Muhimu Afya

Muhimu Afya

Share

Muhimu Afya_Jifunze mambo muhimu kuhusu afya yako pamoja na Tiba kwa kutumia virutubisho. karibu sana

04/10/2023

Juice nzuri ya kuongeza nguvu za kiume

Maandalizi

Ndizi 2
Tikiti Maji Nusu
Tangawizi Gram 10
Limao 5

Osha kwa maji safi na salama kisha menya maganda ya Juu ya ndizi na Tangawizi halafu chukua blender visage kwa Pam kupata mchanyanyiko laini kabisa

Kunywa kwa siku 15...

03/10/2023

NI NANI ANAWEZA KUWA NA UGONJWA WA KISUKARI?

Watu walio katika makundi yafuatayo wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa kisukari:-

– Wenye uzito uliozidi,

– Wenye historia ya kuwa na wagonjwa wa kisukari katika familia zao,

– Wanawake waliozaa watoto wenye kilo 4 au zaidi,

– Watu wasiojishughirisha au wasiofanya mazoezi,

– Wenye shinikizo la damu,

– Wenye msongo wa mawazo na

– Wenye matumizi makubwa ya pombe na sigara.

Watu hawa wanashauriwa kupima sukari yao kila mwaka wakiwa na umri wa miaka 45 na kuendelea.

Kuna hatari kubwa ya kuugua ugonjwa huo ikiwa mtu ana mafuta mengi katika tumbo na kiuno chake kuliko katika mapaja yake. Mafuta katika kongosho na ini huvuruga uwezo wa mwili wa kudhibiti kiasi cha sukari kwenye damu.

Wavutaji wa sigara wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi kwani zoea hilo hudhuru moyo na mfumo wa mzunguko wa damu na kubana mishipa ya damu. Kitabu kimoja kinasema kwamba asilimia 95 ya watu wanaougua kisukari ambao hulazimika kukatwa viungo ni wavutaji wa sigara.

📞 ☎️ 0628064712 Kwa elimu zaidi juu ya Kisukari.

03/10/2023

LENGO NI UJIFUNZE

AFYA YAKO YA AKILI INABEBA DHAMANA KUBWA KATIKA AFYA YAKO YA UZAZI.

》Ili uwe na afya njema ya akili na uzazi ni muhimu kujali na kuzingatia mitindo bora ya maisha.

1. Kula vyakula vyenye afya, Epuka vyakula vyenye sukari nyingi, mafuta na chumvi,

2. Kula matunda, mboga mboga na vyakula vyenye protini k**a mayai, Maini Nk.

3. Fanya mazoezi ya mwili mara kwa mara, Itakujenga kiakili na kimwili, Angalau dakika 30 kwa mazoezi ni muhimu.

4. Epuka uvutaji wa sigara, Unywaji wa pombe kupita kiasi, na matuizi ya madawa pasipo matibabu sahihi.

5. Hakikisha unafanya uchunguzi wa afya yako mara kwa mara, hasa endapo utaona dalili za awali pale mwilini ambapo haupo sawa.

6. Kuhakikisha unapata usingizi wakutosha walau masaa 7-8 wakati wausiku itasaidia ku rekebisha afya ya mwili na akili,

7. Jifunze jinsi ya kudhibiti mawazo, Fanya self meditation 🧘‍♀️ , Itakusaida afya yako ya Akili.

8. Kudhibiti uzito wako nimuhimu sana kwa afya bora, Punguza uzito wako kupitia lishe na mazoezi, nimuhimu kwa afya bora.

NB: Maswala ya afya ya akili, uzazi na Kuepuka na magonjwa yasiyo ambuzwa, husababishwa na mitindo mibovu ya maisha. AMUA SASA ⚖
-OG

Photos from Muhimu Afya's post 02/10/2023

MUHIMU SANA HII ITAKUSAIDIA

Je, unajua kwamba wakati wa Kusafisha Damu (dialisisi), damu Hutolewa mwilini kupitia bomba jekundu, hupita kwenye mashine ya dialisisi, na kisha kurudishwa tena kwenye mfumo wa mwili kupitia bomba la bluu?.

Mchakato huu hurudiwa kwa saa nne huku mgonjwa akibaki kitandani kwa muda wote.

Mchakato huu hufanyika mara tatu kwa wiki, ambayo inafanya jumla ya mara kumi na mbili kwa mwezi, na kila wakati huchukua masaa manne, ambayo inafanya jumla ya masaa arobaini na nane kwa mwezi.

Kwa wale wasioathiriwa, mchakato huu wa kusafisha damuhufanyika moja kwa moja kweye figo mara thelathini na sita kila siku bila jitihada yoyote au usumbufu.

Wakati unasoma post hii,
1.Acha pombe,
2.Acha vyakula vilivyosindikwa (kwenye makopo),
3.Acha chipsi mayai,
4.Acha matumizi yasiyo ya lazima ya sukari, na muhimu zaidi,
5.Fanya mazoezi.
Mambo haya yote ni chaguo rahisi na ya bei nafuu kudumisha afya bora ya figo na ini.

DAIMA KUWA NA SHUKRANI KWA AFYA NJEMA.

16/10/2022

UPIMAJI WA MAGONJWA YA TEZI DUME (PBH, Prostatitis na Prostate Ca).
UCHUNGUZI, VIPIMO NA TIBA

🎲 Uchungizi: Hapa tunatoa wito kwa wanaume wenye umri wa takribani 50 na kuendelea kuweka kipaumbele tabia ya kufanyiwa uchunguzi wa tezi dume angalau mara moja kwa mwaka.

🎲 Vipimo: Kuna vipimo vya uchunguzi wa tezi dume k**a vipimo ashiria kitaalamu Prostate Specific Antigen (PSA) na

🎲 Digital Re**al Examination (DRE). Ongea na daktari wako.

💉💊Tiba: Zipo tiba. Kuna tiba ya uangalizi (active surveillence ), Upasuaji (surgery), homoni (hormonetherapy), mionzi (radiotherapy), dripu kemikali (chemotherapy) nk. Ukigunduliwa una saratani ya tezi dume, shauriana na madaktari wako kuamua aina ya tiba itakayokufaa.

💥WITO KWA WANAUME WOTE:
Kwa wanaume wote wenye umri takribani miaka 50 na kuendelea, tafadhali waoneni madaktari wenu kwa uchunguzi wa afya ukijumuisha uchunguzi wa tezi dume;

💥WITO KWA MADAKTARI WOTE;
Kwa madaktari wote, mnapopata wagonjwa wanaume wenye umri wa takribani miaka 50 na kuendelea washaurini pamoja na matibabu mengine, wafanyiwe uchunguzi wa tezi dume.

⛑️⛑️TAFADHALI TAMBUA:⛑️⛑️
Saratani ikigundulika mapema ni rahisi kutibika.

💊💉WAHI MATIBABU MAPEMA.
WASILIANA NASI KWA USHAURI NA MATIBABU.

☎️☎️TUPIGIE SIMU NAMBA
0628064712

16/10/2022

DALILI ZA SARATANI YA TEZI DUME (PROSTATE CA)..

🩸Dalili za saratani ya tezi dume:

Swali linakuja: Jee mwanamume ataziona dalili zipi zinazoashiria saratani ya tezi dume❓️
💫Jibu: Zipo dalili nyingi na hapa nazitaja baadhi tu.

1️⃣Udhaifu katika kujisaidia haja ndogo na unapotoka unakatizakatiza;
2️⃣Kushindwa kukojoa na kushindwa kuanza pata haja ndogo;
3️⃣Unapohisi haja ndogo unapata shida kujizuia isijitokee yenyewe;
4️⃣Hisia ya kutaka kupata haja ndogo kila wakati hasa nyakati za usiku; hata kukojoa kitandani;
5️⃣Mkojo kujitokea wenyewe;
6️⃣Maumivu au kuhisi mwasho wakati wa haja ndogo;
7️⃣Mbabaa / uume kusimama kwa shida;
8️⃣Maumivu wakati unapotoa manii / shahawa wakati wa kujamiana;
9️⃣Damu damu katika mkojo na katika manii;
1️⃣0️⃣Maumivu viungoni – kiunoni, miguu, mgongo nk.
1️⃣1️⃣Kukosa hamu ya kula na kupungua uzito / kukonda.

⛑️ANGALIZO: Pamoja na kuorodhesha dalili hizo napenda msomaji ujue kwamba mwanaume anapoanza kuziona na kuzihisi kati ya dalili hizo, basi ajue chembe chembe za uhai asi katika tezi dume lake zina umri wa takribani miaka saba na kuendelea.

💉💊KWA USHAURI NA MATIBABU 💊💉

☎️☎️WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA O628064712☎️☎️

13/10/2022

*HOMONAL IMBALANCE (KUVURUGIKA KWA HOMONI)*

:Hili ni tatizo linalowakumba wakina mama(wanawake) wengi ambalo husababishwa na kiwango kidogo cha hormone ya ESTROGEN.

*VYANZO VYA KUVURUGIKA KWA HORMONE*
👉Utoaji wa mimba
👉Uwepo wa sumu mwilini.
👉kutokula mlo uliokamili au mfumo mbovu wa maisha.
👉Family history(upungufu wa ongezeko ya homoni ya progesterone
👉mabadiliko ya mazingira au hali ya hewa.
👉uzito mkubwa
👉Msongo wa mawazo.
👉Kutofanya mazoezi.
👉Matumizi ya kisasa ya uzazi wa mpango.
👉Kukoma kwa hedhi.

*Dalili za kuvurugika kwa homoni*
👉Maumivu wakati wa tendo LA ndoa.
👉Kutoshika mimba.
👉Mzunguko wa hedhi kubadilika.
👉Kuongezeka uzito.
👉Kupungua hamu ya tendo LA ndoa.
👉Kupoteza kumbukumbu.
👉Hasira za Mara kwa Mara.
👉Damu kutoka nyingi wakati wa hedhi au kutoa damu yenye mabongemabonge
👉Uke kuwa mkavu.
👉kutoka jasho jingi usiku.
👉maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
👉mzio wa vyakula/Allerg kuchaguachagua vyakula.

*Madhara ya kuvurugika kwa homoni*
👉kutoshika ujauzito kwa mda mrefu.
👉Mimba kuharibika Mara kwa Mara.
👉Kuwa mgumba.
👉U.t.I Mara kwa Mara.
👉Uvimbe kwenye via vya uzazi wa mwanamke.(fibroids)
👉kuziba kwa mirija ya uzazi.
👉saratani.
☎️Wasiliana nasi kwa namba 0638064712
.Moses #0765562723

01/10/2022

⛑YAJUWE MADHARA ANAYOWEZA KUYAPATA MGONJWA WA KISUKARI.

KISUKARI ni ugonjwa unaoua kimya kimya, pia ni ugonjwa unaotesa wanadamu taratibu!

Mateso ya kisukari yaweza kuwa haya:

🔖Kuwa kipofu
🔖Kukatwa viungo k**a miguu au mikono
🔖Kuugua figo
🔖Kuugua magonjwa ya moyo
🔖Kuugua Ini
🔖Kuugua mishipa ya fahamu
🔖Viungo vya mwili kukak**aa na kufa ganzi
🔖Kupoteza kumbukumbu
🔖Kuchakaa ngozi ya mwili
🔖Kuwa dhaifu kimwili Kumeza vidonge vya
kushusha sukari kila siku
🔖Kujidunga sindano kila siku

💉Dawa na sindano hazitibu sukari bali zinashusha sukari lakini ugonjwa wa sukari upo pale pale!

🪁Ugonjwa wa sukari unachochewa sana na vyakula tunavyokula kisha mfumo wa maisha ya mtu binafsi.

🧩Vyakula vya wanga, mafuta na suakari vinaongeza uzito na mafuta mwilini kiasi kwamba wengine tunakuwa na vitambi visivyo vya kawaida!

Tukisha kula vyakula vya wanga, mafuta na sukari hatufanyi mazoezi na inakuwa tabu kwa watu wanaozoea kazi za ofisini au za dukani, anatoka nyumbani na gari kisha anaingia kazini na akitoka kazini anaingia kwenye gari na kwenda nyumbani kwenye sofa au kitanda.

Afya yako ni muhimu kuliko unavyodhania, ukiisha ugua sukari ndo utajua umuhimu wa kuangalia vyakula tulavyo na kufanya mazoezi, ila kuwahi kabla hujaugua ni vyema.

🧩WASILIANA NASI KWA NAMBA 0628064712, KWA USHAURI NA MATIBABU.

01/10/2022

UNASUMBULIWA NA MAUMIVU YA GOTI?

🧩Sababu tofauti tofauti ambazo zimekuwa chanzo cha maumivu ya magoti na mifupa mingine mwilini hasa katika joints (Maungio).
🧩Ukifanikiwa kuondoa chanzo cha maumivu ndipo utakuwa tayari umeondoa maumivu moja kwa moja na kupona changamoto hiyo.
🧩Mara nyingi tumekuwa tukihisi maumivu basi haraka tunatafuta dawa za kutuliza maumivu kwa muda na tunasahau kuwa kuna chanzo chake... na maumivu ni ishara ambayo mwili unakufahamisha sehemu fulani katika mwili wako kuna tatizo.

💊💊Matumizi ya dawa za maumivu kwa muda mrefu huadhiri mwili na viungo muhimu k**a vile FIGO, INI, MOYO ..... N.K

☘️☘️🌿🌱 ZIPO TIBA ASILIA KWA 100% ZINATATUA CHANGAMOTO NYINGI ZA MIFUPA PASIPO KUKUACHIA MADHARA YOYOTE YALE.

⬇️

☎️☎️ KWA USHAURI NA MATIBABU WA TATIZO LOLOTE LILE LA MIFUPA NA VIUNGO WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA
0628064712

01/10/2022

FAHAMU KUHUSU MAUMIVU YA MGONGO NA TIBA YAKE.

Kitaalamu ni kwamba katika MAUNGIO huwa kuna ute ute uitwao (synonvio fluid) ambao kazi YAKE ni kulainisha MAUNGIO.
Pia kuna kitu k**a sponji au plastiki ya asili iitwayo cartilage au (gegedu) ambayo Kazi YAKE ni kuzuia mfupa na mfupa visisagane.
Hivyo plastiki au sponji (cartilage), hii kwa kushirikiana na ute-ute juu yake, ndio vinavyofanya MAUNGIO yawe salaam salimini, kiasi kwamba unaweza ukakunja mguu, ukainama na kufanya shughuli yoyote bila shida wala maumivu.

Kuanzia umri wa miaka 30 na kuendelea, virutubisho asilia vinavyosaidia kutengeneza ute ute (synovial fluid) vinapungua na hatimaye kuisha kabisa kadri umri unavyoongezeka.
Hivyo ute-ute unapoisha katikati ya viungo na hatimaye gegedu(cartilage) kuanza kulika pole pole na kusababisha mifupa ya kwenye MAUNGIO kusagana.
Hiii kitaalamu huitwa OSTEOARTHRITIS na husababisha maumivu makali kwenye maungio (joints) k**a vile, magoti, nyonga na mgongo.

CHANZO_CHA_TATIZO
•Umri
•Uzito
•Kuumia Kwa Kupata ajali
•Kurithi (genesis)

Endapo usipotibu tatizo hili kuna uwezekano mkubwa wa kufanyiwa upasuaji na kuwekewa cartilage za bandia ambapo kimsingi ni gharama kubwa sana na k**a ni mgongo unaweza usitembee kabisa.

DALILI ZA VIUNGO KUSAGANA
✓maumivu kwenye magoti, nyonga na mgongo.
✓Kushindwa kukunja goti au kuinama.
✓Kushindwa kupanda ngazi kwa urahisi
✓Kusikia milio ya mifupa KUSAGANA kwenye maungio k**a magoti.
✓Kusikia maumivu makali wakati wa kuinama.
✓Kusikia ganzi kwenye mapaja au miguu.

MATIBABU
Kwa hospitalini utapewa dawa au kufanyiwa mazoezi (physiotherapy) ambapo hupunguza au kutuliza maumivu kwa muda tu na baadae maumivu hubakia pale pale kwa sababu hazisaidii kuongeza ute ute wala gegedu.
Badala yake huishia kufanyiwa upasuaji kwa gharama kubwa.

LAKINI:
Habari njema ni Kwamba, sisi tunazo dawa (NI VIRUTUBISHO) asili kabisa zinazoongeza ute ute kwenye maungia na kuziponya cartilage au sponji zinazozuia mifupa kusagana na huondoa maumivu kwenye maungio kabisa.
-Dawa hiii imetengenezwa kwa glucosamine na chondroitin ambavyo ni virutubisho vinavyosaidia kurejesha ute-ute (synovial fluid) na gegedu (cartilage) iliyolika au kusagika.
☎️0628064712

07/06/2022

CD4 (ONGEZA KINGA YA MWILI) ILI USISHAMBULIWE NA MAGONJWA NYEMELEZI.
WASILIANA NASI KWA USHAURI NA MATIBABU. SIMU NAMBA 0628064712

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam