Vaya health solution

Vaya health solution

Share

Tunatatua changamoto hizi��
Tezidume | Bawasiri | Nguvu za kiume
Kisukari | Pressure | PID | Mifupa

15/01/2024

Usikae Bila Kula Kwa Muda Mrefu.
1) Inashauriwa mtu mwenye kisukari asikae na njaa muda mrefu.

2) Ni vizuri kula mara tatu au zaidi kwa siku na ikiwezekana vitafunio vidogo vidogo katikati ya milo mikubwa.

3) Usipendelee kula mlo mmoja mkubwa mchana au jioni.

4) Mfano wa milo kwa siku: Kula chakula cha asubuhi saa 1, kula kidogo saa 4, kula chakula cha mchana saa 7, kula kidogo saa 10, kula chakula cha jioni saa 1.

5) Ukifunga ramadhani, ni lazima kubadilisha muda wako wa kutumia dawa na hata kiasi cha dawa.

Vyakula Anavyopaswa Kula Mgonjwa Mwenye Kisukari Bila Masharti:
Vyakula unavyoweza kula bila masharti ni k**a ifuatavyo;

1) Mboga za majani (mchicha, spinach).

2) Nyanya, matango, bamia, karoti, vitunguu, pilipili hoho, pilipili, viungo vyote vya vyakula (bila chumvi nyingi), maji ya kunywa, chai na kahawa.

Kumbuka:

1) Unashauriwa kula vyenye wanga hasa nafaka zisizokobelewa kwa mfano dona kwani huupatia mwili ‘fibres’ vitamini na madini.

2) Kuwa na uzito wa kawaida.

a) Ikiwa una uzito uliozidi, unashauriwa kuupunguza.

b) Punguza kiasi cha kila aina ya chakula na epuka mafuta mengi.

3) Pamoja na ushauri wa chakula, usiache matibabu ya kisukari.

4) Mambo ya kukumbuka hata k**a hauna ugonjwa wa kisukari.

a) Usivute sigara.

b) Jitahidi kupunguza uzito k**a una uzito ulozidi.

c) Epuka kunywa pombe kupita kiasi.

d) Fanya mazoezi ya viungo mara kwa mara.

5) Hakuna haja ya kupikiwa chakula maalumu badala yake unashauriwa kula vyakula vinavyoliwa na familia yako isipokuwa vile vilvyowekwa au vyenye sukari.

6) Unaweza kula matunda aina zote.

a) Tunda utakalokula k**a ni embe au papai au tunda lolote kiwe ni kipande cha kadiri tu.

b) Unaweza kula zaidi ya mara moja kwa siku.

c) Mfano mzuri wa namna ya kula matunda. Chungwa moja asubuhi, ndizi moja mchana, kipande cha papai au embe jioni.

7)Kula mboga za majani au kachumbari kila siku kwa wingi ambapo inashauriwa nusu ya kila mlo wako unaokula iwe ni mboga mboga .
Kwa Tiba, Elimu Pamoja na Ushauri WASILIANA Nami ☎️ What'sapp 0625 69 59 71

03/01/2024

FAIDA ZA KULA KARANGA MBICHI

Post hii inakwenda kukupa faida kuu 5 za kula karanga mbichi katika afya ya mwili wako.

PROTINI: Karanga mbichi zina kiwango kikubwa cha protini, ambacho ni muhimu kwa ujenzi na ukarabati wa tishu mwilini.

MAFUTA YENYE AFYA: Zina mafuta yenye afya k**a vile omega-3 fatty acids, ambayo yanaweza kuchangia katika afya ya moyo na ubongo.

NYUZINYUZI: Karanga zina nyuzinyuzi ambazo husaidia katika mfumo wa kumeng'enya chakula na kuboresha afya ya mfumo wa utumbo.

MADINI: Zina madini muhimu k**a chuma, zinki, na fosforasi, ambayo ni muhimu kwa afya ya mwili na utendaji wa viungo.

