mjukuu_wa_mfalmetz
single
Pamoja na ubovu tuliyokuwa nao ila huyu refa ana uyanga sana ...hilo halikwepeki na angalia mechi zote za muhimu lazima uto wambebe.mechi za Azam na yanga ,mechi za Simba na yanga na mechi yoyote ngumu uto watashinda hata k**a wamezidiwa siku hiyo ilimradi arajiga yupo
Kwani hamkuona jinsi Azam wakivyonyongwa juzi Zanzibar fainali ya FA?
Anachofanya arajiga ukichezewa faulu anajifanya anatumia busana hakupi faulu na akikupa faulu hatatoa kadi na wakati mwingine ukifanyiwa faulu atajifanya hajaona......ila sasa mfanyie uto ndio utamjua arajiga ni nani.uto atapewa Kila kitu na ukicheza hata penalty apewe
Mara ngapi mechi za Simba na yanga mchezaji wa Simba anafanyiwa rafu ndani ya boksi na hakuna penalty ?
Alichotakiwa afanye arajiga ni kumpa diara red alafu atoe faulu kwa Simba.....sasa alichofanya arajiga ni kuwapa Simba faulu tu ya kawaida na diara akaendelea kudunda uwanjani
Mfano halisi mechi tuyofungwa Tano na uto......angalia faulu aliyofanyiwa kibu na diara .......kwanza diara hakugusa mpira na alikuwa mtu wa mwisho.
Madhara kwa Simba mchezaji muhimu ameumizwa kwa makusudi kabisa na refa yupo anaangalia .......kuanzia hapo kibu alivyotoka ndio Tano zilipoanza kujitengeneza..... Kibu ndio alikuwa anawafanya uto wasipande na wakioanda walikuwa wanapanda kwa uogoa.
Sasa hapo utasema arajiga Yuko sawa?
Kwani hukuona Ile faulu aliyowapa penalty uto yanga wakafunga goli la Tano k**a ilikuwa ya kawaida sana?unafikiri ingekuwa mchezaji wa Simba angepewa penalty
Sawa uto mwaka Jana walikuwa vizuri ndio ila arajiga aliwasaidia sana kwenye mechi muhimu
Mechi ya nusu fainal ya fa ihefu na yanga uliiona?
Kwani hujui kuwa arajiga ndio ametoka kwenye adhabu ya kufungiwa? Inamaana alipendelea timu sio?
Kwenye ukweli tuseme ingawa pia na timu yetu haikuwa vizuri ila na arajiga ana misimu mitatu hivi uto wanamtumia......mechi hata iwe ngumu kiasi gani nikishamuona arajiga Yuko kati lazima uto ashinde
Arajiga ni wakupinga kabisa.....hafai kabisa....achezeshe mechi zingine lakini mechi zinazomuhusu Simba Yanga na Azam asipewe
Utaratbu ufatwe2 kuandikwe barua ykumkataa refa
Simba SC Tanzania Shadrack Simbeye Simba Sc Umoja Wetu Ahmed Ally
Naamka nitafute waliokosa uteuzi na waliotenguliwa
18/07/2024
Fahamu kuhusu Dikteta Pierre Buyoya wa Burundi 🇧🇮
*************************************************************
Pierre Buyoya alikuwa ni Rais wa Burundi 🇧🇮, moja ya madikteta hatari kuwahi kutokea Barani Ukimani…
Aliiongoza nchi hiyo kwa mkono wa chuma, mara mbili, kuanzia mwaka 1987 hadi 1993, kisha tena 1996 hadi 2003…
Hakuwahi kupigiwa kura… Kila alipokuwa akiingia madarakani, alikuwa anapindua tu…
Mwaka 1987 alimpindua Rais Jean-Baptiste Bagaza na kujaribu kurejesha umoja wa kitaifa, kati ya Wahutu walio wengi (85%) na Watutsi wachache (10%)…
Mwaka 1993 Rais Buyoya akaandaa uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia nchini Burundi 🇧🇮, uchaguzi ambao alipoteza baada ya kuzidiwa kura na Rais Melchior Ndadaye (Mhutu), Rais wa kwanza wa Burundi 🇧🇮 kuchaguliwa katika misingi ya kidemokrasia…
Rais Buyoya akamkabidhi funguo za Ikulu mrithi wake, lakini ki shingo upande…
Miezi mitatu tu baada ya Rais Melchior Ndadaye kuingia madarakani, Oktoba 21, 1993, Pierre Buyoya na kundi la wanajeshi kutoka kabila lake la Watutsi, wakaivamia Ikulu na kumfyeka Rais Ndadaye pamoja na mawaziri wake sita…
Waziri Mkuu Sylvie Kinigi aliyenusurika, akakimbilia Ubalozi wa Ufaransa jijini Bujumbura alipopewa hifadhi…
Buyoya na kikundi chake, hawakufanikiwa kuipindua nchi, maana hawakupata ushirikiano kutoka kwa wanajeshi Wahutu (walio wengi), kabila la Rais aliyeuawa…
