man's health solution
Tunatatua changamoto za kiafya kwa wanaume: ��
�Nguvu za kiume.
�Tezi dume.
�Matatizo ya uzazi.
24/05/2024
Je? Katika mda wako wa ziada huwa unafanya nini
05/11/2023
Mwanaume Ili uweze kuwa salama, afya ndio Kila kitu mana katika upambanaji wa Kila siku unahitaji uwe na afya Bora na salama!
Je? Kwa mara ya mwisho chakula Cha kulinda afya ya tezi dume lako umekula lini?
25/09/2023
🍏 MWANAUME CHUKUA HILI🍏
Mwanaume akipimwa tezi dume
“Kwa kawaida tezi ni ndogo gramu 15 lakini kadiri mwana- mume anavyokua kuna vichocheo vinavyozalishwa ambavyo vinaitwa ‘testosterone’ hii inasababisha tezi inakua kadri umri unavyoongezeka.
“Homoni hizi za ‘testosterone’ pia zinahusika kwenye ukuaji wa mfumo wa uzazi kwa mwanamume tangu akiwa tumboni via vya uzazi vya ndani na vya nje vinategemea homoni hizo.
“Huzalishwa kwa wingi kipindi mtoto akiwa tumboni hadi miezi mitatu, lakini baada ya hapo zina- pungua na baadaye kuja kuongeze- ka tena wakati wa balehe,
Baada ya balehe homoni hizo hupungua mwilini kwa sababu wakati huo huwa kuna mabadiliko kadhaa.
“Mvulana anapo balehe homoni huanza kutumika mfano kufanya sauti kuwa nzito, ndevu na nywele sehemu mbalimbali za mwili zote zinategemea homoni hizo.
“Umri ukishasogea matumizi ya ‘testosterone’ katika sehemu nyingine za mwili zinapungua zaidi kwahiyo inatumika zaidi kwenye tezi dume, kadri homoni hizo zinavyoendelea kuongezeka na umri kuongezeka, misuli ya tezi inaongezeka na kuwa kubwa.
“Ikishakuwa kubwa inafinya au kuziba njia ya mkojo ndio hapo sasa mtu anaanza kuwa na dalili kwenye mfumo wa mkojo.
“Lakini pia inawezekana sio kuwa kubwa tu, unaweza kupata saratani k**a sehemu zingine
za mwili na ukipata saratani kwa sababu mfumo wa mkojo unapita utakuwa na dalili za mkojo na dalili katika mfumo wa uzazi pia,”
hali hiyo ikitoka mkojo hushindwa kutoka nje au kutoka kidogo bila kumalizika.
“Ukiwa na mzigo wa mkojo, mfano mkojo kutokuisha kibofu kinaanza kuathirika na mkojo huwa na acid inayoitwa Uric Acid, ikit- uama kwenye kibofu mtu atapata maambukizi ambayo pia yanaweza kusababisha kutengeneza mawe kwenye mafumo wa mkojo.
“Lakini pia k**a mkojo hautoki wote na kuisha, kibofu kinatanuka, kwa kawaida mwili wa binadamu uwezo wa kibofu kutunza mkojo ni mill 350 hadi 500 ikifika 450 hadi 500 lazima ukakojoe.
“K**a kuna mzibo mkojo uta- baki mwingi kwenye kibofu na mi- suli ya kibofu cha mkojo itaathirika baadae mirija inayoleta mkojo kutoka kwenye figo kupeleka chini itaathiri na figo zitaathirika na itashindwa kufanya kazi,” .
Endapo Chumvi ambazo zimezalishwa humo hazitatoka zitachukuliwa na kurudishwa kwenye mzunguko wa mwili kwa sababu mwili unatabia hiyo.
“Ile chumvi ikirudi kwenye mwili mgonjwa anaweza kuone- sha dalili za shida ya figo k**a kichefuchefu, kutapika na men- gine,”
Hivyo basi fanya mamuzi sahihi juu ya afya yako.
25/09/2023
IFAHAMU TEZI DUME NA TIBA YAKE
0717226127
Kila mwanaume anazaliwa na Tezi dume. Tezi dume siyo ugonjwa bali ni kiungo K**a viungo vingine mwilini. Tezi dume inapatikana katika mfumo wa uzazi wa mwanaume katika shingo ya kibofu cha mkojo. Kazi yake kubwa nikutengeneza maji maji ya uzazi wa mwanaume (shahawa), ambayo husaidia kurutubisha mbegu za kiume zilizo tengenezwa kutoka kwenye Korodani; na husaidia mbegu za kiume kubaki hai kwa muda unaostahili.
Tatizo linakuja kiungo hiki kinapoanza kutanuka. Kiungo hiki kinatanuka taratibu taratibu mnoo. Hili ni tatizo linalowakumba wanaume wengi. Takwimu zinaonesha kwamba kati ya wanaume 10, wa 5 na kuendelea wana dalili za kutanuka kwa Tezi dume.
🔥 Ukuaji wa Tezi dume ni ile hali ya chembe chembe hai katika tezi ya kiume kukua bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili katika eneo linalo zunguka mirija ya kupitisha mkojo na mbegu za kiume. Tatizo hili kwa sasa linawapata wanaume kuanzia umri wa miaka 25 na kuendelea, tofauti na awali lilikuwa miaka zaidi ya 50.
🔥 Takwimu kutoka kwenye shirika la CHRP (Centre for Human Right Promotion), zinaonesha kwamba kiujumla kila mwanaume katika maisha yake ana 16% za kugundulika na saratani ya Tezi Dume, mtu 1 kati ya watu 6 analo hili tatizo; 3% (1 kati 33) wanakufa kwasababu ya Saratani ya Tezi Dume. Saratani hii inaua mwanaume mmoja kila baada ya dakika 13.
🍏 VYANZO VINAVYOPELEKEA TEZI DUME KUTANUKA
🔥Tatizo la kutanuka kwa tezi dume limekuwa kwa kasi sana hii ni kutokana na mitindo ya maisha wanaume wengi wanayoishi. Pia na elimu ndogo iliyoko kwenye jamii kuhusu afya zao.
🍏 Vifuatavyo ni vyanzo vya kutanuka kwa tezi dume:
🔥Ukosefu wa lishe kamili na Virutubisho muhimu mwilini.
🔥Uwepo wa sumu nyingi mwilini.
🔥Kutokufanya mazoezi.
🔥Matumizi ya pombe kali, na uvutaji wa sigara.
🔥Uzito mkubwa (uliopindukia, uliokithiri), na Kitambi.
🔥Kutokukaa sawa kwa vichocheo vya mwili (Hormone Imbalance)
🔥Msongo wa mawazo (Stress).
🔥Magonjwa ya zinaa.
🔥Umri mkubwa.
🔥Upasuaji wa korodani, kuzaliwa na korodani moja.
🔥Historia ya Familia (Kurithi).
🔥Mazingira (Ethnicity).
🍏DALILI ZA KUTANUKA KWA TEZI DUME
Mpaka mtu apate saratani ya Tezi Dume (Prostate Cancer), ujue amekaa na tatizo hilo kwa muda mrefu, si chini ya miaka isiyopungua 10.
Hii hutokana na mrundikano wa mkojo unaobaki kwenye kibofu na kwenye mrija wa mkojo (Urethra) wakati unakojoa; ukiendelea kujirundika kwenye kibofu na mrija; baada ya muda unazalisha “Uric Acid” na ndio inatengeneza saratani (cancer).
Saratani ziko stage nne. Ya kwanza na yapili ukiwahi unaweza kupona; lakini ikishafika stage ya 3 na 4, hazitibiki. Unasaidiwa kupunguza makali kwa mionzi ukijitayarisha kupoteza maisha muda wowote.
🍏Hivyo ukiona dalili mojawapo kati ya hizi chukua tahadhari na hatua mapema kabla hujaharibu mfumo wako mzima wa uzazi wa mwanaume.
a) Dalili za awali
- Kukojoa mkojo uliochanganyikana na damu
- Kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu
- Maumivu kwenye mfumo wa mkojo
- Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
- Kuhisi kibofu kimeja mkojo muda wote na ukienda kukojoa mkojo hautoki, lakini ukirudi kukaa unahisi kukojoa tena.
- Homa
- Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
b) Dalili za mtu aliyeathirika
- Maumivu ya mifupa hasa chini ya mgongo, kiuno na mbavu
- Miguu kuwa dhaifu
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa, au Kuhisi maumivu makali wakati unamaliza tendo la ndoa
- Kushindwa kuzuia mkojo, pindi unapohisi kukojoa
- Kushindwa kuzuia haja kubwa (kinyesi cha maji maji)
- Tumbo kuja gesi mara kwa mara
🍏MADHARA YA TEZI ILIYOTANUKA
Katika hatua za awali, tezi inapotanuka hugunduliwa kwa kupimwa kwa njia ya kidole. Hii ni njia ambayo daktari huingiza kidole kwenye njia ya haja kubwa ili kuweza kubaini k**a tezi imetanuka. Kipimo hiki ndicho rahisi kinacho kubalika duniani kote na kisicho na gharama. Lakini kimekuwa kikipata upinzani kutoka kwa wanaume kutokana na imani potofu ya wahusika wa tatizo hili kuona ni udhalilishaji.
