Marther bee nutrition
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Marther bee nutrition, Health/Beauty, Mlimani city, Dar es Salaam.
Fahamu kwa kina kuhusu Tezi dume👇
ASILIMIA KUBWA YA WANAUME WANAOFIKIA UMRI WA MIAKA 40+ WAPO KWENYE HATARI YA KUPATA TATIZO LA KUTANUKA KWA TEZI DUME.
Habari ndugu!!!!!
Elimu hii inawezekana haikuhusu moja kwa moja,lakini naamini inakugusa kwa njia moja au nyingine,inawezekana wewe sio mwanaume,lakini una ndugu,jamaa,rafiki wa kiume au mume au Baba.
Hivyo soma kwa makini kwa niaba ya hao ndugu zako wa kiume,na k**a wewe ni mwanaume,soma kwa makini zaidi.
Kuna kitu ambacho watu wengi huwa hawakielewi vizuri, wanakisikia sikia tuu juu juu lakini hawaelewi hasa kiundani,kinasababishwa na nini,na madhara yake ni nini.
Na mpaka wengine wanashangaa kwanini viongozi wakubwa wanaugua huo ugonjwa mpaka wengine wanakufa wakati wana pesa za kutosha. Kumbe suala sio pesa, suala ni elimu ya hilo tatizo lakini pia woga wa mwanaume wengi hawasemi na wanaona aibu.
PROSTATE GLAND (TEZI DUME).
Ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume.Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (re**um) na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra). Ina umbo la yai,ina ukubwa wa kawaida japo ukubwa huongezeka kadri umri unavyoongezeka.
Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la kujamiiana(sex).
Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hufanya shahawa (semen). Aidha majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya fallopian tayari kwa utungisho na yai la k**e.
Vilevile husaidia kupunguza hali ya kitindikali iliyopo katika uke, ambayo k**a isiporekebishwa, huweza kuua mbegu nyingi za kiume na kufanya utungisho kuwa wa tabu.
Vile vile inafanya kazi ya kuzuia mkojo usitoke wakati wa tendo la ndoa.
UKUBWA WA TEZI DUME.
Ukubwa wa kawaida wa tezi dume kwa mtu mzima ni kati ya 15 na 30 c
Na uzito wa kawaida ni kati ya 20 na 25 grams.
Na vipimo vya kawaida ni 4×2×3 centimeters, sawa na 1.6×1×1.2 inches.
SEHEMU KUU ZA TEZI DUME.
1.PERIPHERAL ZONE(SEHEMU YA NJE)
~Hii ni sehemu ya nje ya tezi ambayo madakari wengi hutumia hii tezi kubaina k**a kuna tatizo kwenye tezi kwani ni virahisi kiugusa k**a daktari akiingiza index fingure(kidole cha kusontea) kwenye njia ya haja kubwa. Kukua kwa sehemu hii hakuwezi kuathiri utokaji wa mkojo.
2.TRANSITIONAL ZONE(SEHEMU YA KATI)
~ Hii ni sehemu ya tezi ambayo ikikua yani ikiongezeka ukubwa tunasema KUVIMBA KWA TEZI TUME kitalamu BENIGN PROSTATIC HYPERPLASIA (BPH) kuna uwezekano mkubwa wa tezi dume iliyovimba kuzuia njia ya mkojo kupita. Kwani ndio sehemu ya tezi iliyo karibu kabisa na njia ya mkojo. Mara nyingi hii sehemu ikikua ndio inayo sababisha matatizo ya kukojoa(obstructive symptoms).
Tezi hii pia daktari anaweza kuibaini kwa kutumia kidole kipimo hiki huitwa DIGITAL RE**AL EXAMINATION(DRE)
hii ni kwa sababu ikikua inasukuma ile sehemu ya pembezoni yani peripheral zone kuelekea njia ya haja kubwa. Hivyo dakatri anaweza kubaini k**a tezi imekua au laa.
KUKUA/KUTANUKA KWA TEZI DUME.
Kukua au kutanuka kwa tezi ya kiume kitalamu tunaita BEGINNING PROSTATIC HYPERPLASIA (BPH).
