Afya bora wanawake

Afya bora wanawake

Share

Tunasaidia kutatua changamoto zote za uzazi kwa wanawake

04/11/2022

*~ SABABU ZA MVURUGIKO WA HOMONI:-*
1. Utoaji wa mimba
2. Uwepo wa sumu mwilini
3. Kutokula mlo uliokamili au mfumo mbovu wa maisha
4. Family history (Upungufu au ongezeko ya homoni ya progesterone na Estrogen)
5. Mabadiliko ya mazingira au hali ya hewa
6. Uzito mkubwa au kitambi
7. Msongo wa mawazo
7. Kutofanya mazoezi
8. Matumizi ya kisasa ya uzazi wa mpango
9. Kukoma kwa hedhi
*DALILI ZA MVURUGIKO WA HOMONI*
1. Maumivu wakati wa tendo la ndoa
2. Kutoshika mimba
3. Mzunguko wa hedhi kubadilika
4. Kuongezeka uzito au kitambi
5. Kupungua hamu ya tendo la ndoa
6. Kupoteza kumbukumbu
7. Hasira za Mara kwa Mara
8. Damu kutoka nyingi wakati wa hedhi au kutoa damu yenye mabonge mabonge
9. Uke kuwa mkavu
10. Kutoka jasho jingi usiku
11. Maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
12. Mzio wa vyakula (Allergie), kuchagua chagua vyakula
*MADHARA YA MVURUGIKO WA HOMONI*
1. Kutoshika ujauzito kwa muda mrefu
2. Mimba kuharibika mara kwa mara
3. Kukosa mtoto au Ugumba
4. Maumivu wakati wa tendo la ndoa
5. Kuwa na tabia na maumbile ya kiume
6. UTI (Urinary Tract Infection) ya mara kwa mara
7. Kuzeeka mapema
8. Kuziba kwa mirija ya uzazi
9. Saratani
10. Uvimbe kwenye uzazi wa mwanamke (Fibroids and Cysts)

inatibikaa kwa ushauri na matibabu karibuni sana .

Karibu kwa mawal au karibu ofsn kwetu. Kumbuka afya ndo msingi wa maisha bora

11/10/2022

Acha kuteseka suruhisho lipo, njoo uwe miongoni mwa wanawake wanao furahiya maisha,
Hakuna mwanamke tasa duniani kusudi la Mungu kutuleta Duniani ni kuzaa na kuongezeka
Karibu sana
+255782450945

09/10/2022

*DALILI ZA HATARI KWA MWANAMKE ZINAZO MFANYA ASIPATE MIMBA.*

🙆Ukavu ukeni
🙆Maumivu wakati wa tendo la ndoa
🙆Kutoa jasho usiku
🙆Maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
🙆Upungufu wa hamu ya tendo la ndoa
🙆Mabadiliko ya siku za hedhi na kupata hedhi kwa muda mrefu unaozidi siku 7. (heavy bleeding, au kujaza pedi moja kwa saa moja)
🙆Kukosa hedhi kwa muda mrefu, na kutoa damu yenye mabonge mabonge wakati wa hedhi
🙆Uchovu wa mara kwa mara
🙆Hasira za mara kwa mara
🙆Kukosa usingizi
🙆Homa za usiku na Kizunguzungu cha mara kwa mara
🙆Mzio wa vyakula (Allergie), kuchagua chagua vyakula
🙆Ongezeko ya tumbo na nyama uzembe
🙆Kuharibika kwa ngozi (chunusi, vipele… n.k)
🙆Maumivu ya viungo
🙆Upungufu wa nywele kichwani.
🙆Kusahau sana (kukosa kumbukumbu)
🙆Kupata hedhi wakati wa ujauzito (progesterone ikiwa imezidi)
🙆Kutokupata hedhi (balehe) adi umri wa miaka 20 na kuendelea
🙆Mwili kutokukua, kuonekana k**a binti mdogo, na kutokukua kwa via vya uzazi
🙆Msongo wa mawazo na kukosa kujiamini
🙆Kusinyaa na kupauka kwa ngozi wakati wa

02/10/2022

*UVIMBE KATIKA MFUKO WA KIZAZI (FIBROIDS)*
Hizi ni vimbe ndogo ndogo ambazo hutokea kwenye misuli laini ya mfuko wa uzazi.

*AINA ZA FIBROIDS* (4)
👉🏾Submucosal Fibroids, hutokea kwenye tumbo la kizazi au ndani ya kizazi
👉🏾Intramural Fibroid, unaotokea ndani ya nyama ya kizazi
👉🏾Subserosal Fibroids hii hutokea nje kwenye ukuta wa kizazi na
👉🏾Cervical fibroids, hutokea kwenye shingo ya kizazi.

*KISABABISHI*
☑️Kuongezeka kwa kiwango cha juu kwa vichocheo vya homoni ya estrogeni.
DALILI
☑️Kutokwa damu nyingi kwa muda mrefu wakati wa hedhi ikiambatana na mabonge mabonge isivyo kawaida, au ☑️Kutokwa damu isiyo ya kawaida katikati ya mwezi au
☑️Hedhi zisizokuwa na mpangilio.
☑️Upungufu wa damu
☑️Kupata maumivu ya kiuno hasa wakati wa hedhi
☑️Maumivu makali ya tumbo
☑️Maumivu wakati wa tendo la ndoa
☑️Maumivu ya mgongo
☑️Kukojoa mara kwa mara
☑️Kutotungwa kwa mimba au mimba kuharibika na kutoka
☑️Tumbo kuwa kubwa hasa sehemu ya chini
☑️Maumivu ya miguu
☑️Kukosa choo .

Tupigie kwa ushauri zaidi +255782450945
Tembelea ofs zetu zipo
Mwenge DSM
Zanzibar
Mbeya
Mwanza
Iringa
Moshi
Dodoma
Mtwara.

29/09/2022

_Sababu hasa za kuota kwa fibroids katika viungo vya uzazi vya mwanamke bado hazieleweki vizuri ingawa inaamika kwamba kila uvimbe wa fibroid unatokana na seli ya musuli wa uterus ambayo imeamua kuwa na tabia ya tofauti na nyingine na ikaanza kukua kwa haraka ikichangiwa na uwepo wa homoni ya estrogen.
Wanawake wanaokaribia kufikia ukomo wa kupata siku zao za mwezi wanaonekana kuwa kwenye hatari kubwa zaidi ya kupata fibroids kwa sababu ya kuwa wameishi na homoni ya estrogen kwa muda mrefu zaidi. Wanawake wenye asili ya mchanganyiko wa wamarekani na waafrika (wamarekani weusi) nao wanaonekana kupatwa na fibroids zaidi ya wanawake wengine ingawa sababu bado haijajulikana.
_ Inakadiriwa kuwa kati ya asilimia 20 hadi 50 ya wanawake walio katika umri wa kuzaa, miaka 30 hadi 50, wana uvimbe katika kizazi (fibroids), ingawa wengi wao hawahangaiki kuchukua vipimo. Uvimbe wa fibroids unakuwa na ukubwa tofauti tofauti, unaweza kuwa mdogo k**a haragwe au kufikia ukubwa wa tikiti maji.

15/09/2022

*SHINGO YA KIZAZI NI NINI?*
-Shingo ya kizazi (cervix) ni kiungo cha mwili kinachopatikana kwenye mfumo wa uzazi wa mwanamke. Ni sehemu ya mji wa mimba (Uterus) inayotokezea kwenye uke (tupu) wa mwanamke.

*SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI?*

-Ni mabadiliko hasi (yasiyo ya kawaida) ya chembechembe hai zilizopo kwenye shingo ya kizazi. Mara nyingi saratani hii ikiwa inaanza haionyeshi dalili yoyote hivyo mgonjwa hawezi kuchukua hatua yoyote kukabiliana na tatizo hili kwa wakati huu.

-Kwa kiasi kikubwa saratani hii husababishwa na maambukizi ya mda mrefu (persistence infection) ya virusi viitwavyo Human papilloma, ambavyo huenezwa kwa njia ya kujamiiana. Kawaida mwili una uwezo wa hudhibiti maambukizi haya yaingiapo mwilini, lakini yasipodhibitiwa kikamilifu na kuwepo mwilini kwa mda mrefu husababisha ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi.

*MAMBO MENGINE YANAYOCHANGIA KUPATA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI*

-Kufanya ngono zembe.
-Kuwa na wapenzi wengi.
-Kukoma siku katika umri mkubwa.
-Utumiaji mafuta mengi katika chakula.
-Kutokufanya mazoezi ya mara kwa mara.
-Unene kupita kiasi.
-Uvutaji sigara.
-Utumiaji wa pombe kupita kiasi.
-Historia ya saratani ya matiti katika familia.

*DALILI ZA UGONJWA WA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI*

-Dalili za ugonjwa huu huanza kujitokeza baada ya tatizo kuanza kukomaa, zifuatazo ni baadhi ya dalili

-Kutokwa na maji maji yenye harufu ukeni.
-Kutokwa damu baada ya kujamiiana.
-Kutokwa damu kusiko kwa kawaida (siyo damu ya hedhi)
-Kuumwa mgongo na kiuno.
-Kuumwa miguu.
-Kizunguzungu na kuishiwa nguvu.

*NINI KIFANYIKE?*
-Saratani ya shingo ya kizazi inazuilika au kutibika kabisa endapo itagundulika ikiwa kwenye hatua za awali.

Hivyo ni muhimu kufanya uchunguzi wa afya yako kwa kadiri utakavyoshauriwa na wataalam wa afya

Wanawake wote walio na umri kuanzia miaka 30 na kuendelea wanatakiwa kufanya uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi.

*Kumbuka*: Wakati wa uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi ni sasa usisubiri hadi uone dalili, fika kituo cha huduma za afya kwa ushauri/mwongozo Zaidi. Piga +255782450945 kupata huduma

11/09/2022

USITESEKE TENA TUPO KWAAJIRI YAKO.
Tupigie 0782450945

04/09/2022

Kupata ujauzito inawezekana kwetu, hii ndio kauri mbiu yetu. Acha kulia tena futa machozi tutafute tukupe ushauri nini kinatakiwa kufanyika na matokeo kwetu ni ya lazima usiogope
+255782450945

30/08/2022

Wanawake wengi wamekua wakipitia changamoto mbalimbali za kiafya hasa kwa upande wa uzazi. Sababu za kupelekea changamoto hizi ni mfumo mzima wa maisha hupelekea magongwa mbali mbali kwa kina mama mfano kukosa vyakula vyenye virutubisho, matumizi mabaya za madawa na stress au kukosa mda wa kupumzika

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Website

Address


Mwenge
Dar Es Salaam