Dorah healthcare

Dorah healthcare

Share

Tuntoa ushauri wa afya ya uzazi kwa wanaume na wanawake
Tunasaidia kuongoza watu kupungua uzito

03/07/2023

Package Yetu Inaondosha Kilo 5-10 ndani ya siku Tisa,

:PACKAGE ITAKUPA FAIDA NYINGI
-Inaboresha mmeng’enyo wa chakula
-Unapata choo vizuri
-Inaboresha Mwonekano wa ngozi yako
-Inaondosha mafuta mabaya yote mwilini
-Inasaidia kwenye vimbe za ndani zote
-Inaboresha Afya ya Uzazi
-Kuondosha tumbo

:Kumbuka mimi ndiye nitakayekuongoza Siku zote tisa

:NB KUMBUKA HIZI SIO DAWA NI VIRUTUBISHO

CALL &WHATSAP +255 755206375

17/02/2023

JE UNATATIZO LA MIFUPA (JOINTS), MIGUU KUUMA, MGONGO NA VIUNGO VINGINE?

● KINA MAMA wengi wanapofikia umri Wa kuzeeka yaani miaka 45 na kuendelea miguu na mgongo kuuma imekuwa ni tatizo linalowasumbua.

● WAZEE nao wamekuwa wakisumbuliwa na hili tatizo linalowapelekea wengi wao kushindwa kutembea.

● WAFANYA MAZOEZI na WANAMICHEZO pia wana changamoto hii ya mifupa/viunga kuuma kutokana na ukosefu Wa majimaji kwenye viunga........

● Itambue FOREVER FREEDOM NA KAZI ZAKE KATIKA VIUNGO VYA MWILI.

****FAIDA ZAKE:-****

++ Husaidia mifupa isichakae na kurudisha majimaji yaliyopo katikati ya viungo ili kulainisha viungo na kuondoa maumivu na uvimbe.

++ Ni nzuri kwa wanamichezo na wanaofanya mazoezi.

++Nzuri kwa wanawake na wazee kwani tatizo hili huwaandama sana.

++ Vitamin C iliyoko ni kwa ajili ya kutibu pale inapotokea uhitaji huo na inasaidia ufanisi Wa MSM.

++ Ni kinywaji kinachotengenezwa na kupatikana kiasili.

++ Ni nzuri kwa watu wenye uzito uliopitiliza na wanaofanya kazi nzito.

++ Itakupatia kiasi cha Glucosamine Sulphate, Chondrotin Sulphate, MSM pamoja na vitamin C ambacho kinatakiwa na kuhitajiwa na mwili kila siku.

Kumbuka Bidhaa Hizi Si Dawa, Ni Virutubisho Lishe Vya Asili. Na Pia Havina Kemikali Hatarishi, Hivyo Ni Salama Kwa Afya Ya Mtumiaji.

KWA USHAURI WA HUDUMA HII Karibu inbox .📥..... Andika namba yako ya simu na majina hapa)

11/01/2023

KUPANDA/KUSHUKA(PRESSURE).

SHAMBULIO LA MOYO, KUTANUKA KWA MOYO/KUTANUKA KWA MISULI YA MOYO.

PRESHA/SHINIKIZO LA DAMU.
Ni msukumo wa damu kwenye kuta za mishipa inayo safirisha damu.

Unapo pima shinikizo la damu (presha) majibu yake hutoka na namba mbili:-
1. Namba iliyo juu (systolic)
Hii humaanisha nguvu ambayo moyo wako unasukuma damu kwenda sehemu mbalimbali za mwili.

2. Namba iliyo chini (Diastolic)
Hii humaanisha nguvu ya damu yako inayotembea kwenye mishipa ya damu wakati moyo umepumzika baada ya kusuma damu katika kila pigo.

⏹️ VIWANGO VYA UPIMAJI PRESHA.

√ Chini ya 110/65mmHg Hypotension (Presha ya kushuka au shinikizo la damu la chini)

√ Chini ya 120/80mmHg Normal (Kawaida)

√ Kati ya 120-129/80mmHg Pre- hypertension (Hatari ya kupata presha ya juu

√ Kati ya 130-139/80-89mmHg 1st stage hypertension ( presha ya juu steji ya kwanza)
Ifikapo 130 na kuendelea basi presha yako iko juu ni vyema kuwa makini zaidi kwa Afya yako.

√ 140/90mmHg au zaidi 2nd stage hypertension (presha ya juu steji ya pili)

Kuanzia 180/120 na kuendelea , Hypertensive crisis ( shinikizo la damu la juu zaidi).

Huku visababishi vya presha vikibakiwa kuwa ulaji usiofaa, magonjwa ya moyo, uzito mkubwa/unene/kitambi, matumizi yasiyo sahihi ya dawa za presha, kurithi, uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kali.

⏹️ ISHARA NA DALILI ZA SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA).

Mara nyingi watu wenye shinikizo la damu hawana ishara yeyote na huwa inagunduliwa baada ya kufanya uchunguzi wa kiafya au presha kubwa kwa muda mrefu inapokuwa imefanya uharibifu mkubwa ndani ya mwili ni pamoja na dalili zifuatazo:-

➡️ Maumivu ya kichwa hasa nyakati za asubuhi.
➡️ Kuhisi kizunguzungu
➡️ Mapigo ya moyo kwenda kwa kasi
➡️ Maumivu ya kifua
➡️ Kupoteza fahamu
➡️ Kupumua kwa shida
➡️ Kujisikia uchovu usiokwisha
➡️ kutoona vizuri
➡️ Kukohoa
➡️ Kuhisi ukelele sikioni n.k

⏹️ SABABU/CHANZO CHA SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA).

➡️ Umri
➡️ Msongo wa mawazo (strees)
➡️ Kuwa na mazoea ya kutumia chumvi nyingi kenye chakula
➡️Ulaji usiofaaa
➡️ Ukosefu wa shughuli za kimwili
➡️ Ulevi uliokithiri
➡️ Kuwa na unene uliopitiliza
➡️ Ujauzito

⏹️MADHARA YA KUENDELEA KUISHI NA SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA).

➡️ Moyo kushindwa kufanya kazi (Heart Failure)
➡️ Moyo kutanuka (Cardiomegaly)
➡️ Shambulio la moyo ( Heart attack)
➡️ Kiharusi/Kupooza (stroke)
➡️ Kuharibu figo na figo kushindwa kufanya kazi
➡️Kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.

⏹️ ZINGATIO.
Licha ya uwepo wa dawa mbali mbali za kukabiliana na tatizo hili bado huendelea kuwatesa na kuwaua wengi kila mwaka.

Pamoja na jitihada mbali mbali bado utasikia kila mwaka milioni 8 hufa kutokana na changamoto hii.
Huku watu bilioni moja duniani kote wanaathiriwa na shinikizo la juu la damu likiwapelekea kupata shambulio la moyo, kupooza na moyo kutanuka.
Na ni kwa mujibu wa WHO.

09/01/2023

IJUE AFYA YAKO:
**CHEMBE YA MOYO*

Chembe ya moyo ni tatizo linalowasumbua watu wengi sana kwa sasa. chembe ya moyo ambayo kwa jina la kitaalamu inaitwa angina pectoris hutokea pale ambapo moyo unakua unapata hewa ya oxygen kidogo tofauti na mahitaje yake.

hii hali inaweza kusababishwa na aidha kuziba kwa mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye misuli ya moyo wenyewe na kusababisha misuli hiyo isipate damu ya kutosha inayobeba oxygen hivyo kusabaisha upungufu wa oxygen au pale ambapo moyo unakuwa unafanya kazi kubwa sana ya kusukuma damu kiasi kwamba kiwango cha oxygen ambacho moyo huo unapata kinakua hakitoshi

*WATU AMBAO WAKO KWENYE HATARI YA KUPATA CHEMBE YA MOYO*

1.wanaovuta sigara
2.wanene kupita kiasi
3.watu wenye kisukari

DALILI ZA CHEMBE YA MOYO
Dalili kubwa ya chembe ya moyo ni maumivu katikati ya kifua ambayoa yanakua yanatembea kuelekea mpaka kwanye mkono wa kushoto

Namna ya kuweza kuondokana na tatizo la chembe ya moyo kwanza ni kua mtu wa kufanya mazoezi mara kwa mara lakini pia iliwa wewe ni mnene jitajhidi kupunguza uzito ambavyo hii itasaidia mzunguko wa damu kuwa vizuri

Lakini pia kupata virutubisho muhimu ambavyo vitafanya kazi ya kusafisha mwili na kuboresha katika mishipa ya damu ili damu iweze kusafirishwa vizuri kutoka kwenye moyo hadi kufikia mwili mzima

Niwatakie usiku mwema ndugu zangu

Ikiwa utakua na swali lolote au ushauri nakukaribisha sana

Naitwa Dorah
Mshauri wa Afya
0755206375

07/01/2023

CHANZO NA DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO

Chanzo kinaweza kuwa kongosho, tezi inayojihusisha na masuala ya mmeng'enyo wa chakula. Kongosho hutoa baadhi ya vimeng'enya k**a asidi ili kusaidia kumeng'enya chakula kwa urahisi lakini inaposhindwa kupima kiasi cha asidi na kuzitoa nyingi mno utaandamwa na vidonda vya tumbo; ndiyo maana unashauriwa kunywa maji mengi. Ni kwamba tindikali hizo zinazopatikana ndani ya tumbo humwagika kwa muda ambao tumbo limezoea kupokea chakula. Mtu anapokaa muda mrefu bila kula tindikali hizo humwagika tu na kukuta tumbo likiwa halina chakula, hivyo huanza kuchubua ukuta wa tumbo. Jambo hili linapotokea mara kwa mara michubuko hiyo huongezeka ukubwa na mwisho huwa vidonda. Kwa hiyo vidonda vya tumbo mara nyingi husababishwa na kutokula chakula kwa wakati unaostahili.

Chanzo kingine cha ugonjwa huo ni mawazo: mtu akiwa na msongo wa mawazo yupo kwenye hatari ya kupata vidonda vya tumbo.

Dalili na tiba

Baadhi ya dalili za ugonjwa huo ni kuwa na maumivu makali ya tumbo, hasa mara ya kula chakula, tumbo kuwaka moto baada ya kula baadhi ya vyakula k**a dagaa, mimea ya jamii ya mikunde hasa maharagwe, pia pilipili.

Dalili nyingine ni kizunguzungu, kushindwa kupumua, tumbo kujaa gesi, kufunga choo, kukosa hamu ya tendo la ndoa, kuharibika kwa mimba, homa isiyopona, UTI sugu, choo chenye mchangayiko wa damu, kutapika damu, kupungukiwa damu, maumivu ya mgongo na misuli, kichomi, maumivu ya kichwa, kichefuchefu, kushindwa kula baadhi ya vyakula.

Ugonjwa huo unapozidi kushamiri husababisha pia kupata haja kubwa iliyochanganyika na damu, pia kukosa hamu ya kula chakula na kujisikia k**a kutapika pindi tindikali inapokuwa inamwagika tumboni.

Mara nyingi vidonda vya tumbo vinaambatana na chembe ya moyo yaani tumbo linapokusumbua huuma kwa kuambatana na chembe ya moyo na mgonjwa huteseka sana; kwa sababu huo ugonjwa unampangia mgonjwa chakula ambacho awe anakula; akila chakula tofauti mambo yanakuwa mengine.

Endapo mgonjwa hatapata matibabu kwa wakati kutapelekea kutapakaa kwa tindikali mwilini na kunaweza kuwa chanzo cha magonjwa ya kisukari, ini, moyo, figo, ugumba na saratani. Athari kuu ya vidonda vya tumbo vinaposhamiri ni kuwa husababisha kifo.

WASILIANA NAMI KUPATA VIRUTUBISHO VITAKAVYOKUSAIDIA KUTIBU TATIZO AMBAVYO VIMETENGENEZWA KWA MBOGA MBOGA NA MATUNA
WASILIANA NAMI 0755206375

06/01/2023

Dalili za upungufu wa maji mwilini

Mahitaji ya maji ya mtu yanaweza kutofautiana kulingana na saizi ya mwili wake, kiwango cha shughuli za mwili, na kukabiliwa na halijoto ya mazingira.
Wakati mtu anapokuwa na upungufu wa maji mwilini kidogo, anaweza kupata dalili zinazojumuisha:

mkojo wa gizagiza
kukaukiwa kinywa
uchovu
kizunguzungu
kiu

Kunywa maji ya kutosha kunaweza kusaidia mtu kujisikia vizuri katika viwango kadhaa, ikiwa ni pamoja na utendaji wa tendo la ndoa. Mtu anapaswa kunywa maji ya kutosha, ili mkojo wake uwe wazi kwa rangi, na haoni kiu.

Dalili za upungufu mkali wa maji mwilini

Ikiwa mtu hatakunywa maji au viowevu vingine anapoanza kuwa na dalili za upungufu wa maji mwilini, anaweza kuzidi kupoteza maji mwilini. Hii inaweza kugeuka kuwa dharura ya matibabu.
Dalili za upungufu mkubwa wa maji mwilini ni pamoja na:

mkanganyiko
kuwa na hisia kali ya kiu
ukosefu wa jasho hata katika hali ya hewa ya joto
Shinikizo la chini la damu (presha ya kushuka)
kutoa mkojo kidogo au hakuna
kasi ya moyo

Je k**a haujapungukiwa nguvu za kiume kwa sababu ya maji ni sababu ipi iliyopelekea upungukiwe nguvu za kiume?