Hili tatizo mara nyingi huanza baada ya miaka 40 hivi na dalili huja kujionesha uzeeni. Na mpaka mtu apate Cancer ya Tezi Dume,basi huyo mtu amekua na tatizo la kutanuka kwa tezi dume kwa zaidi ya miaka 7 mpaka 10 bila matibabu yoyote.
Hivyo tezi inaweza ikawa kubwa sana lakini haina dalili, hii ni kutokana na sehemu gani ya tezi iliyovimba au kuongezeka.
Tezi inapoonesha dalili jua tatizo hilo ni sugu na liko katika hali mbaya.
DALILI ZA KUVIMBA KWA TEZI DUME.
1. Kukojoa mara kwa mara.
2. Kubakiza mkojo kwenye kibofu.
3. Kukujoa sana usiku.
4. Maumivu wakati wa kukojoa na mkoja usioenda mbali.
5.Kupungukiwa nguvu za kiume.
6. U.T.I ya mara kwa mara.
7. Mawe kwenye kibofu kutokana na mrundikano wa mkojo.
8. Figo kujaa maji.
9. Kupoteza fahamu.
10. Maumivu ya mara kwa mara ya kiuno kwa nyuma ya mgongo na mapaja.
11. Kutoa damu wakati wa kukojoa au kwenye mbegu za kiume wakati wa tendo la kujamiiana.
12. Uume kushindwa kusimama vizuri.
13. Kuwa na wakati ngumu wakati wa kukojoa na kuzuia mkojo.
JINSI YA KUBAINI KUVIMBA KWA TEZI.
~Kumbuka BPH sio kansa ni uvimbe tu wa kawaida wa tezi lakini kumbuka tezi hii inaweza kuvimba pia kutokana na kansa ya tezi dume (prostate cancer).
1. Uchunguzi wa kawaida kwa kutumia kidole kupitia njia ya haja kubwa kuangalia k**a tezi ina tatizo. Kipimo hiki huitwa DIGITAL RE**AL EXAMINATION. Baada ya kipimo hicho daktari huandika alicho kigusa k**a ni ugonjwa au iko kawaida.
2. Hiki ni kipimo cha kupiga picha kibofu cha mkojo kinaitwa CYTOSCOPE. Kumbuka kipimo hiki una ingiziwa waya flani wenye tochi mbele kwenye njia ya mkojo huku huo waya umeunganishwa kwenye screen. Hivyo chochote huo waya utakacho murika kitaonekana kwenye screen.
Ubaya wa hiki kipimo ni kwamba kinaweza kuumiza kuta za njia ya mkojo na baada ya wiki k**a mbili njia inaweza kuziba jeraha linapo pona. Ila ni kipimo kizuri sana.
3. Kipimo kingine kinaitwa RE**AL UTRASOUND hiki ni kipimo cha kupiga picha kupitia njia ya haja kubwa (re**al) na kutoa picha kwenye jarida gumu kumsaidia daktari kusoma.
4. Kipimo cha kutofautisha kati ya uvimbe wa kawaida(BPH) na kansa(PROSTATE CANCER).
Kipimo hiki kinaitwa PROSTATIC SPECIFIC ANTIGEN. Hii ni protein inayotolea kwa wingi endapo kuna kansa ya tezi dume. Hivyo damu ya mgonjwa itachukuliwa na kupelekwa maabala kuchunguza k**a ni nyingi kupita kiasi kwenye damu. K**a hii protein ipo kawaida basi uvimbe huo sio kansa ni BPH. Lakini k**a kiwango ni kingi uvimbe huo ni KANSA.
Hivyo uchunguzi zaidi unahitajika k**a kuchukua sample ya kinyama kutoka katika tezi na kupeleka maabala.
PSA ya kawaida inapaswa iwe 4 nanogram per milliliter {ng/ml} ya damu.
Lakini kwa wanaume wenye umri wa miaka 59 kushuka chini,PSA yao inatakiwa iwe kati ya 2.5 na 3 ng/ml.
Kwenye umri wa miaka 60 hadi 69,PSA yao inatakiwa uwe 4 ng/ml.
Na wenye umri wa miaka 70 na kuendelea, PSA yao inatakiwa isizidi 5 ng/ml.
