GA healthy products

GA healthy products

Share

I consult people about good health&lifestyle,also provide food supplements to people who have challen

04/03/2024

Namtukuza Mungu ananiwezesha kuhudumia watu wake na wanapata matokeo chanya

Kwa wale wenye changamoto ya kiafya,usisite kuwsiliana nasi kwa;
Kupiga simu/sms/WhatsApp:
+255 743 222 617/+255 657 123 899
Email address:[email protected]

02/03/2024

Namtukuza sana Mungu wa mbinguni kwa jinsi anayoonekana kwa watu anaonikutanisha nao katika huduma hii ya tiba🙏🏽🙏🏽🙏🏽

11/11/2023

FAIDA ZA MMEA WA MWANI
(SEA MOSS)

Mwani ni mmea wa asili unaopatikana baharini;kwa kingereza inaitwa seamoss.

Mmea huu una virutubisho zaidi 90% vijavyohitajika katika mwili wa mwanadamu.

Upekee wa mmea huu wa mwani,unatumiwa na mtu yeyote na rika lolote, mmea huu ni chakula dawa (lishe).

Mwani ni mmea ambao hauhitaji kemikali yeyote kuanzia kuota kwake mpaka kuvunwa kwake pia uhifadhi wake.

Mmea huu wa mwani ni tofauti sana na mazao mengine mengi, ni moja ya chakula au lishe bora na salama zaidi kiafya.

Mbali na mmea huu kutumika k**a chakula,hutumika pia k**a malighafi za kutengeneza bidhaa mbalimbali za kutunza afya ya ngozi na nywele.
Mbali na kusheheni virutubisho, vyakula vyenye asili ya majini(kwenye maji) vina dawalishe ambazo husaidia mwili kupambana na vimelea vinavyosababisha magonjwa k**a vile virusi na bakteria wa aina mbalimbali.

Madini mbalimbali yanayopatikana katika mmea wa mwani;
• Madini joto.
• Madini chuma.
• Calcium.
• Magnesium.
• Copper.
• Zinc.

Aina mbalimbali za vitamini ambazo zinapatikana katika mmea wa mwani ni pamoja na; Vitamin A, B-12, C, D, E na k.

Mmea huu pia hutupatia mafuta mazuri ya Omega-3, ambayo ni mazuri kwa afya na utendaji wa moyo, ini na ubongo.

Mmea huu mbali na kusheheni virutubisho, pia una nyuzi nyuzi ambazo ni lishe muhimu kwa ajili ya utendaji mzuri wa mfumo wa mmeng'enyo wa chakula(Digestion system).

FAIDA ZA MWANI
• Huimarisha kinga ya mwili.
• Huongeza nguvu za mwili.
• Huimarisha afya ya akili na kuipa akili utulivu na kurejesha kumbukumbu.
• Mwani ni mzuri kwa afya ya mifupa, Macho na ini.
• Mwani unasaidia kupunguza au kuzuia uvimbe na maumivu katika mwili.(Uvimbe wa tezi ya shingo Goiter )
• Hupunguza unene
• Huboresha afya ya ngozi na kutibu magonjwa ya ngozi.
• Husaidia kukuza nywele na afya ya nywele kwa ujmla.
• Huboresha mmengenyo wa chakula(Digestion system).
• Mwani unaboresha afya ya mapafu (shida ya kupumua au upungufu wa pumzi).
• Husafisha mapafu kwa wavuta sigara na wanaofanya kazi kwenye maeneo yanayoathiri mapafu.
• Ni tiba ya kikohozi kisichoisha,mafua sugu na Tonsillitis.
• Huboresha afya ya uzazi kwa jinsia zote
• Huboresha tendo la ndoa
• Husaidia kupata usingizi
• Hupunguza maumivu ya hedhi
• Husaidia kudhibiti homoni zinazochochea saratani.
• Husaidia kuchoma mafuta mabaya mwilini(cholesterol)
• Hupunguza kasi ya kupata magonjwa ya moyo, kisukari, kansa, kiarusi na kuboresha afya ya moyo.
• Hutibu matatizo ya tumbo kujaa gesi.
• Husaidia ukuaji wa watoto
• Husaidia kuondoa ganzi mwilini.
• Husaidia kuweka Sawa homoni.
• Huboresha afya ya mama mjamzito na mtoto
• Hupunguza sumu mwilini
• Husafisha utumbo.ni nzuri kwa afya ya tumbo. (Gut health)
faida ni nyingi sana zinazopatikana katika mmea huu wa mwani(sea moss)

Anza kutumia mmea huu ili kuweka sawa mfumo wa mwili wako na kuimarisha afya yako.

Mmea huu unapatikana katika ujazo tofauti na mtindo tofauti;
• Capsules.
• Tablet.
• Powder/unga.
• Oil/mafuta.
• Sabuni n.k.

Gharama za mmea huu ni nafuu zaidi ukilinganisha na umuhimu wake katika mwili wa mwanadamu.

Bei yetu inaanzia 15,000/= na kuendelea, hii hutokana na ujazo na aina mmea huo ulivyoandaliwa.

Kwa maswali, huduma na ushauri wasilian nasi kwa;
Ga healthy and beauty solution
Piga simu/sms/WhatsApp
+255 743 222 617/+255 657 123 899
Email:[email protected]
Dar es salaam -Tanzania

24/10/2023

UGONJWA WA TEZI DUME

TEZI DUME NI NINI?
   Tezi dume ni tezi inayopatikana kwa jinsia ya kiume,tezi hii ina kazi ya kutengezeza  majimaji meupe mepesi yenye unato kidogo ambayo husaidia mbegu za kiume kutembea kwa urahisi.

  Tezi dume iko mwishoni mwa kibofu cha mkojo pia inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na mrija wa mkojo  wa uume (urethra) na iko mbele kidogo ya utumbo mpana ndani ya fupa la nyonga.

NINI MAANA YA SARATANI YA TEZI DUME

   Saratani ya tezi dume ni hali ya chembechembe hai za tezi kuasi na kuanza kujigawanya bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili, chembechembe hizi hutengeneza vivimbe hatari ndani ya tezi dume na hatimaye husambaa mwilini.

SABABU YA TEZI DUME KUWA KUBWA?
Sababu halisi ya tezi dume kuongezeka ukubwa haijajulikana bado,lakini, Kuna mambo kadhaa yanayohusishwa na ukuaji wa tezi hii.
• Umri mkubwa/uzee.
• Kuondolewa kwa korodani kutokana na changamoto mbalimbali za kiafya.

Watu walio katika hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume ni pamoja na:
• Wanaume wenye asili ya Afrika (weusi) ikilinganishwa na wazungu.
• Wanaume kuanzia miaka 45 na kuendelea.
• Wanaume wenye historia ya tatizo hili kwenye familia zao, yaani wale ambao mmoja wa ndugu zake ;kaka/mdogo wa kiume au baba amewahi kuugua ugonjwa huu.
• Wanaume wanaokunywa pombe kupita kiasi.
• Wanaofanya kazi kwenye viwanda vya kutengeneza rangi au wanaofanya kazi ya kupaka rangi.
• Wakulima wanaotumia aina fulani ya mbolea za kemikali.
• Wanaofanya kazi katika viwanda vya utengenezaji matairi.
• Wachimbaji wa madini hususani aina ya cadmium.
• Walaji wa chakula chenye kiasi kikubwa cha mafuta hasa ya wanyama.

    Pamoja na kwamba, tatizo la kukua na kuongezeka kwa tezi dume yaani BPH hutokea kwa wanaume wengi, hali hiyo haiongezi uwezekano/hatari ya kupata saratani ya tezi dume.

Chanzo Cha Tezi Dume

Chanzo hasa cha saratani ya tezi dume hakijulikani, lakini,saratani hii ina uhusiano mkubwa na mambo yafuatayo;
• Umri mkubwa
• Kurithi(Genetics)
• Lishe hatarishi/duni
•   Ulaji kwa wingi wa nyama nyekundu, mafuta (samli), maziwa ya krimu hongeza hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume.
• Unene uliokithiri (Obesity).
• Kutokufanya mazoezi.

