Shamila na Afya

Shamila na Afya

Share

Kwa magonjwa yasiyoambukiza

03/10/2022

TEZI DUME INATIBIKA BILA UPASUAJI

+255767998676

Tezi dume hii kitaalamu hufahamika k**a PROSTATE GLAND.

Hii Ni tezi inayopatikana katika mfumo wa uzazi wa kiume.Tezi hii inapatikana jirani na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo.

Tezi hii Ina kazi ya kuzalisha majimaji ambayo hubeba mbegu za kiume.
Majimaji hayo ndio Yale anayotoa mwanaume anapofikia kilele.

Hivyo tezi hii Ni muhimu sana katika mfumo wa uzazi wa mwanaume.

Tezi hii si kubwa saana, inapata sentimita zisizozidi 4, lakini tezi hii HUKUA kadiri UMRI UNAVYOONGEZEKA.

DALILI ZA KUVIMBA KWA TEZI DUME:-

✓Kukojoa Mara kwa mara.
✓kubakiza mkojo kwenye kibofu.
✓kukojoa saana usiku.
✓Maumivu wakati wa kukojoa na mkojo usioenda mbali.
✓Kupungukiwa nguvu za kiume
✓UTI ya Mara kwa mara.
✓Mawe kwenye kibofu kutokana na mlundikaniko wa mkojo.
✓Figo kujaa maji,hii Ni kwasabab mkojo huo unarudi nyuma kuelekea kwenye figo.
✓Kupoteza fahamu.
✓Maumivu ya Mara kwa mara ya kiuno kwa nyuma ya mgongo na mapaja.
✓Uume kushindwa kusimama vizur.
✓Kuwa na wakati mgumu wakati wa kukojoa na kuzuia mkojo.

ATHARI ZA TEZI DUME K**A HAUTAIWAHI KUTIBIWA:-
1)Kushindwa kabisa kukojoa.
2)Kupatwa na maambukizi ya UTI
3)Kupatwa na vijiwe kwenye kibofu.
4)Uharibifu wa kibofu unaweza kutokea.
5)Figo inaweza kuharibika.

Kwa ushauri Na tiba +255767998676

Au WhatsApp https://wa.me/0686687484

03/10/2022

Suluhisho la Tezi dume

02/10/2022

TEZI DUME NA KANSA YA TEZI DUME NA TIBA YAKE
0767998676
Dalili za kupanuka kwa tezi dume

Dalili huonekana baada ya umri wa miaka ya hamsini . Karibu wanaume wote wenye umri wa sabini na themanini huwa na tatizo hili.Dalili huanza polepole na kuzidi jinsi miaka inavyoongezeka.Dalili hizi ni k**a zifuatazo:

Kukojoa mara nyingi hasa nyakati za usiku.Hii ni dalili ya mapema sana.
Kulazimika, mara nyingi hasa nyakati za usiku, kutumia nguvu kuanzisha mkojo kutoka. Hata pale mgonjwa anahisi kibofu kimejaa. Hii ni dalili ya mapema sana.
Mkojo kutiririka polepole, hukatikakatika na hutumia nguvu kutoka.
Mkojo kushidwa kutoka hata wakati mtu anapohisi kukojoa.
Mkojo kuendelea kutoka kidogokidogo baada ya kukojoa, matone ya mkojo huendelea kutoka hata baada ya kukojoa hivyo nguo za ndani hulowa.
Kibofu hakiishi mkojo.
Matatizo ya tezi dume iliyotanuka

Tezi dume ikitanuka sana huleta matatizo mengi kwa wagonjwa wengine hali hii isipotibiwa. Matatizo hayo ni k**a yafuatayo:

Mkojo kukosa kutoka kabisa
Wagonjwa wenye tatizo hili lazima wawekewe katheta ili kumimina mkojo.
Madhara kwenye kibofu na figo
Kwa sababu ya kibofu kuwa na mkojo wakati wote, ukuta na misuli yake hupanuka na mwishowe hudhoofika hivi kwamba haiwezi kuzuia mkojo.
Kwa sababu ya kibofu kujaa
mkojo hurudi kwenye figo na mwishowe huharibu figo.
Ugonjwa wa tezi dume husababisha mkojo kutiririka polepole na mtu kukojoa mara nyingi hasa usiku.
Maambukizi na mawe
Kwa sababu kibofu hakimimini mkojo wote kuna hatari kubwa ya maambukizi kwenye njia ya mkojo nakuwa na mawe kwenye kibofu.
Kumbuka
Kutanuka kwa tezi dumehakusababishi ugonjwa wa saratani.

Utambuzi wa kupanuka kwa tezi dume
Historia na dalili zikiashiria uwepo wa hali hii, basi uchunguzi ufuatao hufanywe.
Uchunguzi wa ukubwa wa tezi

Uchunguzi huu hufanywa kwa kuingiza kidole chenye glavu nyuma hadi kwenye tezi dume. Daktari huweza kujua ukubwa na hali yake. Iwapo mtu ana ugonjwa huu tezi dume ni kubwa kuliko kawaida, laini na gumu yote pamoja. Iwapo tezi lina vifundo basi inaweza kuwa na kansa (saratani)au inaweza kuwa na

Dalili za tezi kilichopanuka na saratani hufanana.Lazima uchunguzi wa kina ufanywe ili kujua ni ugonjwa upi.

PIGA 0767998676 KWA USHAURI ZAIDI

15/08/2022

Changamoto ya mifupa na viungo imekuwa ni tatizo kubwa sana kwa watu wengi katika kipindi hiki, Ute Ute (Synovial fluid) unapatikana katika maungio ya wengi kupunguza au kuisha kabisa na kupelekewa mifupa kulika hivyo mtu kujikuta akipata maumivu makali na hata kushindwa kufanya shughuli zake kwa uhuru.Lakini tumaini la uponyaji lipo kwani uteute utaweza kuzalishwa kwa wingi na mifupa Milaini (Cartilages) kuweza kuzalishwa upya na kuondoa Yale maumivu ambayo mtu anapitia..Kwa ushauri na msaada kuhusu hili karibu ninaweza kukusaidia.Nipigie kupitia 0767998676

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Kijichi
Dar Es Salaam