P.P.N Natural Products
Narejesha Afya Za Watu Kwa Kutumia Tiba Asili Na Virutubisho...
UJUE UGONJWA WA BAWASILI, MADHARA YAKE
Bawasiri ni mojawapo ya matatizo ambayo mara nyingi inapotokea humfanya muathirika kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba.Bawasiri husababishwa na kuvimba kwa mishipa ya damu aina ya vena katika eneo la mfereji wa haja kubwa.
A.NINI KINASABABISHA BAWASIR ?
Miongoni mwa visababishi vya bawasir ni;
-Tatizo sugu la kuharisha
-Kupata haja kubwa(kinyesi)kigumu
-Uzito kupita kiasi(OBERSITY)
-Ngono ya njia ya haja kubwa(ANAL S*X)
-Umri mkubwa na mambo yanayoongeza shinikizo katika tumbo.
B.DALILI ZA BAWASIR
-Kinyesi kuchanganyika na damu wakati wa kujisaidia
-Maumivu au usumbufu katika njia ya haja kubwa
-Kutokwa na kinyesi bila kujitambua(kuvuja kinyesi)
-Kijiuvimbe katika eneo la tundu(mlango)wa kutolea haja kubwa.
-Ngozi katika eneo la tundu la haja kubwa kuwasha.
-Bawasir kutoka wakati wa kujisaidia haja kubwa.
C.ATHARI ZA BAWASIR
-Upungufu wa damu mwilini(ANEMIA)
-STRAGULATED HEMORRHOID
-Kinyesi kutoka na kuvuja bila kujitambua na kusababisha kunuka kinyesi saa zote.
-Kukupunguzia morali ya kufanya kazi kutokana na maumivu hasa watu wanaokaa muda mrefu maofisini.
-Kuathirika kisaikolojia
-Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
-Kupungukiwa nguvu za kiume. kwa msaada zaidi wasiliana nasi 0628 708 604
07/04/2021
suluhisho la maumivu ya viungo na mifupa kusagana
FAHAMU ATHARI NA JINSI YA KUZUIA BAWASIRI INAWEZA IKAKUSAIDIA
ATHARI ZA BAWASIRI
✳Upungufu wa damu mwilini(ANEMIA)
✳Kinyesi kutoka na kuvuja bila kujitambua na kusababisha kunuka kinyesi saa zote.
✳Kukupunguzia morali ya kufanya kazi kutokana na maumivu hasa watu wanaokaa muda mrefu maofisini.
✳Kuathirika kisaikolojia
✳Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
✳Kupungukiwa nguvu za kiume
JINSI YA KUZUIA BAWASIRI
♨Kula mboga za majani na matunda na nafaka zisizokobolewa kwa wingi
♨Kunywa maji mengi lita sita hadi kumi na mbili kwa siku
♨Punguza kukaa kwa muda mrefu chooni bila kutoa choo.
Kwa ushauri zaidi wasiliana nami kwa:
Simu/whatsapp: 0628 708 604
TATIZO LA MIFUPA AU KUUMWA MIGUU/MAGOTI: OSTEOPOROSIS:
Tatizo hili hujulikana kwa jina la kitaalamu k**a Osteoporosis. Ugonjwa huu unatokana na kupunguka kwa protini na madini kwenye mifupa (madini chokaa/calcium). Hali hii hupelekea mifupa kuwa milaini na myepesi ambapo inaweza kuvunjika kirahisi. Kipindi cha utoto hadi kufikia umri wa miaka 30, ni kipindi ambacho mifupa hujijenga zaidi. Baada ya hapo mifupa huwa ina kawaida ya kupoteza madini zaidi.
Tatizo hili linatokea sana kwa watu wazima, hasa zaidi kwa wanawake ambao wamefikia kipindi cha kukoma hedhi (menopause), kuanzia miaka 50. Ni kipindi ambacho wanawake hupungukiwa na homoni yenye kazi ya kuilinda na kuikinga mifupa. Tatizo hili huwapata wanawake zaidi kwa kuwa wana mifupa midogo na myembamba kuliko wanaume. Miaka mitano (5) hadi aba (7) tangu mwanamke kukoma hedhi hupungukiwa na madini chokaa kwa asilimia ishirini (20%), zaidi ya wanaume. Kuanzia miaka 65 hadi 70 wanawake na wanaume hupoteza madini chokaa kwaasilimia sambamba.
