Natural beauty and health.

Natural beauty and health.

Share

Hii ni page nimeianzisha ili kushare kwa wenzengu ujuzi wa uzuri na afya kwa kutumia vitu vya asili

08/07/2021

Hello..........

16/08/2020

AINA ZA NGOZI.
Kuna Aina nyingi za ngozi ila aina zote hizo zipo chini ya aina hizi zifuatazo.

1. NGOZI YA KAWAIDA (NORMAL SKIN)
Ni ngozi ambayo wachache wanayo, sio kwasababu haiwezekani kuwa nayo ila kujua matunzo yake. Si ya mafuta wala si kavu. Inavutika, haina mikunyo(inategemea na umri), haina matundu makubwa, nyororo, haina vipele wala chunusi. Hujulikana kwa jina lengine k**a ngozi yenye afya.(Healthy skin).

2. NGOZI YA MAFUTA (OILY SKIN)
Ni ngozi ambayo inamafuta zaidi ya mafuta yanayohitajika kwenye ngozi. Haiachi kutoa jasho, inamatundu makubwa, chunusi haziishi, inag'aa mafuta, ngozi inaonekana nene na si nyororo. Japo kunautofauti wa uwepo wa mafuta kwenye ngozi ila hizo juu ni dalili zinazoonyesha unangozi ya mafuta.

3. NGOZI KAVU (DRY SKIN)
Ni aina ya ngozi ambayo haivutiki, ina harara, kavu, rahisi kuumia, inawasha, inamichirizi, na rangi ya ngozi pia haivutii. K**a ilivyo ngozi ya mafuta pia inamatundu makubwa na pia kuna utofauti wa ukavu wa ngozi.

4. NGOZI MCHANGANYIKO (COMBINATION/INTERMEDIATE SKIN)
Hii ni ngozi ambayo sehemu kavu, sehemu inamafuta. Watu wengi wana aina hii ya ngozi ila hatujui. Wengine wanaona sehemu zilizokua kavu wakasema ngozi zao ni kavu, na wengine wanaona sehemu zenye mafuta wakasema ngozi zao za mafuta.
Pia ni aina ya ngozi ambayo utunzaji wake ni mgumu kidogo ila inawezekana.

5. NGOZI NYETI (SENSITIVE SKIN)
Ngozi hii ni kinyume na ngozi ya kawaida. Ngozi hii inadalili zote za kavu na ya mafuta. Ukiongeza kuungua rahisi na jua na kuvimba. Jina lengine inaitwa Allergic skin. Ngozi hii k**a ngozi mchanganyiko pia inahitaji matunzo makubwa kwasababu si ngozi yenye afya. Ni ngozi ambayo ni sensitive kwa vitu vingi hasa harufu.

Hizo juu ni aina za ngozi na tabia zake. Sasa unajuaje ngozi yako ni aina gani? Au unahakikishaje? Wapo wanaojua na wapo wasiojua aina za ngozi zao. Kwa kujua au kuhakikisha unaweza fanya hivi;
1. Osha mwili wako k**a kawaida, au kiungo cha mwili unachotaka kujua.
2. Jifute.
3. Usipake chochote kwa muda wa dakika 15-20.
4. Chukua tissue au kitambaa laini jifute taratibu usijikwaruze.

MATOKEO.

1.K**a hutahisi mabadiliko yoyote na tissue au kitambaa kikawa hakina kitu baada ya kujifuta basi unangozi ya kawaida.

2. K**a utahisi ngozi inakaza au inawamba au kavu, inamistari, au harara basi ngozi hiyo ni kavu.

3. K**a unatokwa na jasho, ngozi inang'aa mafuta, na tissue yako ikawa na mafuta basi unangozi ya mafuta.

4. Na k**a ukahisi kunasehemu zengine kavu na zengine zinamafuta au tisuue ikawa na mafuta sehemu moja na nyengine ukapangusa ikawa haina hiyo ni ngozi mchanganyiko.

N. B
-Ngozi nyeti(sensitive skin) hujulikana bila ya kujaribu haya yote.
-Na ukiwa unatumia tissue basi hakikisha unatumia tofauti kila sehemu. K**a ni usoni basi tissue moja kwenye paji, nyengine mashavuni, nyengine kidevuni na nyengine puani. Kwasababu kutumia moja hutajua k**a ngozi yako ni mchanganyiko. Na hapo ndipo wengi tunakosa kujua aina ya ngozi zetu.

POST IJAYO ITAKUWA UTUNZAJI WA KILA AINA YA NGOZI.
USISITE KUULIZA SWALI LOLOTE. NIPO KWA AJILI YAKO...

USISAHAU KULIKE, COMMENT NA KUSHARE K**A WEWE ULIVYOPATA ELIMU HII BASI MI VIZURI KUWAPA NA WENGINE.

22/05/2020

Habari zenu natumai kila mmoja ni mzima.

Naandaa Mada ya suala la ngozi, wiki ijayo Nitatuma post inayohusiana na Aina mbali mbali za ngozi, jinsi ya kuitunza ili kuepuka mgonjwa mbali mbali. Na pia ntaelezea jinsi ya kujua ngozi yako ni aina gani.

Nawatakia afya njema mpaka wakati ujao. Usisahau kufollow ili uweze kupata kila post ntakayo tuma, usisahau kulike na comment. Na k**a unaswali pia uliza nipo kwa ajili yako.

25/04/2020

Umuhimu wa maji mwilini.

1. Maji yanalainisha viungo vya mwili.
2. Yanasaidia kutengeneza mate (ambayo ni muhimu sana katika mwili. Yanameng'enya Aina ya chakula (Starch), yanalainisha chakula kilichopo mdomoni kurahisisha kutafuna na kumeza, Yanasaidia mdomo kutokuwa mkavu)
3. Maji pia yanasaidia kueneza Oxygen mwilini.
4. Maji yanalinda ubongo, uti wa mgongo na sehemu zengine za mwili.
5. Maji yanasimamia joto la mwili.
6. Maji yanasaidia mfumo wa kumenge'enya chakula.
7. Maji yanatoa uchafu mwilini. (mfano mikojo, jasho hata Choo kikubwa ambacho kiafya kinatakiwa kiwe cha kiasi fulani ya maji na kukosekana kwake husababisha Choo kigumu)
8. Yanasaidia kuweka sawa blood pressure.
9. Maji pia yanasaidia mwili kuweza kuchukua virutubisho.
10. Maji yanasaidia kuepuka na kuponesha magonjwa ya Figo na ini.
11. Yanasaidia wakati wa mazoezi.
12. Yanasaidia pia kupunguza mwili.
13. Yanaipa ngozi afya na uzuri.
14. Yanasaidia kumpa mtu mood nzuri. (hupunguza uchovu, maumivu, hasira, huzuni na mengineyo hata njaa sometimes 😉)

19/04/2020

Hivi unajua? Kunywa maji kwa wingi ni moja kati ya dawa na kinga dhidi ya mgonjwa mbali mbali. Kunywa maji mengi, utapata ahueni ya unachoumwa, utajikinga na mgonjwa mwengine pia utafanya mwili unawirike.

Nitatuma umuhimu wa maji mwilini.

Unatatizo lolote la mwili usisite kunitafuta. Nipo kwa ajili yako.

Please like, comment and share.....

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Muscat?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Musannah
Muscat