EIJAZ natural
herbalist,health consultant,herbs medicine seller.
15/02/2023
(SABABU,USHAURI NA DAWA)
Kukojoa kitandani(Nocturnal enuresis or bedwetting) ni hali ta kutokwa na mkojo wakati umelala.Hali hii ni ishara ya matatizo ya udhibiti wa kibofu cha mkojo hutokea kwa watu wazima na watoto kwa sababu tofauti.Mara nyingi ni tatizo la akili ,wengi hawajui na kulichukulia kawaida hujitokeza wakati wa ukuaji wa mtoto na wazazi kulichukulia kawaida litaisha kadri ya mtoto anavyoendelea kukua lakini wengine huishi nalo mpaka kufikia kwenye ndoa zao na kua kero kwa mwenza.
🤔SABABU
*UGONJWA WA AKILI,mama kukaa na uchungu kwa muda mrefu husababisha athari kwenye ubongo wa mtoto kwani hukosa oxygen ya kutosha,mama akiugua sana kipindi cha ujauzito husababisha athari za ubongo kwa mtoto.
*URITHI,ugonjwa huu hurithiwa kutokana na historia ya familia 77% kma wazazi ni vikojozi na 40% k**a mzazi mmoja ni kikojozi basi mtoto atarithi
*HOMONI,Antidiuretic hormone(ADH)hutengenezwa na mwili wakati umelala ili kupunguza uzalishwaji wa mkojo uzalishwaji wa homoni hiyo ukiwa mdogo basi hupelekea tatizo hili la kujikojolea
*MSONGO WA MAWAZO,UCHOVU KUPITILIZA.ni moja ya visababishi vikubwa tu kwa watu wanaojikojolea kitandani
*SABABU ZA KIMAUMBILE,kuvimba kwa tezi dume,saratani ya kibofu cha mkojo,kufanya kazi kupitiliza kwa misuli ya kibofu cha mkojo,kibofu cha mkojo kidogo hvyo hakiwezi kutunza kiasi kingi cha mkojo. Hizo ni miongoni mwa sababu chache za ugonjwa huu.
🤗DAWA/SULUHISHO
(a)Chukua unga wa Hulinjani na uchanganye na Asali robo lita kisha apewe kikojozi iwe mkubwa ama mdogo kijiko cha chai kabla ya kula chochote Asubuhi na muda wa kulala kwa siku moja ba zaidi
(b)chukua ndevu za mahindi na manyoya ya kuku ya mkiani utachemsha atakunywa kutwa mara 3 kwa wiki moja na zaidii.. ukishindwa unaweza kutumia ndevu za mahindi pekee ni dawa nzuri sana nitatoa faida zake siku nyingine nikijaaliwa.
(c)Siki ya tufaha(APPLE CIDER)vijiko viwili vya chai kwenye glasi moja ya maji ya kunywa unaweza kuchanganya na Asali ili kupata ladha nzuri mgonjwa anywe mchana au wakati wa chakula cha jioni.
Dawa za miti shamba zilizoandaliwa ninazo ila tumia elimu hii kuokoa gharama pia mfundishe na mwengine ni swadaka
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam