Mwana wa Nuru ya ulimwengu

Mwana wa Nuru ya ulimwengu

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mwana wa Nuru ya ulimwengu, Beauty, cosmetic & personal care, Dar es Salaam.

19/05/2024

You know, right?

19/05/2024

Dereva wa pikipiki ya Afisa mifugo Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga, Abel Adamson Mwaipopo (25) amefariki Dunia baada kumgonga ndege aina ya bundi na kisha pikipiki yake kupoteza mwelekeo na kuanguka na hatimaye kupoteza maisha yake.

Mkuu wa Wilaya ya Handeni Albert Msando amesema tukio hilo limetokea mapema leo katika eneo la Sindeni jirani na kona ya PRS ambapo Dereva huyo alikuwa akiendesha pikipiki yenye namba za usajili STM 0232 .

Msando amesema “Kwanza naomba nitolee ufafanuzi jambo hili kwani aliyefariki sio Afusa mifugo k**a wengi walivyosema kwani Afisa mifugo wetu wa Wilaya ni Mwanamke na aliyefariki ni Mwanaume Dereva ambaye anamwendesha Afisa mifugo”

“Ajali ni k**a ajali nyingime lakini akishahusishwa bundi mara zote tayari kunakuwa na hizo imani za kishirikina na hofu kwa Watu kwamba amegonga bundi kafa na yeye mwenye amekufa lakini vilele inawezekana kwa kiasi kikubwa labda alivyomuona bundi katika kujaribu kumkwepa hakuchukua tahadhari akapata ajali ni uwezekano vilevile hakuwa amevaa kofia ngumu hivyo katika kuanguka akajigonga akapata madhara akafariki hivyo inawezekana ikawa ni ajali ya kawaida lakini kwasababu imemuhusisha bundi lazima ita letataharuki kuwa inahusiana na mambo ya kishirikina”

Msando amesema k**a Serikali ngazi ya Wilaya wana amini ni ajali k**a ajali nyingine zinazotokea barabarani na hivyo ametoa wito kwa wale wote wanao tumia vyombo vya moto hususa pikipiki kuvaa kofia ngumu na kuchukua tadhari pindi wanapo kuwa barabarani na kutokwenda kwa spidi ili kuweza kuepuka kupata ajali.

22/03/2024

Kamera ya Nipashe Digital usiku huu imewamulika wajasiriamali wadogo wakiwa pembezoni mwa barabara eneo la Mbezi Stendi Wilaya ya Ubungo mkoani Dar es Salaam wakisubiri wateja.

22/03/2024

Mfanyabiashara na Mdhamini wa Club ya Yanga Ghalib Said Mohammed (GSM) ameonesha nia ya kuona Rais wa TFF Wallace Karia na Haji Manara wanaelewana baada ya kutofautiana Julai 2 2022 kwenye mechi ya fainali ya Kombe la ASFC lililozikutanisha Yanga na Coastal Union katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.

Ghalib amewakutanisha Rais Karia na Haji Manara leo jioni katika Iftar iliyoandaliwa na Kampuni ya GSM na kualika Watu mbalimbali akiwemo Naibu Spika, Mawaziri mbalimbali pamoja na Wadau wengine mbalimbali.

Katika picha walizopigwa usiku wa leo Karia na Manara wameonekana wakizungumza, kutabasamu na mwishowe kushikana mikono na kutazama camera ya huku wakati wote Mpatanishi GSM akiwa na tabasamu katikati yao.

July 21 mwaka huu wa 2024 Haji Manara atakuwa anatimiza miaka miwili toka afungiwe kujihusisha na soka na atakuwa ana maliza adhabu hiyo ambayo pia ilimtaka alipe faini ya milioni 20.

22/03/2024

"Hii sio tu njia ya kunisaidia, lakini njia ya kutoa matumaini kwa maelfu ya watu wanaohitaji upandikizaji ili kuishi."

