Afya bora
health consultant
09/08/2022
Bawasiri ni nini?
Bawasiri ni kuvimba kwa mishipa ya damu iliyopo ndani ya au katika eneo linalozunguka njia ya haja kubwa. Ni hali ambayo inaweza kusababisha nyama kujitokeza nje. Hivyo bawasiri inaweza kuwa bawasiri ya ndani au bawasiri ya nje. Ugonjwa huu unaweza kusababisha mwasho, maumivu na damu au k**asi kutoka wakati wa kujisaidia haja kubwa ingawa wakati mwingine hauna dalili.1 Madhara ya bawasiri ya ndani ni pamoja na damu kutoka wakati wa kujisaidia, damu kuganda ndani ya mishipa ya damu na maumivu.
Kutokea kwa bawasiri kunaweza kuhusishwa na hali k**a uzee, ujauzito, kuharisha au choo kufunga (constipation), saratani kwenye nyonga au kukaa kwa muda mrefu. Tiba ya bawasiri inategemea aina ya bawasiri na ukubwa wa tatizo. Matibabu ya bawasiri yanaweza kuhusisha matumizi ya dawa au upasuaji mdogo.
CHANZO CHA BAWASILI
Bawasiri hutokea pindi mishipa inayozunguka sehemu ya kutolea haja kubwa kwa ndani kwenye kuta zake kuumia au kukandamizwa kwa kushuka chini na kuvimba.
Bawasiri inaweza kukuza kutoka kwa shinikizo lililoongezeka kwenye puru ya chini kwa sababu ya:
1. Kuwa na Kinyesi kigumu (Constipation)
2. Kuketi kwa muda mrefu kwenye choo
3. Kuharisha (Kuhara) mara kwa mara
4. Kuvimbiwa
5. Kuwa mnene au mzito
6. Kuwa mjamzito
7. Kuingiliwa nyuma kimaumbile
8. Kutokula vyakula vyenye nyuzinyuzi
9. Kuinua/Kunyanyua vitu vizito mara kwa mara
10. Kunyoosha wakati wa haja kubwa
DALILI ZA UGONJWA WA BAWASIRI
Ishara na dalili za bawasiri kawaida hutegemea aina ya Bawasiri
BAWASIRI YA NJE
Hizi ziko chini na nje ya ngozi karibu na sehemu ya kutolea haja kubwa. Ishara na dalili zinaweza kujumuisha:
1. Kuwasha katika maeneo yaliyozunguka sehemu ya haja kubwa
2. Maumivu au usumbufu
3. Kuvimba kuzunguka sehemu ya kutolea haja kubwa
4. Mara nyingine yaweza Kuvujadamu au k**a michubuko
5. Kutokwa na kinyama baada ya kwenda haja
BAWASIRI YA NDANI
Bawasiri ya ndani iko ndani ya sehemu ya kutolea haja. Kawaida huwezi kuziona au kuzihisi, na mara chache husababisha jbisha:
1. Kutoa haja/kinyesi chenye damu na maumivu yasiyo makali. Unaweza kuona kiasi kidogo cha damu nyekundu kwenye haja yako.
2. Maumivu na muwasho sehemu ya haja
MADHARA YA BAWASILI.
1.Upungufu wa damu. Mara chache, upotezaji wa damu sugu kutoka kwa bawasiri unaweza kusababisha upungufu wa damu, ambayo hauna seli nyekundu za kutosha za damu kubeba oksijeni kwenye seli zako.
2.Bawasiri sugu /iliyoshonwa. Ambayo inaweza kusababisha maumivu makali.
3.kupata saratani katika njia ya haja kubwa kutokana na ufanyiwaji wa operation za mara kwa mara.
KWA MAELEKEZO ZAID NA TIBA KWANJIA YA ASILI WASILIANA NASI
CALL; 0672988656
WHATSAPP:0672988656
18/10/2021
Upungufu wa Nguvu za Kiume ni hali ya kushindwa kufanya mapenzi kikamililifu au kushindwa kusimamisha vizuri, shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. atizo hili huripotiwa kuwa katika wanaume watano (5) basi mmoja kati yao anatatizo la upungufu wa nguvu za kiume. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kuto kuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.
Hili tatizo huwanyima watu raha kwa kuwa na mawazo, kuwa na matatizo katika mahusiano, watu wengi wenye tatizo hili wanahitaji kutumia dawa zisizo na madhara na kubadilisha mitindo ya maisha yao ili kuweza kurudisha hali zao na kuondoa tatizo, cha msingi ni kuzingatia yale utakayoelekezwa.
Kuna matatizo ya kutofanya mapenzi kikamilifu, nayo ni; kuwahi kumwanga mbegu za uzazi, Kuto kumwaga, kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa.
CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME
Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;
Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo
Kuvuta sigala na unywaji wa pombe
Uzito kupita kiasi na unene uliozidi
Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
Kisukari
Kuwa na mawazo na wasiwasi
Matumizi ya madawa mbalimbali
Umri hasa wazee
Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili
Kuwa na tatizo la kibofu
Tabia za kujichua kwa mda mrefu
Kutopata usingizi kamili
Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa k**a kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine
DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME
Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni k**a;
Kuwahi kufika kileleni
Kukosa hamu ya mapenzi
Kushindwa kurudia tendo la ndoa
Uume kusimama kwa uregevu au kushindwa kusimamisha
Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji
Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo
Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa)
Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji
JINSI YA KUEPUKANA NA KUPATA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME
Fanya mazoezi – Angalau dakika 30 kwa siku
Kula vyakula asilia na usile vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
Tibu magonjwa yako yanayokuweka hatarini k**a kisukari, moyo, punguza unene na mengine
Punguza (balansi) kiwango cha halemu (choresterol) au mafuta yaliyozidi
Balansi usito wako
Usivute sigara
Punguza au acha kunywa pombe
Punguza mawazo
Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali
Lala vizuri kwa muda mzuri – masaa 7 hadi 9
Usitumie dawa zenye kemikali nyingi huathiri mfumo wa uzazi
Kunywa maji ya kutosha
Tuna dawa ya kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume ambayo ni ya asili isiyo na kemikali ambayo hufanya mtu kupona na kuimarika kabisa. Dawa hiyo hutibu kwa mda kulingana na ukubwa wa tatizo, ukianza kutumia baada ya wiki mbili huonesha mabadiliko, pia mgonjwa anapewa mfumo wa maisha ambao inatakiwa utumie kwasababu kuna mtindo wa maisha unaendekea kuongeza tatizo pia kuna mtindo unapunguza hatari ya ugonjwa.
WhatsApp/ calls 0672988656/0621939099
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Mlimanicity
Dar Es Salaam
Opening Hours
| Monday | 09:00 - 17:00 |
| Tuesday | 09:00 - 17:00 |
| Wednesday | 09:00 - 17:00 |
| Thursday | 09:00 - 17:00 |
| Friday | 09:00 - 17:00 |
| Saturday | 09:00 - 17:00 |