Utamu wa simulizi za Mr Lipandu

Utamu wa simulizi za Mr Lipandu

Share

Ni page kwa ajili ya burudani za aina zote zile ambazo ni halali 2

05/06/2022

Laana
Sehemu ya kwanza
Mtunzi ni mr lipandu
Watssp no 0620622316
::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::

Anaonekana mama mmoja ambae yupo nyumbaci kwake maeneo ya sebuleni akiwa amekaa kwenye sofa,sofa ambayo ni yakukaa watu watatu ila mama huyu alikaa peke yake na bado aliona hapatoshi si kwa sababu ya unene hapana ila alionekana ni mwenye mawazo sana tena mawazo yaliomuumiza kichwa na alijiuliza maswali ambayo alikosa majibu,
Dah hivi ni kweli nitafanikiwa hili jambo maana nikifanya na haikua basi nitakua nimeshajizalilisha tayari na nitatafuta pakuficha uso wangu,aliwaza mama yule ndani ya moyo wake.
-------------------------------------------------------
Upande wa pili alionekana kijana mmoja ambae umri wake wapata miaka kumi na nane hivi,kijana huyu alionekana akiwa nje ya maeneo ya shule moja hivi ya sekondari na kwa muda huu ilionesha zahili ni muda wa mapumziko,alikua amekaa sehemu flani hivi akiwa na mwenzie,
Alex rafiki yangu kwa sasa ndugu yako napitia wakatima mgumu sana na hata sielewi kitu gani cha kufanya kiukweli,aliongea kijana yule
Pole sana rafiki yangu maana hata mimi sikuelewi kabisa yasiri umekumbwa na nini maana umekua mtu wa mawazo sana na hata kukonda una konda pia umepatwa na nini ebu funguka kuwa muwazi huenda nikakushauri,aliongea alex,
Ni kweli alex ila hili jambo ni kubwa sana na hata kulisema huwa nawaza naanzia wapi maana ni gumu sana nafikia hatua nawaza niache shule kisha nihame huu mji nikaishi mbali sana na hapa huenda nikawa na amani,aliongea yasiri kumwambia alex,
Haaaaaa yasiri,alishangaa alex na huku akimuangalia usoni yasiri na kusema yani umebakisha mwezi mmoja tu kufanya mtihahi unataka kuacha shule mmmm hiyo haipo sawa yasiri alafu hilo ni jambo gani ambalo wewe unashindwa kulisema hadi unakua hivyo kumbuka maisha ni magumu unatakiwa kupambana yasiri na sio kuwaza hayo mambo yako ila najua cha kufanya nitaenda kwa mama yako kufuatilia hili,
Eti nini hapo unaongeza tatizo na sio kupunguza aliongea yasiri.
Itaendelea

29/05/2022

Laana ni simulizi itakayokujia hivi karibuni kaa mkao wa kula

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Address


Masoko
Dar Es Salaam