21/10/2023

VYANZO VYA SUMU MWILINI

Miili yetu imekuwa ikipokea sumu na uchafu kila siku kutokana na;
• Matumizi ya dawa mara kwa mara.
• Matumizi ya vilevi.
• Mazingira na athari itokanayo na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
• Ukosekanaji wa lishe na mlo kamili.
• Matumizi ya mbolea za kisasa/dawa za kuulia wadudu na  za kukuzia mifugo na mimea/mazao.
• Mitindo mibaya ya maisha(kula bila mpangilio sahihi na kutokufanya mazoezi).
• Njia za uzazi wa mpango za kisasa.

DALILI ZA KUWA SUMU NYINGI MWILINI

• Matatizo ya ngozi k**a chunusi, vipele ,majipu,miwasho na kutoka jasho lenye harufu kali.
• Kuwa na uzito wa kupindukia.
• Kutopata choo au kupata choo kigumu na tumbo kujaa gesi.
• Kukosa usingizi na kujihisi mchovu kupitiliza.
• Kichwa kuuma kila mara.
• Maumivu ya viungo(magoti,nyonga,mgongo n.k)
• Kuwa na hasira mara kwa mara. N.k

MADHARA YA MWILI KUJAA SUMU

• Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
• Maambukizi katika figo na ini.
• Kutokupata watoto (ugumba)
• Vimbe ndani ya kizazi kwa wanawake.
• Shinikizo la damu la juu (high blood pressure)
• Mvurugiko wa homoni(hormone imbalances)
• Vimbe mbalimbali mwilini.

      Weka ratiba na taratibu sahihi ya kuongoza mtindo wako wa maisha ya kila siku...

Tunayo tiba asilia ambayo itaondoa sumu mwilini kwa muda mfupi na kuondoa kabisa madhara ambayo yamesababishwa na uwepo wa sumu mwilini

Kwa ushauri na tiba ,wasiliana nasi kwa;
Ga healthy and beauty solution
Piga simu/WhatsApp/sms
+255 743 222 617 /+255 657 123 899
Email:[email protected]

21/10/2023

Mwanaume kuwa na matiti K**a mwanamke(GYNECOMASTIA)

Tatizo hili linazidi kuongeza siku hata siku kwa wanaume na kupelekea hali ya kutokujiamini na kuongeza idadi kubwa ya wanaume wanao fanya mazoezi ili kutunisha vifua vyao(kutengeneza six-pack)

Kuongezeka kwa ukubwa wa matiti kwa wanaume, husababishwa na  kiwango kikubwa cha homoni ya Estrogen ambayo ni homoni ya k**e na Kuwa na upungufu wa homoni ya Testosterone ambayo ni homoni ya kiume.

Wanaume wote wana homoni za kiume na homoni za k**e kwa kiwango fulani.

Homoni za kiume Testosterone husababisha mtu kuwa na tabia/haiba za kiume k**a vile ;
• Kuota nywele mwilini.
• Ukubwa wa misuli.
• Kuwa na sauti nzito.
Homoni ya k**e ya Estrogen husababisha tabia za k**e.
• Kuota matiti.
• Sauti nyororo n.k

Mabadiliko ya kiwango cha homoni hizi au mabadiliko ya namna mwili unavyozitumia homoni hizi, kunaweza kupelekea kuota matiti kwa wanaume.

SABABU ZA KUOTA MATITI KWA WANAUME

• Kupungua kwa kiwango cha homoni ya Testosterone (homoni ya kiume).
• Mtumizi ya dawa aina ya steroids kwa wajenga misuli, (wanaofanya mazoezi gym).
• Matumizi ya dawa zenye homoni ya Estrogen (homoni ya k**e).
• Ulaji wa vyakula vya kukaangwa( chips na vyakula vyenye calories nyingi mwilini).
• Sababu za Kurithi (genetics).

KINGA NA TIBA
• Achana na tabia za kutumia madawa bila ushauri wa kitaalamu.
• Anza kula mlo sahihi na kupunguza vyakula vya mafuta,sukari n.k(vinono)
• Fanya mazoezi salama(usiongeze dawa yoyote ili kutengeneza umbo lako)

Bado tumaini lipo,tatizo hili la uwiano wa homoni kwa wanaume linatibika na kukuacha mwanaume ukiwa na muonekano thabiti wa kiume(haiba ya kiume)

Tiba asilia/tiba lishe ndio jibu lako ,kwani tiba hizi zina uwezo wa kupambana na chanzo cha tatizo na kuongeza uzalishaji wa homoni zinazotakikana kwa mwanaume na kukurejesha katika haiba ya kiume.

Kwa ushauri na tiba,wasiliana nasi kwa;
Kupiga simu/sms/WhatsApp
+255 743 222 617/+255 657 123 899
Email:[email protected]

21/10/2023

TATIZO LA KUZIDI KWA KIWAGO CHA ACID TUMBONI
(ACID REFLUX-GERD)

Gastroesophageal reflux disease (GERD).
Ni hali inayotokana na kuzid kwa kiwango cha Acid tumboni (Hydrochloric Acid) ambapo hupelekea kupanda kwa acid kutoka tumboni kuelekea katika koo la Chakula (Oesophagus) na kupelekea kudhurika kwa mfumo wa chakula upande wa juu ambao unahusisha koo la chakula na mdomo pia.

Watu wengi sana wanasumbuliwa na tatizo hili, ilihali wao hawajui k**a wanasumbuliwa na tatizo hili, wengine huenda mbali katika hisia zao na kuhusisha tatizo hili na imani za kishirikina,hii ni kutokana na dalili ya tatizo hili.

DALILI ZA KUZIDI KWA ACID TUMBONI

• Kuwaka moto kifuani(Kiungulia) hasa wakati wa usiku au unapolala,hali hii hutokea pia mara baada ya kula.
• Mapigo ya moyo kwenda mbio/kushtuka kwa moyo baadhi ya nyakati(Hali hii hupelekea baadhi ya watu kuhisi wana matatizo ya moyo.)
• Kuhisi k**a kichwa kimevurugika na kuhusi kuchanganyikiwa.
• Kusahau mara kwa mara hata vitu vya kawaida kabisa/Kupungua kwa kumbukumbu.
• Kujisaidia choo kigumu k**a cha mbuzi.
• Kuwa na wasiwasi na hofu kubwa na hufikia hatua hata ukipigiwa simu hasa nyakati za usiku moyo huanza kwenda mbio sana.
• Kukosa usingizi ama kushtuka mara kwa mara kutoka usingizini.
• Kupumua kwa tabu baadhi ya nyakati.
• Kupata maumivu ya kichwa ya mara kwa mara kwa baadhi ya watu wenye tatizo hili.
• Kupata kikokozi kisichoisha.
• Kuvimba Tonsillitis/mafidofido mara kwa mara.
• Mdomo kuwa mchachu na huweza kupelekea kutoa harufu mbaya ya kinywa.
• Kuhisi k**a kuna kitu kimekwama kooni lakini kila unavyojaribu kukitoa hakitoki.
• Kupata fangasi mdomoni(mdomo huanza kutoa ute mweupe ambao una harufu mbaya).
• Huweza kupelekea kuanza kuota ndoto za kutisha pindi ulalapo na kuhisi umerogwa.
• Kupata maumivu ya mgongo hasa sehemu ya mabega,maumivu makali kana kwamba umenyanyua vitu vizito.
• Mwili kuwa na uchovu usioisha utadhani unafanya kazi ngumu kila siku.
• Macho kupunguza uwezo wa kuona vizuri.
• Kupungua uwezo wa kufanya tendo la ndoa.
• Mwili kupata baridi na wakati mwingine kuhisi homa kabisa.
• Maumivu ya tumbo kati ya kifua na tumbo.
• Kichefuchefu na kutapika.

MAMBO YANAYOWEZA KUSABABISHWA KUZIDI KW

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 07:30 - 18:00
Tuesday 07:30 - 18:00
Wednesday 07:30 - 18:00
Thursday 07:30 - 18:00
Friday 07:30 - 18:00
Saturday 07:30 - 14:00