NINI CHA KUFANYA
1. Mazoezi hasa kipindi ambacho umriu mepiga hatua
2. Kwa wale wenye uzito uliozidi, jitahidini kufanya utaratibu wa kupunguz
3. Jitahidi kupata madini chokaa (calcium) kwa wingi (maziwa freshi, maziwa mgando, mboga za majani)
4. Jitahidi kupata Vitamini D (mayai, maziwa, samaki, mboga za majani, pata jua)
VIRUTUBISHI
Kwa ambao tatizo limekuwa kubwa, inawapasa kujitahidi kupata virutubishi ili kuirejeshea mifupa nguvu na uimara, pia kuondokana na maumivu.
Virutubishi vifuatavyo vimewasaidia wengi wenye tatizo hili. Natural calcium
High calcium
KUKOSEKANA KWA UTE KATIKATI YA VIUNGO (JOINTS) - CARTILAGE
Kajiraba fulani ambako hujulikana kwa jina la kitaalamu k**a “Cartilage” (katileji) ambako hupatikana katikati ya mifupa. Kuna kitu fulani huwa kinapatikana katikati ya mifupa miwili ya goti la mnyama (ng’ombe, mbuzi) huwa wengi wanapenda kukila kwenye baada ya kuchemshwa au kupikwa. K**a unaijua hii, basi ndio katileji yenyewe.
Katileji inasaidia kuikinga mifupa isiumie.Vilevile inafanya kazi ya kusaidia kuubeba uzito wakati wa kutembea, kuinama, kunyoosha viungo au kukimbia.
Zaidi ya asilimia 85 (85%) ya katileji ni maji na jinsi umri unavyosonga mbele
20/03/2021
JE WEWE UNATATIZO LA KIWANGO CHA JUU CHA URIC ACID SOMA HII
◾Uric Acid Ni uchafu asilia wa mwili unaotokana na mmeng'enyo wa chakula ambacho kina purine K**a vile nyama nyekundu,vinywaji vyenye sukari K**a soda , coffein ,bia ,na baadhi ya samaki wa baharini km shellfish.
🔹Kwa kawaida mwili huchuja uric acid kupitia Figo na kutoka kwa njia ya mkojo K**a mwili wako ukishindwa kutoa uric acid Basi ujijenga kwenye damu na kusambaa kwenye joint na kushambulia joint hizo.
Viwango vya uric acid kiwango Cha kawaida kwa Mwanamke 2.4-6.0 mg/ld na mwanaume 3.4-7.0 mg/ld kwa mwanaume.
Na kiwango Cha juu Ni 7 nakuendelea Ni Hyperuricemia.
◾SABABU ZA URIC ACID KUWA KUBWA MWILINI
1.Vyakula (diet) K**a nyama nyekundu,soda, Bea,energy drink na
2.Matatizo ya Figo
3.Unene.
4.Ugonjwa wa kisukari
5.Kushuka kwa homoni ya throid
6.Matumizi ya baadhi ya dawa K**a aspirin,dawa za kisukari,
7.Msongo wa mawazo.
◾MADHARA YA KIWANGO KIKUBWA CHA URIC ACID MWILINI
1.matatizo ya Figo
2.Gout (maumivu kwenye joint)
3.Matatizo ya Moyo
4.Matatizo ya mapafu
5 .Mawe kwenye figo.
6.Maumivu makali wakati wa kukojoa
7.Matatizo ya macho.
8.matatizo ya mifupa.
