RanduNutritions
Wekeza Kwenye Ubora Wa Afya Yako maana Utajiri Wa Kwanza ni Afya Bora!
23/03/2024
❗Bado Bawasiri INAKUTESA?
❗Umekata vinyama vyake ila VIMERUDI KUOTA TENA?
❗HUNA AMANI NA KUKAA [KUKETI] maana kukaa kunakusababishia MAUMIVU makali?
❗Pengine unahofia kuvuja kwa majimaji kwake UKIKETI kutaivujisha kwa watu siri hii, uliyoitunza kwa uaminifu, kwa siku nyingi?
❗Pengine sasa maumivu, miwasho, kuungua moto, kutoatoa maji, kuvuja damu ukienda kujisaidia + adha zake zingine HAVIPO ila KERO YA KUKIKALIA hicho kinyama UNAPOKETI, ndiyo inayokutesa?
Hii ni HABARI NJEMA kwako:👇🏼
"Unaweza KUTOKA tena SALAMA tu, katika yote hayo, tena BILA KUPITIA NJIA YA KISU [Operesheni] na yasirudi tena! Ndio tunaweza kukusaidia ktk hili, KARIBU!
Una ndugu/rafiki ULIYECHOKA KUMWONA AKILIA na mateso haya ya Bawasiri? Mfikishie naye pia habari hii njema!
+255 786 428 821
Kumbuka:
1. Maisha Bila Bawasiri, Yanawezekana!
2. Kukupatia amani & raha ni 1 ya kazi ya AfyaBora!
3. AfyaBora Ndio Utajiri Wetu wa Kwanza!
Moja ya ujumbe muhimu sana tulioaswa kuhusu afya zetu. Weka bajeti ya afya yako kwenye yale maeneo matatu[Unayakumbuka? kisha kwenye eneo hili pia la moyo wako [Akili, fikira & hisia zako]. Inalipa asee! Karibu k**a una swali
06/01/2024
*KUDHIBITI hayo pia kuna mchango kwenye KUKUEPUSHA na magonjwa mengine likiwemo hili la moyo kupanuka!Tambua pia hili 👇:
Mabadiliko ktk mtindo wako wa kuishi & aina+ubora wa vyakula na vinywaji vyako, ni 1 ya njia ya kudhibiti & kuyafukuza Magonjwa haya.
UNABADILISHAJE mtindo wako wa kuishi? Kuna namna nyingi ila Anza na hili:👇
2024+ Anza KUWEKEZA kwenye mazoezi, vyakula na vinywaji BORA!
_Kufanya haya ni kutendea kazi kwa FAIDA YETU, tulichoaswa na mdau muhimu sana kwenye sekta ya Afya kwenye nchi yetu. Unamjua? Na amesemaje? Hebu tazama video yake tuliyoambatanisha ktk chapisho linalofuata 👉👉👉
06/01/2024
*DHIBITI mambo hayo makubwa manne ili kujiweka mbali na shambulio hili!
19/07/2023
Umeamkaje mjali afya yako mwenzangu?
Hebu sasa tulijibu swali hilo kwenye picha hii:
Ni kwa sababu ya MADHARA YAKE kwako!
Wewe ambaye huyajui,
Hebu twende 👇🏼 tukayapitie MADHARA HAYO angalau kwa uchache ili upate sababu za msingi za KUCHUKUA TAHADHARI NA HATUA ZA KUISHUGHULIKIA MAPEMA, ili kujiepusha nayo!
Karibu tukayaone 👇🏼
⚠️ MADHARA YA BAWASIRI:
😣 Kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa na kusababisha mishipa ya sehemu ya haja kubwa kukwanguliwa.
😣 Kuna uwezekano mkubwa wa kupata saratani ya utumbo (Cancer) kwa sababu kile kinyama kinakaa k**a kidonda
😣 Kutopata hamu ya tendo la ndoa kwa jinsia zote.
😣 Upungufu wa nguvu za kiume kwa mwanamume , ikiwemo uume kushindwa kusimama kwa muda unaotakiwa hivyo kupelekea kupotea kwa heshima ya ndoa.
😣 Kuathirika kisaikolojia
😣 Kutojiamini/kutokuwa na amani katika hadhara ya watu kutokana na adha zake ikiwemo ile ya kuungua moto puruni & kujikuna sana kutokanako na kuwasha kwa ngozi ya eneo la tundu la haja kubwa (puru).
😣 Wako ambao hulazimika kuvaa pampasi kutokana na kutopona kwa kidonda ilipokatwa [kwa operesheni] Bawasiri hivyo mahali hapo kufanya jipu livujalo...!
Hiyo ndiyo Bawasiri!
🙇🏽♂️⁉️‼️⁉️🙇🏽♂️
Una swali au dukuduku lolote?
Karibu uulize!Ni furaha yetu kukusikiliza na kuyajibu maswali & madukuduku hayo.
K**a huna, basi tukutane sehemu inayofuata ya somo hili adhimu.
Share IF u care!
Tukutakie siku njema!
+255 786 428 821
🕯️wa AfyaBora
©️ RanduNutritions2023
Afya Bora Ndio Utajiri Wako wa Kwanza!
18/07/2023
Habari za asubuhi mwana🕯️wa AfyaBora mwenzangu?
Sasa tuendelee tulipoishia jana na somo letu la bawasiri:
"Je UTAJUAJE UNA BAWASIRI? DALILI GANI INAKUJA NAZO?"
Mshumaa wetu wa AfyaBora utazimulika hizi leo. Karibu tuzione:👇
➖ Kupata muwasho mkali katika eneo la juu la haja kubwa. Yaani Unajikuna hatari!
➖ Kusikia moto [unaungua] puruni/kwenye njia ya haja kubwa.
➖ Kujitokeza kwa kinyama eneo la haja kubwa.
➖ Kutokewa na kiuvimbe katika tundu ya haja kubwa [vinyama vinakua vimeungana]
➖ Kupata kinyesi chenye damu mbichi au wakati mwingine damu ikichuruzika yenyewe kabisa.
➖ Kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.
➖ kutokwa na uteute/usaha sehemu ya haja kubwa maana kuna wakati inafikia vinyama vya bawasiri vinashindwa kupona na kutengeneza majipu.
➖ Kuna uwezekano mkubwa wa kupata saratani ya utumbo (Cancer) hasa pale ile sehemu iliyochanika na kuvuja damu inashindwa kupona na kubaki kuwa kidonda sugu kwa muda mrefu tena kipatacho maambukizi mapya ya bakteria wengi [maana njia ya haja kubwa ina bakteria wengi]
➖ Uume kusinyaa na kuathirika kwenye tendo la ndoa maana kuna uhusiano mkubwa kati ya mishipa & misuli ya njia ya haja kubwa na ya uumeni. Kwa hiyo nguvu za kiume zinapungua.
Hizo ndio dalili kuu za Bawasiri. Sasa hebu twende tuone madhara ya bawasiri.
MADHARA YA BAWASIRI:
Sasa wacha tumulikie baadhi ya madhara ya kuwa na bawasiri. 👇
➖ Upungufu wa damu mwilini
➖Kutokwa na kinyesi bila kujitambua
➖ Kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa
➖ Kupungukiwa nguvu za kiume (kwa wanaume)
➖ Kupungukiwa na uwezo wa kufanya kazi kutokana na maumivu
➖ Kupata tatizo la kisaikolojia maana hukai kwa amani - unawashwa puruni na huwezi jikuna mbele ya watu. Pia hofu ya kukaa maana unahofia maumivu.
Hiyo ndiyo Bawasiri!
🙇🏽♂️⁉️‼️⁉️🙇🏽♂️
Una swali au dukuduku lolote?
Karibu uulize!Ni furaha yetu kukusikiliza na kuyajibu maswali & madukuduku hayo.
Share IF u care!
Tukutakie siku njema!
+255 786 428 821
🕯️wa AfyaBora
©️ RanduNutritions2023
Afya Bora Ndio Utajiri Wako wa Kwanza!
17/07/2023
Bawasiri Ni Nini?
Bawasiri ni ugonjwa unaotokea katika njia ya haja kubwa, hujitokeza k**a uvimbe au kijinyama ambacho huweza kuonekana hadi nje.
Kwa kiingereza hujuliakana k**a piles.
Na kitabibu hujulikana k**a hemorrhoids.
Tuone 👇🏼
AINA ZA BAWASIRI:
1⃣ BAWASIRI YA NJE:
Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa, na huambatana na maumivu, pamoja na kuwashwa kwa ngozi katika eneo hilo.
Mara nyingine mishipa hiyo ya damu (vena) hupasuka na damu huganda na kusababisha aina hii ya bawasiri kitaalamu inaitwa Thrombosed hemorrhoid.
2⃣BAWASIRI YA NDANI:
Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa. Na huwa haimbatani na maumivu.
