Afya ya mifupa

Afya ya mifupa

Share

Tunatatua Changamoto za mifupa na viungo

05/09/2024

Mifupa kurika ni usemi wa Kiswahili unaotumika kuashiria hali ambapo mtu anapozeeka, au hali ya afya ya mifupa inapoendelea kudhoofika, mifupa huwa migumu au yaweza kuwa na maumivu. Usemi huu mara nyingi hutumiwa kuelezea matatizo yanayohusiana na uzee k**a vile arthritis au hali nyingine zinazohusiana na mifupa.

Kwa ujumla, unaweza kutafsiri kuwa hali ambapo mifupa inakuwa migumu na yenye maumivu inavyosababishwa na uzee au magonjwa yanayohusiana na mifupa.

Je, ulikuwa unataka maelezo zaidi kuhusu magonjwa ya mifupa au maana ya kihalisia ya usemi huu?

04/09/2024

MAUMIVU YA VIUNGO NA MAUNGIO YA MWILI

Matatizo ya viungo, miguu kuwaka moto, maumivu ya kiuno na mgongo, yamekua yakiwasumbua watu wengi hasa wenye uzito mkubwa, wanaofanya mazoezi na watu wenye umri kuanzia 45 na kuenderea
Hii ni kwasababu umri unavyozidi kwenda mwili unashindwa kuzalisha ute ute katika viungio vya mifupa, na hivyo kupelekea misuguano ya mifupa, ambapo husababisha maumivu makali sana na kupelekea mtu kushindwa Kukaa, Kuinuka, Kukimbia au Kutembea Kabisa

CHANZO CHA TATIZO LA VIUNGO (JOINTS

Mara Nyingi Ugonjwa Huu Huitwa ARTHRITIS, Unasababishwa na hitilafu yoyote katika sehemu hizo za maungio ya mifupa.
Inaweza kuwa cartilage inalika, upungufu wa synovial fluid(Maji Maji Katika Maungio), maambukizi ya vijidudu katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo Mbali Mbali, Ikiwemo Uzito mkubwa.

Tabia kuu ya magonjwa haya ni maumivu kwenye maungio ya mifupa (joints) ambayo ni endelevu na ambayo hutokea eneo hilo hilo moja.

Chanzo Cha Arthritis Ni Nini...?
Ili Upate Kuelewa Vyema Chanzo cha ugonjwa huu, hebu kwanza tutazame muundo wa joint au sehemu mifupa miwili inapokutana(Maungi)

Mfano Goti ambapo mifupa miwili mmoja wa paja na mwingine wa mguu vinapokutana:

1:Maungio ya mifupa-Ligaments;
-Ndicho kitu kinachoshikilia mifupa hii miwili pamoja,hii ni k**a utepe wa plastiki au mpira unaonyumbuka uliozunguka eneo hilo kwa nje,ukikunja goti inanyumbuka na ukinyoosha mguu inarudi.

2:Cartilage; Huu ni utando unafunika eneo ambalo mifupa hugusana ili kuzuia mifupa hii isisuguane moja kwa moja, Utando huu ambao kwa kiswahili tunauita gegedu huyawezesha maungio hayo kufanya kazi kiulaini pasipo kusababisha maumivu.

3:Capsule; Hiki ni kitu kinachofunika maungio haya kikizunguka pande zote, ndani ya mfuko huu wa capsule kuna synovial fluid ambayo huzalishwa na synovial membrane.
Synovial fluid ni ute ute wa kulainisha sehemu hiyo ya maungio na synovial membrane ni utando ulio kwenye kuta za ndani za capsule.

K**a nilivyoeleza hapo juu, kuwa kuna aina zaidi ya 100 za ugonjwa huu wa joints au arthritis.
Katika mada yetu ya leo tutatazama aina k**a nne hivi za ugonjwa huu, tukielezea chanzo cha kila aina....

4:Osteoarthritis
- Hii ni aina ya arthritis inayosumbua watu wengi zaidi kuliko aina nyingine zote...
Ugonjwa huu huwapata zaidi watu wenye umri mkubwa, Osteoarthritis hutokea pale cartilage inapopoteza uwezo wake wa kubonyea na kuwa ngumu hivyo kuharibika haraka.

Cartilage ni kiungo cha kuhimili migandamizo ya ghafla (shock absorber), Cartilage hii inapopoteza ubora wake, tendons na ligaments huvutika na kusababisha maumivu.
Hali ya uharibifu huu wa cartilage ikiendelea, mwishowe mifupa huanza kusuguana moja kwa moja na ndipo mgonjwa atakapoanza kupata maumivu makali sana sana.

- Athari za ugonjwa huanza taratibu na kuongezeka zaidi, Mgonjwa ataanza kupata maumivu kwenye joint baada ya kufanya shughuli fulani au baada ya mapumziko ya muda mrefu. Joints zitaanza kukaza siku hadi siku, Hasa wakati wa asubuhi unapotaka kuanza shughuli zako za kawaida.
Na siku zinavyosogea ndivyo utakavyoona ni vigumu zaidi kukitumia kiungo chako, Mara nyingine utaona uvimbe kwenye joint.
Osteoarthritis hushambulia zaidi nyonga, mikono, magoti na uti wa mgongo.

2:Rheumatoid arthritis
- Ugonjwa huu hutokea pale mfumo wa kinga ya mwili unapopungua, viungo huanza kushambuliwa, ikiwa ni pamoja na synovial membrane (synovium) na kusababisha uvimbe na maumivu.
Hali hii isipodhibitiwa, huweza kusababisha ulemavu. Ugonjwa huu unaweza pia kushambulia macho, ngozi, mapafu, mdomo, damu na mishipa ya damu. Huu ni ugonjwa ambao zaidi ni wa wanawake na huwatokea zaidi wawapo kati ya umri wa miaka 40 hadi 60.
Mgonjwa atasikia maumivu na kuona uvimbe kwenye joints za pande zote za mwili;
Yaani k**a ni magoti, yote mawili yatashambuliwa na Viungo vinavyoshambuliwa zaidi ni vidole, viwiko vya mikono na miguu.

- Athari zake huonekana zaidi asubuhi unapoamka na maumivu yanaweza kudumu kwa muda wa hadi nusu saa.
Muathirika wa ugonjwa huu hujisikia mchovu muda wote, hukosa hamu ya kula na hupungua uzito, Ugonjwa huu huweza kukua zaidi na Kusababisha matatizo katika viungo vyote vya mwili.
Matatizo yanayoweza kujitokeza ugonjwa ukikua ni k**a yafuatayo:
– Macho kuwa na ukavu, maumivu, wekundu, kutopenda mwanga na kutoona vizuri
– Midomo, Ukavu au kukauka kwa lips za midomo,maumivu na maambukizi ya fizi
– Ngozi,Vijinundu chini ya ngozi kwenye maeneo yenye mifupa.
- Mapafu,Kushindwa kupumua vizuri
– Mishipa Ya Damu, Uharibifu wa mishipa ya damu
– Damu, Upungufu wa chembechembe nyekundu za damu

3:Infectious arthritis (septic arthritic)
- Aina hii ya arthritis inatokana na maambukizi ya bacteria kwenye synovial fluid. Maambukizi haya yanaweza kuwa pia ni ya fungus au virusi.
Wadudu kutoka sehemu nyingine ya mwili iliyo karibu na maungio ya mifupa huweza kusambaa kupitia mfumo wa damu hadi kwenye joint na kuleta maambukizi.

Mara nyingi mtu mwenye aina nyingine ya arthritis ndiye anayepata maambukizi ya namna hii, Mgonjwa ataanza kwanza kupata homa, maumivu na uvimbe kwenye joint.
Maeneo ambayo hushambuliwa zaidi na aina hii ya arthritis ni goti, mabega, kiwiko cha mkono, kiganja (wrist) na vidole na mara nyingi ni eneo moja tu ndilo litakaloshambuliwa

4:Juvenile rheumatoid arthritis (JRA).
- Ni ugonjwa ambao huwapata zaidi vijana walio na umri ulio chini ya miaka 16 na unakuja kwa namna nyingi.
Kuna aina kuu tatu za ugonjwa huu:

Changamoto Kubwa Ya Matatizo Ya Joints Huwapata Wana Michezo,Wanyanyua Vyuma(Body Builder), Watu Wanaofanya Kazi Ngumu, Mafundi Magari, Wabeba Mizigo Na Madereva Wa Masafa Marefu Na Wafanyakazi Wa Mahofisini Wanao Fanya Kazi za Kukaa kwa mdamrefu

SULUHISHO KWA MGONJWA MWENYE TATIZO LA JOINTS NA KUJIKINGA NA MATATIZO YA KULIKA KWA JOINTS

Hakuna Ugonjwa usio na suluhisho k**a ukiuwahi mapema, japo pia ukichelewa ina kuwa ni mbaya zaidi ila suluhisho halikosekani kabisaa!!
Na Suluhisho pekee la Tatizo La Joints kuna programs maalum ya kutatua hiyo changamoto kiujumla

