Afya_talktz1
Afya kwa wanaume UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI NINI?
Hii ni hali ya kupatikana dalili za udhaifu katika tendo ndoa ambapo mtu hushindwa kufanya mapenzi kikamilifu au kushindwa kusimamisha uume vizuri. Kwakuwa tendo la ndoa huhusisha hisia (emotions) na mwili, kupatikana athari kati ya vitu viwili hivi ndizo sababu kuu zinazopelekea tatizo la nguvu za kiume. Tatizo hili ni kubwa, ambapo watafiti wanaripoti ya kwamba wanaume wengi wenye umri kati ya
21/07/2022
UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI NINI?
Hii ni hali ya kupatikana dalili za udhaifu katika tendo ndoa ambapo mtu hushindwa kufanya mapenzi kikamilifu au kushindwa kusimamisha uume vizuri.
Kwakuwa tendo la ndoa huhusisha hisia (emotions) na mwili, kupatikana athari kati ya vitu viwili hivi ndizo sababu kuu zinazopelekea tatizo la nguvu za kiume.
Tatizo hili ni kubwa, ambapo watafiti wanaripoti ya kwamba wanaume wengi wenye umri kati ya miaka 35 na kuendelea ndio wanaosumbuliwa kwa kiasi kikubwa,
ambapo asilimia ishirini (20%) ya wanaume wanakabiliwa na tatizo hili.
Tatizo hili lina athari nyingi sana zikiwemo za kisaikolojia na kifamilia pia, ikiwemo kupelekea mahusiano kutokuwa imara na mara nyengine kuvunjika kabisa.
Hata hivyo tatizo hili linatibika na kupona kabisa k**a mtu alieathrika na tatizo hili atakuwa tayari kufuata maelekezo vizuri yatakayo elezwa kwa upana hapo chini ikiwemo kuzifahamu sababu na taratibu za kulitibu tatizo hili.
Kwa maelezo Zaidi wasiliana nasi call/WhatsApp 0716986163
20/07/2022
Tunafahamu kwamba unene huambatana na magonjwa mbalimbali k**a shinikizo la damu, kisukari, magonjwa ya moyo na kushindwa kupata usingizi wakati wa usiku lakini tatizo lingine la unene ni kupungua nguvu za kiume, kitu ambacho mara nyingi watu hawa wanene au wenye vitambi hawako wazi kukizungumzia.
Tafiti zinasema!
Shirika la kimarekani maarafu k**a AUA au American urology association wanasema kwamba asilimia 53% ya wanaume wenye umri kati ya miaka 40 mpaka 70 wana tatizo la nguvu za kiume ambalo husababishwa na umri, magonjwa ya moyo, shinikizo la damu, unene na kutofanya mazoezi, uvutaji wa sigara na kiwango kidogo cha homoni za kiume yaani testosterone.
Hebu tuone uume unavyosimama.
Uume husimama pale damu inapoingia kwenye mishipa ya damu ya uume na kufanya uume ujae damu, mishipa ya damu hutoa kitu kinaitwa nitric oxide ambayo hufanya uume ubaki kwenye hali ile mpaka mwanaume atakapofika mshindo.(dawa nyingi za kuongeza nguvu za kiume huwekewa kemikali hii). Kitu chochote ambacho kinaweza kuharibu sehemu ya ndani ya mishipa ya damu ya uume husabisha uume kuishiwa nguvu.
Unene huathiri vipi nguvu za kiume?
Mtu akiwa mnene mishipa ya damu pia inakua na mafuta kwa ndani ambayo yanakua yameganda kwenye kuta za mishipa ya damu kitaalamu k**a atherosclerosis, hali hii hufanya damu kupita kwa shida kwenda kwenye uume na lakini pia mfumo wa kutengeneza nitric oxide ambayo kazi yake ni kurelax misuli ya uume ili uweze kusimama unaingiliwa.
Sababu nyingine ni ongezeko la mafuta yaliyopo tumboni au kitambi ambayo hubadilisha homoni ya testosterone kua oestrogen..homoni ya testosterone ndio homoni kuu ya kiume ambayo huleta mabadiko ya yote ya kiume wakati wa kubalehe na huhusika sana na ukubwa na nguvu za kiume na kupungua kwa homoni hii humaliza au kupunguza sana nguvu za kiume.
Mwisho; habari njema ni kwamba wanaume wengi wanene huweza kurudi kwenye hali zao za zamani kwa kupungua uzito tu japokua k**a ukipungua bado shida haijaisha basi kuna uwezekano mkubwa homoni zako za testosterone zilipungua na utahitaji dawa za kumeza kuzisahihisha, kumbuka kwamba kupungua uzito sio rahisi lakini ni muhimu sana.
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi call/WhatsApp 0716986163
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Address
Dar Es Salaam