto kufyonza na kutumia madini ya Calcium na Phosphorus kutoka kwenye chakula. Ukosefu wa mda mrefu au upatikanaji kwa uhafifu wa Vitamini D hupelekea mwili kupata ugumu wa kufyonza na kuyauwianisha madini hayo ya Calcium na Phosphorus mwilini na hali hiyo ikiwa ya mda mrefu hupekea kupata matege.
DALILI
☑️Kuchelewa kwa ukuaji wa mtoto.
☑️Mtoto kulalamika maumivu ya uti wa mgongo mara kwa mara.
☑️Miguu kupinda na kushindwa kugusana magoti
☑️Kuchelewa kwa maendeleo ya mtoto k**a vile;
>Kukaza shingo
>Kukaa
>Kutambaa
>kusimama na kutembea
VIHATARISHI
☑️Ngozi nyeusi.
Ngozi nyeusi ina melanin nyingi, ambayo hupunguza uwezo wa ngozi wa kuzalisha vitamini D kutoka katika mwanga wa jua.
☑️Mama mjamzito kukosa vitamini D wakati wa ujauzito.
☑️Watoto ambao wanaishi katika maeneo ya kijiografia ambapo kuna jua kidogo huwa katika hatari kubwa ya kupata matege.
☑️Watoto waliozaliwa kabla ya tarehe zao zinazofaa huwa na kiwango cha chini cha vitamini D kwa sababu walikuwa na wakati mdogo wa kupokea vitamini kutoka kwa mama zao tumboni.
☑️Matumizi ya dawa za kuongeza kinga mwilini kwa wamama wenye VVU & UKIMWI wakati wa ujauzito hupunguza uwezo wa mwili wa mtoto kutumia vitamini D na huweza kusababisha baadae kupata matege.
☑️Unyonyeshaji wa maziwa tu kwa miezi 6 ya mwanzo bila mtoto kupata matone ya vitamini D.
MADHARA YA MATEGE
☑️Kukosa ukuaji mzuri wa kawaida.
☑️Kibiyongo (Mgongo uliopinda).
☑️Upungufu wa meno.
KINGA YA MATEGE
☑️Kupata mwanga wa jua la asubuhi hadi kabla jua halijawa kali zaidi walau kwa dakika 15.
☑️Epuka kumpa mtoto vyakula vilivotengenezwa kwa mtindi vyakula k**a jibini n.k
☑️Mama mjamzito kutumia virutubisho vyenye vitamini D
☑️Watoto wachanga wenye kulishwa na chupa wanaweza pia kuhitaji virutubisho vya vitamini D ikiwa hawapati vitamini D vya kutosha kutoka kwa lishe wapewayo.
☑️Kuongeza vitamini D au kalsiamu kwenye lishe kwa ujumla hurekebisha shida za mifupa zinazohusiana na kusababisha matege.
Je unahofia mwanao kuzaliwa na shida ya matege au ana tatzo hilo..?
Tuwasilane kwa ushauri na tiba zaidi.
Mawasiliano
Instagram page: Witty_ Afya
Facebook:-witty afya
Simu:- 🇹🇿0626260488
Imeandaliwa na mtaalamu wa afya
comment na uliza chochote
17/03/2025
FAIDA ZA KULA MACHUNGWA KWA WATOTO
leo ntaongelea faida za kutumia machungwa mala kwa mala
Chungwa lina kirutubisho chambata lishe(fibre) inayosaidia kusaga chakula
1.KUKINGA MAPAFU....lina kiasi kikubwa cha vitamin B6 na madini ya chuma..virutubisho hivi ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu ambazo hufanya kazi ya kusafisha hewa ya oksijeni mwilini na kukukinga na ugonjwa wa mapafu.
