AFYA Yangu Furaha Ya Kesho

AFYA Yangu Furaha Ya Kesho

Share

TUNA TIBU KWA KUTUMIA STEM CELL AMBAYO INATIBU CHANZO CHA TATIZO

10/10/2022

SARATANI YA TEZI DUME
Moja ya maradhi yanayoshuhudia kampeni kubwa kukabiliana nayo katika miaka ya hivi karibuni duniani ni pamoja na saratani ya tezi dume kutokana na ukubwa wa athari inazosababisha.
Ni maradhi yanayoshika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na saratani kwa wanaume duniani.
✍️Pia ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa miaka 70 na kuendelea.
Hata hivyo, satarani ya tezi dume kwa sasa inawapata zaidi wanaume kuanzia miaka 25.
✅Maana ya saratani
Saratani maana yake ni ukuaji holela bila mpangilio wa seli baada ya kuparanganyika kwa mfumo wa seli unaodhibiti ukuaji na uhai wake. Na uvimbe wa kawaida wa tezi maana yake ni kuwa seli zimetutumka tu lakini hakuna mparanganyiko wa seli wala kukua kwa kusambaa kiholela k**a ilivyo kwa saratani.
✍️Hivyo, ndio maana kuna tatizo la kuvimba tezi dume na wengine kupata saratani ya tezi dume kwa wanaume wenye umri mkubwa.
✍️Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Inaundwa na sehemu mbili ambazo zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu.
✍️Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (re**um) na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra).
✅Kazi ya tezi dume
Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la kujamiana. Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hutengeneza shahawa (semen).
✍️Majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya uzazi, tayari kwa utungisho na yai la k**e.
✍️Vilevile husaidia kupunguza hali ya kitindikali iliyopo katika uke, ambayo isiporekebishwa, huua mbegu nyingi za kiume na kufanya utungisho kuwa wa tabu..
✅Vyanzo Vinavyopelekea Tezi Dume Kutanuka:
Tatizo la kutanuka kwa tezi dume limekuwa kwa kasi sana hii ni kutokana na mitindo ya maisha wanaume wengi wanayoishi. Pia na elimu ndogo iliyoko kwenye jamii kuhusu afya zao.
✍️📌Vifuatavyo ni vyanzo vya kutanuka kwa tezi dume:
- Ukosefu wa lishe kamili na Virutubisho muhimu mwilini.
- Uwepo wa sumu nyingi mwilini.
- Kutokufanya mazoezi.
- Matumizi ya pombe kali, na uvutaji wa sigara.
- Uzito mkubwa (uliopindukia, uliokithiri), na Kitambi.
- Kutokukaa sawa kwa vichocheo vya mwili (Hormone Imbalance).
- Msongo wa mawazo (Stress).
- Magonjwa ya zinaa.
- Umri mkubwa.
- Upasuaji wa korodani, kuzaliwa na korodani moja.
- Historia ya Familia (Kurithi).
- Mazingira (Ethnicity).
✅Dalili za saratani ya tezi dume ni zipi?
a) Dalili za awali
- Kukojoa mkojo uliochanganyikana na damu
- Kukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu
- Maumivu kwenye mfumo wa mkojo
- Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
- Kuhisi kibofu kimeja mkojo muda wote na ukienda kukojoa mkojo hautoki, lakini ukirudi kukaa unahisi kukojoa tena.
- Homa
- Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
b) Dalili za mtu aliyeathirika
- Maumivu ya mifupa hasa chini ya mgongo, kiuno na mbavu
- Miguu kuwa dhaifu
-Kushindwa kumudu tendo la ndoa, au Kuhisi maumivu makali wakati unamaliza tendo la ndoa
- Kushindwa kuzuia mkojo, pindi unapohisi kukojoa
- Kushindwa kuzuia haja kubwa (kinyesi cha maji maji)
- Tumbo kuja gesi mara kwa mara
✅Vipimo gani vitathibitisha kuwa nina saratani ya tezi dume?
Utambuzi wa saratani ya tezi dume hujumuisha kufahamu historia ya mgonjwa pamoja na familia yake, kufahamu dalili alizo nazo mgonjwa pamoja na kufanya vipimo kadhaa. Vipimo vinavyoweza kufanywa ni pamoja na
📌Digital re**al exam: Daktari ataingiza kidole cha shahada katika puru (re**um) ili kuhisi tezi dume kupitia ukuta wa puru. Aidha atahisi pia sehemu zote zinazozunguka tezi dume kutambua iwapo tezi ni ngumu au k**a ina uvimbe wowote.
📌Kipimo cha damu kuchunguza Prostate Specific Antigen (PSA): PSA ni aina ya protein inayozalishwa na seli za tezi dume. Uzalishaji wake huongezeka wakati wa BPH, tezi dume inapopata uambukizi (prostitis) , na saratani ya tezi dume. DRE pamoja na PSA huonesha uwepo wa tatizo kwenye tezi dume lakini vipimo hivi havina uwezo wa kutofautisha iwapo tatizo hilo linamaanisha saratani au BPH. Hivyo basi, ili kuweza kutofautisha kati ya magonjwa hayo mawili, kipimo kiitwacho Prostate biopsy hufanywa.
📌Prostate biopsy: Kipimo hiki hufanywa kwa kuchukua kipande cha nyama (tishu) kutoka tezi dume kwa ajili ya uchunguzi maabara.
Kipimo kingine huitwa transre**al ultrasound ambacho husaidia kuonesha ukubwa na sura ya tezi dume lilivyo.
✍️Ili kutambua k**a saratani imesambaa sehemu nyingine za mwili vipimo vya CT scan, MRI pamoja na PET navyo vyaweza kufanyika pia.
✅Madhara ya Tezi Dume:
Yafuatayo ni madhara ya tezi iliyotanuka:
- Kibofu cha mkojo kuuma: hivyo hupelekea mkojo kurudi juu, na kuharibu figo na Ini … … n.k.
- Kufunga kwa njia ya mkojo kabisa
- Figo kushindwa kufanya kazi (Kidney Failure)
- Kushindwa kumudu tendo la ndoa (Ndoa zinavunjika)
- Ugumba (Infertility, Frigidity for men)
- Kutokea kwa majipu sehemu ya Tezi Dume
- Kifo
✅Saratani ya tezi dume inatibika?
Tiba kamili ya tezi dume ni kwa Kutibu chanzo cha tatzo kwa maana ya kukarabati seli ya tezi dume na kuondoa madhara yaliyo sababisha tezi kuasilika hivyo STEM CELL ndo jibu kamili unaenda tibu chanzo cha tatzo Pamoja na dalili zake tofauti na tiba zingine zinaishia Kutibu dalili pekee

10/10/2022

UGCare PLUS NI NINI
Ni Stemcell ambayo ina mchanganyiko wa mimea mbali mbali hasa majani ya Dokudami, majani ya Artichoke na honeydew melon na pia matunda ya Acai, blue green algae na ceramide.
Stemcell hii ilitengenezwa maalum kwaajili ya kuboresha afya ya mwili kwa kutibu magonjwa mbali mbali.
Stemcell hii hufanya mambo makuu manne muhimu katika mwili wa binadam ambayo ni;
o Kurekebisha seli zilizoharibika
o Kuimarisha kinga ya mwili
o Kurutubisha seli
o Kutoa sumu mwilini
DOKUDAMI
Dokudami ni mmea wa asili wa Kijapani unaotoa maua yenye majani mazuri yenye umbo la moyo na maua meupe ya kupendeza. Jina lake la kisayansi ni Houttuynia cordata, pia inajulikana k**a Heartleaf. Neno dokudami hutafsiriwa kuwa "kizuizi cha sumu" kwa Kijapani, kuashiria sifa zake za kuzuia mwili na sumu.
HONEYDEW MELON
"Honeydew" ni jina la kimarekani la aina ya White Antibes cultivar ambayo imekuwa ikilimwa kwa miaka mingi kusini mwa Ufaransa na Algeria.
Honeydew ina kiwango kidogo cha mafuta na kolestero na kuifanya kuwa chanzo cha haraka cha nishati kwa mwili wako. Honeydew pia imejaa vitamini na madini, pamoja na:
o Vitamini C
o Vitamini A
o Calcium
o Madini ya Chuma
o Folates
o Vitamini B6
o Potasiamu
o Vitamini K
o Magnesiamu
Huimarisha mifupa
Huboresha afya ya Ngozi
ACAI BERRIES
Berries za Acai ni matunda bora ya Brazili. Haya matunda ni asili ya Amazon ambapo ni chakula kikuu. Hata hivyo, hivi majuzi yamepata umaarufu ulimwenguni kote na yanasifiwa kwa kuwa na manufaa hasa kwa afya na ustawi.
ARTICHOKE LEAVES
Mmea huu ulianzia Bahari ya Mediterania na umetumika kwa karne nyingi kwa sifa zake za kua ni dawa.
Manufaa yake ya kiafya yanayodaiwa ni pamoja na kupunguza viwango vya sukari kwenye damu, umeng’enyaji wa chakula, afya ya moyo, na afya ya ini.
Artichokes zina kiwango kidogo cha mafuta na kiwango kikubwa sana cha fiber, vitamini, madini, na antioxidants. Zina kiasi kikubwa cha madini ya folate na vitamini C na K, pia hutoa madini muhimu, k**a vile magnesiamu, fosforasi, potasiamu na chuma.
FIKA OFISINI KWETU UJIPATIE STEMCELL YAKO YA UGCAREPLUS.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Address


Dar Es Salaam
0000