Madaktari wa upasuaji wa Marekani wanasema Rick Slayman, 62, ni "shujaa halisi" kwa kujaribu upasuaji huo.

28/10/2023
28/10/2023

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Paul Makonda, amefika katika Ofisi Ndogo za CCM mtaa wa Lumumba Jijini DSM akiwa anaendesha Pikipiki huku idadi kubwa ya wanachama hasa Vijana wakimsindikiza katika mapokezi yanayofanyika katika ofisi hizo.

Picha na Clouds Tv

15/10/2023
02/10/2023

VILIO vimetawala kwa wafugaji 3000 wa jamii ya kimasai wanaoishi katika eneo la Mazoka, Kata ya Magomeni wilayani Kilosa mkoani Morogoro kutokana na eneo wanaloishi tangu mwaka 1958 kuchimbwa mfereji na kuzuia mifugo yao, kuvunja nyumba zao pamoja na mazizi ya mifugo na mwekezaji aliyepewa eneo hilo.

Wafugaji hao wamemuomba Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuingilia kati suala hilo ili kuwapatia ufumbuzi kwakuwa kila walipofikisha hakuna jawabu wanalopata zaidi ya kupigwa danadana na kuonekana k**a sio watanzania wenye haki ya kumiliki ardhi. /https://www.ippmedia.com/sw/biashara/wafuagaji-waangua-kilio-kuporwa-maeneo-yao

02/10/2023

Days of our lives!

25/09/2023

⚠️😳 Licha ya kuwa na mke wa ndoa kisheria Akon(50) bado agawa waziwazi muda kuwapa atensheni na mapenzi wanawake wake wengine. Siku chache zilizopita Akon alikuwa nchini Senegal kusherehekea birthday ya Ammirah mwanamke wake ambaye pia ni mwanamuziki, Amirrah amepost picha wakiwa pamoja k**a kawaida yake anavyofanya mara kwa mara

Kabla ya kwenda Senegal, Akon alikuwa Dubai kula maisha na mwanamke wake mwingine anayeitwa Rozina ambaye nae ameachia mapichapicha wakiwa pamoja Dubai na wote hao anawaita wake zake ingawa inaelezwa hajawaoa rasmi na bado ana wanawake wengine anaowaita girlfriends

Ingawa mwanamuziki huyo wa Marekani anayetokea Senegal, ana mke mmoja anayetambulika kisheria. mkewe rasmi anaitwa Tomeka Thiam(48) aliyevaa nguo ya bluu pichani, ambaye walikutana enzi hizo Akon akiwa na miaka 20 na Tomeka akiwa na miaka 18. Wamejaaliwa kupata watoto 5 katika ndoa yao mtoto wao wa kwanza akiwa kazaliwa 1996

Akon ana watoto wengine 4 aliozaa na wanawake tofauti hivyo kiujumla Akon ana watoto 9

Akon anasema haamini dhana ya mwanaume kuwa na mke mmoja hivyo anaona hata mataifa ya Ulaya na Marekani yanapaswa kuiga mataifa ya Afrika yenye utamaduni wa wanaume kuoa mke zaidi ya mmoja. Akon anaamini kazi ya mwanamke ni kukaa nyumbani kulea watoto huku mume akiwa ndio mtafutaji

Lakini hata hivyo, Akon mwenye utajiri wa shilingi bilioni 149.7($60 million), hivi karibuni alisema yeye ndie mwanaume bahili zaidi duniani huwa hatapanyi pesa ovyo ovyo au kuwa na matumizi mabaya ya pesa

Mke rasmi wa Akon kisheria ni huyo mwenye nguo ya blue pichani ambaye ana miaka 48, mwenye nywele za rangi ya chungwa ni Ammirah na mwenye gauni la kijani na nyeusi ni Rozina

Kwenye comments section picha zaidi na wanawake wake

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Culinary Team

Attire

Website

Address


Dar Es Salaam
SEGEREA