Dotto-Health-Care
SULUHISHO LA CHANGAMOTO ZA UZAZI KWA MWANAMKE. Mawasiano:0758293345
# Ewe mwanamke jifunze zaidi kuhusu maambukizi katika njia ya uzazi( p.i.d)
15/06/2024
⭐U.T.I(MAAMBUKIZI YA NJIA YA MKOJO) (URINARY TRACT INFECTIONS )⭐
🪵U.T.Is, ni kifupisho cha Urinary Tract Infections, ambayo kwa lugha yetu ni mambukizi ya njia ya mkojo. Tunapozungumzia njia ya mkojo, ni kutoka eneo la nje hadi kwenye kibofu, na kutoka kwenye kibofu hadi kwenye figo.K**a maambukizi yako eneo la kutoka kwenye kibofu hadi kwenye figo(ikihusisha na figo pia), inaitwa Lower Urinary Tract Infect. Na ikihusisha eneo la juu ya kibofu, inaitwa Upper Urinary Tract Infection.
🪵Tatizo hili huwapata wote, wanaume na wanawake. Lakini huwapata zaidi wanawake kutokana na tofauti za kimaumbile. Hii ni kwa sababu kuu mbili.
🌿njia ya haja ndogo ya mwanamke iko jirani zaidi na njia ya haja kubwa ambapo vijidudu vingi vinavyosababisha U.T.I ndipo vinapoishi.
🌿mrija wa mkojo (urethra) wa mwanamke ni mfupi ukilinganisha na wa mwanaume, hivyo kufanya iwe rahisi kwa maambukizi kufika kwenye kibofu kwa mwanamke kuliko kwa mwanaume.
🪵Visababishi vya U.T.I
Tatizo hili husababishwa kwa kiasi kikubwa na bacteria ambao makazi yao ya kawaida ni kwenye utumbo mpana, na hivyo huwa wanapatikana pia kwenye haja kubwa, mfano Escherichia coli na wengineo. Pia, linaweza likasababisha na fungus' na visababishi vingine, japo ni mara chache sana.
🪵KWA MWANAMKE.
🌿Kujamiiana hii huweza kuamisha bacteria walio kwenye uume moja kwa moja, ama watokanao na maambukizi ya ukeni kuingia moja kwa moja njia ya mkojo.
🌿Kuchezea ama kuchezewa na mikono michafu maeneo ya uke kunaweza kusababisha maambukizi.
🌿Njia mbaya ya kujisafisha baada ya haja kubwa au ndogo inaweza kuhamisha bacteria walio ktk njia ya haja kubwa na kuingia njia ya mkojo.
🌿Matumizi ya pedi za k**e zenye kemikali ya kukata harufu ambao huua bacteria wa asili wa eneo la uke na kukaribisha bacteria wanaosababisha maradhi kuzaliana kwa wingi
🌿Ujauzito mara nyingi hushusha kinga ya mwili ya mjamzito
🌿Upungufu wa homon ya ya k**e Oestrogen husababisha bacteria wasababishao U.T.I kuzaliana kirahisi
,🪵DALILI ZA U.T.I
⭐Kwa eneo la chini la njia ya mkojo.
🌿 Hali ya kujisikia kutaka kukojoa muda wote.
🌿Maumivu, au hali ya kujisikia kuchoma choma wakati wa kukojoa.
🌿Kukojoa mara kwa mara na mara zote mkojo ni mdogo.
🌿Mkojo unaweza kuonekana una ukungu, na mara nyingine unatoa harufu kali.
🌿Maumivu ya nyonga kwa wanawake.
🌿Na mara nyingine damu kwenye mkojo.
⭐Kwa eneo la juu la njia ya mkojo.
🌿Maumivu ya tumbo(hasa eneo la juu kwa pembeni chini ya mbavu)
🌿Homa kali
🌿Kutetemeka na kujihisi baridi
🌿Kichefuchefu na /au kutapika
🪵Madhara yatokanayo na U.T.I isipopata tiba sahihi.
🌿Inaweza ikasababisha maambukizi makubwa ya figo (pyenephritis) ambayo yanaweza kusababisha uharibifu wa kudumu wa figo na hivyo kutishia maisha.
🌿Kwa wajawazito inaweza kuhatarisha maisha ya wote mama, na motto aliye tumboni.
🌿Bakteria wanaweza kuingia mfumo wa damu na kusababisha ama kwenda kusababisha madhala mengine.
🌿Inaweza kusababisha shinikizo la damu kuwa kubwa kwenye figo na hata kusababisha ufanyaji wa kazi mbovu wa figo.