ANTIOXIDANTS: Karanga zina antioxidants ambazo husaidia kupunguza madhara ya viini vya oksidishaji, hivyo kusaidia kulinda seli na tishu dhidi ya madhara ya muda mrefu.

kwa Tiba , Elimu Pamoja na Ushauri WASILIANA Nami
What'sapp ☎️0625 69 59 71

24/12/2023

*Mchanganyiko wa juice ya karoti na tangawizi inaweza kuwa na mchango katika kudumisha kinga ya mwili wa binadamu kwa sababu zifuatazo:*

1. Vitamini na madini: Karoti ni chanzo kizuri cha vitamini A, C na K, ambazo zote ni muhimu kwa afya ya kinga ya mwili. Tangawizi ina madini ya shaba, manganese na magnesiamu ambayo yanaweza kusaidia kuboresha kinga ya mwili.

2. Antioxidants: Karoti na tangawizi zina antioxidants ambazo zinaweza kusaidia kupunguza uharibifu wa seli za mwilini.

3. Husaidia katika kupambana na Maradhi: Tangawizi ina sifa za kupambana na uvimbe ambazo zinaweza kusaidia kupunguza hatari ya magonjwa yanayohusiana na uvimbe, k**a vile kansa.

4. Kuimarisha mmeng'enyo wa chakula: Juice ya karoti na tangawizi inaweza kusaidia kuimarisha digestion na kupunguza matatizo ya utumbo, ambayo inaweza kusaidia kuimarisha afya ya kinga ya mwili.

14/12/2023
14/12/2023

VYAKULA VYA KUONDOA GESI TUMBONI

Watu wengi walikua wakiomba mada hii japo nilishawahi kuitoa kiufupi huko nyuma. Watu wengi wamekua wakihangaika sana matumbo Yao kujaa gesi mara kwa mara na kuvimbiwa bila sababu.Leo nitaelezea jinsi ya kulitatua hili kwa kutumia vyakula na matunda, k**a tatizo hili limekusumbua kwa mda mrefu, pia kuna dawa maalumu kabisa kwaajili ya tatizo hili.

Kwa njia Moja au nyingine unaweza kukuta tumbo limechafuka kwa kuuma,kujaa gesi na hata kunguruma na unaweza kuhisi unaweza kunywa dawa Ili litulie.

Katika makala niliyokuandalia Leo nimekuandalia njia Bora sana za kutuliza mchafuko wa tumbo kwakutumia vyakula na matunda badala ya dawa ambazo haziondoi chanzo Cha tatizo

JE NI NINI CHANZO?
Kabla ya kukimbilia kwenye tatizo lenyewe na matibabu ngoja tujue kwanza chanzo huanzia wapi.
Vipo vyakula na vinywaji ambavyo huchangia sana katika tatizo hili,
Vyakula na vinjwaji vinavyochangia tumbo kujaa na kukosa choo kwa mda mrefu, vinywaji ni k**a;
Soda
Vilevi/pombe
Vyakula ni vyakula vyenye mafuta mengi pamoja na vyakula vyenye chumvi nyingi sana.Vyakula hivi vinapoingia tumboni huchelewa kumeng'enywa hivyo hupelekea ucheleweshaji wa usagaji wa chakula tumboni na uondoaji wa uchafu kwenye utumbo hivyo huleta kikwazo au ukinzani katika mfumo mzima wa usagaji chakula tumboni kwa urahisi.
Ili kujiepusha na matatizo ya mda mrefu na hata kuzuia uwezekano wa kuugua au magonjwa ya mara kwa mara, Huwa tunashauri kula vifuatavyo ili kusaidia usagaji mzuri wa chakula tumboni

PAPAI
Papai ni tunda ambalo Lina kimeng'enya(enzyme) ambazo husaidia usagaji mzuri wa chakula tumboni na kulifanya tumbo na utumbo kuwa laini katika usagaji wa chakula.
Watafiti wamebaini kuwa tunda hili lina harufu nzuri na ladha nzuri huboresha usagaji wa chakula,husafisha utumbo na imebainika husaidia kuondoa na kuzuia magonjwa na uvimbe tumboni na huimarisha mfumo wa Kinga mwilini.

Virutubisho vya papai pamoja na vitamin zake Zina faida nyingi sana mwilini.Papai limekuwa likitumika k**a tiba tangu Karne ya 18. Kirutubisho Cha papain ambacho kipo kwenye papai ambacho kina uwezo mkubwa sana katika usagaji wa chakula tumboni, watu wengi ambao wamekuwa wakisumbuliwa na kushikwa tumbo na kupata choo kigumu Huwa wanashauriwa kutumia papai k**a kilainisha tumbo.

MTINDI(YOGURT)
Mtindi ni mzuri sana katika kuondoa tatizo la gesi tumboni hata k**a hupendi mtindi jitahidi kunywa k**a dawa ni mzuri sana katika umeng'enyaji wa chakula tumboni. Mtindi mzuri niule ambao unatumika wenyewe bila kitu chochote. Wapo bacteria wazuri kwenye mtindi ambao husaidia sana katika uchakataji wa chakula tumboni na chakula kuwa chepesi.

UKWAJU
Kuboresha mfumo wa mmeng 'enyo na kuondoa gesi, tumia juisi ya ukwaju kurekebisha mfumo wako wa kumeng'enya chakula mwilini

Kuwa na utaratibu wakutumia vyakula hivi mara kwa mara

Kwa Maelezo zaidi WASILIANA Nami What'sapp
☎️0625 69 59 71
☎️0762 95 70 99

30/11/2023

*PID( PELVIC INFLAMMATORY DISEASE)
-Haya ni maambukizi ya bakteria wabaya kwenye mfumo wa uzazi wa mwanamke.
-Maambukizi haya hupelekea uharibifu mkubwa kwenye mfuko wa uzazi wa uzazi, mirija ya uzazi au sehemu nyingine za uzazi wa mwanamke pia ni chanzo cha ugumba.

DALILI ZA MAAMBUKIZI KWENYE MFUMO WA UZAZI WA MWANAUMKE( PID)
1.Maumivu makali ya nyonga, tumbo au chini ya kitovu.
2.Kutoka maji maji yasiyo ya kawaida yenye harufu mbaya.
3. Kutoka maji maji yasiyo ya kawaida baada ya kufanya tendo la ndoa au baada ya kuingia hedhi.
4. Maumivu makali wakati wa kufanya tendo la ndoa.
5. Homa kali
6. Maumivu kipindi cha kukojoa, kukojoa mara kwa mara, kukojoa kwa shida.
7.Maumivu makali chini ya kitovu, kichefuchefu, kutapika, homa kali kupita kiasi.
8. Kutokwa na uchafu sehemu ya siri wa rangi ya maziwa mtindi, kijani au mweupe unaoambatana na harufu kali.

MADHARA YA PID
1. Kupata ugumba na kupata utasa.
2. Kukosa kujiamini.
3. Mimba kutoka.
4.kuharibu mfumo wa uzazi.
5. Kuvurugika kwa homoni na mtu huanza kupata hedhi isiyo na mpangilio.
6. Kati ya wanawake 10 waliathiriwa na PID, Mmoja anakuwa tasa kwasababu ya PID hupelekea makovu kwenye mirija ya uzazi.
7. Kutofurahia tendo la ndoa.

KWA MAHITAJI NA MAWASILIANO
☎️0625 69 69 71

Photos from Vaya health solution's post 24/11/2023

AINA ZA UCHAFU UNAOTOKA UKENI,RANGI NA DALILI ZAKE,

Kutokwa na uchafu ukeni unaoambatana na kuwashwa au kutokewa na vipele, hii huashiria kwamba kuna tatizo ukeni, na katika makala hii tumechambua aina mbali mbali za uchafu ukeni kwa kuangalia rangi zake na dalili za magonjwa.

1. UCHAFU WENYE RANGI YA KAHAWIA AU DAMU

Huu uchafu huonyesha dalili ya kuwa mzunguko wako wa hedhi umevurugika na wakati mwingine ni dalili ya magonjwa k**a kansa ya kizazi,
mwanamke anayepata tatizo hili hutoa damu nyingi pamoja na kuumwa sana nyonga, hivo ukiona dalili k**a hizi nenda kafanye vipimo hospital na kuanza tiba mapema

2. UCHAFU WENYE RANGI YA NJANO /KIJANI WENYE HARUFU MBAYA

Endapo uchafu huo utatoka k**a povu na wenye rangi ya kijani au njano na ukiambatana na harufu mbaya huwa ni dalili ya ugonjwa wa trichomonas,PID(pelvic inflammatory disease), maambukizi ya parasite yanatokana na ngono zembe,
dalili Yake nyingine ni maumivu na kuwashwa wakati wa kutoa haja ndogo,maumivu wakati wa tendo la ndoa,kutokwa na damu ukeni wakati wa tendo la ndoa n.k.

3. UCHAFU MWEUPE MZITO K**A JIBINI

Mara nyingi hii huwa ni dalili ya maambukizi ya fangasi(YEAST INFECTION) na dalili nyingine huwa ni kuvimba sehemu ya nje ya siri, kuwashwa na kupata maumivu makali wakati wa tendo la ndoa.
Ngozi ya eneo la nje kubadilika rangi na kuwa nyekundu,kuhisi hali ya kuungua wakati wa kutembea,
uchafu mzito kutoka ukeni na wa rangi mithili ya maziwa mgando,uchafu huu huweza kuambatana na harufu mbaya kutoka ukeni

4. UCHAFU MWEUPE/KIJIVU WENYE HARUFU YA SAMAKI

Uchafu wa Aina hii ni dalili ya maambukizi ya bacteria vaginosis, mara nyingi mwenye tatizo hili husikia muwasho na maumivu sehem ya nje ya uke.
KUMBUKA: Jua kutofautisha kati ya ute ute ambao ni kawaida kumtoka mwanamke akiwa kwenye siku za hatari na aina za uchafu unaotoka ukeni ambao nimetoa maelezo yake.
Ute ute wa siku za hatari unakuwa wa kuvutika k**a vile ule wa kwenye yai la kuku,na hauna harufu yoyote mbaya.Kwa Maelezo zaidi WASILIANA Nami What'sapp
☎️0762 95 70 99

23/11/2023

Dalili Za Saratani Ya Tezi Dume:

Katika hatua za awali, dalili hazitofautiani sana na zile za kuvimba kwa tezi dume lisilokuwa saratani (Benign Prostate Hyperplasia).

Dalili hizo ni pamoja na;

a) Kusikia kupata haja ndogo mara kwa mara hasa nyakati za usiku.

b) Haja ndogo kuchelewa kutoka unapoanza kukojoa.

c) Kutoa mkojo wenye mtiririko dhaifu na kuchuruzika kidogo kidogo baada ya kumaliza kukojoa.

d) Kujikakamua wakati wa kukojoa na kushindwa kumaliza mkojo wote.

e) Kutoa mkojo au manii yaliyochanganyika na damu.

f) Maumivu makali sehemu mbalimbali za mwili k**a saratani imesambaa.

g) Kupungua uzito, kuhisi kichefuchefu, uchovu na kizunguzungu.

Kumbuka: Mtu mwenye tatizo katika tezi dume huanza kwa dalili ndogo ndogo sana mpaka mtu apate saratani ya tezi dume(prosate cancer) ujue amekaa na tatizo hilo bila kulipatia ufumbuzi, nitafute Kwa msaada zaidi.kwamaelezo zaidi WASILIANA Nami What'sapp
☎️0762 95 70 99

17/11/2023

MAUMIVU WAKATI WA S*X
*HORMON IMBALANCE (KUVURUGIKA KWA HOMONI)*
:Hili ni tatizo linalowakumba wakina mama(wanawake) wengi ambalo husababishwa na
kiwango kidogo cha hormone ya ESTROGEN.

*VYANZO VYA KUVURUGIKA KWA HORMONE*
👉Utoaji wa mimba
👉Uwepo wa sumu mwilini.
👉kutokula mlo uliokamili au mfumo mbovu wa maisha.
👉Family history(upungufu wa ongezeko ya homoni ya progesterone
👉mabadiliko ya mazingira au hali ya hewa.
👉uzito mkubwa
👉Msongo wa mawazo.
👉Kutofanya mazoezi.
👉Matumizi ya kisasa ya uzazi wa mpango.
👉Kukoma kwa hedhi.

*Dalili za kuvurugika kwa homoni*
👉Maumivu wakati wa tendo LA ndoa.
👉Kutoshika mimba.
👉Mzunguko wa hedhi kubadilika.
👉Kuongezeka uzito.
👉Kupungua hamu ya tendo LA ndoa.
👉Kupoteza kumbukumbu.
👉Hasira za Mara kwa Mara.
👉Damu kutoka nyingi wakati wa hedhi au kutoa damu yenye mabongemabonge
👉Uke kuwa mkavu.
👉kutoka jasho jingi usiku.
👉maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
👉mzio wa vyakula/Allerg kuchaguachagua vyakula.

*Madhara ya kuvurugika kwa homoni*
👉kutoshika ujauzito kwa mda mrefu.
👉Mimba kuharibika Mara kwa Mara.
👉Kuwa mgumba.
👉U.t.I Mara kwa Mara.
👉Uvimbe kwenye via vya uzazi wa mwanamke.(fibroids)
👉kuziba kwa mirija ya uzazi.
👉saratani.

Hormone imbalance inatibika ondoa shaka...Jifunze kujali afya yako.
Kwa Maelezo zaidi WASILIANA Nami
WhatsApp 0625 69 5971.
Text/Call/ 0762 95 70 99

15/11/2023

TATIZO LA KUZIDI KWA KIWAGO CHA ACID TUMBONI (ACID REFLUX-GERD)

𝐊𝐀𝐑𝐈𝐁𝐔

Gastroesophageal reflux disease (GERD).
-Ni hali inayotokana na kuzid kwa kiwango cha Acid tumboni (Hydrochloric Acid) ambapo hupelekea kupanda kwa acid kutoka tumboni kuelekea katika koo la Chakula (Oesophagus) na kupelekea kudhurika kwa mfumo wa chakula upande wa juu ambao unahusisha koo la chakula na mdomo pia.

Watu wengi sana wanasumbuliwa na tatzo hili bila wao kujua wanasumbuliwa na tatzo hili na hufikia hatua wengine kudhani wamerogwa kutokana na dalili ya tatzo hili. Tutaangalia dalili ambazo mtu anaweza kugundua kuwa anasumbuliwa na tatzo hili.

DALILI ZA MTU ANAYESUMBULIWA NA KUZID KWA ACID TUMBONI (GERD-Acid Reflux
-Zipo dalili nyingi ambazo huashiria mtu kusumbuliwa na tatizo la kuzidi kwa Acid tumboni,dalili hizo ni zifuatazo:⤵️⤵️

1.🖇️ Kuwaka moto kifuani(Kiungulia) hasa wakati wa usiku au unapolala,hali hii hutokea pia mara baada ya kula.
2.🖇️ Mapigo ya moyo kwenda mbio/kushtuka kwa moyo baadhi ya nyakati.Hali hii hupelekea baadhi ya watu kuhisi wana matatizo ya moyo.
3.🖇️ Kuhisi k**a kichwa kimevurugika na kuhusi kuchanganyikiwa.
4.🖇️ Kusahau mara kwa mara hata vitu vya kawaida kabisa/Kupungua kwa kumbukumbu.
5.🖇️ Kujisaidia choo kigumu k**a cha mbuzi.
6.🖇️ Kuwa na wasiwasi na khofu kubwa na hufikia hatua hata ukipigiwa simu hasa nyakati za usiku moyo huanza kwenda mbio na kujawa na wasiwasi mkubwa.
7.🖇️ Kukosa usingizi ama kushtuka mara kwa mara kutoka usingizini.
8.🖇️ Kupumua kwa tabu baadhi ya nyakati.
9.🖇️ Kupata maumivu ya kichwa ya mara kwa mara kwa baadhi ya watu wenye tatizo hili.
10.🖇️ Kupata kikokozi kisichoisha
11.🖇️ Kuvimba Tonsillitis/mafidofido mara kwa mara.
12.🖇️ Mdomo kuwa mchachu na huwez kupelekea kutoa harufu mbaya ya kinywa.
13.🖇️ Kuhisi k**a kuna kitu kimekwama kooni lakin kila unavyojaribu kukitoa hakitoki
14.🖇️ Kupata fangasi mdomoni(mdomo huanza kutoa ute mweupe ambao una harufu mbaya).
15.🖇️ Huweza kupelekea ukaanza kuota ndoto za kutisha pindi ulalapo na kuhisi umerogwa.
16.🖇️ Kupata maumivu ya mgongo hasa sehemu ya mabega,maumivu makali kana kwamba umenyanyua vitu vizito.
17.🖇️ Mwili kuwa na uchovu usioisha utadhani unafanyakaz ngumu kila siku.
18.🖇️ Macho kupunguza uwezo wa kuona vizuri.
19.🖇️ Kupungua uwezo wa kufanya tendo la ndoa.
20.🖇️ Mwili kupata baridi na wakat mwingine kuhisi homa kabisa.
21.🖇️ Maumivu ya tumbo kati ya kifua na tumbo.
22.🖇️Kichefuchefu na kutapika.

MAMBO YANAYOWEZA KUCHOCHEA TATIZO LA KUZIDI KWA ACID TUMBONI
1.🖇️ Uvutaji wa sigara
2.🖇️ Unywaji wa pombe
3.🖇️ Utumiaji wa vyakula au vinywaji vywenye Caffeine k**a vile Kahawa,Chocolate, Soda nk
4.🖇️ Kula vyakula vyenye mafuta mengi/vyakula vilivyokaangwa
5.🖇️ Kula chakula kingi kupita kiasi ama kula usiku sana.
6.🖇 Kutumia baadhi ya Madawa k**a vile ASPIRIN
7.🖇️ Ngiri ya kifua pia husababisha GERD lakin pia GERD huweza kisababisha Ngiri ya Kifua(Huatal hernia)
8.🖇️ Kuwa Mjamzito
9.🖇️ Uzito kupita kiasi (Obesity)
10.🖇️ Matatzo ya mmeng'enyo wa chakula au kuchewa Kujisaidia pindi uhisipo haja kubwa.

MATIBABU YA TATIZO LA KUZIDI KWA ACID TUMBONI-GERD
-Matibabu ya KUZIDI kwa Acid tumbon yamegawanyika katika aina mbili k**a ifuatavyo:⤵️⤵️

1️⃣ MATIBABU YA KISASA
-Matibabu haya yanahusisha utumiaji ya njia za hospital katika matibabu ikiwemo utumiaji wa PPIs(Proton pump inhibitors),Antacids,Histamine, H-2 Blockers k**a vile Cimetidine (tagament HB),famotidine (Pepcid AC),Nizatidine (Axid AR)
-esomeprazole (Nexium), lansoprazole (Prevacid), omeprazole (Prilosec), pantoprazole (Protonix), rabeprazole (Aciphex) and dexlansoprazole (Dexilant) .Magnesium nk.
Dawa hizi zimekuwa zikitumiwa sana na watu wenye changamoto za Acid nying tumboni na miongoni mwa changamoto ni kwamba dawa hizi zimekuwa zikionesha msaada mdogo sana kwa asilimia kubwa ya wagonjwa na hutoa naafuu ya muda tu.

2️⃣ MATIBABU KWA TIBA ASILI/TIBA MBADALA.
-Njia hii inahusisha matibabu kwa kutumia mimea tiba na imeonekana kuwa na ufanisi mkubwa kutokana na uwezo mkubwa wa mimea mingi katika kupambana na magonjwa mbalimbali kwasababu mimea kutibu kiini cha tatzo kwa kuzifanya kuwa mpya seli za mwili hivyo kuufanya mwili kuwa na uwezo mpya katika kufanyakazi zake.

Wasiliana nami kwa msaada zaidi wa kitaalamu katika kupambana na tatizo hili. WhatsApp/Text/Call:0762 95 70 99

13/11/2023

YA FANGASI SUGU NA INAYOJIRUDIA RUDIA - VYANZO NA KINGA.

Fangasi Inasababishwa na jamii ya fungi anaitwa CANDIDA. Seli za fangasi na bacteria wazuri huishi ukeni bila tatizo lolote. Tatizo linakuja endapo ukuaji wa fangasi hawa ukeni watakuwa wengi kushinda wazuri. Basi hapo ndio inapotokea ugonjwa wa fangas na miwasho mingi.

K**a unapata maambukizi ya fangasi zaidi ya mara nne kwa mwaka basi kitaalamu hali hii hiyo hujulikana k**a vulvovaginal candidiasis (fangasi sugu au inayojirudia rudia). Na ni hatari sana K**a ukichelewa kuipatia matibabu sahihi mapema kwani upelekea tatizo la PID ambalo nalo upelekea tatizo la ugumba Kwa wanawake wengi asa kwa sasa.

VYANZO VYA FANGASI SUGU/INAYOJIRUDIARUDIA;

Zipo sababu kadhaa zinazoweza kupelekea fangasi kuwa sugu/kujirudia rudia. Sababu hizo ni:-

1. Vitu vinavyoweza kusababisha mvurugiko wa homoni k**a ujauzito, dawa za uzazi wa mpango, na matibabu ya estrogen.

2. Matumizi ya mara kwa mara ya antibiotic ambazo huondoa bakteria ambao husaidia kupunguza idadi ya candida.

3. Magonjwa yanayoshambulia kinga ya mwili k**a VVU (HIV)

4. Unene, unaoweza kusababisha joto na unyevu mazingira yanayofanya candida kuongezeka kwa wingi.

5. Nguo za kubana na zisizo za pamba zinazofanya maeneo ya via vya uzazi kuwa na joto na unyevunyevu. Mazingira ya joto hii inamaanisha nguo ambazo tunatakiwa kuvaa k**a vile chupi za cotton hasa kwa wanawake, hazihitaji joto sababu bacteria wabaya wanakuwa wengi sana na kusababisha miwasho na FANGASI.

6. Maambukizi kutoka kwa mtu unaeshirikiana nae tendo la ndoa.

7. Kukosa usingizi stress, vidonda sehemu za siri,matumizi ya antibiotics, kuweka marashi sehemu za siri.

8. Watu wanaougua kisukari ambao hawawezi kudhibiti kwa kutumia dawa za kisukari, inakuwa kwenye damu na hicho kisukari ndiyo chakula kikuu cha hao fangasi.

9. Hata wanawake ambao wanapenda kula vyakula vya sukari nyingi k**a vile chocolates, soda, na vingine vyenye sukari nyingi ambavyo ni chakula cha fangasi.

DALILI ZA FANGASI SUGU.

Kuna dalili nyingi zinazoonyesha kuwa una dalili za kua na fangasi ukeni k**a zifuatazo;

— Kuwa na miwasho sehemu za siri mara kwa mara.
— Vipele vidogo vidogo ukeni.
— Vidonda au kuwa na michubuko ukeni.
— Kutokwa na harufu mbaya ukeni.
— Kupatwa na maumivu makali wakati wa tendo la ndoa.
— Kuvimba au kuwa mwekundu katika mdomo wa nje ya uke.
— Kuwaka moto ndani na nje ya uke.
— Maumivu ya misuli na tumbo hasa chini ya kitovu.
— Maumivu ya kiuno.
— Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri baada ya tendo la ndoa.
— Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au kijivu unaoweza kuwa mwepesi au mzito au majimaji.

MADHARA MAKUBWA YA FANGASI

Kuwa na Fangasi sugu kwa muda mrefu ambayo inajirudia mara kwa mara bila kupata matibabu sahihi upelekea Kupatwa na ugonjwa wa Pelvic Inflammatory Disease (PID) maambukizi katika via za uzazi na kupelekea kuwa mgumba, ndio maana wanawake wengi ni wagumba. Pamoja na kuwa na muwasho wa kudumu sehemu za siri inayosababisha kukosa raha na Uhuru wakati wote.

JINSI YA KUJIKINGA DHIDI YA MAAMBUKIZI YA FANGASI YANAYOJIRUDIARUDIA.

1. Vaa nguo za ndani zilizotengenezwa na pamba.

2. Epuka nguo za kubana.

3. Jisafishe kutoka mbele kwenda nyuma baada ya kujisaidia haja kubwa.

4. Tumia antibiotics pale tu unaposhauriwa na daktari.

5. Epuka kujisafisha kwa kuingiza vidole kwenye via vya uzazi.

6. Epuka kufanya mapenzi hadi utakapopona maambukizi ya fangasi.

MATIBABU YA FANGASI SUGU NA MUWASHO SEHEMU ZA SIRI.

SULUHISHO LA WENGI.

Watu wengi wanapokuwa na Fangasi Sugu huenda hospital au duka la dawa na kupewa antibiotics ambazo uwa kawaida upelekea kutuliza tatizo na Siyo kutibu na hatimaye huenda kuua bakteria wazuri na matokeo yake baada ya muda upelekea tatizo kubwa zaidi ambalo ni PID ( maambukizi Kwenye via vya Uzazi). Na ikifika hatua hii upelekea Mirija ya uzazi kujaa Maji au kuziba, matatizo ya hormones, na mwisho upelekea tatizo la UGUMBA, K**a utakuwa umechelewa kupata Tiba sahihi mapema. Na ndio sababu kubwa moja wapo ya wanawake wengi kwa sasa kupata tatizo la ugumba.

SULUHISHO LA KUDUMU.

K**a una tatizo la fangasi inayojirudia mara kwa mara njia ambayo itakusaidia na ni ambayo imekuwa mkombozi na msaada mkubwa kwa wanawake wengi ni kupitia supplement na Tiba lishe ya Femicarewash (kwa bei ya 50,000/= tumetoa offer kwa week hii kutoka bei yake ya kawaida 65,700/= weka order K**a unahitaji maana zipo chache). Hii ni njia ya asili ya kutibu tatizo ili la fangasi sugu na muwasho ukeni na kuondokana na tatizo ili kabisa, haijalishi tatizo lina muda gani, na pia ni njia ambayo haina kemikali yoyote ndani yake na hivyo ni njia salama zaidi kiafya ambayo ninakushauri.

Mambo ya muhimu kufahamu kuhusiana na Tiba lishe hii ya FEMICARE WASH;

FEMICARE WASH.
Hii huwa inafahamika k**a mkombozi wa wanawake kwa maambukizi ya sehemu za siri.
Imeandaliwa maalum kwa ajili ya wanawake

Imetengenezwa kwa vyakula,mimea na madini na viua sumu mwilini.
Inamadini yanayohuisha uke na kuwa na ulinzi asilia,inaviua sumu vinavyozuia uke kuzeeka(mashavu),uke uliolegea,
Ina mafuta mazuri yanaitwa *essential oil* kwa ajili ya kufanya uke urudishe mnato wake wa asili.

Faida ambazo Mwanamke anazipata unapotumia FEMICARE Wash.

-Huondoa harufu mbaya ukeni
-Huondoa bacteria wabaya na kuzuia U.T.I
-Huondoa fangasi na miwasho ukeni
-Hurudisha size nzuri ya uke
-Huondoa maji maji yatokayo ukeni yenye Harufu mbaya
-Huondoa maumivu wakati wa tendo la ndoa
-Hufanya mwanamke kujiamini muda wote
-Huzibua mirija ya uzazi hivyo kusaidia wenye shida ya kutoshika mimba
-Humkinga mwanamke na maambukizi mabaya hasa u.t.i kwenye vyoo,kemikali za swimming pool, maambukizi Mabaya kutoka kwa mwanaume.n.k

Mwisho kabisa napenda kushauri wanawake wote uwe unaumwa au huumwi hii supplement ni vizuri kuwa nayo ndani itakusaidia kwenye mazingira usiotegemea.

USHAURI;

Unapaswa mwanamke usijioshee ndani ya uke wako kila siku na pia kutoweka marashi au sabuni za chemical kwaajili ya kuondoa harufu mbaya ukeni, maana kwa kufanya hvyo zaidi huuwa bacteria wazuri na kuwaacha wale wabaya. Na pia kutumia dawa bila ushauri kutoka kwa daktari ni hatari kwa afya yako pia kwani kuna wengine wanatumia dawa za kuweka ukeni na baada ya muda ujikuta uchafu unaanza kutoka na mwisho wa siku tatizo uwa kubwa zaidi na zaidi.Kwa Maelezo zaidi WASILIANA Nami
WhatsApp/Call/Msg:0625 69 59 71

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Address


Mliman City
Dar Es Salaam