Afya yangu
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Afya yangu, Health/Beauty, Ilala boma, Dar es Salaam.
TEZI DUME NI NINI MADHARA YA KUVIMBA KWA TEZI DUME NA TIBA
TEZI DUME
Tezi dume ni moja ya tezi ya uzazi ya kiume ambayo kila mwanaume anayo, tezi hii lipo chini ya kibofu cha mkojo na inazunguka njia ya mkojo toka kwenye kibofu kwenda kwenye uume.
NOTE:Jinsi umri unavyoongezeka tezi dume nayo huongezeka ukubwa ambao unaweza kuwa wa kawaida au Saratani.
Kuna aina tatu za magonjwa ya tezi dume.
•Maambukizi ya Bakteria (Prostatitis).
•Kukua kwa tezi dume ambayo sio Saratani (Benign Prostatic
Hypertrophy-BPH).
•Saratani ya tezi dume.
KAZI YA TEZI DUME
•Kutoa majimaji anayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) kutengeneza manii (semen).
SARATANI YA TEZI DUME
Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vitokanavyo na saratani kwa wanaume duniani.
Pia ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa miaka 40 na kuendelea.
VISABABISHI VYA SARATANI YA TEZI DUME
Chanzo hasa cha saratani ya tezi dume hakijulikani, saratani hii ina uhusiano mkubwa na;
•Umri, Wanaume wenye umri kuanzia
miaka 40 na kuendelea wanapata zaidi saratani ya tezi dume.
•Vyakula vyenye kiasi kikubwa cha mafuta, hasa ya wanyama.
•Historia ya tatizo hili kwenye familia (Genetic).
•Kuwa na uzito uliokithiri.
DALILI ZA SARATANI YA TEZI DUME.
Katika hatua za awali, dalili hazitofautiani sana na zile za kuvimba kwa tezi dume Isiyokuwa Saratani (BPH).
Dalili hizo ni pamoja na;
•Kusikia kupata haja ndogo mara kwa mara hasa nyakati za usiku.
•Haja ndogo kuchelewa kutoka unapoanza kukojoa.
•Kutoa mkojo wenye mtiririko dhaifu na kuchuruzika kidogo kidogo baada ya kumaliza kukojoa.
•Kujikakamua wakati wa kukojoa na kushindwa kumaliza mkojo wote.
•Kutoa mkojo au manii
yaliyochanganyika na damu.
•Maumivu makali sehemu mbalimbali za mwili k**a Saratani imesambaa.
•Kupungua uzito, kuhisi kichefuchefu, uchovu na kizunguzungu.
UCHUNGUZI / UPIMAJI
•Uchunguzi kwa kutumia kidole cha shahada kupitia njia ya haja kubwa na kuhisi ukubwa wa tezi kwenye ukuta wa puru.
•Kipimo cha damu kuangalia kiwango cha aina ya ‘protein’ iitwayo ‘Prostate
Specific Antigen (PSA), proten’ hii huwa juu kuliko kawaida k**a mtu ana Saratani ya Tezi Dume na wakati mwingine k**a ana maambukizi (prostatitis).
•Kuchukua kipande cha nyama kwenye tezi (Prostate Biopsy) kwa uchunguzi wa kimaabara.
•Kipimo cha mawimbi sauti (Ultrasound) ambacho husaidia kuonyesha ukubwa na sura ya tezi dume.
•Vipimo vya CT scan, MRI kutambua k**a Saratani imesambaa sehemu nyingine za mwili.
K**A USIPO TIBU TEZI DUME, haya ndo madhara utayopata
* Mrija wa mkojo kuziba, hivo kushindwa kukojoa.
* Mawe kwenye kibofu Cha mkojo.
* UTI
* Figo kushindwa kufanya KAZI.
* Mawe kwenye Figo.
* Kupoteza nguvu za kiume
* Kushindwa kuzuia mkojo
* Mashambulizi kwenye mifupa,na n.k
*TIBA YA UVIMBE,SARATANI YA TEZI DUME IPO KWA NJIA YA ASILI BILA UPASUAJI :
K**a unasumbuliwa na tatizo la Tezi Dume TUWASILIANE kwa msaada zaid ushaur ni bure kabisa
0754296293 na 0624408762
Afya yangu Health/beauty
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Ilala Boma
Dar Es Salaam