🪵Njia za Kujikinga na U.T.I
🌿Kunywa maji kwa wingi kila siku. Hii itakusaidia ukojoe mara kwa mara na kutoruhusu bacteria kujenga makazi kwenye njia ya mkojo
🌿Kojoa kila ujisikiapo mkojo na usiubane kwa muda mrefu.
🌿Nenda ukakojoe mara tu umalizapo tendo la kujamiiana. Hii itasaidia kutoruhusu bacteria kuingia na kujenga makazi kwenye njia ya mkojo.
🌿Badili pedi mara kwa mara uwapo hedhini.
🌿Epuka kujisafisha ukeni na maji yarukayo kwa kasi.🌿 Epuka kupulizia marashi ukeni, ama kutumia pedi zenye kemikali ya kukata harufu. Hizo huua bacteria wa asili wa ukeni hali ambayo hukaribisha bacteria wa maradhi kuzaliana kwa wingi
🌿Ujisafishapo baada ya kujisaidia anzia mbele kwenda nyuma kuepusha kuhamisha bacteria walio eneo la haja kubwa kuingia njia ya mkojo
N.B Kwa wale walio katika kipindi cha ukomo wa hedhi, wanaweza kushauliana na daktari juu ya kutumia oestrogen ya ukeni kuwasaidia kujikinga na maambukizi.
Tunatumia dawa za asili zenye tiba lishe na virutubisho kutatua changamoto yako
Nitafute kupitia mawasiliano 0717 226 127
20/04/2023
SABABU ZA MWANAMKE KUPATA UVIMBE KWENYE KIZAZI
Chanzo cha moja kwa moja cha ugonjwa huu bado hakijulikani wazi, hata hivyo baadhi ya sababu za kutokea huu uvimbe ni pamoja na;
1. ❤️🔥Kuongezeka sana vichocheo vya progesterone na estrogen kuzidi kiwango mwilini.
2.🌀 Ujauzito.
3.❤️🔥 Uzito/ unene kupita kiasi.
4.🌀 Jenetiki zisizo za kawaida.
5.❤️🔥 Mfumo usio sawa wa mishipa ya damu.
6.🌀Sababu za kurithi.
7.❤️🔥Lishe isiyo sawa/Lishe duni.
8.🌀Sumu na taka mbalimbali mwilini.
MATIBABU/TIBA ASILI KWA UVIMBE KWENYE KIZAZI.
Tiba asili ndio njia salama na rahisi katika matibabu ya uvimbe kwenye kizazi endapo mgonjwa atafuata ushauri na matumizi sahihihi ya dawa.
Zipo dawa asili zenye ufanisi mkubwa sana katika kutibu uvimbe kwenye kizazi.
Wasiliana nami kwa Ushauri, matibabu na miongozo mbali mbali ya kitabibu: 0717226127.
JE? NINI CHANZO CHA MAUMIVU YA KWENYE NYONGA UPANDE WA MWANAMKE.
Asilimia 60 % ya wanawake wengi hawajapata ufumbuzi juu ya nini kinachopelekea wapate Maumivu makali ya kwenye Nyonga, lakini hivyo ndivyo visababishi vya hayo Maumivu👇👇👇
🌿Maumivu wakati wa hedhi.
🌿P.i.d (mambukizi katika njia ya uzazi wa mwanamke)
🌿 Utoaji wa mimba.
🌿 Fibroids ( uvimbe ambao sio saratani)
🌿 Endometriosis (kutanuka kwa ukuta wa ndani ya mfuko wa mimba).
🌿Ovarian cysts( mkusanyiko wa vimbe ndogondogo zilizojaa maji kwenye mifuko ya mayai ya mwanamke)
K**a unahisi unahayo Maumivu wasiliana nasi Dotto-Health-Care kwa ushauri zaidi wa kiafya kwa kupitia watsup namba 0717226127/0758293345.
DALILI ZA P.I.D (PELVIC INFLAMATION DISEASE).
🌿 Maumivu makali sana wakati wa tendo la ndoa.
🌿Maumivu makali ya kwenye Nyonga na tumbo.
🌿Kupata Maumivu makali sana wakati wa kukojoa au kukojoa mara kwa mara.
🌿Kutokwa na damu nyingi sana wakati wa hedhi.
🌿Kutokwa na uchafu mwingi ukeni(mweupe) unaoambatana na harufu mbaya.
🌿Kuvurugika kwa hedhi.
🌿Miwasho mikali sana sehemu za Siri.
Hizo ndizo dalili za p.i.d hivyo basi ukihisi unadalili hizo tambua fika una mambukizi hayo , usikae na p.i.d mana inaenda kuathiri mfumo mzima wa uzazi na hatimaye kuleta madhara makubwa baadae k**a vile mwanamke kushindwa kubeba ujauzito, na kuwa mgumba au tasa.
Wasiliana nasi kupitia watsup namba 0717 226127/ 0758293345 kwa ushauri zaidi wa kiafya.
18/01/2023
*HORMONAL IMBALANCE*( MVURUGIKO WA HOMONI)
Hormone ni nini👇
Ni chemical zinapatikana kwenye damu, na zinazalishwa kupitia tenzi.Kazi kubwa ya hormone ni kubeba taarifa kutoka kwenye DNA na kupeleka sehemu nyengine za mwili kwa ajili ya kazi maalum.
Hormone imbalance ni 👇👇
Ni kitendo cha kupungua au kuongezeka kwa vichochezi katika mwili wa mwanamke pale anapopata hedhi hivyo mwili kubadilika , na baadhi ya hivyo vichochezi ni 👇
HOMONI ya ESTROGEN kazi yake kubwa ni kusaidia kubalehe kwa mwanamke na pia hufanya uke wa mwanamke ukomae kwajili ya kushiriki tendo la ndoa.
HOMONI YA PROGESTERONE kazi yake ni kusaidia kutunza usalama wa mimba .
Kuna vyanzo vingi sana vya mvurugiko wa HOMONI baadhi yake ni.
,🫒Matumizi ya dawa kiholela .
🫒Uwepo wa sumu mwilini.
🫒Utoaji mimba .
🫒Matumizi ya Tiba ya Kansa k**a mionzi.
🫒Magonjwa ya U.T.I, Fungusi na P.I.D ya mda mrefu
🫒Magonjwa k**a Kisukari na Goita.
Hizo ni moja ya sababu zinazopelekea mvurugiko wa HOMONI.
👉 Dalili za mvurugiko wa hormone*
Moja ya dalili za mvurugiko wa HOMONI ni pamoja na .
🫒Kupungua kwa matamanio ya kufanya s*x
🫒Uke kuwa mkavu.
🫒 Maumivu makali wakati wa tendo la ndoa.
🫒Kuvuruga mzunguko wa mwezi na kutoka mabonge yenye damu wakati wa hedhi.
🫒 Kushindwa kubeba ujauzito
🫒 Maumivu ya kiuno au chini ya kitovu
🫒Kuongezeka uzito.
🫒Kuota nywele na ndevu sehemu mbalimbali za mwili.
👉 Madhara ya mvurugiko wa HOMONI.
🫒U.TI , P.I.D za mara kwa mara.
🫒Ugumba au mimba kuharibika mara kwa mara.
🫒Uvimbe kwenye kizazi (FIBROID) .
🫒Kuwa na tabia ya maumbile ya kiume.
👉Kulingana na changamoto hizo za mvurugiko wa Homoni Dotto-Health-Care clinic Tumewasaidia watu wengi sana kutatua changamoto ya mvurugiko wa Homoni kwa kuwapatia Tiba lishe na virutubisho ambavyo huenda kuweka uwiano wa Homoni, kwa ushauri wa kiafya na Tiba tuwasiliane kupitia watsup namba 0758293345.
05/11/2022
FUNGUSI YA UKENI.
Fungus hutokea ukeni baada ya bacteria mzuri anae itwa lactobacillus kukosa nguvu ya kupambana na Maambukizi,
Na huyo bacteria anapatikana ukeni, hata hivyo uyo bacteria lactobacillus,
huzalisha Lactic acid ( hydrogen peroxide)
Ambayo hu ballance PH kwenye uke.
*Kinacho sababisha Fungus ukeni(Vaginal fungus)*
⛔ Candida albicans,
Huyu ndiye kisababishi kikuu Cha fungus wa ukeni,
*DALILI ZA FUNGUS UKENI*
🔴 Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa
🔴 Uke kuwashaa Sanaa
🔴 Kutoka vipele sehem ya ukeni,
🔴 Kutoa maji maji ukeni
🔴 Kutoa Ute ute wenye harufu ukeni wenye rangi nyeusi au yellow,
*VITU VINAVYO PELEKEA BACTERIA LACTOBACILLUS KUSHINDWA KUPAMBANA NA MAAMBUKIZI*
💠kutumia Mara kwa mara dawa aina ya Antibiotics
💠msongo wa mawazo
💠kuto zingatia mlo kamili hasa wale wanao kula vyakula vyenye sukari Sanaa wapo hatarin,
💠ujauzito
💠kushuka kwa Kinga ya mwili,
💠 ugonjwa wa kisukari,
💠kula vyakula vya sukarii,
💠 Hormonal imbalance,
Hakikisha una tibu tatizo Lako ikiwa Bado halijawa sugu.call 0758293345
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Daresalaam Tanzanian
Dar Es Salaam