2.Ina antioxidants inayosaidia kuleta afya ya ngozi
3.UKUAJI WA UBONGO...chungwa lina asilimia 10 ya folic acid inayohitajika mwilini kila siku...madini haya ni muhimu kwa ajili ya ukuaji wa ubongo...na kuimarisha kumbukumbu na uwezo wa mtu kufikiria.....
4.KUPUNGUZA NA KUKINGA UGONJWA WA MAFUA....chungwa linavirutubisho vingi vinavyosaidia sana kukuepusha na uambukizwaji wa virusi vinavyosababisha magonjwa k**a mafua
5.KUIMARISHA MIFUPA NΑ ΜΕΝΟ
Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya calcium amabayo ni muhimu kww uimariahaji wa mifupa na meno
6.KINGA YA MWILI...
chungwa lina vitamini c ambayo huimarisha uzalishaji wa seli nyeupe ambazo ni muhimu kwa uimarishaji wa kinga ya mwili
CHUNGWA NI MUHIMU SANA KATIKA AFYA YA UKUAJI...NA KWA SASA KWA KUA TUSHAZIJUA FAIDA ZA MACHUNGWA MWILINI TUWAPE WATOTO WETU KWA WINGI.....TUTENGENEZE MBINU TOFAUTI TOFAUTI ZATOFAUTI ZA KUWAPATIA MATUNDA HAYA MAANA NNAJUA KUNA WATOTO WENGINE HAWAPENDI MATUNDA.... MAMA KUA CREATIVE SANA ILO MTOTO APATE KILICHO BORA ZAIDI MWILINI
MWENYE KUJUA FAIDA ZAIDI ZA MATUNDA ATAWEKA KWENYE KOMENTI ILI WATU TUJIFUNZE
TAG MZAZI AMBAYE ANAPASWA KUSOMA FAIDA ZA MACHUNGWA KWA WATOTO...
Nawapenda sana watu wangu lakini pian naomb msisahau kufollow page na kulike videos
ELIMU KUHUSU UZAZI WA MPANGO TUANGALIE FAIDA NA HASARA.
🔷 Njia za uzazi wa mpango ni zipi?
Kuna njia nyingi za uzazi wa mpango ambazo zinaweza kutumiwa na mtu au wenza waweze kusubiri, kuchelewesha, au kupunguza idadi ya watoto watakaowazaa. Zipo njia za mda mfupi, mda mrefu na za kudumu.
🔶 Njia za muda mfupi:
Hizi ni njia za kisasa za uzazi wa mpango ambazo unaweza kuzibadilisha. Unaweza kupata ujauzito pindi utakapoacha kuzitumia. Njia hizi ni nzuri kwa mama anayetaka kupata ujauzito baada ya miaka miwili baada ya kujifungua. Nazo ni:
👉🏿 Vidonge vya kuzuia mimba (vidonge vya majira)
Vidonge vya kuzuia mimba vina homoni ambazo zinafanana na homoni za asili kwenye mwili wa mwanamke. Huzuia mimba kwa kusimamisha ovari za mwanamke kuachia yai au kufanya yai lisipevuke ili kuzuia lisiweze kurutubishwa na mbegu za kiume (manii).
Kuna aina kuu 2 za vidonge vya majira: vidonge mseto vyenye homoni 2, estrojeni na projestini, na vidonge vidogo ambavyo vina homoni moja tu ya projestini. Baadhi ya majina ya kibiashara maarufu yanaoneshwa kwenye sehemu ya Vidonge vya majira vya kumeza. Vidonge vya majira havitoi kinga dhidi ya VVU au maambukizi mengine kupitia ngono. Ili uweze kujilinda dhidi ya magonjwa hayo, unapaswa kutumia pamoja na kondomu.
Baadhi ya wanawake huamua kutumia vidonge vya majira kwa sababu vidonge hivyo husaidia kuweka vizuri mpangilio wa hedhi, ili waweze kujua lini siku zao za hedhi zitaanza. Vidonge vya majira pia hupunguza wingi wa damu ya hedhi, na mabonge ya damu na maumivu wakati wa hedhi. Vidonge vya majira havisabishi saratani.