◾WASILIANA NASI
0628 708 604
20/03/2021
DALILI ZA MTU MWENYE TATIZO LA MENO
Mara nyingi dalili hujionesha wazi wengi hujijua kuwa tayari wanatatizo na mara nyingi huwa haiitajiki vipimo, zaidi huhitajika uchunguzi kujua chanzo, dalili zake ni k**a
Meno kuuma wakati wa kula au mda wa baridi au joto
Kutokwa na damu kwenye fizi
Meno kuanza kulegea na kuachana na fizi
Kutoa harufu mbaya mdomoni, hii huonesha kuna tatizo
Meno kubadirika rangi mfano nyeusi, njano, kahawia na rangi zingine zisizo za kawaida
Fizi huwa nyekundu k**a damu ikiwezekana kuna na vidonda
Mdomo kuwa mkavu
Meno kufa ganzi
Meno kuchomoka au kutikisika
JINSI YA KUEPUKA MAGONJWA YA MENO
Ondoa mabaki ya chakula kwa kusukutua mdomoni na maji baada ya kutoka kula pia Kunywa maji mengi dakika 30 baada ya kutoka kula
Safisha meno yako hata mara mbili kwa siku
Punguza mawazo
Usivute sigara
Punguza au acha kunywa pombe
Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali, vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi
TIBA YA MATATIZO YA MENO
Matatizo ya meno linatibika kufuatana na mda wa tatizo, mara nyingi wagonjwa wamekuwa wakizalau dalili za tatizo la meno na kudhani kuwa hakuna madhara makubwa.
Tuna dawa ya kutibu Meno ambayo ni ya asili isiyo na kemikali ambayo hufanya mtu kupona na kuimarika kabisa. Dawa hiyo hutibu kwa mda kulingana na mda wa tatizo, tatizo halirudi tena maana huondoa chanzo pamoja na ugonjwa sio kituliza maumivu, ukianza kutumia ndani ya wiki moja huanza kutibu na huonesha mabadiliko, pia mgonjwa anapewa mfumo wa maisha ambao inatakiwa autumie kwasababu kuna mtindo wa maisha unaendelea kuongeza tatizo pia kuna mtindo unapunguza hatari ya ugonjwa.
Tunamshukru Mungu kwa uumbaji wake na kutupa dawa ambazo alizileta ili kutuimarisha na kutuponya, Mungu hakuumba dawa nyingine zaidi ya mimea na vitu vingine vya asili, japo wengi hudharau. Mungu tunaomba utuokoe na kutuponya.
20/03/2021
GANZI MIGUUNI/MIKONONI/ MWILINI & MIGUU KUWAKA MOTO
Ganzi ni moja ya tatizo/ugonjwa unaowakumba watu wengine sana na ni tatizo ambalo linakera sana kwa sababu hata unapoenda hospitali Mara nyingi hawapati tatizo lolote
NINI HASWA CHANZO CHA TATIZO HILI
1:UMRI
Kawaida mtu anapokua umri umeenda, mwili mzima uzeeka pamoja na mfumo mzima wa damu, hii husababisha mishipa midogo midogo ya damu kufa, au kuziba hii husababisha chakula na hewa ya oksijeni kutofika kwa ufasaha maeneo ya mbali k**a miguuni na vidoleni hali hii hupeleekea mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa safi hivyo ganzi hutokea
2:KISUKARI
Sukari inapokua nyingi kwenye mzunguuko wa damu hupelekea kuunguza mishipa ya damu halo hii husababisha mishipa kusinyaa ambalo hupelekea hewa ya oksijeni na chakula kutofika kwa ufadsaha maeneo ya mbali sana k**a miguuni na mikononi hali hii husababisha mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa hivyo husababisha ganzi
3:DAMU NZITO
Damu inapokua nzito pia hupelekea MTU kupata tatizo LA ganzi kwa ni husababisha kutofika kwa damu kwenye mishipa midogo midogo ya damu hii hupelekea ganzi pia
Kwa mawasiliano zaid tutafute kupitia hiyo namba hapo chini ili tukusaidie.
........0628 708 604......
20/03/2021
MGONGO ,MIGUU MIFUPA YA NYONGA NA JOINTS
Maumivu ya viungo kwa walio wengi husababishwa na kukauka kwa uteute na kuondolewa kwa Cartilage iliyo katika viungo.
Uteute na Cartilage Kwa pamoja husaidia kuondoa msuguano kati ya mifupa miwili inayokutana. Na hivyo kufanya kusiwe na maumivu yoyote.
Pamoja na kwamba tatizo hili linawakuta watu wengi hasa wanapofikia umri wa miaka 40 na kuendelea, lakini bado matibabu yake ni gharama kubwa na huchukua muda mrefu kupona na wengine hua hawaponi kabisa.
NINI UFANYE KUONDOKANA NATATIZO HILI?
Tumia Tiba zetu za Asili zitakazo kuongezea madini ya Chondroitin Glucosamine na calcium ambavyo ni dawa asilia zinazo Saidia kuongeza utengenezaji wa uteute kwenye joints hvyo kuzuia msuguano wa mifupa, pia huongeza afya na uimara wa cartilage kufanya joints kuwa imara zaid,
Kuwa na umri mkubwa (uzee) kusikukoseshe raha, Chukua hatua jali
Afya yako tulia elimu hii, unufaike
Wasaidie wengine kwa kuwafikishia hii taarifa.
Mawasiliano ni 0628 708 604...
20/03/2021
NINI CHANZO CHA MIGUU KUWAKA MOTO
Katika mwili wa binadamu, kuna tatizo la kiafya ambalo huambatana na dalili za mtu kuhisi maumivu, kuhisi kuwaka moto na kufa ganzi kwa viungo vya pembezoni mwa mwili yaani miguu na mikono. Tatizo hili kitaalamu hujulikana kwa jina la Peripheral Neuropathy.
Mwili wa binadamu hutawaliwa na mifumo ya neva au kwa kitaalamu Nervous System, ambapo katika mifumo hii kuna mfumo mkuu, central nervous system (ubongo na uti wa mgongo) na pia kuna mfumo wa pembezoni ambao ni kazi za mwili mbali na ubongo na uti wa mgongo (peripheral nervous system), mfumo huu wa pembezoni hujumuisha kazi za misuli, mapigo ya moyo, mmeng’enyo wa chakula tumboni, uwezo wa kuhisi baridi au joto, kugusa vitu na kujua ukali wa ncha ya kitu na kadhalika.
Matatizo haya ya kiafya (miguu au mikono kuhisi ganzi, baridi au maumivu) husababishwa na kuumia au kudhoofika kwa neva za pembezoni mwa mwili (miguuni au mikononi) na hivyo kupotea kwa uwezo wa kufanya kazi wa neva katika sehemu husika, miguuni au mikononi.
Dalili zinazoambatana na ugonjwa huu ni hizi zifuatazo:
1. Mtu kuhisi ganzi
2.Maumivu au kuwaka moto maeneo ya miguuni au mikononi,
3. Kuhisi k**a umevaa soksi au gloves wakati hujavaa,
4. Kuhisi k**a kuna kitu cha ncha kali kinakuchoma miguuni au kwenye vidole,
5. Kushindwa kushika au kunyanyua kitu,
6. Kuchoka kwa misuli na kadhalika.
Miongoni mwa mambo ambayo hupelekea neva hizi za pembezoni kudhoofika na kushindwa kufanya kazi vizuri ni haya yafuatayo naomba uyafahamu:
1. Kupungua kwa virutubisho mwilini, katika hili tunamaanisha mwili kutokuwa na vitamini vya kutosha na hasa mkusanyiko wa vitamini B, (Vitamin B Complex).
2.Matumizi ya dawa, mtu kuwa katika matumizi ya baadhi ya dawa, mfano dawa za kutibu kifua kikuu au za kupambana na virusi vya ukimwi huweza kumsababishia mtumiaji matatizo ya neva.
3. Uzito mkubwa wa mwili: Hali hii hupelekea maumbile ya viungo vya mwili mfano umbile la uti wa mgongo lionekane tofauti na ilivyo kawaida, kubadilika huku husababisha baadhi ya neva katika uti wa mgongo zikandamizwe zaidi na misuli au uzito wa mwili na hivyo kusababisha neva hizo zishindwe kufanya kazi vizuri, matokeo yake ni wewe kuanza kuhisi maumivi au kufa ganzi kwa miguu.
