Mbunge LAKI

Mbunge LAKI

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mbunge LAKI, Health/Beauty, KWAHANI, Zanzibar.

05/07/2026

Mh. Mohamed Laki, Mbunge wa Jimbo la Kwahani, alihudhuria mechi ya Kombe la Yamle Yamle Cup iliyowakutanisha Kwahani dhidi ya Mwene Combine. Timu ya Kwahani iliibuka na ushindi mnono wa mabao 4–1. Uwepo wa Mh. Mbunge katika mechi hiyo umeonyesha mshik**ano, hamasa na sapoti yake kwa vijana, pamoja na kuendelea kuhimiza ushiriki wao katika michezo k**a njia ya kukuza vipaji, kuimarisha afya na kuendeleza umoja wa jamii.

Aidha, Mh. Mohamed Laki aliwapongeza waandaaji na wasimamizi wa Yamle Yamle Cup kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuandaa mashindano hayo kwa weledi na mafanikio. Aliwashukuru kwa kuanzisha na kuendeleza mpango wenye maono mapana unaochangia kukuza vipaji vya vijana, kuimarisha mshik**ano wa jamii na kuitangaza Zanzibar pamoja na Tanzania kwa ujumla kupitia michezo. Alisisitiza kuwa jitihada k**a hizi zinastahili kuungwa mkono na wadau wote kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

29/05/2026

Ijumaa Mubarak.

Photos from Mbunge LAKI's post 28/05/2026

Furaha, upendo, umoja na amani hujengwa pale tunapovitekeleza kwa vitendo. Mimi, M. Mohamed Laki, Mbunge wa Jimbo la Kwahani, nimeungana na wananchi wa jimbo langu pamoja na viongozi wa shehia na wadi mbalimbali kutembea mguu kwa mguu kuwajulia hali wananchi pamoja na kuwapatia watoto zawadi na mkono wa Eid katika kusherehekea Sikukuu ya Eid Al-Adha.

Hatua hii inatokana na mapenzi yangu ya dhati kwa wananchi wa Jimbo la Kwahani, kuwa karibu nao, kusikiliza changamoto zao na kushirikiana kuzitafutia ufumbuzi kwa pamoja. Hakika furaha kubwa ni kuona watoto, ambao ndio kizazi cha taifa la kesho, wakifurahia sikukuu hii muhimu wakiwa na tabasamu na matumaini mema.

Nawatakia wananchi wote wa Jimbo la Kwahani na Waislamu kwa ujumla Eid Al-Adha njema yenye amani, mshik**ano, upendo na baraka tele.

27/05/2026

Mh. Mohamed Laki ambae ni mbunge wa jimbo la Kwahani, akifanya ziara katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Kwahani kwa lengo la kujionea hali ya wananchi pamoja na kuwapatia watoto sadaka ya sikukuu ya Eid al-Adha katika kila kona ya jimbo.

Katika ziara hiyo, Mh. Mohamed Laki huyo aliwasisitiza wazee na walezi kuendelea kuwalinda, kuwalea katika maadili mema na kuwajali watoto kwani wao ndio taifa la kesho na msingi wa maendeleo ya jamii.

Aidha, anawatakia wananchi wote kwa ujumla sikukuu njema ya Eid Hajj yenye amani, upendo na mshik**ano.

26/05/2026

Mbunge wa Jimbo la Kwahani Mh. Mohamed Laki, anawatakia Eid Al Adha njema, yenye furaha, amani na baraka tele kwa wananchi wote.

Mwenyezi Mungu azidi kuwaletea afya, upendo na mafanikio katika maisha yenu.

Eid Mubarak!

26/05/2026

Mh. Mohamed Laki ambae ni mbunge wa jimbo la Kwahani, akiendelea kuonesha mshik**ano na kujali wananchi wake kwa kukabidhi sadaka ya sikukuu ya Eid al-Adha kwa viongozi wa Jimbo la Kwahani ikiwemo wadi, matawi pamoja na jumuiya za chama, mara baada ya kufanya mazungumzo yaliyolenga kuimarisha umoja, ushirikiano na kuendeleza utamaduni wa kusaidiana katika jamii.

Aidha, hafla hiyo imeonesha dhamira yake ya ubunge katika kuwatumikia wananchi wake na kushiriki nao katika nyakati muhimu za kidini na kijamii.

Photos from Mbunge LAKI's post 25/05/2026

Tuwatunze na kuwawezesha vijana wetu, kwani wao ndio wabeba kesho yetu na msingi wa taifa la leo na la baadaye.

Hakika vijana ndio nguvu, matumaini na mategemeo katika kujenga jamii yenye maendeleo na taifa imara.

Nikiwa Mbunge wa Jimbo la Kwahani, nitaendelea kudumisha, kuenzi na kusimamia nguvu na mchango wa vijana kwa kuwawekea mazingira bora ya kukuza vipaji, elimu na fursa mbalimbali, ili waweze kufanikisha ndoto na malengo yao kwa manufaa ya taifa letu.

22/05/2026

Nawatakia wananchi wangu wote wa Jimbo la Kwahani pamoja na waumini wote Ijumaa Mubarak yenye kheri, baraka na amani.

21/05/2026

Mbunge wa Jimbo la Kwahani na Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Elimu, Habari, Utamaduni na Michezo, Mh. Mohamed Laki, akiwa pamoja na wabunge wenzake wa k**ati hiyo walipokutana na nyota wa zamani wa soka wa Uingereza, Rio Ferdinand, jijini Dodoma.

Rio Ferdinand, ambaye aliwahi kung’ara katika klabu ya mashetani wekundu Manchester United pamoja na timu ya taifa ya Uingereza, alishiriki mazungumzo yaliyojikita katika maendeleo ya michezo, hususan soka, na nafasi yake katika kukuza vipaji na kuwajengea vijana fursa za maendeleo nchini.

Aidha, mkutano huo uliibua hamasa na mtazamo mpya kuhusu mchango wa michezo katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

16/05/2026

Mh. Mohamed Laki ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kwahani, ampongeza Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa kutimiza ahadi yake kwa vijana, aliahidi wakati wa kampeni na sasa ametenda kwa vitendo, jambo linalodhihirisha kuwa ni kiongozi mtekelezaji mwenye uongozi unaoacha alama.

Hatua hiyo imeleta faraja na matumaini makubwa kwa vijana, huku ikionesha dhamira ya kweli ya Dk. Mwinyi katika kutekeleza yale aliyowaahidi wananchi wakati wa kampeni.

Hakika huu ni uongozi unaowacha alama.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Zanzibar?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Address

KWAHANI
Zanzibar
255