Kwa mujibu wa Katiba ya Burundi 🇧🇮, Rais akifariki, anayechukua madaraka ni Spika wa Bunge… Bahati mbaya sasa, Spika naye alifyekwa katika jaribio hilo la mapinduzi…
Ikabidi sasa Bi. Sylvie Kinigi (Waziri Mkuu kutoka kabila la Watutsi) aweze kukaimu nafasi ya Urais na kuwa miongoni mwa wanawake wa kwanza marais, Barani Ukimani…
Miezi mitatu baadae, wakati moto mkali ukiwa umewaka Burundi, February 1994, Bunge likamteua Cyprien Ntaryamira (Mhutu) kuwa Rais mpya…
Huyu jamaa akapambana sasa kuzima huo moto kati ya Wahutu na Watutsi, lakini miezi miwili tu baada ya kuingia Ikulu, naye akafyekwa katika ile ajali ya ndege iliyomuua pia Rais wa Rwanda 🇷🇼, Juvenal Habyarimana… (Hii story nishawahi kuisimulia humu)…
Baada ya Rais Ntaryamira kufariki, Sylvestre Ntibatunganya akaingia Ikulu ya Burundi 🇧🇮 na kuiongoza nchi kwa muda wa miaka miwili tu…
Mwaka 1996, Pierre Buyoya akafanya «come back» yaani akarudi tena madarakani kwa njia ile ile (mapinduzi), baada ya kumpindua Rais Ntibatunganya…
Jamaa (Buyoya) akaiongoza nchi hadi mwaka 2003, baadae akatimkia nchini Mali 🇲🇱 ambapo alikuwa mwakilishi maalum wa Umoja wa Afrika…
Lakini jinai haiozi buana…
Miaka mingi baadae (2019), Burundi 🇧🇮 ikiwa inaongozwa na Rais Pierre Nkurunzinza, Pierre Buyoya akiwa nchini Mali 🇲🇱, mahak**a kuu nchini Burundi ikamuhukumu kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mrithi wake, Melchior Ndadaye, Oktoba 1993…
Tafsiri ya hukumu hiyo ni kwamba, jamaa hawezi tena kurudi nyumbani Burundi 🇧🇮…
Basi akaendelea na maisha yake huko Mali 🇲🇱 na kula bata Ufaransa 🇫🇷 ambapo umauti ukamkuta December 2020, baada ya kufyekwa na corona 🦠😷
Mwili wake ukazikwa Mali 🇲🇱 huku mazishi yake yakihudhuriwa na watu wachache sana…
Baada ya Rais Pierre Nkurunzinza naye kufyekwa na corona, kijana wa Rais Pierre Buyoya (Olivier Buyoya), akaomba kukutana na Rais mpya, Évariste Ndayishimiye, na kumuomba mabaki ya babake yaletwe nyumbani Burundi 🇧🇮 na kuzikwa upya…
Ombi ambalo Rais Ndayishimiye alilikubali, na juzi, Julai 16, 2024, mabaki ya Rais wa zamani wa Burundi Meja Pierre Buyoya yalirejeshwa Burundi 🇧🇮 katika nchi aliyozaliwa, miaka minne baada ya kufariki Dunia nchini Ufaransa 🇫🇷 na kuzikwa Mali 🇲🇱...
Hakuna kiongozi yeyote serikalini aliyekuwepo uwanja wa ndege wa Bujumbura kupokea mabaki hayo na yalizikwa jana, kimya kimya, kijijini kwake…
Na huo ndio mwisho wa Dikteta uchwara Pierre Buyoya, aliyeliongoza taifa la Burundi 🇧🇮 mithili ya Kambare wa Tanzania 🇹🇿…
18/07/2024
Wanaume Karibu
18/02/2024
Tujitahidi kuenziwa na kukumbukwa kwa mema
18/02/2024
Hii siku baada ya Kuchinja Jina la Edward Ngoyai Lowassa pale Dodoma tulijua game imeisha na tumeshinda vita.
Watu wa Kidugalo-Diguzi na Mindukene-Lugoba,Mindutulieni,,Miono,Ubena zomozi tulishangilia sana na Ankoli wetu.
Si unajua tena Mjomba ni Mama,furaha ya mjomba ni furaha yetu,na huzuni ya mjomba ni huzuni yetu.
Basi Ankoli aliposhangilia na sisi huku Vijijini Ngerengere, Dutumi,Dakawa,Kinole,Kiroka,Mbuyuni tulishangilia balaaaaa.
Ila kwa ile hali ya Jana pale NGARASH-MONDULI Kuna haja sasa tukae chini na mjomba tujipange upya, Hali siyo shwari.
Tulishinda pambano,hatukushinda Vita.
Vita bado mbichi sana hii,Sisi watu wa Diguzi tunasimama na Ankoli
Kidugalo,Diguzi
Morogoro kwa Mzee Kobelo.
17/01/2024
Kutoka kwa Wazee
08/01/2024
The killer of utoporo😂😂
Distance from Arusha to Dodoma Distance between Arusha and Dodoma is 329 kilometers (204 miles) in Tanzania. Also calculate the driving distance and how far is it the travel time.
15/08/2023
Hatariiii
13/08/2023
Mabingwa wapya wa Ngao ya Jamii
06/08/2023
Unyama ni mwingi
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Arusha