Nywele Natural Secret

Nywele Natural Secret

Share

Tunatoa ushauri wa nywele natural, tunauza original products za nywele. Nywele natural ni matunzo tu

14/02/2022

KWA NINI NYWELE ZAKO NI KAVU NA ZINAKATIKA SANA

1. Unatumia/Unapaka mafuta kwenye nywele kavu

2. Haujui hair porosity yako kwa hiyo inakua ngumu kujua namna ya kutumia/kupanga bidhaa zako.

3. Unatumia protein sana kwa nywele yako.

4. Hufanyi deep condition/Steaming mara kwa mara

5. Unaosha sana nywele kwa shampoo mpaka unaondoa zile natural oils

6. Unatumia maji tu kumoisturize jaribu kuongezea mambo mengine k**a vile..eg Hair tea ni nzuri sana

7. Hautumii Satin Bonet/kofia ya satini/Kitambaa cha satini wakati wa kulala

8. Nywele zinahitaji trimming/ kukata ncha na haujagundua hilo

JE, Ni sababu ipi inakusumbua wewe binafsi?

12/02/2022

Hello followers wangu so nimekuja kugundua watu wengi hawajui namna ya kuziosha nywele zao yaan njia sahihi za uoshaji nywele asili au zenye dawa ☹️☹️☹️

Leo naomba tuongelee hatua za kuosha nywele za asili uwe saloon au hata nyumban ni kwa wote wakubwa na wadogo pia hata wenye nywele za dawa

🎄Hatua ya kwanza ni pre shampoo au prepoo hatua hii ni baada ya kufumua nywele unataka kuziosha unachotakiwa kufanya pasha mafuta yako ya maji N**i ni mazur zaidi au alovera fresh ile gel yake unapaka kwenye nywele mpaka kwenye ngozi.

Mimi natumia sana sana alovera maana inanisaidia na kutoa mba Paka kisha zifunike kwenye plastic  ndani ya nusu saa baada ya hapo unaziosha.

🎄hatua ya pili ni shampoo:
hii njia hapa wengi huwa wanakosea yaan mtu anapaka stiming alafu anakuja kuosha na shampoo Hajui kuwa virutubisho vyote vinabebwa na kuondolewa na shampoo.

Hivyo basi kitu cha kufanya baada ya prepoo paka shampoo yako vizur zioshe nywele zako vizur

🎄hatua inayofuata paka stiming :
stiming zipo za aina mbili hapa kwahyo ww utachagua ipi nzr kwa nywele yako kwa wakati huo kuna stiming ya kawaida na stiming zenye protein baada ya kupaka kichwa kizima vaa plastic kofia kaa kulingana na maelezo ya kwenye hiyo stiming yanatakaje yaan hapa tujitahidi kusoma maelezo ya bidhaa tunazonunua mfano ukiambiwa nusu saa iwe Ivo kisha baada ya huo mda osha hizo nywele bila kupaka shampoo

🎄hatua inayofuata paka leave in conditioner:
haya ni mafuta au kimiminika chepesi ambacho ukipaka kwenye nywele zako nywele inakuwa laini na unachana bila maumivu kwawale ambao wanalalamika kuchana nywele kavu zinauma tumia hii baada ya kupaka hatua inayofuata ni kulingana na aina ya nywele zako K**a utatumia LOC au LCO METHOD

🎄hatua inayofuata unapaka mafuta au Shea butter :
hii ndo itakayo tunza unyevu wako wa nywele ili zisiwe kavu yaan itakusaidia nywele isiwahi kukauka haraka hapo kwenye mafuta paka mafuta mazito mfano kasto oil n.k

Na hizo ndo hatua za kuosha nywele 🤗🤗🤗K**a unahisi haujaelewa uliza chochote ntakujibu.

06/02/2022

UzuriAsilia tunawatakia wote Jumapili njema yenye baraka tele!

Karibuni sana.

04/02/2022

Mafuta ya asili na matumizi yake.

1.mafuta ya rosemary.
Hufanya nywele kuwa Nene. hufanya nywele zisiwe nyepesi na huzuia mvi za haraka kabla ya mda wa uzee.

2. Mafuta ya olive.
Hufanya nywele kung'ara kuwa soft Pia hufanya nywele kuwa nyeusi.

3.Mafuta ya N**i
Huzuia ukavu, hufanya nywele zinyooke,hupambana na MBA, hung'arisha nywele.