Kipimo kingine ni kipimo cha damu. Damu huchunguzwa aina ya protein inayozailishwa na seli za tezi dume, kiitwacho Prostate Antigen (PSA). PSA huonesha kuwapo kwa tatizo kwenye Tezi Dume, lakini kipimo hiki hakina uwezo wa kutofautisha endapo tatizo hilo linamaanisha saratani.
Yafuatayo ni madhara ya tezi iliyotanuka:
- Kibofu cha mkojo kuuma: hivyo hupelekea mkojo kurudi juu, na kuharibu figo na Ini … … n.k.
- Kufunga kwa njia ya mkojo kabisa
- Figo kushindwa kufanya kazi (Kidney Failure)
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa (Ndoa zinavunjika)
- Ugumba (Infertility, Frigidity for men)
- Kutokea kwa majipu sehemu ya Tezi Dume
- Kifo
Epuka madhara yasababishwayo na tezi dume kwa kutumia Dawa zenye Tiba lishe na virutubisho maalum kwa matatizo ya tezi dume bila operation... Tumia K**a tiba au kinga, Hii ni ya uhakika kabisa kwa ubora wa afya yako!
Wasiliana nasi kupitia simu Namba 0717226127 kwa msaada wa kitiba
17/08/2023
🍏SARATANI YA TEZI DUME👎
🌀Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na saratani kwa wanaume wa umri mbalimbali duniani.
Aidha ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wa umri miaka 70 na kuendelea. Hata hivyo, ni nadra sana kwa saratani hii kuwapata wanaume chini ya miaka 40.
🍏Nani yupo katika hatari ya kupata saratani ya tezi dume?👎
🌀Watu walio katika hatari kubwa ya kupata saratani ya tezi dume ni pamoja na:
🔥Wanaume wenye asili ya Afrika (weusi) ikilinganishwa na wazungu
🔥Wanaume kuanzia miaka 60 na kuendelea
🔥Wanaume wenye historia ya tatizo hili kwenye familia zao, yaani wale ambao mmoja wa ndugu zake (kaka au mdogo wa kiume) au baba amewahi kuugua ugonjwa huu.
🔥Wanaume wanaokunywa pombe kupindukia
🔥Wanaofanya kazi kwenye viwanda vya kutengeneza rangi au wanaofanya kazi ya kupaka rangi
🔥Wakulima wanaotumia aina fulani ya mbolea za kemikali
🔥Wanaofanya kazi katika viwanda vya utengenezaji matairi
🔥Wachimbaji wa madini hususani aina ya cadmium
🔥Walaji wa chakula chenye kiasi kikubwa cha mafuta hasa ya wanyama.
🍏DALILI ZA SARATANI ZA TEZI DUME?
Katika hatua zake za awali, dalili za saratani ya tezi dume hazitofautiani sana na zile za kuvimba kwa tezi dume (BPH). Dalili hizo ni pamoja na
🔥Kupata shida unapoanza kukojoa au Kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu.
🔥Kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usikuna kujikakamua wakati wa kukojoa na kushindwa kumaliza mkojo wote.
🔥Kutoa mkojo uliochanganyika na damu .
🔥Kutoa shahawa zilizochanganyika na damu.
N:B
Iwapo saratani imesambaa mwilini kiasi cha kuhusisha sehemu za jirani ya mwili, mgonjwa anaweza kuwa na
🔥Maumivu makali ya mifupa katika maeneo ya nyonga, mapajani na kiunoni.
🔥Uume kushindwa kusimama (uhanithi)
🍏Vipimo gani vitathibitisha kuwa nina saratani ya tezi dume?
🌀Utambuzi wa saratani ya tezi dume hujumuisha kufahamu historia ya mgonjwa pamoja na familia yake, kufahamu dalili alizo nazo mgonjwa pamoja na kufanya vipimo kadhaa. Vipimo vinavyoweza kufanywa ni pamoja na
🔥Digital re**al exam:
Daktari ataingiza kidole cha shahada katika puru (re**um) ili kuhisi tezi dume kupitia ukuta wa puru. Aidha atahisi pia sehemu zote zinazozunguka tezi dume kutambua iwapo tezi ni ngumu au k**a ina uvimbe wowote.
🔥Kipimo cha damu kuchunguza Prostate Specific Antigen (PSA):
PSA ni aina ya protein inayozalishwa na seli za tezi dume. Uzalishaji wake huongezeka wakati wa BPH, tezi dume inapopata uambukizi (prostitis) , na saratani ya tezi dume.
DRE pamoja na PSA huonesha uwepo wa tatizo kwenye tezi dume lakini vipimo hivi havina uwezo wa kutofautisha iwapo tatizo hilo linamaanisha saratani au BPH. Hivyo basi, ili kuweza kutofautisha kati ya magonjwa hayo mawili, kipimo kiitwacho Prostate biopsy hufanywa.
🔥Prostate biopsy:
Kipimo hiki hufanywa kwa kuchukua kipande cha nyama (tishu) kutoka tezi dume kwa ajili ya uchunguzi maabara.
Kipimo kingine huitwa transre**al ultrasound ambacho husaidia kuonesha ukubwa na sura ya tezi dume lilivyo.
Ili kutambua k**a saratani imesambaa sehemu nyingine za mwili vipimo vya CT scan, MRI pamoja na PET navyo vyaweza kufanyika pia.
Saratani ya tezi dume inatibika?
Ndiyo! Kuna njia kadhaa za matibabu ya saratani ya tezi dume. Hata hivyo uamuzi wa njia gani itumike unategemea ushauri na maoni ya daktari kulingana na hatua ya ugonjwa ulipofikia na umri wa mgonjwa husika.
Katika hatua za awali za ugonjwa, daktari anaweza kushauri mgonjwa atibiwe kwa kufanyiwa upasuaji na tiba ya mionzi, wakati kwa wagonjwa wazee, daktari anaweza kushauri kumfuatilia mgonjwa kwa ukaribu bila kumfanyia upasuaji au bila kumpatia tiba ya mionzi.
Iwapo saratani imesambaa na kuathiri sehemu nyingine za mwili, matibabu yake yanaweza kujumuisha upasuaji wa kuondoa korodani, matumizi ya dawa za kupunguza kiwango cha homoni ya testosterone katika damu (hormonal therapy), au matumizi ya kemikali za kuua seli za saratani (chemotherapy).
Upasuaji
Upasuaji hufanyika kwa wagonjwa walio katika hatua za awali za ugonjwa (stage I na stage II) ingawa pia hufanywa kwa baadhi ya wagonjwa walio katika hatua za mwisho za ugonjwa huu yaani stage III na stage IV. Upasuaji unaofanywa ni ule wa kuondoa tezi dume pamoja na baadhi ya tishu zinazozunguka tezi hiyo.
Tiba ya Mionzi
Hii ni aina ya tiba inayotumia mionzi kuua seli zenye saratani. Tiba ya mionzi hutumika kutibu saratani ya tezi dume ambayo haijasambaa kwenye sehemu nyingine za mwili. Aidha inaweza pia kutumika kuua masalia ya tishu zenye saratani mara baada ya kufanyika kwa upasuaji.
Kwa wagonjwa walio katika hatua ya mwisho ya saratani yaani wale ambao saratani tayari imeshasambaa mwilini, mionzi hutumika kupunguza maumivu makali ya mifupa.
Madhara anayoweza kupata mgonjwa kutokana na aina hii ya tiba ni pamoja na kushindwa kusimamisha uume au uhanithi, kukosa hamu ya kula, uchovu, ngozi kubabuka, kuharisha na kutoa mkojo uliochanganyika na damu.
Tiba ya Homoni
Hii ni aina ya tiba inayotumia dawa zinazopunguza kiwango au ufanyakazi wa homoni ya testosterone mwilini. Testosterone ni homoni ya kiume inayochochea ukuaji wa tezi dume, hivyo basi matumizi ya dawa hizi husaidia kupunguza ukuaji huu na kusambaa kwa seli za saratani.
Tiba ya homoni hutolewa kwa wanaume walio katika hatua za mwisho za ugonjwa huu kwa nia ya kupunguza maumivu na kutibu dalili za ugonjwa. Dawa zinazotumika kwa tiba ya aina hii zimegawanyika katika makundi mawili, zile zinazochagiza uzalishaji wa homoni ya luteinizing (luteinizing hormone-releasing hormones, LH-RH) kwa mfano goserelin, nafarelin na leprolide; na zile zinazozuia ufanyaji kazi wa homoni ya androgen kwa mfano flutamide, bicalutamide na nilutamide.
Madhara yanayoweza kusababishwa na utumiaji wa dawa hizi ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, upungufu wa damu, kuongezeka uzito, uhanithi na kukosa hamu ya tendo la ngono, matatizo katika ini na matiti kuwa makubwa.
Baadhi ya madaktari hutumia upasuaji wa kuondoa korodani k**a njia ya kupunguza kiwango cha homoni za kiume mwilini kwa kigezo kwamba kiwango kikubwa cha homoni hizi huzalishwa kwenye korodani. Hata hivyo tiba hii haifanyiki mara kwa mara.
Kutokana na changamoto hizo tumekuja na tiba za asili zenye Tiba lishe na virutubisho zitakusaidia kutatua changamoto Yako ya kiafya bila kufanyiwa upasuaji.
Kwa maelezo zaidi piga simu namba 0717226127.
17/08/2023
🍏Tezi Dume Inapatikana Wapi Katika Mwili?👎
🌀Tezi dume inapatikana chini ya kibofu cha mkojo na inazunguka njia ya mkojo toka kwenye kibofu kwenda kwenye uume.
🍏Kazi Za Tezi Dume Katika Mfumo Wa Uzazi:👎
🌀kutengeneza majimaji ya uzazi wa mwanaume (shahawa) ambayo husaidia kurutubisha mbegu za kiume zilizotengenezwa kutoka kwenye korodani, ambapo wakati wa tendo la ndoa, mwanaume anapofika kileleni, tezi dume hukamulia majimaji (shahawa) ndani ya mrija wa mkojo na kutolewa pamoja na mbegu za kiume k**a manii (Semen).
🌀Pia husaidia mbegu za kiume kubaki na uhai kwa muda unaostahili.
🍏Aina Za Magonjwa Ya Tezi Dume:
Kuna aina tatu za magonjwa ya tezi dume ambazo ni;
1) Maambukizi ya bakteria (Prostatitis).
2) Kukua kwa tezi dume ambalo sio saratani (Benign Prostate Hyperplasia-BPH)).
3) Saratani ya tezi dume.
17/08/2023
🍏Magonjwa yanayosumbua Tezi dume.👎
Wanaume wote wapo kwenye hatari ya kupata magonjwa ya tezi dume na hasa wanapofikia umri wa miaka 50. Hapa chini tutapitia baadhi ya matatizo yanayowasumbua zaidi wanaume:
🌀Benign Prostatic Hyperplasia (BPH) au Prostate Enlargement
Hii ni hali ambapo tezi dume huongezeka ukubwa. Zaidi ya theluthi ya wanaume wote walio juu ya miaka 50 wana dalili za kuvimba kwa tezi dume. Haijajulikana kwa uhakika ni kwa nini tezi dume huwa kubwa zaidi kadri umri unavyoongezeka, lakini kukua huku si dalili ya kansa na wala hakuongezi uwezekano wa kupata kansa. Hili si tatizo kubwa sana la kiafya.
Tezi dume iliyoongezeka ukubwa huleta msukumo juu ya mrija wa mkojo na kibofu cha mkojo hali ambayo inaweza kuathiri namna mkojo utakavyotoka.
17/08/2023
🍏Saratani ya tezi dume 👎
Ni tezi dume imepata ugonjwa wa saratani (cancer). Tatizo Linakuja pale kiungo hiki (tezi dume) kinapoanza kutanuka kutokana na kugawanyika Kwa chembe chembe hai zake bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili.
Chembechembe hizi mwishowe hutengeneza vivimbe hatari ndani ya tezi dume na hatimaye husambaa mwilini. Takwimu zinaonesha kwamba kati ya wanaume 10, wa 5 na kuendelea wana dalili za kutanuka kwa tezi dume.
Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vitokanavyo na saratani kwa wanaume duniani. Pia ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa miaka 70 na kuendelea.
N:B
UCHUNGUZI
🌀Wanaume wote wanpaswa kufanya uchunguzi wa saratani ya tezi dume kuanzia miaka 50. Kwa wale wenye historia katika familia wanapaswa kuanza wakiwa na umri wa miaka 45.
17/08/2023
Tezi dume ni tezi inayopatikana kwa jinsia ya kiume. Tezi hii ina kazi ya kutengezeza majimaji meupe mepesi yenye unato kidogo. Majimaji haya husaidia mbegu za kiume kutembea kwa urahisi.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Mabibo
Dar Es Salaam