Afya yangu.

Afya yangu.

Share

This page is about providing health education to the community

Photos from Afya yangu.'s post 24/01/2025

Chukua Hatua..!

24/01/2025

Jikinge na Ugonjwa wa Marburg, Unazuilika!

06/11/2023

Ulaji Unaofaa Kwa Wagonjwa wa Moyo

2. Protein

04/11/2023

Ulaji unaofaa kwa wagonjwa wa Moyo

1. Carbohydrates

22/10/2022

MAAMBUKIZI YA NJIA YA MKOJO ( UTI )
Urinary Tract Infection (UTI) ni maambukizi ya bakteria kwenye kibofu cha mkojo na njia ya kupitisha mkojo. Kwa hivyo inaweza kuhusisha njia ya juu au ya chini ya mkojo na maambukizo haya yanaweza kuwa 'complicated' au yasiyo 'complicated'. UTI isiyo 'complicated' pia inajulikana k**a cystitis au UTI ya chini kwa mwanamke ambaye sio mjamzito wa umri wa kuzaa na yule aliye na njia ya mkojo iliyo sawa. UTI zingine zote zinapaswa kuzingatiwa kuwa 'complicated'. Wanawake ndio wapo kwenye hatari kubwa, na hupatwa na UTI ya mara kwa mara kuliko wanaume.

Bacteria wanaohusika na kusababisha UTI nchini Tanzania ni Escherichia coli (E.coli) kwa idadi kubwa ikifuatiwa na Klebsiella, lakini Bacteria wengine ni Proteus spp, na Staphylococcus aureus.

DALILI.
Dalili za kawaida za UTI ni pamoja na:-
1. Homa,
2. Kukojoa sana,
3. Maumivu chini ya kitovu,
4. Maumivu au kusikia kuwaka moto wakati wa kukojoa.

MATIBABU.
UTI isiyo na dalili (asymptomatic) ni ya kawaida kabisa na haitaji matibabu, isipokuwa kwa wanawake wajawazito.

•Matibabu yasiyo ya Dawa.
1. Hakikisha unakunywa maji ya kutosha.
2. Epuka kubana mkojo kwa muda mrefu unapohisi kukojoa; au baada ya ngono katika watu wazima.
3. Kutoa catheter ya kibofu cha mkojo iliyokaa kwa muda mrefu.

•Matibabu ya Dawa kwa watu wazima.
1. Nitrofurantoin kwa siku 5.
AU
1. flucloxacillin + amoxicillin kwa siku 5.

Mgonjwa anapaswa kutumia dawa atakazopewa na Daktari kwa usahihi na kwa muda sahihi. Na asiache dawa katikati hata ikiwa anahisi dalili za UTI zimekwisha.
Haishauriwi kuchukua dawa za kuzuia bacteria bila taarifa kutoka kwa Daktari kwani dawa hizo huongeza upinzani na kupelekea kuchekewesha kupona haraka.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam
Dar Es Salaam