Aina hii imeainishwa katika mainisho ya madaraja manne yafuatayo:
Daraja la 1 - Bawasiri kutotoka katika mahali pake pa kawaida
Daraja la 2 - Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe baada ya haja.
Daraja la 3 - Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kuirudisha mwenyewe baada ya haja.
Daraja la 4 - Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na vigumu mtu kuirudisha baada ya haja.
BAWASIRI HUSABABISHWA NA NINI?
Vipo visababishi mbalimbali vikuu vikiwemo vifuatavyo:
-Kufunga choo au kupata choo kigumu kwa muda mrefu
-Ujauzito – wakati wa ujauzito watu wengine wanaweza kupatwa na bawasiri sababu ya msukumo wa mtoto karibu na sehemu ya kutolea haja kubwa
-Kushiriki mapenzi kinyume na maumbile
-Uzee – kadri miaka inavyosogea ndivyo inavyokuwa rahisi kwako kupatwa na ugonjwa huu kwa baadhi ya watu
-Sababu za kurithi – baadhi ya watu wanaweza kurithi udhaifu wa ukuta huo wa njia haja kubwa ingawa ni asilimia ndogo sana.
-Kuharisha sana kwa muda mrefu
-Kutumia vyoo vya kukaa
-Kunyanyua vyuma vizito
-Mfadhaiko/stress
-Uzito na unene kupita kiasi.
Hivyo ni baadhi ya vyanzo vikuu.
Je utajuaje una bawasiri?
Dalili gani inakuja nazo?
Kesho tutaziona kwa kina hizo, usipange kukosa bando 😃 ili usikose sehemu hii inayofuata!!
Share IF u care!
Nikutakie jioni njema!
+255 786 428 821
🕯️wa AfyaBora
©️ RanduNutritions
Afya Bora Ndio Utajiri wa Kwanza
31/05/2023
Habari za asubuhi mwana🕯️wa AfyaBora mwenzangu?
LEO MEI 31,2023 NI SIKU YA KUADHIMISHA KUPINGA MATUMIZI TUMBAKU DUNIANI.
Hebu tuongee kidogo kuhusu TUMBAKU!
Unafahamu 1 ya dalili ya KUUCHUKIA mwili Wako ni KUULISHA vitu visivyo na thamani kilishe, TUMBAKU ikiwemo?
Na Unafahamu pia ktk ORODHA ya MAHITAJI muhimu & ya msingi kwa KUUTUNZA mwili Wako, TUMBAKU Haimo? Ndio haimo!
UNAUPENDA Mwili wako? Acha kuulisha TUMBAKU na Anza kuulisha Chakula maana TUMBAKU SIO CHAKULA!
Tambua pia hili: 👇
Mwili wako UNAHITAJI CHAKULA, sio TUMBAKU, hivyo Utunze kwa Chakula Bora, na sio kwa TUMBAKU bora!
Hamisha bajeti yako toka KUNUNULIA PAKTI za sigara,ugoro,vitu vya AR nk na kuanza kununulia vikapu vya MATUNDA!
By the way, inawezekana hupendi kuvuta na umejitahidi kwa kila njia kuacha ila ndo ivyo IMEKUSHINDA! k**a wewe ni mtu huyu, HII NI GUD NYUZ KWAKO! Tuna namna ya kukusaidia kutoka hapo. KARIBU!
Umeanza kuathirika na MADHARA YAKE [mf: kifua/Kikohozi kisichoisha,saratani ya mapafu,meno kuharibika, nguvu za kiume kufa, kunuka sigara mwili mzima/kutoa jasho la moshi wake, kuharibika kwa mbegu zako za kiume nk] na unataka KUYAONDOA mwilini mwako? pia TUWASILIANE!
⚠️ WE NEED FOOD, NOT TO***CO, TUNAHITAJI CHAKULA, SIO TUMBAKU - hii ndio kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho haya!
Share IF u care!
Nikutakie maadhimisho mema ya siku hii na siku njema pia!
+255 786 428 821
🕯️wa AfyaBora
©️ RanduNutritions2023
Afya Bora Ndio Utajiri Wako wa Kwanza!
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Makumbusho
Dar Es Salaam
Opening Hours
| Monday | 09:00 - 22:00 |
| Tuesday | 09:00 - 22:00 |
| Wednesday | 09:00 - 22:00 |
| Thursday | 09:00 - 22:00 |
| Friday | 09:00 - 22:00 |
| Saturday | 09:00 - 22:00 |
| Sunday | 10:00 - 22:00 |