Mr Sir-zmo

Mr Sir-zmo

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mr Sir-zmo, Health/Beauty, Dar es Salaam.

22/02/2025

Wanaume!

K**a mwanamke anaanza kuwa na tabia ya dharau, kutoa visingizio, kuomba mapumziko, au kuwa mbali bila sababu—kuwa makini. Acha kufikiria sana, acha kuomba msamaha bila sababu, na usikubali kupotoshwa. Wanawake huwa na hisia nyingi, na tabia zao zinapobadilika, mara nyingi kuna sababu. Inawezekana tayari amepoteza umakini, uaminifu, au heshima kwake kwako.

Ukweli ni huu: k**a hujafanya kosa lolote, basi mabadiliko yake hayawezi kuwa juu yako—yanamhusu yeye. Huenda tayari amekusaliti, anafikiria kufanya hivyo, au anamtazama mtu mwingine. Wanawake mara nyingi huonyesha dalili wanapobadilika kihisia, na ishara hizo ziko wazi. Unachohitaji ni kuziona.

Usianze kuuliza, "Kuna shida gani?" au "Nimekosea nini?" Hiyo ni dalili ya udhaifu na haitakusaidia. Unapomwomba maelezo au kumsihi abadilike, unapoteza nguvu zako. Badala yake, tulia, angalia kwa makini, na acha vitendo vyake viongee.

Wanaume, fahamuni hili: mwanamke anayekuheshimu atazungumza na wewe kwa uwazi, hatakuchanganya. K**a anaanza kubadilika, kutoa visingizio, au kuwa mbali, tayari hajali k**a awali. Usikimbizane na mtu anayekutoka—hifadhi heshima yako, simama kwenye msimamo wako, na ondoka inapobidi.

Unastahili uaminifu, heshima, na ukweli. Usijidhalilishe kwa kumbembeleza mtu asiye tayari kukupa hayo. Wewe ni mwanaume—simama imara. Kaa na msimamo.

KUWA WEWE....

22/02/2025

Habar za majukumu kiongozi,
Najua huwezi kunikumbuka, lakini mimi nakukumbuka kwa sababu labda umeniokoa na kuwa single mother. Nilikutafuta mwaka jana mwezi wa kumi nikikwambia kuhusu mwanaume wangu ambaye tulipanga kabisa kuhusu mimi kubeba mimba yake, lakini baada ya kujifungua, niliona k**a alibadilika.

Siku niliyokupigia ndiyo siku nilikuwa nimetoka kumtukana mwanaume kwa kumwambia ni tapeli, hivyo akae mbali na mimi. Nilikupigia nikiwa na hasira sana, lakini ulinisikiliza. Niliongea sana, na mwisho ukaniuliza, "Unajua kwa nini unaachwa?" Nikakwambia ni kwa sababu mwanaume ni mshenzi!

Nakumbuka uliniambia, "Hembu fikiria kipindi uko kwenye mahusiano na huyo mwanaume kabla ya kubeba mimba, jinsi ulivyokuwa. Jinsi mlivyokuwa mnaongea, unampigia simu, jinsi ulivyokuwa mwanamke mstaarabu. Akiwa na stress anakupigia simu, mnaongea hata masaa 3!"

Ukaniambia, "Jiangalie sasa ambapo kila ukimpigia simu unalalamika, unalia, mnagombana. Hivi k**a ni wewe, ukiambiwa uoane na mtu ambaye ana kisirani k**a ulichonacho sasa, utakubali?" Nikajibu, "Ndio, nakubali," lakini ukaniambia, "Hapana. Hembu usijibu hili swali sasa, kaa baada ya siku tatu, nipigie!"

Nilikata simu nikiwa na hasira, lakini baada ya kufikiria siku mbili tu, nilituliza kichwa na kujiona jinsi nilivyokuwa nimebadilika.

Nilivyo na kisirani, niliamua hata nisikutafute. nikakisoma, na nikaamua kuwa na amani. Kaka, huwezi kuamini, wiki mbili nilikaa bila kumtafuta mwanaume huyo, na yeye ndiye aliyekuja kunitafuta na kuniuliza kuhusu ujauzito. Nikamjibu kwa ustaarabu mpaka hakuamini.

Nimekutafuta leo kwa sababu tumerudiana. Ndoa bado, lakini tuna furaha na amani. Mungu akipenda, mwakani tutakamilisha kila kitu. Ila, niliacha kisirani chote siku ile, na nakushukuru sana. Nina furaha

22/02/2025

Habar kaka
Mimi naishi na mwanaume huu ni mwaka wa tatu. Hajawahi kuja kwetu kujitambulisha wala kutaka kunio,familia yangu haimjui. Kila kitu kilikuwa vizuri mpaka wiki tatu zilizopita, ambapo alinifahamisha kuwa anaenda kwao kusalimia kwani mama yake ni mgonjwa kiasi fulan

Baada ya kufika huko, alianza kupuuza simu zangu. Nilipoongea na rafiki yake, alinieleza kuwa ameenda kuoa. Kwa kweli nilichanganyikiwa, nilipanda gari na kuelekea kijijini kwao. Nilipoenda, niligundua kuwa harusi ilikuwa tayari imeshafanyika, na mwanaume alikuwa kwenye fungate na mke wake mpya,nilimiumia sana kaka.

Nilijitambulisha kwa wazazi wake na kuwaambia kuwa mimi ni mchumba wake na tumeishi pamoja k**a mke na mume kwa miaka miwili. Mwanaume alitafutwa na mwanzoni alinikataa, lakini baada ya kuonyesha ushahidi wa picha zetu nikiwa kwake, alikubali kuwa ni kweli tumeishi pamoja. Hata hivyo, alisema kuwa hakuwahi kuniambia anataka kunioa. Alisema alikuwa na mpango wa kunioa, lakini baada ya kukutana na huyo mwanamke mwingine, aliamua kumuoa badala yangu.

Nilipata maumivu makali, lakini sikuruhusu anipotezee muda wangu bure. Nilimwambia sitahama pale tulipokuwa tukiishi. Kweli, hakurudi na akaamua kuishi na huyo mke wake mpya sehemu nyingine. Mwanamke ingawa alijua mimi nipo, hakujali.

Sasa sababu ya kuandika ni kwamba, mwanaume amerudi hapa nilipoishi na kuniomba msamaha. Anasema hajui kilichotokea mpaka akaamua kumuoa huyo mwanamke. Hata hivyo, anakiri kuwa tayari ameshaoa, hivyo hakuna namna ya kubadilisha. Ananiomba tukubaliane tuendelee kuwa wapenzi na aniahidi kuwa atanioa k**a mke wa pili. Anasema hataki kukurupuka, bali anataka kwanza kumshawishi mke wake wa sasa ili akubali.

Nilimuuliza, "Ikiwa mke wake hatakubali, itakuwaje?" Akanijibu kuwa akimbebesha mimba, mke wake atalazimika kukubali kwa sababu hatakuwa na pa kwenda. Kwa kweli nimechanganyikiwa, sijui la kufanya. Nampenda huyo mwanaume, lakini amenipotezea miaka miwili ya maisha yangu. Sasa najiuliza, nifanye nini...

22/02/2025

Pole na majukum kiongoz, mm ni yule mama mwenye umri wa miaka thelethini na mbili niliwahi kuleta Mkasa wangu hapa wa kuachwa na mwanaume aliondoka nyumbani na kuamia kwa mwanamke mwingine akisingizia changamoto kubwa tuliyokwa nayoo kwenye ndoa ya kukosa mtoto kwa miaka Saba Sasa basi jamaa huyo kakaaa huko wee Sasa hivi karudi anaomba misamaha na kuwashilikisha wazee na ndg zake wamwombee msamaha eti aliteleza na mambo kibao nilivyosimamia msimamo wangu wa kwamba simtaki karudi kwa force akisema akisingizia eti sababu mm ni mke wake wa ndoa kwa ufupi nimeshindwa kumsamehe

Sasa Jana narudi kutoka kazini namkuta nyumbani sababu ilikuwa siku yake ya off analia k**a mtoto akisema eti simpendi Tena k**a zamani alilia Sana nikajikuta namwinea huruma Hadi naanza kumbeleleza basi bhana baadae ikabidi nianze kumwogelesha vizuri lakini ukweli ilikuwa ni kinafiki tu sababu kipindi ambacho ameondoka nimejikuta nimeangukia penzini mwa mtu mwingine na kibaya zaidi anajua kuwa nilishaachika na hili linaloendelea mwenzangu mpya simjamshilikisha sababu ya kwanza yupo mbali Bro naomba unifikishie kwa wadau na wanawake wenzangu wanipe mawazo yao na mitazamo yao nione nalitatua vipi hili sababu ushauri wa kwanza niliufanyia kazi wa kumpoteza huyu mtu ambaye anadai ni mme wangu wa ndoa nikampotozea kweli nilifuata huo ushauri naisi ndio jambo linalomtesa

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam