AFYA YAKO Kipaumbele
Page hii inahusika na utoaji elimu na suluhisho juu afya ya binadamu kutokana na magonjwa mbalimbali
JE UNATAKA KUEPUKA MAISHA YA KUIGIZA KIROHO???
UNAWAZA KULIPIZA KISASI KWA MTU ALIYEKUUDHI???
SOMA KWA MAKINI MANENO HAYA UTAJIFUNZA KITU.
Kuna tofauti kubwa na yakushangaza katika utakaso uliofanywa katika maisha ya Yohana na uzoefu wa mfuasi mwenzake, Yuda. K**a mshirika wake, Yuda alidaikuwa mfuasi wa Kristo, lakini alikuwa na namna tu ya utauwa. Hakuwa na hisia kwa uzuri wa tabia ya Kristo; na mara
nyingi, aliposikiliza Maneno ya Mwokozi, usadikisho ulimjia, lakini hakuunyenyekeza moyo wake au kuungama dhambi zake. Kwa kuupinga ushawishi wa Mungu, alimvunjia heshima Bwana ambaye alidaikumpenda. Yohana alipambana kwa dhati na bidi dhidi ya makosa yake; lakini Yuda alikiuka dhamiri yake na kuangukia kwenye majaribu, akijifunga mwenyewe kwa usalama
zaidi na mazoea yake ya uovu. Uzoefu wa zile Kweli ambazo Kristo alizifundisha zilikuwa zinapingana na tamaa na makusudi yake, na hakuweza kujizuia kuyaacha mawazo yake ili kupokea hekima kutoka mbinguni. Badala ya kutembea katika nuru, alichagua kutembea gizani. Tamaa za kutenda uovu, kutamani, tamaa za kulipiza kisasi, mawazo ya giza na ya huzuni, yalithaminiwa hadi Shetani alipopata udhibiti kamili juu yake. AA 557.2
BWANA AKUBARIKI SANA.
22/11/2024
SIKU YA TISA:
KANUNI ZA MAZOEZI YA MWILI
3. KANUNI ZA MAZOEZI YA MWILI.
Mwanzo 2.15 “Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.”
Mojawapo ya kanuni bora kabisa katika kutunza afya bora ni kufanya mazoezi ya viungo vyote vya mwili.
Mwili unatengenezwa kwa namna ambayo kila kiungo kinayo kazi yake na iwapo hakikuandaliwa vizuri misuli hulegea na uwezo wa kufanya kazi hupungua.
Baada ya uumbaji Adamu na Hawa walipewa kazi ya kufanya haikuwa kuwapa majina wanyama wote na viumbe vingine na kutawala tu ila alipewa kazi ambayo ilikuwa ni ya kuzoelesha viungo vyake.
Kazi yake ilikuwa kulima kutunza bustani, kufanya kazi kwa mikono yake kwa hivyo mazoezi ni kanuni ya mbinguni.
Binadamu alitakiwa kutoka nje kwenye hewa safi na viwango vizuri wa jua ili alime na kutunza bustani kufanya mazoezi ya viungo yenye faida kubwa kwa afya yake.
KUNA FAIDA NYINGI KUELEWA KANUNI HII YA AFYA:
Viungo vya Binadamu vimeumbwa kwa kulenga utendaji shughuli mbalimbali, ndiyo maana mkono usiofanya kazi husinyaa, miguu isiyofanya kazi hulemaa, misuli inayofanya kazi huongezeka na kuwa yenye nguvu zaidi kwa hiyo mazoezi huongeza nguvu ya kufanya kazi.
Mwili wa Binadamu unayo mishipa mingi ya damu ile iendayo mwilini toka kwenye moyo (arteries) na ile iendayo moyoni toka mwilini katikati yao kuna mapafu.
Damu chafu toka mwilini huingia mapafuni, husafishwa na kurudi moyoni hana pampu maana pampu ni moyo. Husafiri kutegemea na kubanwa na misuli.
Mazoezi huongeza kiwango cha damu inayoingia moyoni, pia husababisha mapafu kufanya kazi yake vizuri zaidi.
Mazoezi huondoa uchafu mwingi mwilini kwa kutumia ngozi k**a jasho, mapafu na figo hivyo husababisha mwili kuwa safi.
Mwili ulivyoumbwa unahitaji mazoezi ya kila siku ili uwe na nguvu za kutosha.
Kutokana na mazoezi mazuri ya mwili wote viungo vyote huhusika na hata kuuweka ubongo katika hali nzuri ya kufikiri ikiwa mtu anafanya mazoezi.
Wachungaji, Wainjilisti wangekuwa na Afya Bora sana k**a wangefanya mazoezi kwa utaratibu unaofaa na kufanya kazi iliyo nzuri na kubwa zaidi.
Tunapokuwa vijana lazima tuweze kujifunza kulinganisha na kuweka urari unaofaa kwa mazoezi ya mwili na Akili isiwe kwamba sehemu moja inaendelezwa vizuri lakini nyingine inaachwa na kusinyaa.
Lazima kila kijana apange ni muda gani atautumia na upi atautumia kufanya mazoezi.
Wanafunzi wasiofanya mazoezi wana vichwa vya moto na miguu baridi na matokeo yake ni afya mbaya.
Kutembea nje kwenye hewa safi ni mojawapo ya kanuni bora sana za kutunza Afya zetu hii inasaidia hata wagonjwa waliolazwa wanapopata nafuu watembee kwenye hewa safi nje wataburudika na afya zao zitarudi haraka zaidi.
Matembezi mafupi baada ya milo husaidia mwili kusaga chakula vizuri zaidi lakini kazi nzito za akili na mwili huathiri usagaji chakula.
Mazoezi ya viungo yanayopanua vifua na kurekebisha sauti yatakuongezea siku zako za kuishi.
Watoto wanahitaji kutumia miaka yao 8-10 ya kwanza na maisha katika kushughulikia bustani ili wajenge msingi mzuri wa mienendo ya Afya zao ukubwani ili akirudi kutoka shule atambue umuhimu wa kufanua kazi ya mikono yenye manufaa.
Mazoezi yasiyotosha yanaacha akili zisizofanya kazi vizuri, mawazo yasiyopangika sawasawa hufanya watu kutofikiri vyema kabla ya kufanya chochote.
MAZOEZI GANI?
1: TEMBEA.
Siku sita kila siku saa 1.
Spidi baada ya miezi mitatu utembee hatua 120 kwa dakika.
Ujihadhari ukiwa una umri zaidi ya 35.
Tumia kiatu cha sport (raba) nzuri za kutembelea.
Tumia dk 5 kupunguza kasi taratibu kwa kumalizia.
Chunguza mapigo ya moyo wako – ikiwa umepumzika, kila dk 5 hesabu mapigo sekunde 10 zidisha mara 6 (ikizidi 100) punguza kwenda ukiwa na umri miaka 35.
2: KIMBIA, ENDESHA BAISKELI
Hakikisha unatoka jasho la kutosha.
Mazoezi yanapokuletea maumivu ya misuli na unapojisikia vibaya baada ya mazoezi ya mwili ni dalili ya kuamka kwa misuli yako na haina hatari yoyote ukiendelea na mazoezi hali hiyo itatoweka
KABLA YA KUFANYA MAZOEZI ZINGATIA YAFUATAYO:
Ufahamu uwezo wa moyo wako kwa kupima mapigo ya moyo kwa dakika mapigo machache zaidi moyo una nguvu zaidi zipo gredi 5.
GRADE A Chini ya mapigo 55 dk-Fanya mazoezi uwezavyo.
GRADE B 55-65/dk- Fanya mazoezi ya kutosha.
GRADE C 66-79/dk- Fanya mazoezi ya kawaida.
GRADE D 80-90/dk- Fanya mazoezi kwa uangalifu.
GRADE E Zaidi ya 90/dk-Mwone daktari kabla ya kufanya mazoezi.
EPUKA YAFUATAYO:
Mazoezi yasiyo na mpangilio.
Kuacha mazoezi ghafla.
Mabadiliko makubwa ya hewa
CHANZO: MASOMO YA IDARA YA HUDUMA ZA AFYA, SOUTHERN TANZANIA UNION MISSION
22/11/2024
SIKU YA NANE:
KANUNI BORA ZA MATUMIZI YA MAJI NDANI NA NJE YA MWILI.
2. KANUNI BORA ZA MATUMIZI YA MAJI NDANI NA NJE YA MWILI.
“Mto wa maji mema ukatoka Eden –ukainyweshea ile bustani nzuri” Mwanzo 2:10 “Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne.”
Maji ni Kitu cha muhimu sana katika maisha ya viumbe vyote vilivyo hai. Ndiyo maana maji yalipewa umuhimu wa pekee sana na Mungu katika Uumbaji wa Ulimwengu.
Mwanzo 1:1,2 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.”
Umuhimu wa maji ndani na nje ya mwili unajitokeze tunapoangalia mambo yafuatayo:
a) Usafi wa mazingira ya ndani ya mwili.
b) Usafi wa mazingira nje ya mwili.
USAFI WA MWILI
Baada ya kutumika vyakula, ndani ya mwili, masazo na chembechembe za uchafu na sumu mbalimbali vinahitajika kuondolewa kutoka ndani ya mwili.
Taka hizi ngumu hutoka mwilini kupitia njia zifuatazo, Figo k**a mkojo, ngozi k**a jasho, Mapafu katika hewa iliyopumuliwa, na tumboni k**a haja kubwa.
Uchafu huu wote unahitaji maji ili uweze kutoka vizuri. Na baada ya hapo mwili wote kusafishwa kwa maji kwa nje ili kuuweka katika hali ya usafi.
MAJI NDANI YA MWILI
Je unajua kwamba wewe umetengenezwa kutumia maji mengi zaidi ya vitu vingine?
Asilimia 50%-70% ya uzito wako ni maji.
Kila chembechembe ya mwili wako imechanganyika na maji.
Vichocheo mbalimbali mwilini vinafanya kazi kubwa sana, vikitumia maji k**a kiwezeshi kikuu (Hufanya kazi katika hali ya majimaji).
Kila kiungo mwilini kinahitaji maji maji ili kufanya kazi zake vizuri.
Damu yako inazo chembechembe zinazotegemea maji ili kufanya kazi ya kusafisha hewa pamoja na mamia ya virutubisho vingine toka sehemu moja ya mwili hadi sehemu nyingine ya mwili.
Maji ni muhimu ili kurekebisha joto la mwili wako ili libaki katika hali ile inayokubalika. Joto la mwili likizidi sana, mwili wako hulegea na kukosa nguvu haraka, vichocheo vyote vya mwilini, vinavyofanya kazi mbalimbali hufanya kazi kwa kuzingatia maji maji, pamoja na viwango maalumu vya joto.
Usafi wa figo, akili, kongosho, an viungo vingine yote hutegemea maji mtu aliyotatumia.
Maji huondoa uchafu kutoka kwenye kila chembechembe ya mwili na kuisafisha damu kupitia, vinyweleo vya ngozi, k**a, jasho, figo, k**a mkojo, chooo kikubwa na hata mapafu.
KANUNI GANI ZA UTUMIAJI WA MAJI?
Kunywa maji mengi glasi 6-10 za maji kila siku ni muhimu.
Usinywe maji wakati wa kula chakula. Kunywa dk 30 kabla ya kula chakula na pia saa 1 – 2 baada ya kula chakula.
Kunywa maji mengi katikati ya mlo na mlo na hasa ukiamka asubuhi.
Maji yote ya kunywa yachemshwe sana ili kuua vimelea vya magonjwa.
FAIDA GANI?
Kinga kuu ya magonjwa mbalimbali moyo, kibofu, figo n.k.
Kuondoa uchafu kutoka ndani ya mwili.
Kuondoa vijidudu mbalimbali kutoka ndani ya mwili.
MAJI NJE YA MWILI
Watu wengi Sana hawafahamu umuhimu na namna ya kutumia maji nje ya mwili.
Kuiosha miili yetu kwa mpangilio siyo tu kunaondoa uchafu tunaoupata kutoka nje ya mwili bali pia kunasafisha uchafu kutoka ndani ya miili unaolundikana kila wakati katika ngozi kupitia vinywekeo ambavyo wakati mwingine kuziba.
Harufu mbaya kutokana na jasho, kuganda na kuoza kwa uchafu uliolundukana katika ngozi. Ukungu, Chawa, Upele na magonjwa mengine ya ngozi.
JE ULIJUA KUWA UNAPASWA KUSAFISHA MWILI WAKO NJE YA MWILI K**A VILE NDANI KILA SIKU?
Mwili wako unaposaga chakula na kutengenezea nguvu za kufanyia kazi wakati huo hutokeza masazo, mabaki na takataka na chembechembe za uchafu zinazohitajika kutolewa nje.
Figo hufanya kazi ya kusafisha damu.
Uchafu ulioyeyushwa kwenye maji kutoka kila kiungo unahitajika kusafishwa katika figo, katika hali ya majimaji ili damu safi itoke kwenye mwilikupitia kwenye mapafu pamoja na moyo.
Uchafu hutoka k**a mkojo na jasho.
Kwa ajili ya uchujaji huu mkubwa kufanya kazi yake vyema kunahitajika maji mengi ya kunywa: Lazima unywe glasi 6-10 (yaani lita 2-3) za maji kila siku ili kufanya mwili ufanye kazi yake vyema.
Huwezi kuondoa uchafu mwilini bila glasi 6 na zaidi za maji kila siku.
FAIDA YA MAJI NJE YA MWILI
Kuondoa uchafu nje ya mwili
Huondoa magonjwa ya ngozi, harufu mbaya, na kusafisha mazingira ya binadamu, nguo safi, Nyumba, Kupiga deki, na vitu vyote vinavyosafishika kwa maji.
KANUNI ZA KUSAFISHA MWILI
1: KUOGA.
Oga maji baridi au uvuguvugu.
Oga mara baada ya kuwa mchafu.
Oga ukitumia sabuni ya kawaida,na dodoki la kawaida.
Usisugue ngozi sana hasa kwa jiwe la kuogea maana utaiumiza ngozi na kuufanya mwili uumie na kuviruhusu vijidudu mbalimbali kuingia kirahisi katika mwili.
2: KUNAWA.
Nawa baada ya kwenda haja kubwa na ndogo
Nawa kabla ya kula na baada ya kula
Nawa uso kila ukiamka
Ukifika nyumbani kutoka kazini nawa mikono na hata k**a ikiwezekana nawa na miguu—Oga
CHANZO: MASOMO YA IDARA YA HUDUMA ZA AFYA, SOUTHERN TANZANIA UNION MISSION
21/11/2024
SIKU YA SABA (07):
KANUNI MUHIMU ZA KUZINGATIA KATIKA ULAJI NA UNYWAJI
Kanuni muhimu za kuzingatia katika ulaji na unywaji;
Mtu anahitaji kula vyakula vya aina zote ili awe na afya njema.
1. Kula mlo wenye michanganyiko ya vyakula vyote ikiwezekana.
Mchanganyiko wa Mchanganyiko wa vyakula vyakula katika katika kiwango kiwango kinachotakiwa kinachotakiwa ni ni vya vya lazima ili mwili upate lazima ili mwili upate lishe kamili lishe kamili inayotakiwa inayotakiwa. .
2. Badilisha chakula chako kila mlo.
Usile aina moja tu ya vyakula kila siku au kila mlo, badili badili mara kwa mara.
3. Usile katikati ya mlo.
Ule wakati ule ule uliowekwa kwa milo kila siku, acha angalau masaa 4-5 katika mlo na mlo. Zingatia masaa ya kula chakula – wakati wa kula usibadilishwebadilishwe ili mwili ujizoeze kujijenga vema.
4. Kula milo miwili au mitatu kwa siku.
K**a ukichagua kula milo miwili zingatia kiasi cha chakula kulingana. K**a utachagua kule milo mitatu milo miwili ya kwanza ilingane, na ule mlo wa tatu au wa mwisho uwe nusu tu ya mlo wa kwanza au wa pili yaani asubuhi 2/5 ya mlo wote wa siku mchana 2/5 ya mlo wote wa usiku, jioni 1/5 ya mlo wote wa siku. Mabadiliko madogo hayawezi kuleta athari kubwa.
5. Usile chakula kingi Sana, hupumbaza akili.
Ule chakula cha kutosha asubuhi. kamwe chakula kisiliwe kabisa usiku jitahidi kupata mlo wa jioni mapema ili tumbo lipate kupumzika vyema wakati wa kulala.
6. Punguza ulaji wa vyakula vitamu sana ukiepuka vingine vidogo vidogo Katikati ya milo vikiwemo soda, biskuti, p**i, n.k.
7. Usinywe pamoja na chakula.
Kunywa maji mengi katikati ya mlo mmoja na mwingine ukizingatia kunywa zaidi sehemu zenye joto kali pamoja na unapofanya mazoezi au kazi ngumu, unashauriwa kwa kawaida kutumia glasi 8-10 za maji kila siku.
8. Usikoboe nafaka.
Jitahidi kula vyakula katika hali yake ya asilia. Usipendelee vyakula vilivyokobolewa vinavyooshwa sana ingawaje unaweza kutumia kiasi kidogo mfano tumia ngano nyeupe, sukari nyeupe kiasi tu, (kwa ujumla vyakula katika hali ya asili ni bora zaidi).
9. Tumia vyakula vya kukaanga kidogo sana maana vyakula hivi kwanza vina mafuta mengi, pili ni vigumu sana kusagwa tumboni na kusababisha matatizo ya uyeyushaji katika chakula.
10. Kula polepole, utafune vizuri. Tafuna chakula mpaka kilainike usimeze tu.
Ndani ya mdomo kuna vilainishi (enzymes) ambavyo vina umuhimu wa pekee katika ulainishaji, usagaji na utayarishaji wa chakula kinywaji kabla ya kumezwa. Chakula kisichotafunwa hulipa shida kubwa tumbo kufanya kazi ya ziada isiyo ya lazima na matokeo yake watu wengi wana malalamiko mbalimbali.
11. Usitumie chumvi nyingi.
Chumvi nyingi imeonekana kuchangia kuongezeka kwa magonjwa mbalimbali k**a vile shinikizo la damu na moyo. Unashauriwa kuchanganya chumvi katika chakula wakati wa kupika na siyo kwenye meza ya chakula kilichopakuliwa. Usitumie zaidi ya ½ kijiko cha chai kwa mtu mzima kwa siku.
12. Usitumie mafuta mengi.
Tumia mafuta kiasi kidogo tu kiasi siyo zaidi ya kijiko 1 cha chai kwa siku.
NJIA SABA YA MAKOSA KATIKA ULAJI;
1.Vyakula vilivyokobolewa sana:
Havina vitu vinavyoitwa Fiber (aina ya nyuzi nyuzi ndogo sana) ambavyo husaidia kuzuia cancer(Saratani).
2.Kula chumvi nyingi:
Huleta magonjwa ya mishipa ya damu na hata ugonjwa wa moyo.
3.Kula sukari nyingi:
Husababisha matatizo ya unene.
4. Kula bila utaratibu maalum.
Kunaharibu mfumo wa umeng’enyaji wa chakula.
5.Mafuta ya wanyama:
Yana kiasi kikubwa cha Lehemu-cholesterol (mafuta mabaya) nyingi na hufupisha maisha ya mtu.
6. Vinywaji:
(Soda, chai, beer, juice)
Hivi vimejaa sukari, caffeine, vileo, huleta hatari kubwa mwilini.
7. Vitafunwa:
Vyakula vidogovidogo vinavyoliwa kila wakati huharibu uyeyushwaji wa mfumo wa chakula.
CHANZO: MASOMO YA IDARA YA HUDUMA ZA AFYA, SOUTHERN TANZANIA UNION MISSION
21/11/2024
SIKU YA SITA:
UPUNGUFU WA VIRUTUBISHO NA MADHARA YAKE 2
E: VITAMINI:
Ni aina ya kemikali inayopatikana katika chakula na ni muhimu katika afya ya mwili katika ukuaji na katika uzazi. Ukosefu wa aina fulani ya vitamini huleta ugonjwa wa ukosefu wa vitamini hiyo.
AINA ZA VITAMINI;
Kuna aina nyingi za vitamini na kila moja ina kazi yake mwilini, kwa hiyo kila mtu huhitaji vitamini hizo.
Zile zinazoyeyuka kwenye mafuta.
Zinazoyeyuka kwenye maji.
VITAMINI ZINAZOYEYUKA KWENYE MAFUTA:
RETINOL(VITAMINI A)
Hupatikana katika mafuta ya wanyama k**a
Samuli,
Maziwa,
Mafuta ya Samaki.
Pia hupatikana katika mimea.
Mafuta mbegu – mawese.
Matunda mf. Mapapai, maembe
Mboga za majani ya kijani na ya njano.
CAROTENE.
Hupatikana katika mimea k**a vile karoti,
Kazi zake;
Huitajika katika ukuaji wa chembechembe za mwili.
Husaidia kuona usiku, pia hukinga magonjwa ya macho.
Humlinda mtu dhidi ya uambukizo.
Upungufu/ukosefu:
Humfanya mtu awe na upofu wa usiku.
Kupata maambukizo ya ngozi kwa urahisi.
VITAMINI D. (CALCIFEROL)
Hupatikana katika:
Mafuta ya samaki,
maziwa,
yai kiini cha njano,
mafuta ya wanyama.
Pia katika mionzi ya jua (Ultra Violet rays) hukutana na ergosterol iliyoko katika ngozi na kutengeneza Vit. D.
Kazi zake;
Kusaidia kunyonywa kwa madini ya chokaa mwilini
Ukuaji mzuri kwa watoto. Kujengeka vizuri kwa mifupa.
Ukosefu/upungufu;
Mtoto hupata matege miguu hujipinda.
Ukuaji usioridhisha hasa mifupa.
Kutokukua kwa meno vizuri.
Ugonjwa wa mifupa (osteoimalacia).
VITAMINI E (TOCOPHEROL)
Hupatikana:
Katika mayai,
Mboga za majani
Nafaka,
Karanga.
Husaidia kazi ya vitamini A.
VITAMIN K
Hupatikana katika:
Samaki,
maini,
mboga za majani ya kijani,
matunda
na mayai.
Husaidia ugandaji wa kawaida wa damu.
Ukosefu/Upungufu.
Husababisha kutoka damu hasa walio na ugonjwa wa ini.
Kuvuja damu kwa watoto wachanga.
VITAMINI ZINAZOYEYUKA KWENYE MAJI:
VITAMINI B ;
Hili ni kundi la zaidi ya makundi 12, ni rahisi sana kuharibika na maji wakati wa kupika. Kundi hili la vitamin hupatikana katika nafaka, karanga, yai kiini cha njano, chakula aina ya kunde na nyama.
KAZI ZAKE;
a)-Vitamin B 1 (Thiamine)
huhitajika katika uyeyushwaaji mzuri wa chakula cha wanga.
Ukosefu wa Vitamin B1
Husababisha ugonjwa wa beriberi:-
dalili zake:
kukosa hamu ya kula, kuvimba mwili, moyo hushindwa kufanya kazi.
b)-Vitamin B 2 (Riboflavine)
Husaidia wanga na Protini kuyeyushwa.
Husaidia kutengeneza vineng’enyo (enzymes) na kuzuia midomo isipasuke. Pia pua na macho.
Ukosefu wake mwilini husababisha:
kupasuka midomo,
pua ugonjwa wa ngozi,
vidonda,
kubanduka ngozi.
c)-Niacini (Nicotinic Acid):
huzuia ugonjwa wa pellagra, unaambatana na ulegevu wa mwili, magonjwa ya ngozi, kuharisha.
d)-Folic Acid:
Huitajika katika kutengeneza damu, ukosefu husababisha upungufu wa damu.
e)-Vitamin. B 6 (Pyridoxine):
Husaidia katika uyeyushwaji wa Protini na mafuta.
Ukosefu husababisha upungufu wa damu.
f)-Vitamin.B12 (Cyanocbalamine)
Ni muhimu kwa utengenezaji wa chembechembe nyekundu ndani ya mifupa.
Ukosefu huleta upungufu wa damu.
VITAMINI C. (ASCORBIC ACID):
Hupatikana katika machungwa, malimao, zabibu, maembe, mboga za majani,ukwaju.
KAZI ZAKE;
Ni muhimu katika ukuaji wa watoto.
Kuponya vidonda na mivunjiko.
Kutengenezwa kwa kinga mwilini.
Kuimarisha ngozi na meno.
Ukosefu wake husababisha;
Kuchelewa vidonda kupona
Ugonjwa wa fizi.
Kutoka damu kwenye fizi.
CHANZO: MASOMO YA IDARA YA HUDUMA ZA AFYA, SOUTHERN TANZANIA UNION MISSION
18/11/2024
SIKU YA TANO: UPUNGUFU WA VIRUTUBISHO NA MADHARA YAKE 1
UPUNGUFU WA PROTINI NA MATOKEO YAKE:
Madhara makubwa hasa kwa watoto wadogo.
UGONJWA WA UNYAFUZI (KWASHIORKOR)
Huathiri sana watoto wa umri wa mwaka 1-3 na hasa kipindi mtoto anapoachishwa kunyonya maziwa ya mama na kupewa vyakula vya wanga tu bila protini ya kutosha.
DALILI ZAKE KWA MTOTO;
(i) Kuvimba miguu,
(ii) ngozi kubanduka hasa miguuni,
(iii) kuvimba tumbo,
(iv) Mikono sehemu ya juu hukonda kuliko sehemu ya chini.
(v) Uso huvimba na kuwa wa mviringo, uso wa mwezi mpevu.
(vi) Huonekana amezubaa; hana furaha.
(vii) Nywele huwa nyembamba zilizonyooka nyepesi kunyofoka.
(viii) Anaweza kuharisha.
(ix) Upungufu wa damu.
TIBA YA UPUNGUFU:
(i) Mpe chakula kingi cha Protini (utomwili),
(ii) Ukifuata maelekezo ya daktari.
KINGA:
(i) Mpe mwanao lishe kamili yenye protini ya kutosha.
B: WANGA:
Hivi ni vyakula vya kutia nguvu na joto mwilini - (Carboydrates – wanga): Ni chakula kipatikanacho kwenye nafaka.
UPATIKANAJI WAKE:
Chakula cha nafaka K**a vile;-
Mahindi,
mtama,
ulezi,
mawele,
mchele,
ngano,
Shayiri,
viazi,
mihogo,
magimbi,
ndizi,
sukari,
asali.
KAZI ZAKE
Kuleta nguvu na joto mwilini.
Gari linahitaji dizeli au Petrol ili likimbie. Mtu anahitaji chakula cha wanga ili awe na nguvu za kufanya kazi. Watoto huhitaji chakula hiki kwa wingi kwa vile hutumia muda mwingi katika michezo pia katika makuzi yao. Wanga ukiliwa wa kutosha husaidia chakula cha Protini kisibadilishwe kufanya kazi ya wanga. Chakula cha wanga kikiliwa kingi hutunzwa mwilini kwa mfumo wa mafuta kwa matumizi ya baadae.
WAHITAJI WAKUU.
Watoto huhitaji wanga kwa wingi ili waweze kukua.
Wajawazito huhitaji kwa ajili ya ukuaji wa mtoto tumboni
Mama wakati wa kunyonyesha na wao pia wanahitaji sana.
Wagonjwa k.m wenye majeraha, waliongua na hata magonjwa mengine.
Wazee.
UPUNGUFU WA WANGA NA MATOKEO YAKE:
Madhara makubwa hasa kwa watoto wadogo
UGONJWA WA (MARASMUS-UPOJAZO)
Huathiri sana watoto wa umri wa mwaka 1 na hasa mtoto anapofiwa na wazazi.
Wakati wa njaa,
Na kwenye maeneo ya vita n.k.
DALILI ZAKE KWA MTOTO;
(i) Kukonda sana,
(ii) Ana njaa sana,
(iii) Amechangamkia sana chakula,
(iv) Kusinyaa ngozi na tumbo
(v) Upungufu wa damu.
(vi) Dalili kadhaa za Kwashiokor ikiwa ana upungufu wa protini pia.
TIBA YA UPUNGUFU:
Mpe chakula kingi cha wanga, Ukifuata maelekezo ya daktari.
KINGA:
Mpe mwanao lishe kamili yenye mchanganyiko wa vyakula vyote na vya kutosha.
C: MAFUTA.
(Chakula cha kutia joto na kutia nguvu mwilini)
AINA ZA MAFUTA:-
(i)Mafuta ya mbegu (k**a vile karanga, ufuta, alizeti, pamba, mahindi, n.k.), Mafuta ya n**i, Mafuta ya mawese. Hayana cholesterol (Lehemu) mbaya inayoweza kuziba mifumo ya damu.
(ii)Mafuta ya wanyama.
Yana kiwango kikubwa cha utoaji joto mwilini, mafuta hayana mipaka katika kutunzwa mwilini hujilundika na kuleta shida kubwa mwilini. Mafuta hasa ya wanyama yana Cholestrol {Lehemu} nyingi ambayo huleta matatizo ya magonjwa ya mishipa ya damu na moyo.
D: MADINI.
(Madini katika vyakula husawazisha mifumo mbalimbali ya mwili kufanya kazi vizuri, pia husaidia utengenezaji wa damu pamoja na utendaji katika figo).
Kuna aina nyingi ya madini yapatikanayo ardhini, Mwili hupata madini hayo kupitia mimea na maji ya kunywa.
AINA ZA MADINI;-
Calcium – Chokaa
Iron – Chuma
Iodine – Madini joto
Sodium - Chumvi
Potassium – Chumvi
Fluorine
KAZI YA MADINI MWILINI.
CALCIUM – CHOKAA:
(i)Hukomaza mifupa na meno.
(ii)Husaidia kuganda kwa damu.
(iii)Husaidia misuli isijifinye.
Hupatikana toka kwenye vyakula k**a maziwa, samaki wakavu k**a dagaa, nafaka, mayai, mboga za rangi ya kijani.
Madini haya huhitajika sana katika:-
ukuaji,
wakati wa ujauzito
na wakati wa kunyonyesha.
IRON – CHUMA:
(i)Huhitajika kwa ajili ya kutengeneza damu.
(ii)Hupatikana katika;-
Mboga za majani ya kijani
Nyama:- maini, nyama nyekundu
Mayai
Madini haya yanahitajika sana katika nchi yetu kwa vile kuna magonjwa mengine yaletayo upungufu wa damu k**a malaria na minyoo hasa kwa watoto.
IODINE- (MADINI JOTO):
(i)Huitajika kwa ajili ya ukuaji mzuri wa tezi ya shingo thyroid. Ikikosekana mtu hupata ugonjwa wa Goita (Kuvimba tezi shingoni)
Hupatikana wapi? : -
Katika chumvi
Mboga za majani zilizoota katika mchanga wenye madini hayo.
Vyakula toka baharini k**a samaki.
SODIUM-CHUMVI:
Huitajika katika chembechembe za uhai za mwili. Pia katika maji ya mwili.
POTTASIUM-CHUMVI:
Huitajika kwa kuweka uwiano wa chumvichumvi mwilini, kujifinya kwa misuli na kazi zingine ndani ya chembechembe za mwili.
Hupatikana kwenye: -
Maji ya n**i,
ndizi,
maziwa,
mayai,
Samaki
Na nyanya.
FLUORINE:
Kazi yake ni kuzuia meno kwa watoto yasitoboke.
CHANZO: MASOMO YA IDARA YA HUDUMA ZA AFYA, SOUTHERN TANZANIA UNION MISSION
18/11/2024
SIKU YA NNE: VIRUTUBISHO VYA MWILI NI VIPI?
Virutubisho vya mwili. Hebu tuchunguze kundi mojamoja la vyakula tulavyo;
PROTINI:
(Chakula cha kujenga mwili) au utomwili hufanya kazi mbili mwilini:-
Kujenga mwili pale palipobomoka, na kufanya mwili ukue na pia kuleta nguvu mwilini.
Mwanadamu huhitaji chakula hiki ili aweze kukua akiwa mtoto baada ya kuzaliwa huhitaji kula ili akue vivyo hivyo anapokuwa mtu mzima basi huacha kurefuka isipokuwa anaendelea kunenepa; kwa hiyo kwa kipindi hiki hakihitaji chakula hiki ili akue bali anahitaji chakuka hiki kwa kujenga palipobomoka, kwa mfano mtu akijikata sehemu yoyote ya mwili, hupona na kuunga vizuri, hivyo ni kazi ya Protini.
Mwili una chembechembe za uhai ambazo huishi kwa muda maalum ndani ya mwili halafu hufa ili zitengenezwe zingine chakula cha Protini huhitajika ili kuujenga mwili.Mfano; Chembechembe nyekundu za damu zina uwezo wa kuishi siku 120; na huhitaji kutengenezwa zingine. Waweza kushangaa mtu akivaa viatu sole ya kiatu huisha lakini mtu akitembea bila viatu unyayo hauishi, hii ni sababu ya chakula cha Protini.
Protini huleta nguvu mwilini pia ; Mwili unapopungukiwa na chakula cha wanga na mafuta ambavyo ndivyo muhimu kwa kuleta nguvu na joto Protin hubadilishwa na kufanya kazi hiyo.
AINA ZA PROTINI
Zipo aina mbili za protini:
(i) Protein inayopatikana katika mimea.
(ii) Protein inayopatikana kwa wanyama.
PROTINI YA MIMEA:
Ndio protini bora zaidi na isiyo na madhara yoyote kwa mtumiaji. Hupatikana kirahisi katika; Karanga,
Dengu,
Maharage,
Njegere,
Choroko,
Mbaazi,
Soya,
Kunde,
Njugu mawe
Mwanzo 1:29 “Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu..”
PROTINI YA WANYAMA:
Hupatikana katika;
Samaki,
Maziwa,
Mayai,
Na hata wadudu.
Kwa ujumla vyakula vya protini vina vitamin A, B, D & K.
WAHITAJI WAKUU:
Watoto huhitaji Protini nyingi ili waweze kukua.
Wajawazito huhitaji kwa ajili ya ukuaji wa mtoto tumboni
Mama wakati wa kunyonyesha na wao pia wanahitaji sana.
Wagonjwa k.m wenye majeraha, waliongua na hata magonjwa mengine.
Wazee
CHANZO: MASOMO YA IDARA YA HUDUMA ZA AFYA, SOUTHERN TANZANIA UNION MISSION
PESA PESA PESA
08/11/2024
SIKU YA TATU:
KANUNI ZA ULAJI BORA NA UNYWAJI BORA
1. KANUNI ZA ULAJI BORA NA UNYWAJI BORA.
Ubora na ukuaji wa miili yetu na akili zetu hutegemea aina ya vyakula Tunvyokula na vinywaji tunavyokunywa, pia hutegemea NAMNA tunavyovitumia.
Chakula tuchaguacho kula husaidia kuifanya miili Chakula tuchaguacho kula husaidia kuifanya miili yetu kuwa na Afya njema yetu kuwa na Afya njema au au kusababisha kusababisha udumavu udumavu, ,ulemavu ulemavu au au vifo visivyo vya lazima vifo visivyo vya lazima.
AINA ZA VYAKULA:
Aina tano za vyakula ni muhimu kwa maisha yetu ya kila siku.
Vyakula vya wanga: Hivi ni vyakula vinavyotia nguvu mwilini. Mifano yake ni vyakula vyote vya nafaka, ndizi za kupika, viazi n.k
Vyakula vya Protini: Vyakula hivi ni vile vinavyojenga mwili k**a vile mbegu, mboga mboga, nyama, mayai, maziwa n.k
Vyakula vya vitamin: Hivi ni vyakula vinavyolinda mwili, k**a vile matunda ya aina mbalimbali na mboga za aina mbalimbali.
Vyakula vya mafuta: Hivi hutia joto mwilini na kutia nguvu mwilini.
Vyakula vyenye Madini ya aina mbalimbali: Haya yanasaidia kendesha mifumo ya mwili na ogani mbalimbali mwilini na kuleta utendaji mzuri wa mwili
LISHE BORA:
Watu hula chakula au kunywa wanaposikia njaa au kiu, na hapo ndipo mwili unapohitaji maji au chakula, au hula kwa kukidhi haja ya uchu walio nao, au mtindo wa maisha.
Ulaji wa chakula kwaweza kusababisha mtu kuwa na afya njema au magonjwa kwa , kutojali au kula chakula kisichofaa mwili.
Lishe bora huzinatia ulaji na unyaji unaozingatia mahusiano ya vyakula mwilini.
LISHE NI NINI?
Ni elimu au sayansi ya jinsi mwili unavyoweza kukitumia chakula katika njia mbalimbali.
Kwa kuupatia mwili nguvu.
Kuujenga mwili.
Kuukinga mwili dhidi ya magonjwa.
Na kuupa mwili afya.
Kwa ujumla vyakula vimegawanyika katika makundi makuu sita.
Chakula cha kujenga mwili (Protein)
Chakula cha wanga (Carbohydrates)
Mafuta (Fats)
Madini (Minerals)
Vitamini (Vitamin)
Maji (Water)
CHANZO: MASOMO YA IDARA YA HUDUMA ZA AFYA, SOUTHERN TANZANIA UNION MISSION
08/11/2024
SIKU YA PILI:
SABABU ZA UKIUKWAJI WA KANUNI ZA AFYA
JE, ZIPO SABABU ZA UKIUKAJI WA KANUNI?
Kuna sababu nyingi kwa watu kuendelea kukiuka kanuni za Afya zifuatazo ni muhimu zaidi.
Ujinga – Kutokufahamu, kutokuelimika (mfano, kutokunawa mikono inavyostahili kunaongeza uwezekano wa kupata kipindupindu.
Uzembe, kutokuwa makini, kupuuzia (mfano kuendesha gari umelewa n.k.)
Kutokuwa na kiasi. (Mienendo isiyofaa, k**a vile-uzinzi, na ulevi – unaweza kusababisha magonjwa k**a vile VVU/UKIMWI na kansa za aina mbalimbali).
Uwezo duni, kifedha, mali, hata kielimu. Mfano, nyumba bora zina gharama kubwa, kujenga matibabu bora ni ghali n.k).
Udhaifu wa kurithi. (kuzaliwa kilema, kuambukizwa na wazazi tumboni n.k)
MATOKEO GANI YA KUTOJALI KANUNI ZA AFYA?
Endapo mtu atakiuka kanuni hizi kwa kutokujua, makusudi au uzembe yafuatayo yaambatana naye;
Ulemavu wa muda mfupi – mrefu,
Udhaifu (kimwili, kiroho)
Maambukizi – Magonjwa.
Vifo kimwili, kiroho.
Shida katika jamii (umaskini, mahangaiko).
Uduni kifamilia, kijamii na hata kitaifa
DAWA GANI YA KUJIEPUSHA NA MATATIZO HAYA?
Kuzifahamu na kuzizingatia Kanuni bora za Afya.
KANUNI BORA ZA AFYA NI ZIPI?
Zipo kanuni nyingi sana za Afya ambazo zinahitaji kuzingatiwa nazo zimegawanywa kwa makundi makubwa manane.
Kanuni za Ulaji bora na unywaji bora.
Kanuni za Matumizi bora ya maji ndani na nje ya mwili.
Kanuni za Mazoezi ya mwili.
Kanuni za utumiaji wa Hewa Safi.
Kanuni za utumiaji wa Mwanga wa jua.
Kanuni za Mapumziko.
Kanuni ya kuwa na kiasi katika tabia tabia.
Kanuni ya ufahamu na Imani kwa Mungu wa Kweli, aliye hai na Mtoa kanuni.
Mungu ameweka kanuni mbali mbali ili ziweze kutawala mienendo ya binadamu, ili kuwaepusha na madhara makubwa yatokanayo na ukiukaji wa kanuni hizi
CHANZO: MASOMO YA IDARA YA HUDUMA ZA AFYA, SOUTHERN TANZANIA UNION MISSION
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Telephone
Website
Address
Tegeta Dar Es Salaam
Dar Es Salaam