Niima na Afya
Jifunze mambo muhimu kuhusu Afya yako. Pata elimu ya afya ,magonjwa na TIBA. Tunatibu magonjwa sugu kwa kutumia virutubisho Tiba (FOOD SUPPLEMENTS).
ELIMU NA USHAURI NI BURE KABISA
14/03/2022
SABABU YA KUSAGIKA KWA VIUNGO (ARTHRITIS)
👉Ugonjwa wa viungo unasababishwa na hitilafu yoyote katika sehemu hizo za maungio ya mifupa.
👉Inaweza kuwa mifupa laini (Gegedu) kwa jina la kigeni linafahamika kwa Articular cartilage inalika.
👉Gegedu kwa kawaida hulinda viungo na kuvifanya viwe laini ili vifanye kazi vizuri na kwa uhuru.
👉Aidha Gegedu pia husaidia kupunguza shinikizo(pressure) kwenye viungo,
kwa mfano:- mtu anapotembea shinikizo kubwa huwa kwenye viungo vya miguu, Gegedu huisaidia mifupa kuhimili shinikizo hili.
👉Bila kiwango cha kawaida cha Gegedu au k**a Gegedu imeharibika, mifupa huanza husagana na kusababisha maumivu makali, kuvimba na kukak**aa kwa viungo(Joints).
👉Upungufu wa kilainisho cha mwili (synovial fluid),maambukizi ya vijidudu(infection) katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo yote.
👉Ugonjwa huu husababishwa na kuharibika kwa Gegedu, kuvimba kwa viungo kunaweza kusababishwa na magonjwa yanayosababishwa na mfumo wa kinga (autoimmune) haya ni magonjwa yanayosababishwa na mfumo wa kinga kushambulia tishu za mwili kimakosa na kuziharibu.
👉Kwa kawaida, uvimbe wa viungo huondoka baada ya kutibiwa hata hivyo baadhi ya wakati uvimbe hauondoki.Hili linapotokea, una yabisi-kavu sugu,ambapo ugonjwa huu naweza kutokea kwa wanaume au wanawake lakini aina nyingi za ugonjwa huu huwapata zaidi wanawake kuliko wanaume.
TATIZO LINATIBIKA, WAHI SASA!!
☎️Wasiliana nasi kwa simu namba 0657984202
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Ilala Boma
Dar Es Salaam