4.Mafuta ya nyonyo.
Hukuza nywele,hung'arisha nywele ,huzuia nywele kukatika hufanya nywele ziwe na afya.

5.Mafuta ya jojoba
Huimarisha nywele,huzuia nywele kupungua na kutunza ngozi ya kichwa ,huondoa uchafu kwenye nywele.

6.Mafuta ya parachichi.
Yanalainisha nywele, huzuia nywele kuharibika, yanajaza nywele.

7.Mafuta ya almond.
Hulainisha nywele, hupambana na mba husaidia mzunguko wa damu kwenye ngozi ya kichwa.

04/02/2022

Bei 27,000/=

"American Dream body cream ambayo imeundwa kwa mchanganyiko wa mmea wa cocoa na limao , pia inang'arisha ngozi .

Faida zake
🔻 inaondoa ukavu wa ngozi
🔻ndani yake kuna vitamin E kwa wingi ambavyo ni muhimu kwa ngozi
🔻Ni nzuri kwa ngozi za Mafuta
🔻Inamanukato yenye harufu nzuri ndani yake .

Inatoka U.K(uingereza) "

Original kabisa

Gender: Unisex

Nywele Natural Secret Tunatoa ushauri wa nywele natural, tunauza original products za nywele. Nywele natural ni matunzo tu

Photos from Nywele Natural Secret's post 04/02/2022

K**a kweli unazipenda na kuzijali nywele zako hakikisha hukosi hizi bidhaa kwenye ratiba yako ya nywele.

Photos from Nywele Natural Secret's post 02/02/2022

Kila picha ina bei yake!

Karibuni sana! Utapewa maelekezo ya jinsi ya kutumia kila bidhaa kupata matokeo mazuri

0717712827

01/02/2022

Una changamoto gani ya nywele njoo tujadiliane!

22/01/2022

1. Kuzisumbua nywele kwa kuchana mara kwa mara, kusuka misuko ya kuvuta nywele ndio chanzo kikubwa cha nywele kukatika na kutoona k**a zinakuwa.

2. Kuchana natural hair zikiwa kavu ni lazima zitakatika na kusababisha nywele kutokua vizuri.

3. Kutumia vichana vidogo kuchania nywele pia ni sababu nyingine ya nywele kukatika na kudumaa.

4. Kupaka nywele mafuta tu badala ya kuzipa unyevu (moisturizing) pia husababiaha nywele kukatika na kutokukua vizuri.

5. Kuchana nywele kuanzia kwenye ngozi balada ya kuanzia juu pia husababisha nywele kukatika.

6. Pia kutopunguza ncha za nywele zilichoka husababisha nywele kukatika.

7. Kukaa zaidi ya week 4 bila kuosha nywele na kufanya deep conditioner zinasababisha ukavu kwenye nywele zinazopelekea nywele kukatika.

8. Kusuka style za kukaza sana nywele zinasababisha nywele kukatika pia.

9. Matumizi ya moto (blow drying) mara kwa mara inasababisha nywele kuwa nyepesi na kukatika.

10. Kulala bila satin cape au mto pia husababisha msuguano wa nywele hatimaye zinakatika.

11. Hakikisha una utaratibu/ratiba maalumu ya kutunza nywele zako ambao ni lazima uufuate.

12. Kuwa na mawazo hasi ju ya nywele zako kwamba haziwezi kukua basi ni kweli hazitakua hakikisha unakuwa na positive attitude juu ya nywele zako.

Ukiweza zingatia yote hayo basi kuwa na nywele nzuri na zenye afya ni lazima

Karibu kwa maswali na kujifunza zaidi.

Photos from Nywele Natural Secret's post 22/01/2022

Kwa wote wenye shida ya
🔻Ngozi kavu na ya kupauka
🔻Nwele kavu na za kukatika
🔻Nywele hazikui na zimedumaa
🔻Nywele hazina mngao na rangi ya kuvutia

Basi hakikisha hukosi raw shear butter kwenye moja ya bidhaa muhimu kwenye swala zima la ngozi na nywele.

Bei elfu 25,000/=

Tupigie 0717712827

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Telephone

Address


Studio Kinondoni
Dar Es Salaam