Gaudensia na Afya
Together we are solving the problems to various diseases by using Natural made plants medical,
18/07/2023
Value a people
Violence against Children | Global Campaign | World Vision International Our Global advocacy campaign, It Takes a World to End Violence Against Children, is founded on our desire to end violence against children - highlighting when it occurs, empowering young people to speak out and holding those responsible to account.
*BAWASIRI/MGOLO*
β
Bawasiri ni ugonjwa unaotokea katika njia ya haja kubwa, hujitokeza k**a uvimbe au kijinyama ambacho huweza kuonekana hadi nje.
β
Kwa kiingereza hujuliakana k**a piles.
β
Na kitaalam hujulikana k**a hemorrhoids
πAINA ZA BAWASIRIπ
1. BAWASIRI YA NJE
Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa, na huambatana na maumivu, pamoja na kuwashwa kwa ngozi katika eneo hilo. Mara nyingine mishipa hiyo ya damu (vena) hupasuka na damu huganda na kusababisha aina hii ya bawasiri kitaalamu inaitwa Thrombosed hemorrhoid.
2.BAWASIRI YA NDANI
Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa. Na huwa haimbatani na maumivu.
β
Aina hii imeainishwa katika mainisho ya madaraja manne yafuatayo:
β
Daraja la 1 - Bawasiri kutotoka katika mahali pake pa kawaida
β
Daraja la 2 - Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe baada ya haja.
β
Daraja la 3 - Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kuirudisha mwenyewe baada ya haja.
β
Daraja la 4 - Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na vigumu mtu kuirudisha baada ya haja.
*DALILI ZA BAWASIRI*
β
Maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa
β
Damu kunuka kinyesi wakati wa kujisaidia
β
Muwasho sehemu ya tundu la haja kubwa
β
Uvimbe au kinyama kujitokeza sehemu ya tundu la haja kubwa
β
Haja kubwa yaweza kujitokea tu muda wowote
17/07/2021
Suluhisho lipo sasa
07/07/2021
FANGASI UKENI NA UCHAFU KWA MWANAMKE NI HATARI ZAIDI WAHI TIBA MAPEMA
03/07/2021
BAWASIRI ni mojawapo ya matatizo ambayo mara nyingi inapotokea humfanya muathirika kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba.Bawasiri husababishwa na kuvimba kwa mishipa ya damu aina ya vena katika eneo la mfereji wa haja kubwa.
A.KUNA AINA MBILI ZA BAWASIRI(HEMORRHOIDS)
1.Ya nje ya puru- Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na mara nyingi huambatana na maumivu na muwasho katika sehemu hiyo.Mara nyingi mishipa hiyo ya damu(vena)hupasuka na damu huganda na kusababisha hali iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS kitaalamu.
2.Ndani ya puru/tupu/duburi-Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa na haiambatani na maumivu hivyo kuwafanya wengi kutotambua kuwa wana tatizo hili.
Aina hii imegawanyika katika sehemu zifuatazo;
i.Bawasir kutotoka katika mahali pake(iliyosimama)
ii.Bawasir inayotoka wakati wa haja kubwa kurudi yenyewe baada ya kumaliza kujisaidia
iii.Bawasir inayotoka wakati wa haja kubwa na hairudi yenyewe baada ya kujisaidia mpaka mwathirika airudishe mwenyewe.
iv.Bawasir inayotoka wakati wa haja kubwa na ni vigumu mtu kuirudisha baada ya kumaliza kujisaidia.
[6/30, 5:48 PM] Irene HI: Je nini kinasababisha??
[6/30, 5:50 PM] Irene HI: D.ATHARI ZA BAWASIR
-Upungufu wa damu mwilini(ANEMIA)
-STRAGULATED HEMORRHOID
-Kinyesi kutoka na kuvuja bila kujitambua na kusababisha kunuka kinyesi saa zote.
-Kukupunguzia morali ya kufanya kazi kutokana na maumivu hasa watu wanaokaa muda mrefu maofisini.
-Kuathirika kisaikolojia
-Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
-Kupungukiwa nguvu za kiume
[6/30, 5:51 PM] Irene HI: E.JINSI YA KUZUIA BAWASIR
-Kula mboga za majani na matunda na nafaka zisizokobolewa kwa wingi
-Kunywa maji mengi lita sita hadi kumi na mbili kwa siku
-Punguza kukaa kwa muda mrefu chooni bila kutoa choo
02/07/2021
27/06/2021
UGONJWA WA PRESSURE (SHINIKIZO LA DAMU ) NA TIBA YAKE
Nini maana ya shinikizo la damu?
Ni msukumo wa damu ulio juu kuliko inavyotakiwa kwa muda mrefu. Msukumo wa damu huhitajika mwilini ili kusambaza chakula, oksijeni na kutoa uchafu.
Shinikizo la damu hupimwa kwa kutumia kifaa kinachoitwa Sphygmomanometer
Shinikizo la damu husababishwa na nini?
Vitu vifuatavyo vinaweza kusababisha shinikizo la juu la damu:
- Uvutaji sigara
- Unene na uzito kupita kiasi
- Unywaji wa pombe
- Upungufu wa madini ya potassium
- Upungufu wa vitamin D
- Umri mkubwa
- Ongezeko la kemikali kwenye figo (renin)
- Kushindwa kufanyakazi kwa kichocheo kiitwacho insulin
*Uanishaji wa shinikizo la damu
- Presha ya kawaida
24/06/2021
Tatua changamoto ya kiAfya BAWASIRI,, Bila upasuaji kwa Tiba asilia Na Tiba lishe bila chemical sasa, Rudisha Tabasamu kwa Maisha Bora. Sasa Inawezekana
19/06/2021
DR. TS TOOTHPASTE
DAWA YA MENO MADHUBUTI
DR. Ts dawa ya meno iliyotengenezwa kwa mitishamba ya kichina yenye kusaidia matatizo mengi ya kinywa ikiwemo, meno kuoza, fizi kutoka damu na kuvimba inaondoa harufu mbaya kinywani na kuondoa bacteria na masalia kwenye meno.
β Dawa ya meno ya DR. TS inasaidia kupunguza gesi tumboni hivyo ni nzuri kwa wenye vidonda vya tumbo.
β Ni dawa nzuri kwa kuondoa chunusi sugu usoni na vipele na vijipu vidogovidogo.
βInaweza kutumika k**a scrub usoni.
β Unaweza kupaka kwenye fungus miguuni na vidonda ilikuharakisha kupona haraka.
β Nidawa nzuri kwa watoto wenye vijipu na mapele pia nisalama hata wakimeza kwa kuwa inawasaidia kupunguza gesi tumboni.
β Unaweza kutumia k**a after shalve baada ya kunyoa ndevu au mengineyo.
β Inaongeza kinga zidi ya magonjwa ya kinywa.
MATUMIZI MENGINE YA DR.TS
β Tumia kwa kuondoa rangi na kung'arisha kucha zako.
β Tumia kung'arisha masinki ya jikoni hapo nyumbani.
β Tumia kusafisha pasi yako nyumbani.
β Tumia kuondoa madoa kwenye nguo yako na makapeti pia.
β Tumia kusafisha CDs na DVD kwa kuondoa schrach.
β Tumia kwa kung'arisha sori za viatu hasa raba (simple).
β Tumia pia k**a jelly kwenye nywele.
β Tumia kwa kuondoa chewing gum iliyo nasa kwenye nywele.
β Tumia kuondoa shombo kwenye mikono inayotokana na vitunguu saumu, samaki,na vinginevyo.
β Tumia kusafisha chupa au container za watoto zinazotumika kuwekea vinywaji k**a maziwa,chupa za chai ili kung'arisha na kuondoa harufu.
β Tumia kwa kusafisha madoa ya chai,kahawa na kung'arisha meza yako.
β Tumia kwa kusafisha na kung'arisha vitu vya thamani k**a, silver,dimond, rings,gorld, bracelete, gamestone.
β Tumia kwa kusafisha makapeti yenye madoa.
16/06/2021
JE, UNAWEZAJE KUTAMBUA UTE UTE WA SIKU ZA HATARI?
Katika mzunguko wote wa hedhi, ute wa shingo ya kizazi hubadirika. Aina hiyo ya ute huwa ni nzuri na ndio ishara ya siku zisizobadirika za upevushaji yai. Mwanamke anapokuwa katika siku za hatari, ute wa shingo ya kizazi huwa ni wa majimaji, mwepesi, wenye kuteleza, na unaweza kuonekana k**a yai ute wa yai.
[6/11, 8:43 PM] Irene HI: Je, Ute Wa Siku Za Hatari Unaanza Kutoka Nyakati Gani?
Uteute wa siku za hatari hutofautina kidogo kwa kila mtu. Kwahiyo, ili kutambua ute wa siku za hatari, basi mwanamke anapaswa afuatilie mzunguko wake kwa muda wa miezi kadhaa. Siku ambazo ute hubadirika hutofautiana kwa kila mwanamke. Wanawake wanaochelewa kupevusha mayai yao, kwa mfano, wanaweza kutarajia kupata ute ute wa siku za hatari baada ya siku ya 14.
Kwa ujumla, mzunguko wa uteute huendana na mfano huu:
1. Mzunguko mfupi(siku ya 1-5):
Hii ni pale damu ya hedhi inapotoka
2. Baada Ya Kipindi Cha Hedhi(Siku ya 5-10):
Mwanzoni, kunaweza kukawa na ute kidogo au ukakosekana kabisa, lakini uteute wa kunata k**a gundi unaweza kufuatia. Hiki ni kipindi cha uwezo mdogo sana wa mwanamke kupata ujauzito.
[6/11, 10:10 PM] Irene HI: 5. Baada Ya Yai Kupevuka(Siku ya 14-22):
Baada ya yai kupevuka, mwili huachilia homoni ya progesterone, ambayo hukausha uteute unaotoka kwenye shingo ya kizazi. Uteute huo unaweza kuonekana wa kijivu hapo awali, baadaye unakuwa mzito.
6. Kabla Ya Kipindi Cha Hedhi(siku ya 22-28):
Kipindi cha hedhi kinapowadia, ute ute unaweza kuwa na uthabiti k**a gundi tena. Kunaonekana kuwa na ute kidogo au kusiwepo kabisa kwa muda wa siku 1-2 kabla ya damu ya hedhi kuanza kutoka. Baadhi ya wanawake wao huona matone matone kabla ya damu ya dhi kuanza kutoka.
[6/11, 10:18 PM] Irene HI: 6. Kabla Ya Kipindi Cha Hedhi(siku ya 22-28):
Kipindi cha hedhi kinapowadia, ute ute unaweza kuwa na uthabiti k**a gundi tena. Kunaonekana kuwa na ute kidogo au kusiwepo kabisa kwa muda wa siku 1-2 kabla ya damu ya hedhi kuanza kutoka. Baadhi ya wanawake wao huona matone matone kabla ya damu ya dhi kuanza kutoka.
Yai linapopevuka hufanya kazi muhimu sana katika kuweka muonekano mzuri wa uteute wa shingo ya kizazi. Mwanamke ambaye hapevushi mayai yake anaweza akaona mabadiriko machache katika ute unaomtoka ukeni.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Dar Es Salaam