Ijali afya yako

26/06/2023

Osteoarthritis Ni Nini

Ulisha wahi kwenda hospitalini ukaambiwa kuwa mifupa inasagana au uteute umekwisha ama umekauka, Maneno haya yanaelezea tatizo la kiafya ambalo kitaalamu huitwa osteoarthritis. Osteoarthritis ni ugonjwa wa maungio ya mifupa (joints). Ugonjwa huu wa osteoarthritis huonekana zaidi umri wa mtu unapokuwa mkubwa.kati ya miaka 45 hadi 55, Kabla ya umri wa miaka 45, ugonjwa huu unaonekana zaidi kwa wanaume. Baada ya 55, na kuederea. ugonjwa huonekana zaidi kwa wanawake. Osteoarthritis hufupishwa OA na majina mengine ni arthritis au degenerative joint disease.Tofauti na aina nyingine za arthritis, k**a rheumatoid arthritis na systemic lupus, osteoarthritis haishambulii sehemu nyingine za mwili.

Osteoarthritis hushambulia zaidi mikono, miguu, uti wa mgongo, na maungio yanayobeba uzito mkubwa k**a nyonga na magoti. Primary osteoarthritis ni pale chanzo cha ugonjwa hakijafahamiki na k**a chanzo kinaeleweka ugonjwa huu huitwa secondary osteoarthritis. Hapo sasa ni pale ambapo dalili zote zimefahanika,

06/06/2023

NJIA SAHIHI YA KUPONA KUPONA MAUMIVU YA VIUNGO NA MIFUPA KUSAGANA BILA UPASUAJI: (0756560562)

UNAPASWA KUPATA VIRUTUBISHO VYENYE MADINI MUHIMU KWA AJILI YA VIUNGO NA MIFUPA.

MCHANGANYIKO WA MADINI YA CHONDROTIN NA GLUCOSE AMINE KWA WINGI PAMOJA NA MCHANGANYIKO WA CALCIUM,ZINC,AMINO ACID NA MAGNESIUM.
HII NI TIBA YA MIFUPA KUSAGANA KATIKA MAUNGIO,, NA TIBA YA MAUMIVU YA VIUNGO )mfano
mgongo,nyonga,magoti, shingo,mabega,ganzi nk.
HADI KUFIKIA HATUA YA VIUNO NA MIFUPA KUSAGANA MAANA YAKE NI KWAMBA HUWA KUNA UPOTEVU MKUBWA WA MADINI HAYA KUPOTEA KWA WINGI MWILINI NA KUSABABISHA UPOTEVU WA UTEUTE NA KULIKA KWA GEGEDU/CARTILAGE.

KWANZA, TUJIELIMISHE KIDOGO.🖐
KWA NINI MIFUPA HUSAGANA KWENYE VIUNGO NA KULETA MAUMIVU MAKUBWA?
=>KICHWA CHA MFUPA KATIKA VIUNGO KIMEZUNGUKWA NA MFUPA LAINI UITWAO GEGEDU(CARTILAGE)
KAZI YA GEGEDU(CARTILAGE ) NI KUZUIA MFUPA USISAGANE NA MFUPA MWENZAKE KWENYE VIUNGO,
PIA KUNA UTE UTE (SYNOVIAL FLUID) AMBAO NI GRISI YA VIUNGO,,HUSAIDA KULAINISHA MJONGEO(MOVEMENT)

MTU ANAPOFIKISHA MIAKA 30 CARTILAGE HUANZA KULIKA NA KUSABABISHA MIFUPA KUGUSANA NA KUSAGANA KWENYE VIUNGO HADI ULE UTE KUPOTEA,

HII HUSABABISHA MAUMIVU MAKALI KWENYE VIUNGO, HADI KUPELEKEA MTU KUSHINDWA KUJONGEA IPASAVYO,
TATIZO HUONGEZEKA UMRI UNAPOZIDI KUWA MKUBWA NA UZITO UNAPOONGEZEKA,
ARTHROEXTRA NA ZAMINOCAL PLUS NI ZA ASILI HAZINA KEMIKALI, NA KUTHIBITISHWA NA TMDA,kupata huduma piga (0756560562).

04/06/2023
Photos from Afya ya mifupa's post 24/05/2023

Mifupa ni nguzo kuu inayo beba mwili,mifupa ikiadhirika mwili kwa kawaida utapata shida. Huu mifupa unauona umeadhirika na unamugu ama tunaweza sema unachubuka. Nini kinapelekea mifupa huu kuchubuka? mfupa huu unachubuka kwa sababu ya musuguano na mfupa mwingine ambao unagusana nao, na huu musuguano unatokea kwa sababu ya kurika kwa gegedu au cartilage. na hizi gegedu zikipungua ujazo wake au unene husababisha viungo vya mwili kukaukiwa na (uteute) synovial fluid baada ya uteute kukauka na gegedu kupungua ndipa sasa maumivu huanza kusumbua na michubuko huanza kutokea kwenye viungo vya mwili yaweza kuwa magoti uti wa mgongo au kiungo chochote Cha mwili. Na huu wekundu unaouna kwenye picha ya pili ni Hali ya kuadhirika kwa mifupa kwa sababu ya mugandamizo wa gegedu, na mishipa ikiadhirika husababisha viungo vya mwili kuhisi ganzi na muda mwingine kuwaka moto, epuka kuadhiri mifupa kuwa na mifupa imala na Bora.

11/05/2023

Leo tutazungumzia tatizo linalowapata watu wengi sana pale umri wao unapokuwa umezidi miaka 55 na hasa wale wenye miili mikubwa. Nina uhakika kuwa umewaona akina mama na akina baba wenye umri mkubwa na miili mikubwa wanavyopata shida kutembea huku wakiinama toka upande mmoja hadi upande mwingine kila wakipiga hatua kwa shida na inapowabidi kupanda ngazi au kukuchuchumaa. kwao huwa ni chang'amoto zaidi. “ugonjwa wa kuumwa joints, maumivu ya joints” na maumivu ya mifupa umeyasikia mara kwa mara. Tatizo hapa ni nini? kwanza kanisa umuri unavyokuwa mukubwa mifupa inachoka, na uteute kupungua kwenye jointi hivyo hufanya michubuko kwenye maungio na kufanya musuguano kwenye mifupa. hivyo basi inatubidi kuepuka visababishi na hatari zinazoweza kutupelekea chang'amoto na uharibifu wa mifupa.

Photos from Afya ya mifupa's post 17/04/2023

Fanya mazoezi ang'arau kwà dakika 30 kwa siku ili kuweka mifupa na maungio yoko kuwa na ubora ili uweze ketembea na kupiga hatua bila shida na kukimbia pia.

06/04/2023

Miguu ama viungo vya mwili kuwaka moto ni tatizo kubwa kwa watu wengi mara nyingi husababishwa na uzito mukubwa mishipa ya damu kuziba na damu pamoja na okisijeni kushidwa kusafiri hivyo basi miguu kuwaka moto huenda sambamba na viungo kupata ganzi na hata mara nyingine utaona na miguu kuvimba endapo tatizo litawa linamsumbua mtu kwa muda mrefu, uvutaji wa sigara na utumiaji wa pombe kupita kiasi huchangia tatizo hili kukua kwa kasi, hivyo basi k**a una tatizo la miguu kuwaka moto chukua tahadhari maana madhara yake ni makubwa.

03/04/2023

Nini Maana Ya Miguu Kuwaka Moto?
Miguu kuwaka moto ni tatizo kubwa sana kwa sasa. Maumivu haya yanaweza kuwa ya mda mfupi au yakakaa mda mrefu bila kuisha. Miguu yako itahisi hali ya kuungua na kufa ganzi. Maumivu huwa makali sana hasa nyakati za usiku.

Matibabu ya changamoto ya miguu kuwaka moto yanategemea na chazo cha tatizo lako. Endelea kusoma zaidi makala hii ili ujue chanzo cha tatizo lako na tiba sahihi inayokufaa.

Sababu zinazokufanya Upate Tatizo La Miguu Kuwaka Moto
1.Miguu kuwaka moto kwasababu ya kisukari-Diabetic Neuropathy
Kisukari kinapokusumbua kwa mda mrefu kinapelekea mishipa midogo ya fahamu kuathirika. Mishipa inapoathirika inakwamisha pia usafirishaji wa taarifa ndani ya mwili.

Taarifa zisiposafirishwa vyema inapelekea changamoto kwenye kuhisi matukio ya ndani na nje ya mwili. Pia kisukari kinaharibu mishipa ya damu ambayo inabeba hewa safi ya oksijeni ndani ya mwili.

Mishipa ya fahamu inaweza kuathiriwa maeneo mbalimbali ya mwili. Na athari hii inaongeza endapo hizi pointi unazo ua unatumia vitu hivi

1:uzito mkubwa
2:presha
3:unavuta sigara
4:kunywa pombe kupitia kiasi

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Ilala
Dar Es Salaam