4. Ugonjwa wa kisukari: Mtu mwenye tatizo la kisukari huwa hatarini zaidi kuugua au kupata matatizo ya neva, (diabetic polyneuropathy).
Shinikizo la damu: Mtu kuwa na shinikizo kubwa la damu (High blood pressure) pia ni kihatarishi kinachoweza kumfanya mtu apate ugonjwa huu wa neva.
Baadhi ya vitu hatarishi vinavyoweza kumfanya mtu apate matatizo haya, vinaweza kuepukika kwa mtu kuyabadili maisha yake mfano, k**a ulikuwa hufanyi mazoezi ya mwili, basi ujitahidi kuupa mwili mazoezi ili kupunguza uzito wa mwili, kuepuka magonjwa ya kisukari na kuepuka kuwa na shinikizo kubwa la damu, kula chakula chenye virutubisho vya kutosha k**a vile PHYTOGUARD, NEOTONIC, nk.
K**a UKIMWI , PRESSURE, KISUKARI, KANSA, MATATIZO YA UZAZI,........ na mengine mengi tu
Kwa Maelezo zaidi tupigie number 0628 708 604
19/03/2021
UKISIKIA TATIZO LA UMEME WA MOYO(ATRIAL FIBRILLATION) UNAELEWA NINI?
Tatizo la umeme wa Moyo ni pale ambapo vyumba vya juu vya moyo vinavyohusika na kusukuma damu kunywe moyo (Atria) vinashindwa kufanya kazi sawa sawa kupelekea kushindwa kushirikiana na vyumba viingine vya chini (Ventricle) kuisukuma damu kuingia na kutoka kwenye moyo kwenda sehemu ziingine za mwili.
Umeme wenyewe wa moyo ni pale ambako moyo wenyewe unazalisha nguvu(umeme) itakayosaidia hivi vyumba vyake kusukuma damu. Umeme huu uzalishwa na seli ambazo hupatika katika chumba cha juu kulia(Right atrium).
DALILI ZA TATIZO LA UMEME WA MOYO
Mtu anapopata tatizo hili mapigo yake ya moyo huenda kasi sana kufikia mapigo100 hadi 175 kwa dakika,Maumivu ya kifua sehemu ya kulia, kuishiwa pumzi na kuchoka mwili mzima.
NINI VISABABISHI VYA TATIZO
Visababishi vya tatizo hili viko vingi vikiwemo mtu kuzaliwa na matatizo ya moyo kutofanya kazi vizuri, Shinikizo la damu, k**a mtu alishawahi kufanyiwa upasuaji wa moyo, moyo kupata maambukizi, Umri kua mkubwa moyo kufifia uwezo wake wa kufanya kazi nk.
Chukua darasa hili litakufaa!
contact us 0628 708 604....
14/03/2021
UGONJWA WA FIGO hutokea pale figo zinazopoteza uwezo wa kutenda kazi unaotokea taratibu na kudumu baada ya kitambo fulani. Hali hii hutokea taratibu, na huchukua muda wa takribani miezi kadhaa hata miaka. Ugonjwa sugu wa figo umegawanywa katika hatua kuu tano, kulingana na ukubwa wa tatizo.
Figo linapopoteza uwezo wake wa kutenda kazi, kusanyiko na limbikizo la maji, uchafu na sumu hutokea mwilini mwa mgonjwa. Aidha kushindwa kufanya kazi kwa figo husababisha pia kutokea kwa maradhi mengine k**a vile upungufu wa damu mwilini (anemia), shinikizo la damu (hypertension), ongezeko la tindikali kwenye damu (acidosis), ongezeko la lehemu na mafuta kwenye damu, na magonjwa ya mifupa.
Hatua ya tano ya ugonjwa sugu wa figo hujulikana pia k**a kushindwa kufanya kazi sugu kwa figo (chronic kidney disease au end-stage-renal disease).
Tofauti ya Ugonjwa sugu wa figo na kushindwa kufanya kazi kwa figo kwa ghafla (AKI) ni kwamba AKI hutokea ghafla, huchukua muda mfupi kati ya siku hadi wiki kadhaa kuwa tatizo kubwa zaidi. Tofauti nyingine ni kuwa AKI hutokana na tatizo linaloathiri figo moja kwa moja, mishipa yake ya damu au mtiririko wa mkojo unaotoka kwenye figo. Aidha ARF mara nyingi huweza kurekebishwa na mgonjwa akapona kabisa, ingawa kwa baadhi ya wagonjwa sehemu fulani ya figo inaweza isipate nafuu na ikaendelea kudorora kiutendaji kazi.
Hatua za Ugonjwa Sugu wa Figo
Hatua hizi zimegawanywa kulingana na kiwango cha GFR kilichofikiwa na figo husika. GFR kwa kirefu Glomerular Filtration Rate ni kiwango kinachoonesha uwezo wa utendaji kazi wa figo. GFR hupima uwezo wa glomeruli (chujio) la figo katika kuchuja uchafu, maji pamoja na sumu nyingine kwa kila dakika moja kwa mtu mwenye wastani wa urefu wa mita za mraba 1.73. Kadiri jinsi GFR inavyopungua, ndivyo inavyoashiria ukubwa wa tatizo katika figo.
Hatua ya kwanza huwa na GFR ya zaidi ya 90mL/dakika/1.73mita za mraba – mgonjwa huwa na madhara kidogo katika figo, huku figo zake zikiendelea kuchuja uchafu k**a kawaida.
Hatua ya pili ina GFR ya kati ya 60-89 mL/dakika/1.73mita za mraba - katika hatua hii, kiwango cha utendaji kazi cha figo hushuka kwa kiasi kidogo.
Hatua ya tatu, GFR huwa kati ya 30-59 mL/dakika/1.73mita za mraba. Katika hatua hii utendaji kazi wa figo hupungua zaidi,
wakati katika hatua ya nne GFR hushuka zaidi na kuwa kati ya 15-29 mL/dakika/1.73mita za mraba. Hapa utendaji kazi wa figo huwa wa chini mno;
na hatua ya tano mgonjwa huwa na GFR chini ya 15 mL/dakika/1.73mita za mraba. Hatua hii huitwa pia kushindwa kufanya kazi sugu kwa figo au CRF.
Katika makala tutatumia zaidi kifupisho cha CRF kumaanisha kushindwa kufanya kazi sugu kwa figo (chronic renal failure).
Ukubwa wa tatizo (epidemiology)
Ugonjwa sugu wa figo ni maarufu zaidi miongoni mwa watu wenye umri wa miaka 60 na kuendelea. Kwa mujibu wa ripoti ya kituo cha uthibiti wa magonjwa cha nchini marekani (CDC), Ugonjwa sugu wa figo ni miongoni mwa matatizo ya kiafya yanayojitokeza kuchukua chati za juu sana nchini humo. Ripoti hiyo ilionesha kuwa karibu asilimia 17 ya watu wazima wenye umri wa miaka 20 na kuendelea wanasumbuliwa na ugonjwa sugu wa figo.
Aidha ripoti hiyo ilionesha kuwa kribu watu nusu milioni wapo katika dialysis au wameshawahi kubadilishiwa figo. Mambo kadhaa yanahusishwa na ongezeko la ugonjwa sugu wa figo, miongoni mwayo ni ugonjwa kisukari, shinikizo la damu, unene na uzee. Aidha mabadiliko katika tabia na namna watu wanavyoishi pia vimeonekana kuchangia ongezeko hili kwa kiasi kikubwa.
Visababishi vya ugonjwa sugu wa figo
Pamoja na kwamba ugonjwa sugu wa figo hutokana na magonjwa kadhaa ambayo kimsingi yanaathiri figo lenyewe, visababishi vikuu vya ugonjwa sugu wa figo ni kisukari na shinikizo la damu.
Kisukari cha aina ya 1 na ya 2 husababisha hali iitwayo kisukari cha figo au kwa lugha nyingine diabetic nephropathy.
Shinikizo la damu k**a lisipothibitiwa vema, baada ya muda fulani, husababisha madhara katika figo, hali inayoitwa hypertensive nephropathy.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam