Elimika na Kisauti

Elimika na Kisauti

Share

Elimu ya afya na lishe bora kwa mtoto kabla na baada ya kuzaliwa.

25/03/2022

Utapiamlo ni hali inayotokana na kukosa chakula kabisa ama kupata chakula kidogo ambacho virutubisho vyake havitoshi au kupata aina moja ya chakula kwa wingi hadi kusababisha matatizo kiafya.
Utapiamlo hutokea :
1.Kama mtu ana uhaba wa chakula na kuwa na njaa ya kudumu
2.Mtu anapokosa sehemu muhimu ya vyakula mfano protini,vitamini au Minerali
3.Mtu anapokula aina moja ya chakula kwa wingi.
Aina za vyakula vinavyo hitajika mwilini ni Wanga, Protini,Vitamini ,Maji,Fati /mafuta na Madini (Minerali).
Aina za utapiamlo
1.Unyafuzi - husabishwa na ukosefu wa vyakula vya protini tu
2.Nyongea - husababishwa na ukosefu wa vyakula protini na wanga.
3.Kiribatumbo - husababishwa na ulaji wa vyakula vya wanga,mafuta na sukari kwa wingi.

08/03/2022

Kurasa yetu inahusisha elimu ya afya na lishe bora kwa mtoto aliye tumboni na baada ya kuzaliwa.Lengo ni kumkomboa mtoto huyu dhidi ya lishe duni na maradhi ya hapa na pale anayo kumbana nayo kabla na baada ya kuzaliwa.Elimu uliyonayo ni msingi wa kwanza na ulio imara katika uimarishaji wa afya ya mtoto hivyo ukielimika wewe na kuelimisha jamii unakuwa umeikomboa dhidi ya maradhi ya utapiamlo.Harakati za kutokomeza utapiamlo si la watumishi wa afya tu kupambana nalo hata wewe ukiweza ama kuthubutu kumuelimisha mwingine unatengeneza kizazi bora kijacho na jamii iliyoelimika pia.Ungana nami katika vita hii na uwe huru kuchangia kile ulichonacho kuelimishana na kuikomboa jamii yetu dhidi ya utapiamlo.Karibuni sana wapendwa 🙏🙏.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Kibamba
Dar Es Salaam