Vidonge vya majira mseto (vyenye homoni za estrojeni na projestini)
Aina tofauti za vidonge mseto vya majira vina dozi tofauti za homoni hizi mbili. Kuna mseto wenye dozi za kawaida k**a vile miligramu 1 au chini yake ya projestini na maikrogramu 30 au 35 za estrojeni (ethinyl estradiol), au maikrogramu 50 ya estrojeni nyingine iitwayo mestranol. Baadhi ya vidonge vya majira vina homoni ya projestini tu.
Vidonge vya majira hufanya kazi vizuri kuzuia mimba vinapotumika kila siku na muda ule ule. Ni salama kwa wanawake walio wengi.
Jinsi ya kutumia vidonge mseto vya majira
K**a una uhakika kuwa huna ujauzito, unaweza kuanza kutumia vidonge vya majira wakati wote. Vidonge vya majira havitazuia mimba hadi uwe umekua ukivitumia angalau kwa wiki. Hivyo katika siku 7 za mwanzo baada ya kuanza kutumia vidonge vya majira, tumia kondomu au epuka ngono.
Unatakiwa kutumia kidonge 1 cha majira kila siku kuzuia mimba, hata k**a hutafanya tendo la ngono siku hiyo. Jitahidi kutumia kidonge muda ule ule kila siku. Kuweka vidonge mahali unapolala, kunaweza kukusaidia kukumbuka kumeza kidonge kila siku kabla hujalala. Aina nyingi za vidonge vya majira mseto huwa katika paketi ya vidonge 28 au 21.
Madhara ya pembeni ambayo yanaweza kuhusiana na vidonge mseto vya majira
Madhara ya pembeni siyo hatari sana lakini mengine yanaweza kukera. Kawaida hupungua au kutoweka baada ya miezi 3. Wakati mwingine unaweza kujaribu aina nyingine ya vidonge vya majira.
💊Mabadiliko ya kihisia k**a vile kuwa na huzuni au kukasirika kwa haraka.
💊Maumivu ya kichwa
💊Kichefuchefu
💊Kutokwa na damu kidogo katikati ya vipindi ya hedhi.
💊Matiti kuvimba na kuuma
Vidongo mseto vya majira vinaweza kutumika kupitia njia 3
Kutumia siku 28: Tumia vidonge vyenye homoni kwa siku 21 na baada ya hapo, kwa siku 7, tumia vidonge vilivyobaki. (Vidonge vya ziada kwenye paketi havina homoni), au usitumie tena vidonge. Utakuwa unapata hedhi kila mwezi wakati wa siku hizo 7 k**a hedhi nyingine ya kawaida.
”K**a una paketi ya siku 28, tumia kidonge 1 kila siku. Vidonge 7 vya mwisho ni kwa ajili ya kukukumbusha kuwa havina homoni – Vimewekwa kukusaidia kukumbuka kutumia kidonge cha majira kila siku. Vidonge 7 vya mwisho kwenye paketi vitakuwa vya rangi tofauti”.
”K**a una paketi ya siku 21, tumia kidonge 1 kila siku kwa siku 21 – paketi nzima. Basi usitumie kidonge kwa siku 7. Anza paketi nyingine”.
Matumizi ya muda mrefu: Tumia vidonge vyenye homoni kwa siku 84 vinavyofuatana na baada ya hapo pumzika kwa siku 7. Wakati mwingine vidonge huwa kwenye paketi zenye vidonge 91 (84 vyenye homoni na 7 kwa ajili ya kukumbusha tu ambavyo havina homoni). Wakati wa siku hizo 7, utakuwa unapata hedhi k**a inavyokuwa katika hedhi ya kawaida lakini mara moja tu katika kipindi cha miezi 3. Matone ya damu (hedhi nyepesi sana) yanaweza kutokea lakini hutoweka baada ya miezi michache.
Matumizi endelevu: Tumia vidonge vyenye homoni kila siku bila kuacha. K**a utaona usumbufu na hedhi isiyotabirika, acha kutumia vidonge kwa siku 3 au 4 ili kupata siku chache za hedhi ya kawaida, halafu endelea kutumia kidonge tena kila siku.
Utaratibu wote huu wa kutumia vidonge mseto ni salama. Mtu yeyote ambaye anatumia vidonge mseto vya majira anatakiwa kujua afanye nini k**a ataruka kemeza kidonge kimoja au viwili:
K**a utasahau kumeza kidonge 1 au 2, tumia kidonge 1 haraka mara utakapokumbuka. Baada ya hapo tumia kidonge kinachofuata katika muda wa kawaida. Hii inaweza kumaanisha kwamba utatumia vidonge 2 katika siku moja.
K**a utasahau kutumia vidonge 3, siku 3 zinazofuatana, tumia kidonge 1 mara moja. Baada ya hapo, tumia kidonge 1 kila siku katika muda ule ule. Tumia kondomu hadi utakapoanza hedhi yako, au usifanye ngono hadi utakapokuwa umetumia kidonge kila siku kwa siku 7 mfululizo.
K**a hedhi yako haitakuja muda wake wa kawaida na umesahau kumeza baadhi ya vidonge, endelea kutumia vidonge vyako, lakini pata kipimo cha mimba. K**a utakuta una mimba, simamisha kutumia vidonge.
Kusitisha matumizi ya vidonge mseto vya majira
Unaweza kusimamisha matumizi ya vidonge wakati wote. Unaweza kupata mimba mara moja, hivyo iwapo unataka kuepuka kupata mimba, tumia kondomu au njia nyingine.
Nani hapaswi kutumia vidonge mseto vya majira
Baadhi ya wanawake wana matatizo ya kiafya na matumizi ya vidonge mseto vya majira vinaweza kuhatarisha maisha yao. Usitumie vidonge mseto vya majira iwapo:
👉🏿Una tatizo la presha kubwa ya juu (160/110 au juu zaidi).
👉🏿Ugonjwa wa kisukari kwa zaidi ya miaka 20.
👉🏿K**a una zaidi ya miaka 35 na ni mvutaji wa sigara.
👉🏿Tatizo la maumivu makali ya kichwa (maumivu ya kichwa makali yakiambatana na kichefuchefu) k**a yakiambatana na kufa ganzi au na matatizo makubwa katika kuona.
👉🏿Saratani ya matiti, saratani ya ini, au saratani ya kibofu cha mkojo.
👉🏿Ugonjwa wa kibofu cha nyongo.
👉🏿Uliwahi kupatwa na kiharusi.
👉🏿Damu kuganda kwenye mshipa (hali hii kawaida husababisha joto na maumivu kwenye mguu mmoja).
👉🏿Ugonjwa wa ini au homa ya manjano au hepatitis.
Wanawake wengi wenye tatizo moja la kiafya wanaweza kutumia kwa usalama vidonge vya majira vyenye projestini tu au njia ya vijiti au sindano za projestini tu. Wanawake wenye ugonjwa wa saratani ya matiti au saratani ya tumboni hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango zenye homoni, na badala yake watumie njia nyingine.
Dawa ambazo zinaingiliana na vidonge mseto vya majira
Rifampicin (dawa ya kifua kikuu), ritonavir (dawa ya VVU) na baadhi ya dawa za kifafa huathiri utendaji wa vidonge vya majira. K**a utatumia dawa hizi, chagua njia tofauti ya uzazi wa mpango. Wanawake wanaotumia insulini kwa ajili ya kisukari wanaweza kuhitaji kurekebisha kiasi cha insulini baada ya kuanza kutumia vidonge vya majira.
Nani wanapaswa kufikiria njia zingine k**a zipo
Kuna matatizo machache ya kiafya ambayo hufanya njia ya vidonge vya mseto vya majira kutofaa baadhi ya watu. Ni bora zaidi kwa wanawake wenye matatizo haya kutumia njia nyingine ya kupanga uzazi:
👉🏿Tatizo la shinikizo la juu la damu-presha ya juu (zaidi ya 140/90).
👉🏿K**a una zaidi ya miaka 35 na una matatizo ya kuumwa kichwa (maumivu ya kichwa yanayoambatana na kichefuchefu).
K**a mwanamke mwenye matatizo atatumia vidonge mseto vya majira, angaliwe kwa karibu kuhakikisha matatizo hayo ya kiafya yasizidi. K**a hakuna mabadiliko, basi ni bora kuendelea kutumia vidonge mseto vya majira. K**a matatizo yataongezeka, asimamishe mara moja kutumia vidonge hivyo haraka
Kwa leo ningependa tuishie hapa na tujiandae kwa somo linalofuata (sehemu ya tatu) tuendelee kuangalia njia nyingine mbalimbali za uzazi wa mpango.
Ahsanteni sana na nawapenda sana pia usisahau kulike na kufollow page ya wity Afya
17/03/2025
Kwa mahitaji ya huduma yeyote ya lishe kwa mtoto tuchek kwa namba hii ya
whtsap 0626260488
TikTok · wittie 🌹 Check out wittie 🌹’s post.
17/03/2025
Mayai yana protini nyingi ambayo husaidia kwenye ukuaji wa misuli na ubongo wa mtoto. Ndizi mbivu zina madini ya potassium na fiber, muhimu kwa nguvu na mmeng'enyo mzuri wa chakula. Lakini chipsi je? K**a zimeandaliwa kwa mafuta mengi, zinaweza kuwa hatari! Badala yake, chagua viazi vya kuchoma au kuchemsha kwa afya bora ya mtoto wako
Visit TikTok to discover videos! Watch, follow, and discover more trending content.
17/03/2025
TikTok · wittie 🌹 Check out wittie 🌹’s post.
14/03/2025
KUHARISHA KWA WATOTO,,
Kuharisha kwa watoto ni tatizo linaloshika nafasi ya pili duniani kwa kusababisha vifo miongoni mwa watoto chini ya miaka mitano. Inakadiriwa kwamba kwa kila watoto 5 wanaofariki , 1 hufa kwa sababu ya kuharisha. Watoto milioni 1.5 kila mwaka hufa kutokana na kuharisha.
Leo hii, inakadiriwa asilimia 39 tu ya watoto wanaoharisha katika nchi zinazoendelea hupata matibabu sahihi.Hata hivyo, mwenendo wa kitakwimu unaonesha kwamba kumekuwa na mafanikio kidogo tangu mwaka 2000.
Kuharisha huelezwa kuwa ni upotevu wa maji na madini muhimu kwa mwili wa binadamu (electrolytes) kupitia kinyesi na kupelekea upungufu wa maji mwilini. Katika hali ya kawaida, watoto wachanga hutoa kiasi cha gramu 5 za kinyesi kwa kila kilo ya mtoto (5g/ kg) kwa siku, wakati mtu mzima hutoa wastani wa gramu 200 kwa siku.
SABABU ZA KUHARISHA KWA WATOTO
Kuharisha kunaweza kusababishwa na aina mbalimbali za vimelea ingawa pia kunaweza kusitokane na maambukizi ya vimelea (non-infectious causes). Vimelea vinavyosababisha kuharisha ni
1.Virusi: Virusi vinaongoza katika kusababisha tatizo la kuharisha kwa watoto katika nchi zilizoendelea na zinazoendelea.
2.Bakteria: Wanasababisha kuharisha kwa asilimia chache 2-10%. Kuharisha kunakosababishwa na bacteria husababisha upotevu mdogo wa maji ukilinganishwa na virusi. Mfano wa bakteria wanaoweza kusababisha tatizo hili ni Campylobacter, Salmonella, Shigella, na Escherichia coli
3.Parasite pia husababisha kuhara, lakini aina hii ya kuhara huwa ni sugu zaidi (chronic diarrhea) kwa ujumla na mara nyingi haiambatani na homa, kutapika, na upungufu wa maji mwilini. Giardia lamblia na Cryptosporidium parvum ni moja ya aina hii za parasire wanaosababisha kuhara.
Sababu ambazo hazihusiani na maambukizi ya vimelea yaani noninfectious causes ni pamoja na kula chakula kilichochanganywa na sumu au kumeza sumu, matatizo katika sehemu ya utumbo mwembamba na mnene, na matatizo ya usagaji chakula (metabolic abnormalities).
MUONEKANO WA MGONJWA
Watoto wanaohara kwa sababu ya virusi huwa na dalili kuu tatu ambazo ni homa, kutapika na kuharisha. Kawaida choo kinakuwa cha majimaji sana. Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 63 ya watoto wanaolazwa hospitalini kwa tatizo hili wanaonyesha dalili zote 3, asilimia 25 wanakuwa na dalili 2 tu.
Wakati mwingine kuharisha kunaweza kujitokeza baadaye baada ya kutapika au homa. Joto la mtoto huwa si kali sana ingawa baadhi ya watoto wanaweza kuwa na joto kali linalozidi nyuzi joto 39 za sentigradi.
Kutapika kunaweza kusiwe zaidi ya masaa 24. Vilevile wanaweza kuwa na kuchefuchefu, maumivu ya tumbo (abdominal cramping), kulia pasipo kutulia akibembelezwa (irritability) na uchovu.
kupoteza fahamu
kuwa na mapigo ya moyo ya kasi
kushindwa kula na kunywa
kuwa na macho yaliyolegea kulegea na kuingia ndani sana (severe sunken eyes)
kushindwa kutoa mkojo kabisa
kutotoa machozi na mdomo kuwa mkavu sana.
macho ya mtoto huingia ndani (sunken eyes)
ngozi kurudi taratibu pindi inapovutwa (loss of skin turgor).
mapigo ya moyo kuwa kasi.
kuwa na ubonyeo katika sehemu ya mbele ya kichwa (depressed anterior frontanele)
uchovu.
kiu na kunywa maji kwa haraka.
mtoto kutoa machozi kidogo sana pindi anapolia
midomo kuwa mikavu na
kupumua kwa haraka kuliko kawaida.
MATIBABU.
Ingawa yawezekana mtoto kupona bila hata matibabu lakini ni jambo muhimu kuchunguza madhara yanayoweza kusababishwa na upungufu wa maji mwilini. Ieleweke kuwa watoto wapo katika hatari kubwa zaidi ya ya kupungukiwa na maji mwilini kutokana na kuharisha, hivyo basi msingi wa matibabu ni kurudisha kiasi cha maji kilichopotea.
Hali kadhalika, matumizi ya madini ya zinc yamehusishwa na kupungua kwa makali ya ugonjwa na kupunguza muda wa kuharisha.
ORS ambayo ni mchanganyiko wenye uwiano mzuri wa chumvi na sukari ni aina ya tiba inayopendekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa ajili ya matibabu. Uwiano uliopo katika ORS huwezesha utumbo wa mtoto kufyonza vizuri maji na madini mengine.
NAMNA YA KUZUIA MAAMBUKIZI
Kuzingatia usafi wa chakula (kupika na kuhifadhi).
Kunawa mikono kila baada ya kutoka chooni, kabla ya kushika chakula na wakati wa kula
Kuwa makini na watoto wanaoharisha ikiwezekana kuwatenga na wenzao
Kwa maelezo zaid piga kuhus Afya ya mtoto na mama Kwa ujumla pig simu 0626260488
Click here to claim your Sponsored Listing.