Angalia video ya Dr. kutoka hospital ya moyo ya Jakaya Kikwete akielezea PSA ambayo mwanaume anatakiwa ku nayo,na madhara ya Operation ikiwemo kuvaa pumpers na kutoweza kufanya tendo la ndoa kwa miezi 6 mpaka mwaka.
Na kumbuka mpaka mtu mwenye tatizo la tezi dume,afikie hatua ya kupata SARATANI ya TEZI DUME, basi amekaa na hili tatizo si chini ya miaka7 mpaka 10.
Hivyo kwa kwa lugha nyepesi,tunasema mtu kupata SARATANI ya TEZI DUME ni uzembe na aibu ya kutokusema mapema.
MATIBABU YA KUKUA KWA TEZI DUME.
1. Tezi dume k**a haina dalili zozote mara nyingi huwa haishughulikiwi sana hospitali lakini dawa za kupunguza kasi anaweza pewa mgonjwa. Lakini ni mara chache.
2. K**a tezi imesha anza kuleta dalili k**a usumbufu wakati wa kukojoa siku hizi kuna operation ya bila kukata inaitwa TRANS URETHRAL RECTIONING OF PROSTATE AU CHANNEL TURP.
Hii operation inafanywa k**a akiwa anafanya kipimo cha CYSTOSCOPE. Lakini hapa anaweka wire mbele kiko cha mviringo kinapitishwa kwenye njia ya mkojo kina enda kukata kinyama kinachoziba, i mean tezi iliyovimba. Hapa inazibua njia ya mkojo ili mtu akojoe. Ukifanyiwa operation hii vizuri tezi hujirudia baada ya miaka k**a 3-5 tangu siku ya operation.
MADHARA YA TIBA HII
-Kukosa uwezo wa kufikia kishindo yani hutoi shahawa(RETROGRADE EJ*******ON) wazee wengi hulalamika sana baada ya hii operation hivyo ushauri nasaha lazima utolewe ili mgonjwa ajue nini madhara yake kabla ya operation.
-Kuziba kwa njia ya mkojo kutokana na kuumia kwa njia hizo wakati wa kitendo hicho. Panapokua panapona hilo kovu linaziba njia ya mkojo.
3. Operation kubwa ya kuondoa tezi hio hufanyika kwa kufungua kibofu cha mkojo na kutoa hiyo tezi. Madhara ni mengi sana kuhusu hii bora ile namba mbili.
4. Mionzi(X-Ray) hufanywa kwa mgonjwa ambae amesha athirika na saratani ya tezi dume na ipo kwenye stage mbaya ili kupunguza makari. Sio njia nzuri sana maana huua cells za mwili ambapo hupunguza umri wa kuisha.
VYANZO VYA TATIZO LA KUKUA KWA TEZI DUME.
1. CHAKULA(DIET FACTOR).
- Utafiti unaonesha chanzo kikuu cha kukua kwa TEZI DUME ni upungufu wa virutubisho na madini muhimu sana ya ZINK,IRON(MADINI YA CHUMA) na LYCOPENE.
Na hii ni kwasababu mtu anapofikisha umri wa miaka 40 na kuendelea,mwili unapoteza uwezo wa kufyonza virutubisho kutoka kwenye chakula kwa 6% mpaka 10%.
Na wanaume wengi wanaopenda kula nyama nyekundu sana na wasiopenda kula matunda na mboga za majani wapo kwenye hatari kubwa ya kupata Cancer ya TEZI DUME.
LYCOPENE.
-Hivi ni virutunisho vinavyotokana na nyanya,hivyo mwanaume anasahuriwa kula(kutafuta) nyanya 8 mpaka 10 kila siku. Lakini pia virutubisho hivi hupatikana kwenye mbegu za maboga na tikiti maji.
Lycopene ina uwezo wa kupenya kwenye tezi dume na kuondoa tatizo lolote na kuzuia kabisa kukua kwa tezi dume. Pia ina uwezo mkubwa wa kuzuia kansa ya tezi dume.
2. UMRI(AGE).
Hii ni factor muhimu na kubwa sana ya kupata TEZI DUME. Wanaume wengi wanapofikisha umri wa miaka 40 na kuendelea,tezi dume inaanza kuongezeka kwa haraka sana ukilinganisha na wanaume ambao hawajafikisha umri huo,na hii ni kwasababu,unapofika umri huo mwilini unapoteza uwezo wake wa kufyonza virutubisho kutoka kwenye vyakula kwa asilimia kubwa.
Uwioano unaonesha kati wanaume 5 wenye umri wa kuanzia miaka 40,mmoja(1) kati yao ana tatizo la kukua kwa tezi dume.
Lakini kati ya wanaume 10 wanaokutwa na saratani ya tezi dume,sita(6) kati yao wanakua kwenye umri wa miaka 65.
3. NCHI/BARA/KANDA(ETHNICITY).
Kutokana na tafiti za National Cancer Institute,zinaonesha WANAUME wengi wa bara la Africa ndio wanaopata matatizo ya TEZI DUME zaidi kuliko Wazungu.
Katika utafiti uliohusisha waafrika 2000 na wazungu 2000,ilibainika kua 8.3% ya waafika walikua wanatatizo la tezi DUME,lakini wazungu 3.3%.
Na hii ni kwasababu waafrika wengi hatuna utaratibu wa kwenda hospital kuchunguza afya zetu mara kwa mara,wakati wazungu kwao ni lazima.
Lakini pia kutokana na rangi ya ngozi zetu zina sharabu sana mwanga hivyo kufanya mvurugiko wa cells bila kua na vitu mbadala(supplements) vya kurekebisha cells hizo.
4. FAMILIA (FAMILY HISTORY).
K**a una baba au kaka aliewahi kupata tatizo la Cancer ya TEZI DUME, hii inaongeza uwezekano mara mbili zaidi ya wewe kupata pia hili tatizo.
5. MABADILIKO YA HOMONI (HORMONE IMBALANCE).
Mabadiliko ya hormone yanachangia sana kutanuka kwa Tezi Dume,na sababu kubwa ya hormone imbalance ni pamoja na sumu tunazoingiza kwenye miili yetu kila siku,na sumu hizi tunazipata kwenye mazingira yetu ya kila siku,kwasababu aina ya maisha tunayoishi yamekua na uchafuzi mwingi wa mazingira na kujikuta tunaingiza sumu nyingi sana mwilini,ambazo pia zinapunguza ufanisi wa vyakula tunavyokula,na sumu hizi tunazipata kwenye maji,vinywaji vingine k**a soda,bia,juice,hewa tunayovuta,viwanda,mioshi ya magari,mioshi ya sigara,AC,vumbi,dawa za hospital,sumu na mbolea zinazowekwa kwenye vyakula wakati wa kulima,dawa za kutunzia mazao,na kwa uzalishaji wa karne hii watu wanatumia kemikali nyingi kulimia na kutunzia nyanya,matikiti maji,maboga na matunda mengine mengi,wafanya biashara wanachoma sindano za sumu ili zisioze au ziwahi kuiva kabla wakati.
Pia uzito mkubwa unachangia pia kubadilika kwa hormone.
VITU VYA KUZINGATIA ILI KUJIKINGA NA UKUAJI WA TEZI DUME.
• Kula samaki wenye omega 3 na 9 nyingi k**a Salmon fish.
• Mafuta mzuri yanayopatikana kwenye Mbegu,Karanga,korosho,mzaituni na parachichi.
• Kula mboga za majani kwa wingi.
• Protein hasa inayopatikana kwenye mimea zaidi kuliko kwenye wanyama.
• Epuka kula vyakula vya viwandani,spicy food,mikate,sukari,nyama nyekundu,pombe,chumvi,caffeine, kahawa,chai na soda.
• Fanya mazoezi mara kwa Mara.
• Punguza Uzito{Loose Weight}.
• Kusawazisha Hormone{Manage Hormone}.
• Punguza msongo wa mawazo{Manage Stress}.
• Kunywa maji mengi hasa wakati wa mchana.
• Tumia virutubisho{Take Supplements}.
- Virutubisho vyenye madini yafuatayo kwa wingi.
~Pollen Extract.
~Zink.
~Vitamin D.
~Lycopene.
~Iron.
SURUHISHO NA NAMNA YA KUJIKINGA.
Huyu Dr. Linus Pauling,aliepata tuzo ya Nobel Prize mara mbili,kwa uchunguzi aliofanya,akasema;-
" Karibia magonjwa yoote yanayomkumba mwanadamu,ukiyafuatilia na kuchunguza kwa makini,chanzo chake kikuu ni upungufu au ukosefu wa lishe/virutubisho mwilini"
Hivyo k**a unataka kutatua tatizo hilo,mpatie lishe/virutubisho vilivyokosekana na sio dawa.
NINI MAANA YA VIRUTUBISHO?
Virutubisho ni vyakula,matunda,mboga mboga na mimea yenye madini na vitamins nyingi,zilizolimwa na kuandaliwa kiasili bila kuwekewa kemikali hatarishi,na zikawekwa kwenye mfumo rahisi kutumia ili kumpatia mwanadamu lishe kamili na Kiwango kikubwa cha madini ambayo mwili wa binadamu unavikosa kutoka kwenye vyakula vya kawaida tunavyonunua sokoni na kupika.
Hivyo tunashauri kila mtu mwenye umri wa miaka 30 ikiwezekana miaka 25 na kuendele aanze kutumia virutubisho vifuatavyo ili kujilinda na tezi kukua. Utumiapo virutubisho hivi vyenye vyenye madini ya lycopene,Zinc na Iron ambayo yametengenezwa kwa kiwango kingi(concentrated and chemical free) kuna uwezekano mkubwa wa kutopata kabisa tatizo la tezi dume hata k**a kwenye ukoo wenu wote walipata tatizo hili.
MUHIMU ZAIDI:
Mara nyingi watu tumekua tukitumia dozi ya dawa au lishe bila kupona au kupata nafuu au matokeo mazuri na tuaanza kulalamika kua dawa fulani haifanyi kazi,sio kweli....
Tatizo ni kwamba,mifumo yetu ya mmeng'enyo wa chakula inayoruhusu ufyonzwaji wa dawa na lishe haifanyi kazi vizuri, na hii ni kutokana na kuzibwa na sumu,uchafu na mafuta ambayo tumekua tukila kila siku kwenye chakula ambavyo ndio hupunguza ufanisi wa ufyonzwaji wa sawa au lishe.
Hivyo,kitu cha kwanza cha msingi cha kufanya kitakacho saidia ufyonzwaji mzuri wa lishe na dawa na zikafanye kazi kwa haraka na vizuri zaidi kabla hujaanza kutumia hivyo virutubisho au dawa,lazima ufanye program ya kuusafisha mwili kwa kuondoa sumu na kusafisha mfumo mzima wa mmeng'enyo wa chakula halafu ndio utumie dozi au virutubisho, utapata matokeo haraka sana.
Na pia tatizo hili ina uhusiano wa karibu sana wa kusababisha kupungua kwa uwezo wa mwanaume kwenye tendo la ndoa(nguvu za kiume).
Hivyo kwa maelezo zaidi ya kujua vyanzo vingine vya kupungua kwa uwezo wa mwanaume kwenye tendo la ndoa,bofya hapa
Sasa sijui upo serious kiasi gani na hili tatizo kutokana na umri wako,baba yako,mmeo au ndugu yako.
Chukua hatua sasa,usisubiri mpaka ufikie kwenye hali mbaya ya saratani ambayo haiwezi kutibika tena.
:
Watu wazima wengi wanaogopa kusema k**a wana tatizo hilo,mpaka tatizo linapofikia kwenye hatua mbaya sana,hivyo k**a una kaka,mume au baba mwenye umri wa kuanzia miaka 40+ usisubiri akuambie,mtafutie Kinga mapema.
Kwa ushauri zaidi kujua na kupata lishe/virutubisho vyenye Kiwango kikubwa cha madini tajwa hapo juu kwa ajili ya tatizo hili na kwa lengo la kujikinga maana kinga ni bora kuliko tiba na kuondokana na tatizo hili,tuwasiliane.........
kwa elimu na msaada,zaidi kuhusu afya yako piga simu+255625322817
Marthernutritionist
whatsapp 0625322817
TUNZA AFYA YAKO IJE IKUSAIDIE UZEENI
#
07/10/2024
K**A HUPATI UJAUZITO JIULIZE MASWALI YAFUATAYO;
1. Je, mzunguko wa siku zako upo vizuri?
2. Je, unapata maumivu ya tumbo wakati wa hedhi?
3. Je, una uvimbe kwenye kizazi?
4. Je, unapata maumivu ya tumbo chini ya kitovu upande wa kulia na kushoto?
5. Je, unatokwa na uchafu wa aina yeyote ile ukeni?
6. Je, unapata siku zako vile inavotakiwa? Yaani mzunguko wa siku zako upo sawa?
7. Je, unapata maumivu wakati wa tendo la ndoa?
8. Je, unapata ukavu wakati wa tendo la ndoa?
9. Je, unakosa hisia za tendo la ndoa?
10. Je, huwa unapata ute wa uzazi Siku za habari (ovulation days)?
k**a jibu ni ndio kwa sababu mojawapo tajwa hapo juu
Basi hiyo ndiyo sababu inayokuzuia kupata ujauzito.
Je wewe ni sababu ipi unayo kati ya tajwa hapo juu?
/255625322817
Piga 0625322817
07/10/2024
K**A HUPATI UJAUZITO JIULIZE MASWALI YAFUATAYO;
1. Je, mzunguko wa siku zako upo vizuri?
2. Je, unapata maumivu ya tumbo wakati wa hedhi?
3. Je, una uvimbe kwenye kizazi?
4. Je, unapata maumivu ya tumbo chini ya kitovu upande wa kulia na kushoto?
5. Je, unatokwa na uchafu wa aina yeyote ile ukeni?
6. Je, unapata siku zako vile inavotakiwa? Yaani mzunguko wa siku zako upo sawa?
7. Je, unapata maumivu wakati wa tendo la ndoa?
8. Je, unapata ukavu wakati wa tendo la ndoa?
9. Je, unakosa hisia za tendo la ndoa?
10. Je, huwa unapata ute wa uzazi Siku za habari (ovulation days)?
k**a jibu ni ndio kwa sababu mojawapo tajwa hapo juu
Basi hiyo ndiyo sababu inayokuzuia kupata ujauzito.
Je wewe ni sababu ipi unayo kati ya tajwa hapo juu?
/255625322817
Piga 0625322817
07/10/2024
K**A HUPATI UJAUZITO JIULIZE MASWALI YAFUATAYO;
1• Je, mzunguko WA Siku zako upo vizuri?
2• je, unapata Maumivu ya Tumbo Wakati WA hedhi?
3• Je, una Uvimbe kwenye kizazi?
4• Je, unapata Maumivu ya tumbo chini ya kitovu upande WA kulia na kushoto?
5• Je, unatokwa na uchafu WA aina yeyote ile ukeni?
6• Je, unapata Siku zako vile inavotakiwa? Yaani mzunguko WA Siku zako upo sawa?
7• Je, unapata Maumivu Wakati WA tendo la ndoa?
8• Je, unapata Ukavu Wakati WA tendo la ndoa?
9• Je, unakosa hisia za tendo la ndoa?
10• Je, huwa unapata ute WA uzazi Siku za habari (ovulation days)?
k**a jibu ni ndio kwa SABABU mojawapo tajwa hapo juu basi hiyo ndiyo SABABU inayokuzuia kupata ujauzito.
Je wewe ni sababu ipi unayo kati ya tajwa hapo juu?
/255625322817
Piga 0625322817
04/09/2024
TATIZO LA KUCHEUA TINDIKALI NA TIBA YAKE (acid reflux)
KUCHEUA TINDIKALI MAANA YAKE NINI ?
Kucheua tindikali (gastroesophageal reflux disease, au chronic acid reflux) ni hali ambapo mchanganyiko wa chakula wenye tindikali uliopo tumboni kila wakati hupanda juu kupitia umio (esophagus). Hali hii hutokea kwa sababu vali iliyopo unapoishia umio, lower esophageal sphincter, haifungi vizuri chakula kinapokuwa kimeingia tumboni. Tindikali, kwa hiyo, hupanda kupitia umio kuingia kooni na kisha mdomoni, na kukufanya usikie ladha ya uchungu.
DALILI ZA ACID REFLUX
Dalili kuu za acid reflux ni kiungulia na kucheua tindikali. Watu wengine wana acid reflux bila kiungulia. Badala yake, wanasikia maumivu kwenye kifua, sauti kukwaruza asubuhi au matatizo ya kumeza. Unaweza kuhisi kuwa chakula kimekwama kwenye koo, au k**a unakosa pumzi au koo limekabwa. GERD inaweza pia kusababisha kikohozi kikavu au kutoa harufu mbaya kinywani.
Ukiona kiungulia na kucheua tindikali vinakusumbua kila baada ya muda mfupi -utando laini juu ya umio unaunguzwa kila wakati na tindikali kutoka tumboni. Hatimaye utando huu huharibika. Tatizo hili likiwa sugu, tabia zako za ulaji na kulala vitabadilika.
DALILI ZAKE
1. Kiungulia
2 . Kucheua chakula
3. Hisia kwamba chakula kinakwama kooni
4. Kukohoa
5. Maumivu ya kifuani
6. Shida wakati wa kumeza
7. Kutapika
8. Kukauka koo na sauti kukwaruza.
DALILI KWA WATOTO WADOGO :
A. Vipindi vifupi vya kutapika vya mara kwa mara
B. Kulia kupita kiasi, kukataa kula (watoto na vichanga)
C. Matatizo mengine ya upumuaji
D. Ladha ya tindikali ya mara kwa mara, hasa ukiwa umelala
E. Koo linalokwaruza
F. Kusikia kukabwa ambako kunaweza kumwamsha mtoto
G. Harufu mbaya akipumua
H. Shida kulala baada ya kula, hasa kwa watoto.
ACID REFLUX HUSABABISHWA NA NINI ?
Acid reflux husababishwa na udhaifu au kulegea kwa vali ya chini ya umio (lower esophageal sphincter). Kwa kawaida vali hii hufunga kikamilifu mara baada yat chakula kuingia tumboni. Ikijilegeza wakati ambapo haitakiwi, mchanganyiko wa chakula wa tumboni hupanda kwenye umio, na kusababisha acid reflux.
VIPENGELE AMBAVYO VINAVYOSABABISHA HALI HII KUTOKEA NI PAMOJA NA :
@. Msukumo mkubwa mno kwenye tumbo
K**a unasumbuliwa na magonjwa ya uzazi usisite kunitafuta. Ushaur unatolewa bure
0625322817
23/08/2024
*ZIJUE SABABU ZA MWILI KUFA GANZI*
KATIKA mwili wa binadamu, kuna tatizo la kiafya ambalo huambatana na dalili za mtu kuhisi maumivu, kuhisi kufa ganzi kwa viungo vya mwili yaani miguu na mikono. Tatizo hili kitaalamu huitwa *Peripheral Neuropathy*.
_Matatizo haya ya kiafya ya miguu/mikono kuhisi ganzi, baridi au maumivu husababishwa na kuumia au kudhoofika kwa neva za pembezoni mwa mwili (miguuni au mikononi) hivyo kupotea kwa uwezo wa kufanya kazi wa neva katika sehemu husika_ .
*Je, Dalili Zake Zinakuwaje?*
Dalili zinazoambatana na ugonjwa huu huwa sio nyingi mno nazo huwa k**a hivi ifuatavyo:
👉. Mtu kuhisi ganzi,
👉. Kushindwa kushika au kunyanyua kitu,
👉. Kuchoka kwa misuli na kadhalika,
👉. Maumivu au kuwaka moto maeneo ya miguuni au mikononi.
Miongoni mwa mambo ambayo husababisha neva hizi za pembezoni kudhoofika na kushindwa kufanya kazi vizuri ni haya yafuatayo:
👉. Kupungua kwa virutubisho mwilini, hasa mkusanyiko wa vitamini B, (Vitamin B Complex),
Kwa maelezo Zaid piga/wasap 0625322817
23/08/2024
*FAHAMU TATIZO LA UVIMBE KATIKA MAYAI YA MWANAMKE (OVARIAN CYST)*
🛑OVARIAN CYST NI NINI???
✍️Ni uvimbe unaotokea katika mayai ya mwanamke(ovarian)
✍️Uvimbe huo hutokana na mkusanyiko wa maji maji yanayozungukwa na kutu nyembamba ndani ya mayai ya mwanamke
✍️Mara nyingi tatizo hili hutokea kwa wanawake wa rika tofauti na mara nyingi huonekana kwa wanawake waliofika umri wa kushika ujauzito, pia uvimbe huo huweza kuwa wa ukubwa wa cm3_cm30 na unaweza kujaza tumbo lote na kufanya uonekane mjamzito
🛑SABABU ZA UVIMBE
👉kuwa na mzunguko wa hedhi usioeleweka (IRREGULAR MENSTRUATION CYCLE)
👉kuwa na mafuta mengi tumboni
👉kukosekana kwa uwiano wa vichocheo mwilini (hormone imbalance)
👉kuvunja ungo mapema (katika umri wa miaka 11_kushuka chini)
👉kutumia dawa za matibabu ya saratani ya matiti (tamoxifen)
👉ugumba
DALILI NA VIASHIRIA VYA TATIZO HILI
👉kupata maumivu makali ambayo huchoma katika nyonga, uke, tumbo, mapajani, mgongoni NK
👉kuhisi tumbo kuwa zito limejaa au kuvimba
👉kupata maumivu katika matiti
👉kutopata hed
Kwa mawasiliano Zaid 0625322817
13/08/2024
X POWER MAN☕️ * Hii ni DAWA iliyotengenezwa Kwa mchanganyiko Wa ; ✔️Fresh maca Ginseng powder ✔️Tongkat ali ✔️Epimedium ✔️Viambata hivi vimetoka nchi za 🔹KOREA,CHINA,USA,INDIA,PERU Kahawa hii haina CAFFEINE,imetolewa Kwa kutumia teknolojia bora ili kuwafaa watu Wa aina zote. Kazi muhimu za Hii Kahawa; ♻️Kuimarisha misuli ya uume kuwa bora zaidi na Nguvu mara dufu wakati Wa tendo. ♻️Kuupa mwili Nguvu zaidi ♻️Kusaidia kurudia tendo la ndoa mara nyingi zaidi yani ukimaliza mshindo Wa kwanza unauwezo Wa kuendelea zaidi. ♻️Kumpa mtu hamu ya tendo la ndoa hata k**a iliisha kabisa. ♻️Kuondoa uchovu na stress,kuzuia hatari ya kupata Magonjwa ya moyo. ♻️Kuilinda na kuipa afya tezi ya mwanaume ♻️Kuufanya uume usimame barabara k**a msumari ♻️Kusafisha mishipa ya damu ♻️Kuongeza ubora Wa mbegu za mwanaume na kuzifanya ziwe na kasi zaidi ✅Haina kemikali ni ya asili kabisa 100% *BORESHA MFUMO WA UZAZI KWA KUTUMIA DAWAHII . Mwanamme rudisha furaha ya ndoa yako🌚🏃
0625322817
12/08/2024
Uvimbe kwenye kizazi ukishakuwa mkubwa HUWEZA KUSABABISHA athari kubwa kwa mwanamke.
Dalili zitakazokuonyesha una uvimbe kwenye kizazi ni pamoja na;
➡️ Kupata damu nyingi wakati wa hedhi.
➡️Maumivu makala wakati wa siku za hedhi.
➡️ Unaweza kuhisi una ujauzito.
➡️Maumivu wakati wa tendo la ndoa.
➡️Kupata haja ndogo kwa taabu
➡️Kutokwa na uchafu ukeni usio kawaida.
➡️Kupata choo kigumu au kufunga choo.
➡️Maumivu nyuma ya mgongo.
➡️Kuvimba sehemu ya chini ya tumbo.
➡️ Maumivu ya nyonga.
Uonapo DALILI hizi basi unaweza kunitafuta kwa namba hii ili upate suluhisho mapema 0625322817
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Telephone
Website
Address
Mlimani City
Dar Es Salaam