Kwa hakika, upungufu wa nguvu za kiume ni jambo la maarufu sana katika zama hizi za sayansi na teknolojia - takriban watu tisa kati ya kila wanaume 10 wana changamoto ya nguvu za kiume. Kwa watu wengine, upungufu wa nguvu za kiume ni dalili ya matatizo ya kiafya, k**a vile madhara ya kujichua, ugonjwa wa mishipa, ugonjwa wa neva, au hali k**a vile kuvuja kwa venous, orodha ni ndefu kuna zaidi ya sababu 100.

Upungufu wa nguvu za kiume wa muda mrefu katika umri wowote si kitu cha kawaida, na inapaswa kutathminiwa na daktari wa mbobezi wa mfumo wa uzazi wa mwanaume. Sio kila tabibu anaweza kutibu upungufu wa nguvu za kiume.

Mwanaume anaweza kupata upungufu wa nguvu za kiume kwa sababu kadhaa. Wanaume wa umri wote wanaweza kupata hali hiyo. Ingawa watu wanahusisha kuzeeka na nguvu za kiume, si lazima iwe hivyo. Hali fulani zinazoathiri mtiririko wa damu zinaweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume, ikiwa ni pamoja na:

Kisukari
shinikizo la damu
historia ya matumizi ya pombe na tumbaku
historia ya majeraha ya ubongo au uti wa mgongo
historia ya mionzi kwenye tezidume
ugonjwa wa sclerosis
ugonjwa wa Parkinson
upasuaji wa tezidume
kiharusi
Baadhi ya dawa za hospitali
Kujichua
Bawasiri
Ngiri
Kitambi/uzito mkubwa

06/01/2023

Wasiliana nami Kwa maelezo zaidi
0755206375

06/01/2023

FOREVER SUPERGREAN ni products ambayo imetengenezwa na mboga mboga pamoja na matunda Zaid ya ishrini

Pia inasaidia sana Kwa mtu anayefanya mazoezi ya kunyanyua vyuma inasaidia kumpa nguvu na kuijenga mwili

Wasiliana Mani kupata maelezo zaidi
Whatsapp 0755206375

03/01/2023

Dalili Za Bawasiri


Dalili za bawasiri hutofautiana. Wakati mwingine hakuna dalili zinazojitokeza na mtu anaweza asijue kuwa ana bawasiri.

Dalili ya kawaida kabisa ni kutokwa na damu wakati ukienda kujisaidia haja kubwa. Damu huonekana iliyo mbichi, nyekundu, juu ya toilet tissue, kwenye sahani ya choo au ikiwa imekizunguka kinyesi.

Bawasiri huweza kuchomoza na kuning’inia nje. Mara
nyingi unaweza kuzisukuma na vidole zikarudi ndani baada ya kujisaidia. Lakini bawasiri zilizofikia hali mbaya huning’inia moja kwa moja nje na huweza kuzisukuma ndani.

Bawasiri ndogo za ndani kwa kawaida hazina maumivu. Bawasiri kubwa huweza kutoa majimaji, kuwa na maumivu, na kuwasha. Majimaji yatokayo yanaweza kuchubua eneo linalolizunguka tundu la haja kubwa. Unaweza kuwa na hisia za kuwa na haja kubwa au kuwa hujamaliza vizuri haja zako ukiwa unatoka msalani.

Matokea mabaya ya bawasiri zinazoning’inia ni kuwa zinaweza zikajifinyanga na kusababisha damu kushindwa kupita kuelekea kwenye bawasiri hizo, hali ambayo inaweza kuleta maumivu makali sana. Mara chache inaweza ikatokea kuwa damu ikaganda ndani ya bawasiri (thrombosis) hizo, hali ambayo huleta maumivu makali pia.



Tiba Ya Bawasiri


Kukwepa Kufunga Choo Na Kutumia Nguvu Wakati Wa Haja Kubwa

Jaribu kuweka kinyesi kuwa laini na usitumie nguvu wakati wa kujisaidia haja kubwa. Unaweza kufanya yafuatayo:

Tumia nyuzinyuzi kwa wingi k**a matunda, mboga za majani, nafaka n.k.

02/01/2023

FAHAMU BAADHI YA VYANZO VYA UKUWAJI WA TEZI TUME EPUKA HAYA...

TEZI DUME NI NINI?

Tezi dume ni moja ya tezi la uzazi la kiume ambalo kila mwanaume analo, tezi hili lipo chini ya kibofu cha mkojo na linazunguka njia ya mkojo toka kwenye kibofu kwenda kwenye uume. Jinsi umri unavyoongezeka tezi dume
nalo huongezeka ukubwa ambao unaweza kuwa wa kawaida au saratani.

Kuna aina tatu za magonjwa ya tezi dume.
1.Maambukizi ya Bakteria
(Prostatitis).

2•Kukua kwa tezi dume ambalo
sio saratani (Benign Prostatic
Hypertrophy-BPH).

*3.SARATANI YA TEZI DUME*

Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vitokanavyo na saratani kwa wanaume duniani.

*VITU VINAVYOSABABISHA SARATANI YA TEZI DUME*

💥Chanzo hasa cha saratani ya tezi dume
hakijulikani, saratani hii ina uhusiano
mkubwa na;

1.Umri,
kadri umri unavyo kwenda uwezekano wa mwanaume kupata /tezi kukuwa ni mkubwa zamani tulikuwa tunaongelea wanaume wenye miaka 40,50 kuendelea but sahivi kulingana na tafiti wanaume baadhi wenye umri miaka 25 plus pia wapo hatarini kupatwa na saratani ya tezi dume.

2 Vyakula vyenye kiasi kikubwa cha mafuta, hasa ya wanyama.

3.Historia ya tatizo hili kwenye familia (Genetic).

4 Kuwa na uzito uliokithiri.

5.UPUNGUFU wa nguvu za kiume kwa muda mrefu.

6.Maradhi,
Tafiti zinaonyesha kuwa kuna baadhi ya maradhi huweza kupelekea kupatwa na tatizo la tezi dume. Kwa mfano watu wenye maradhi ya sukari, na maradhi ya moyo wapo hatarini kupatwa na tezi dume ukilinganisha na watu wengine.

7.Staili za maisha.
Hapa tunazungumzia vyakula, vinywaji , kukaa kwa muda mrefu, kubana mkojo kwa muda mrefu .nk pia tafiti zinaonyesha kuwa watu wasiofanya mazoei wapo hatarini kupatwa na tatizo la tezi dume

Kujua zaidi kuusu afya yako ya uzazi.
Wasiliana nami
0755206375
Mr Dorah

28/12/2022

MWANAUME KUMBUKA KUTUMIA VURUTUBISHO acha kutumia dawaa Kwa sababu DAWA nyingi azitibu nguvu za kiume ila zitakupunguzia tatizo

Kwa ushauri zaidi https://chat.whatsapp.com/Gewtp589H7q9kzvK8VZpvR

28/12/2022

FAIDA ZA KUFANYA MAZOEZI YA MWILI

Zipo faida nyingi sana kwa mtu ambaye anafanya mazoezi mbali mbali ya mwili, unashauriwa kutenga muda angalau wa Nusu saa(dakika 30) kwa ajili ya kufanya mazoezi ili kuimarisha afya yako.

FAIDA ZA KUFANYA MAZOEZI YA MWILI NI PAMOJA NA;

- Mazoezi husaidia kuzuia tatizo la uzito kupita kiasi yaani Overweight/Obesity,

KUMBUKA: ufanyaji wa mazoezi pamoja na chakula(Diet) ndyo vitu vikubwa sana vya kuzingatia ili kuweka uzito wako wa mwili kuwa sawa.

- Mazoezi husaidia kuimarisha afya yako,Kinga yako ya mwili kuwa imara pamoja na kukukinga na magonjwa mbali mbali k**a vile;

• magonjwa ya moyo

• Ugonjwa wa Presha

• Tatizo la kiharusi au STROKE

• Aina mbali mbali za kansa/saratani

• Tatizo la Arthritis

• Ugonjwa wa kisukari(Type 2 diabetes) n.k

- Mazoezi husaidia kuondoa lehemu(Choletrol) pamoja na mafuta mabaya mwilini

- Mazoezi husaidia kuboresha mfumo mzima wa chakula na kuondoa matatizo kwenye mfumo wa umeng'enyaji wa chakula pamoja na matatizo mengine k**a vile; Kiungulia(Heartburn), Acid reflux, Metabolic syndrome n.k

- Mazoezi humsaidia mtu kuwa na furaha,kurelax, kuondoa msongo wa mawazo n.k

- Mazoezi husaidia sana kuboresha uwezo wako wa kufikiria ikiwa ni pamoja na kuimarisha afya ya ubongo

- Mazoezi husaidia kuwe na mzunguko mzuri wa damu mwilini

- Mazoezi huimarisha misuli pamoja na viungo mbali mbali vya mwili

- Mazoezi husaidia sana kuboresha afya ya Uzazi

- Mazoezi husaidia sana mtu kupata usingizi mzuri

- Mazoezi huupa mwili nguvu n.k

FANYA MAZOEZI BORESHA AFYA YAKO

Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi Kwa number 0755206375

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam