Afya na ushauri
Ushauri kuhusu afya yako Kwa bei nafuu. Tunatoa huduma mbalimbali k**a
Ultrasound, Vipimo vya maabara, ECG, Kuonanana na Daktari (Consultation) na chanjo.
Pia utoaji wa dawa za kwenye mishipa (IV)
Tunasafisha vidonda mbalimbali
MWENYE CHANGAMOTO YA DAMU ANICHEKI INBOX
05/03/2025
UJUMBE MZURI KWAKO MAMA MJAMZITO, USIPITE BILA KUSOMA UJUMBE HUU...
Kwanini tunasema muhimu sana Mama mjamzito utumie OMEGA 3?
Tufahamu kwanza OMEGA 3 ninini, ,OMEGA 3 ni kurutubisho kinachojumuisha mafuta ya samaki, Vitamin E, na pia inajumuishwa na hizi Fatts Acid EPA pamoja na DHA.
OMEGA 3, nimuhimu sana Kwa Mama na mtoto aliyetumboni kwasababu matumizi ya OMEGA 3 yanaenda kukusaidia k**a ifuatavyo.
1: OMEGA 3 zinasaidia katika ukuaji wa kawaida wa mwili na kuimarisha ya afya ya ubongo wa mtoto,
✨Hivyo k**a unapenda uzae mtoto mwenye afya nzuri ya Akili tumia Omega 3, kwani atakuwa shapu sana.
2:Pia inasaidia katika mfumo wa msukumo wa damu na moyo kwa ujumla.
3:Pia Itakusaidia Kuepuka kuzaa mtoto mwenye tatizo la Utindio wa ubongo.
4: Itakusaidia Kuepuka kuzaa mtoto njiti.
5:Inasaidia kuepukana na kuzaa mtoto kwenye ulemavu wa viungo.
6:OMEGA 3 inasaidia uzae mtoto mwenye afya nzuri na Bora ya macho.
Hivyo OMEGA 3 nimuhimu sana Kwa afya ya Mama na Kwa afya ya mtoto aliyeyoko tumboni,
Kwani kutumia OMEGA-3 itakupa Faida nyingi zaidiii, Kwa mahitaji ya kupata hii OMEGA -3
Piga siku Kwa namba 0787326406
05/03/2025
*UZAZI WA MPANGO NA MATIBABU YAKE.
-ni uamuzi wa hiari unaofanywa na mtu binafsi mwanaume/mwanamke katika kupanga ni lini upate mtoto
-kuna njia mbalimbali za uzazi wa mpango k**a;
🔵Vidonge
🔵Njiti
🔵 Sindano
🔵Kitanzi
⚫️MADHARA YA VIDONGE
-Huharibu mfumo wa uzazi(uterus/mirija) kwa ndani
-Inaongeza uzito wa ute ili kuzuia mimba kutunga
-Kuumwa kichwa mara kwa mara
-Kuhisi kichef chef
-Kutokupata hedhi
-Inaharibu mzunguko wa hedhi
-Husababisha ugonjwa wa moyo
-Husababisha mtu kupooza upande mmoja
⚫️MADHARA YA NJITI
-cancer ya shingo ya kizazi
-shinikizo la damu
-maumivu wakati wa tendo la ndoa
-kukosa hamu ya tendo la ndoa
⚫️MADHARA YA SINDANO
-kupata hedhi ya mabonge mabonge
-kichwa kuuma mara kwa mara
-kuwa na kizungu zungu
-kuongezeka uzito zaidi
-usumbufu wa hedhi mfululizo
⚫️MADHARA YA KITANZI
-husababisha ugumba
-husababisha mama mjamzito kujifungua kwa operation
-husababisha nyonga kutanuka
-husababisha infection, hormone imbalance na kupelekea uvimbe kwenye kizazi n.k
Usisite kwasiliana nasi kwa 0787326406 Kwa matibabu na Ushauri zaidi.
05/03/2025
KARIBU UPIME UMEME WA MOYO WAKO KWA KIPIMO CHA ECG KWA BEI RAHISI.
TUPIGE 0787326406.
TUPO UPANGA MASHARIKI.
07/02/2025
*MATATIZO YANAYOSABABISHA KUTOSHIKA UJAUZITO AU MIMBA KUHARIBIKA*
Kuna maradhi kadhaa yanayosababisha wanawake wengi kwenye suala zima la uzazi, hivyo unahitaji matibabu sahihi kulingana na tatizo lako.
1. POLYCYSTIC OVARIAN SYNDROME
Hali hii huathiri homoni za mwanamke na kusababisha Matatizo ktk uzalishwaji wa mayai ya uzazi.
2. ENDOMETRIOSIS
Hali hii hutokea ambapo tishu zinazofanana na zile zinazopatikana kwenye mji wa mimba hukua nje ya mji wa mimba na kusababisha maumivu na Matatizo ya uzazi na kupelekea kutobeba ujauzito.
3. FIBROIDS
Hivi ni vivimbe vidogovido visivo vya saratani, hivi hutokea ktk mji wa mimba na kusababisha matatizo ya uzazi na maumivu makali wakati wa hedhi.
4. PELVIC INFLAMMATORY DISEASE (P. I. D)
Ni maambukizi ya viungo vya uzazi yanayosababisha mirija ya uzazi kuvimba na usipo tibu haraka maambukizi haya hupelekea mirija ya uzazi kuziba, uvimbe, kutoshika ujauzito au mimba kuharibika na kuathiri kizazi chenyewe.
5. OVULATION DISORDER
Ni Matatizo yanayosababisha kutokuwa nauwezo wa kutoa yai kila mwezi k**a vile Ovulation dysfunction, Unajikuta unaingia hedhi kila mwezi ila hakuna ovulation inayotokea.
6. PRIMARY OVARIAN INSUFFICIENCY
Ni hali ambayo Ovari za mwanamke zinashindwa kufanya kazi kabla ya kufika Miaka 40.
7.HORMONE IMBALANCE
Ni matatizo ya mvurugiko wa vichocheo aina ya PROGESTERONE na OESTROGEN kukosa uwiano na kupelekea kuathiri mfumo wa hedhi kiujumla, mfumo wa hedhi ukiharibika huleta changamoto kwenye uzazi.
8.THYROID DISEASE
Matatizo ya tezi ya thyroid yanaweza kuathiri uzazi k**a vile Hypothyroidism au Hyperthyroidism hii hupelekea mwanamke kukosa hedhi ya kila mwezi pia.
FANYA UCHUNGUZI MAPEMA ILI UWAHI MATIBABU KUEPUKA MADHARA KUWA MAKUBWA.
Wasiliana nasi kwa kupiga simu namba 0787326406
07/02/2025
TATUZO LA UTE KIWA MKAVU
Ukavu wa uke ni hali ambapo tishu za uke huwa kavu, au kuwa na kilainishi kidogo, na inaweza kusababisha usumbufu wakati wa tendo la ndoa.
Hii inaweza kusababisha dalili k**a vile kuwashwa ukeni, maumivu wakati wa tendo la ndoa, na ukavu wakati wa tendo la ndoa.
Pia ni kawaida zaidi kwa wanawake wenye umrj mkubwa, hasa baada ya kukoma kwa hedhi, wakati viwango vya estrojeni hupungua.
NINI KINASABABISHA UKE MKAVU?
1: Mabadiliko ya homoni k**a kufika ukomo wa hedhi, magonjwa sugu k**a PID.
2: Matumizi ya dawa kali k**a dawa za kutibu kansa na uzazi wa mpango.
3: Msongo wa mawazo na wasiwasi mwingi
4: Sabuni zenye kemikali kali na bidhaa za usafi wa uke zisizofaa
5: Upungufu wa maji mwilini na lishe duni
ATHARI ZA UTE MKAVU
~ Maumivu wakati wa tendo la ndoa
~ Kuwashwa na hisia za kuchoma
~ Kuongezeka kwa hatari ya maambukizi ya uke
~ Kukosa raha katika mahusiano ya ndoa
NJIA ZA KUPUNGUZA TATIZO LA UTE MKAVU
1: Kunywa maji ya kutosha kila siku angalau lita moja na nusu kwa siku.
2: Pendelea Kula vyakula vyenye mafuta mazuri ya asili k**a parachichi, mbegu za maboga, samaki wenye Omega-3 k**a pweza, chaza na uroto wa mifupa ya ng'ombe.
3. Acha matumizi ya sabuni zenye kemikali kali na tumia bidhaa za asili.
4. Punguza msongo wa mawazo kwa kufanya mazoezi mepesi.
Muhimu pia kumuona daktari wetu ili uweze kutatuliwa changamoto yako kwa weledi na wakati!.
Tupige namba hii 0787326406.
07/02/2025
SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUPATA UGONJWA WA NGIRI.
Ngiri huchangiwa zaidi na udhaifu wa misuli au mishipa iliyoshikilia viungo au maeneo ya mwili pamoja na ongezeko la presha katika viungo vilivyo dhaifu vya mwili (Muscle weakness/Fascia).
Hivyo huwapata zaidi watu walio katika mazingira yafuatayo⤵️;
➡️Kuwa na uzito mkubwa/Kitambi.
➡️Kunyanyua vitu vizito/kufanya mazoezi mazito.
➡️Kupata choo kigumu/kuharisha.
➡️Ulaji usiofata taratibu za kitabibu.
➡️Uvutaji sigara.
➡️Kuwa na umri mkubwa.
➡️Eneo liliwahi kufanyiwa upasuaji.
➡️Kuwa mjamzito.
Sababu zote hizi hupelekea kudhoofu misuli au viungo vya mwili na kupelekea tatizo hili kujitokeza.
Iwapo una dalili au ugonjwa huu wa ngiri/hernia tupigie kupitia namba 0787326406.
Kuonana na Daktari wetu ni bei nafuu ili kutibiwa tatizo lako!
07/02/2025
FAIDA ZA KUTUMIA KARANGA MBICHI
Karanga ni muhimu sana katika afya ya mwili wa binadamu, hivyo siyo chakula cha kupuuzwa, iwapo nitakapo kutajia faida zake hapo chini.
Zifuatazo ni faida chache za kutumia karanga mbichi;
1• Kutibu magonjwa ya moyo, ambapo kwa kawaida karanga ni chanzo kizuri cha mafuta mazuri aina ya Monounsaturated fats ambayo yanatiliwa mkazo kutumia kwa afya ya moyo. Kwa utafiti watu wengi wanaotumia karanga mara kwa mara hupunguza hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo kitaalamu uitwao CARDIOVASCULAR HEART DISEASE.
2• Kinga dhidi ya kiharusi (stroke)
Ugonjwa huu hatari unaweza kujikinga nao kwa kuwa na mazoea ya kula karanga tu, hi Ni faida nyingine ya kula karanga. Utafiti unanyesha kuwa kirutubisho aina ya Resveratrol ambacho pia hipatikana kwenye zabibu na mvinyo mwekundu (Red wine). Katika utafiti uliofanywa na Jarida la Kilimo na Kemia ya Chakula umeonyesha kuwa kirutubisho hicho cha karanga kinaimarisha utembeaji wa damu kwenye mishipa inayokwenda kwenye ubongo kwa kiasi Cha asilimia 30.
3• Kinga dhidi ya saratani(cancer)
Hii ni faida nyingine inayopatikana kutokana na ulaji wa karanga, ni Kinga dhidi ya ugonjwa wa saratani ya tumbo. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa unaonyesha kuwa virutubisho vya Folic acid, Phytosterols na Phytic acid na Resveratrol vinavyopatikana kwenye karanga huweza kutoa kinga dhidi ya ugonjwa wa saratani ya tumbo. Jarida la Kilimo na Kemia ya Chakula katika utafiti wao umeonyesha kuwa ulaji wa karanga hata mara mbili kwa wiki una uwezo wa kupunguza uwezekano wa kupatwa na saratani ya tumbo kwa 58% kwa wanawake na 27% kwa wanaume.
USHAURI
Kutokana na faida tajwa hapo juu tunapaswa kufanya karanga k**a kipaumbele katika vyakula vyetu vya kila siku ili tupate faida tajwa hapo juu na kuepukana na matatizo mbalimbali k**a stroke n.k
Hivyo kula karanga sio tu kwamba inafanya watu wafurahie mbegu hiyo, bali kiafya kuna faida zaidi.
Acha comment yako hapo chini
Share it as much as u can
Unaweza kuuuliza swali lolote.
Au tupigie kwa namba 0787326406.
19/07/2024
Mtindi una faida kadhaa kwa mfumo wa uzazi wa mwanamke, ikiwa ni pamoja na:
1. Kuboresha afya ya utumbo:
Mtindi una bakteria wenye faida (probiotics) ambao husaidia kuweka utumbo katika hali nzuri, kuzuia maambukizi ya fangasi na bakteria kwenye mfumo wa uzazi.
2. Kuzuia maambukizi ya fangasi:
Probiotics kwenye mtindi husaidia kupunguza kiwango cha fangasi katika mwili, hivyo kuzuia maambukizi ya fangasi ambayo yanaweza kuathiri mfumo wa uzazi.
3. Kukuza afya ya uke:
Mtindi unaweza kusaidia kudumisha uwiano wa bakteria wenye faida kwenye uke, kupunguza hatari ya kupata maambukizi ya bakteria (bacterial vaginosis).
4. Virutubishi muhimu:
Mtindi una vitamini na madini muhimu k**a kalsiamu, vitamini D, na protini ambazo ni muhimu kwa afya ya mifupa na misuli, ambayo inahusiana moja kwa moja na afya ya mfumo wa uzazi.
5. Kuimarisha mfumo wa kinga:
Probiotics kwenye mtindi husaidia kuboresha mfumo wa kinga, hivyo kuongeza uwezo wa mwili kupambana na maambukizi mbalimbali, ikiwemo yale yanayohusiana na mfumo wa uzazi.
Kuhakikisha mtindi una faida hizi, ni muhimu kuchagua mtindi wenye probiotics asilia na kuepuka ule wenye sukari nyingi na vihifadhi.
Watafute SerenOx Africa Kwa huduma nzuri na nafuu!
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Address
Dar Es Salaam
6838