Marseline Mushi
Tunatatua changamoto za mifupa na uzazi kwa wanaume na wanawake
20/02/2023
WANAWAKE WENYE HATARI YA KUPATA UVIMBE KWENYE KIZAZI
-Ambao hawajazaa kabisaa
-Wanawake wanene (hasa ile wa kujiongeza na sindano)
-Wanaopata hedhi mapema
-Wanawake /wasichana ambao wako katika umri wa kupata ujauzito
DALILI ZA UVIMBE KWENYE KIZAZI
-Kutokutunga mimba/mimba kutoka au kuharibika wakati mwingine ugumba
-Kukohoa mara kwa mara(uvimbe kukandamiza kibofu cha mkojo)
-Kutoka damu nyingi kwa muda mrefu wakati wa hedhi ikiambatana na mabonge isivyo kawaida
-Kupata maumivu ya kiuno wakati wa hedhi(kutokana na ugonjwa kubana viungo vingine vya mwili)
-Hedhi zisizokuwa na mpango na kutokwa damu isivyokawaida katikati ya mwezi
-Maumivu wakati wa tendo la ndoa
-Maumivu ya mgongo
31/01/2023
DALILI ZA FANGASI UKENI
Kuwashwa sehemu za siri (kwenye tupu ya mwanamke)
• Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri (burning sensation)
• Kufanya k**a vidonda katika sehemu za siri (soreness)
• Maumivu wakati wa kujamiana (superficial dyspareunia)
• Maumivu au usumbufu wakati wa kujisaidia haja ndogo (wakati mtu anakojoa)
• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwa mdomo wa nje wa tupu ya mwanamke (l***a minora)
• Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au nyeupe kijivu, unaoweza kuwa mwepesi, majimaji au mzito na ambao umefanana na jibini (cottage cheese like discharge) wenye muonekano unaojulikana pia k**a curd-like appearance
30/01/2023
MIWASHO SEHEMU ZA SIRI.
Tatizo hili limekuwa likuwasumbua wanawake walio wengi. Na pia wanalichukulia ni tatizo la kawaida tyu lakini usipolipatia ufumbuzi mapema linaweza kukusababishia matatizo makubwa sana. Hivyo basiiii ukiona tatizo hili usisite kulitafutia ufumbuzi mapema .
Kwa tiba na ushauri tutafute kupitia +255659719243.
26/01/2023
Madhara yatokanayo na PID
Mimba nje ya mirija (ectopic pregnancy). PID ndiyo sababu kubwa ya mimba kutunga nje ya kizazi. Mimba huweza kutunga nje ya kizazi endapo PID imesababisha makovu ndani ya mirija ya uzazi. Makovu haya husababisha yai lililopevushwa kushindwa kusafiri ndani ya mirija ya uzazi kuelekea kwenye nyumba ya uzazi. Badala yake yai hunata ndani ya mirija ya uzazi . Mimba nje ya kizazi husababisha utokaji wa damu usio wa kawaida unaoweza kukatisha maisha ya mwanamke.
Ugumba. Uharibifu wa viungo vya uzazi huweza kusababisha ugumba – kushindwa kupata ujauzito. Kadiri unavyozidi kupata PID mara nyingi zaidi, ndivyo hatari ya ugumba inavyozidi. Kuchelewa kupata tiba ya PID kunaongeza hatari ya ugumba.
Maumivu sugu ya nyonga. PID inaweza kusababisha maumivu ya nyonga yanayoweza kudumu kwa miaka mingi. Makovu ndani ya mirija ya uzazi na viungo vingine vya uzazi huweza kuleta maumivu wakati wa kujamiiana na wakati yai linadodondoshwa (ovulation).
Tubo-ovarian abscess. PID huweza kusababisha kutunga kwa usaha na kufanya majipu ndani ya njia ya uzazi. Mara nyingi majibu haya hutokea ndani ya mirija ya uzazi na ovari, ingawa huweza kuota ndani ya nyumba ya uzazi na shingo ya kizazi. K**a tiba haitatolewa, unaweza kupata maambukizo hatarishi kwa maisha.
UKIENDELEA KULIFUMBIA MACHO TAZIZO UNAWEZA KUPATA KANSA YA KATIKA MFUKO WA UZAZI NA MATATIZO YA FIGO
24/01/2023
VYAKULA AMBAVYO HUSAIDIA KUPUNGUZA PRESHA YA KUPANDA AMA HULINDA MWILI DHIDI YA PRESHA YA KUPANDA.
Presha ya kupanda inaweza kupelekea athari kubwa na mbaya sana kwenye afya ya mtu. Presha ya kupanda isipotibiwa ama mtu asipofuata masharti ya kuishi na ugonjwa huu madhara makubwa yanaweza kutokea. Kifo, kupasuka kwa mishipa ya damu, kupalalaizi, kuharibika kwa figo na moyo kushindwa kufanya kazi na kupata shambulio la moyo yote haya yanaweza kuwa ni matokeo ya presha ya kupanda pindi isipotibiwa ama mtu asipofata masharti.:-
Unaweza kupamana na presha kwa kufuata mashari k**a kufanya mazoezi, kula vyakula salama kwa presha, kupunguza misongo ya mawazo, kupunguza kula chumvi, kupunguza uzito, kupunguza ama kuacha sigara na pombe. Miongoni mwa vyakula salama kwa presha ni k**a
1.Mboga za majani ambazo zina madini ya potassium kwa wingi. Madini haya ni mujarabu sana katika kulinda na kuimarisha afya ya moyo. Ulaji wa mboga hizi unaweza kuwa ni njia ya kujilinda na presha ya kupanda. Miongoni mwa mboga hizi ni k**a spinachi
2.Maziwa: maziwa ni katika vyakula vyenye madini ya calcium kwa wingi na pia yana mafuta kwa uchache. Hali zote mbili hizi ni muhimu kwa afya ya moyo.
3.Ndizi; ndizi ni katika matunda yenye madini ya potassium kwa wingi. Ulaji wa ndizi unaweza kuwa ni msaada mzuri kwa kulinda mwili dhidi ya presha ya kupamda.
4.Mayai
5.Samaki aina ya salmon na wanaofanana nao.
6.Ulaji wa mbegu za mimea k**a maboga na alizeti
7.Kitunguu thaumu: unaweza kutumia vitunguu thaumu kwa kula ama kutafuna, ni vyema kufunga mdomo wakati unapotafuna.
8.Makomamanga; unaweza kula atunda hili k**a juisi ama kula kawaida.
23/01/2023
UNASHAURIWA KULA VYAKULA HIVI KWA AJILI YA KUIMARISHA MIFUPA
Mifupa imeundwa kwa madini mbalimbali ikiwemo madini ya calcium na phosphorus kwa kiasi kikubwa hvyo ili uweze kuwa na mifupa imara unahitaji kula vyakula vyenye calcium na phosphorus kwa wingi.vyakula hvyo ni k**a ifuatavyo
*Samaki.samaki wana madini k**a calcium ambayo ni muhimu katika mifupa pia mafuta ya samaki (omega 3 fatty acids) yana umuhimu sana katika afya ya mifupa pamoja na mfumo wa damu.
*Mboga za majani.tunapata calcium na vitamin mbalimbali ambavyo vinaweza kuimarisha mifupa na viunga pia zina uwezo wa kuzuia vimeng'enya hatari vinavyoweza kusababisha kuvimba na maumivu katika viunga.
*Matunda.baadhi ya matunda yana lycopene na anthocyanins na vitamin C ambazo huepusha madhaifu ya mifupa matunda hayo ni k**a machungwa, nyanya,limao, strawberries, ndizi mbivu nk
*Mafuta.vyakula vyenye kiasi kikubwa cha omega 3 mfano mafuta ya parachichi na mafuta ya mzeituni
*Maharage.baadhi ya maharage ni mazuri katika afya mifupa mfano maharage ya
soya,maharage meusi nk haya virutubisho ambavyo vinaweza kuimarisha mifupa.
*Maziwa.maziwa yana calcium na vitamin mbalimbali ikiwemo vitamin D ambayo husaidia ufyonzaji mzur wa calcium.
*Mayai. Haya yana madini mbalimbali ikiwemo calcium na vitamins kwa wingi hvyo husaidia kuwa na mifupa imara.
Vyakula vyenye phosphorus ni k**a ndizi
Saratani ya tezi dume maana yake ni tezi dume imepata ugonjwa wa saratani..Na hii hutokea pale ambapo chembechembe hai za tezi huasi na kuanza kujigawanya bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili, chembechembe asi hizi mwishowe hutengeneza vivimbe hatari ndani ya tezi dume na hatimaye husambaa mwilini
VISABABISHI HATARISHI VYA TEZI DUMEUmri Mkubwa kuanzia miaka 50Nasaba (ukoo wenye historia a saratani hiiLishe hatarishi-nyama nyekundu kwa wingi, mafuta/samli,maziwa ya krimuUnene uliokithiriUkosefu wa mazoeziUpungufu wa virutubisho,mfano vit D.Maambukizi ya mara kwa mara kwenye tezi dume
DALILI ZA TEZI DUME
Udhaifu katika utoaji wa mkojo, mkojo hauishi.
Kwenda kukojoa mara kwa mara.
Damu ndani ya mkojo.
Kushindwa kukojoa.
Maumivu ya kiuno na mifupa ya nyonga.
Wagonjwa wengi huanza maumivu ya nyonga k**a ni dalili za awali.
Udhaifu katika utoaji wa mkojo pia kunaweza kutokea kwa kuvimba kwa tezi dume bila ya saratani.
Damu kwenye mkojo nakushindwa kumaliza mkojo ni ishara tosha ya kuwa tezi dume imeathirika.
MADHARA MAKUBWA YA FANGASI NA U.T.I.
Kupatwa kwa ugonjwa wa Pelvic Inflammatory Disease (PID) maambukizi katika via za uzazi na kupelekea kuwa ngumba, ndio maana wanawake wengi ni wagumba.
NAMNA YA KUJILINDA NA U.T.I NA FANGASI.
1. Tumia viini lishe na virutubisho i.e food supplements.
2. Kunywa maji mengi angalau glasi nane kwa siku.
3. Epuka matumizi ya pombe na kahawa.
4. Kunywa maji kabla ya kufanya mapenzi na kojoa baada ya kufanya mapenzi.
5. Jitawaze kuanzia mbele kwenda nyuma. (Front to Back)
6. Kata makucha marefu kwa sababu unavyokwenda chooni kujitawaza huwa baadhi ya uchafu unabaki kwenye makucha na ndio chanzo cha wanawake wengi kuwa na U.T.I inayojirudia mara kwa mara.
7. Tumia pads ukiwa kwenye period.
8. Ebuka kujipulizia pafyumu kwenye sehemu za siri.
9. Vaa nguo za ndani za pamba na epuka nguo zilizobana sana.
22/01/2023
FAHAMU KUHUSU U.T.I NA FANGASI SUGU.
U.T.I na fangasi ni tatizo kubwa ambalo huwapata wanawake wengi duniani mara kwa mara. Husababishwa na bakteria anaitwa E. coli ambaye huwa wanaishi kwenye utumbo mnene sehemu za tundu la haja kubwa, mwanamke anaambukizwa kirahisi sababu anapokuwa anachuchumaa kwenye haja kubwa au ndogo.
Madhara yake kwenye kibofu cha mkojo baada ya kuwa wengi wanahamia mwenye figo, ndio maana leo hii wanawake wengi wanaumwa figo. Figo zao zimeharibika sababu ya U.T.I. na kufa kifo cha ghafla.
Tafiti zinaonyeshwa kuwa nchini marekani watu milioni nane (8.1m) hupata U.T.I kila mwaka.
MIWASHO.
Kawaida mwanamke ana ulinzi ukeni kwake, yaani bakteria wazuri wanaishi kule kwa ajili ya kulinda uke, japo pia bakteria wabaya wanaishi kule lakini kwa uwiano, ya kwamba wale wazuri wanakuwa wengi ,kuliko wabaya . Sasa ikitokea kwamba wale bacteria wabaya wakawa wengi, hapo ndio utaona miwasho kwa mwanawake haishi kujikuna mara kwa mara.
FANGASI.
Inasababishwa na jamii ya fungi anaitwa CANDIDA. Seli za fangasi na bacteria wazuri huishi ukeni bila tatizo lolote.Tatizo linakuja endapo ukuaji wa fangasi hawa ukeni watakuwa wengi kushinda wazuri. Basi hapo ndio inapotokea ugonjwa wa fangas na miwasho mingi.
DALILI ZA U.T.I
1. Kukojoa mara kwa mara.
2. Mkojo kuwa na harufu kali.
3. Kusikia kichefu chefu na kupatika.
4. Maumivu ya misuli na tumbo hasa chini ya kitovu.
5. Kusikia maumivu wakati wa kukojoa.
6. Maumivu ya kiuno.
7. Kuwashwa sehemu za siri.
8. Kuhisi maumivu wakati wa kujamiiana.
9. Kupata vidonda vya ukeni.
10. Kuvimba na kuwa mwekundu kwa mdomo wa inje wa uke.
11. Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri baada ya tendo la ndoa.
12. Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au kijivu unaoweza kuwa mwepesi au mzito au majimaji.
VISABABISHI VYA FANGASI.
1. Mabadiliko ya homoni katika kipindi cha upevushwaji wa mayai kwa mwanamke kipindi cha ujauzito, utumiwaji wa uzazi, wa mpango na kukoma kwa hedhi.
2. Upungifu wa kinga mwilini: Mtu mwenye upungufu wa kinga mwilini k**a vile mwenye kuugua kansa, ukimwi, magonjwa mbalimbali yenye kupunguza kinga ya mwili.
3. Kukosa usingizi stress, vidonda sehemu za siri,matumizi ya antibiotics, kuweka marashi sehemu za siri.
4. Watu wanaougua kisukari ambao hawawezi kudhibiti kwa kutumia dawa za kisukari, inakuwa kwenye damu na hicho kisukari ndiyo chakula kikuu cha hao fangasi.
Hata wanawake ambao wanapenda kula vyakula vya sukari nyingi k**a vile chocolates, soda, na vingine vyenye sukari nyingi ambavyo ni chakula cha fangasi.
5. Mazingira ya joto hii inamaanisha nguo ambazo tunatakiwa kuvaa k**a vile chupi za cotton hasa kwa wanawake, hazihitaji joto sababu bacteria wabaya wanakuwa wengi sana na kusababisha miwasho na FANGAS
6. Kondomu na mbegu za kiume huharibu hali ya asidi iliyopo ukeni ambayo ni ya muhimu sana maana inasaidia kukinga uke usiingiliwe na bacteria wabaya.
21/01/2023
Vyakula vya kuongeza ute kwenye viungo
Samaki wa aina ya Salmon,Maziwa fresh ya Ng'ombe,Jibini,Samaki wa aina ya
Sardines,Mtindi,Totu,Ufuta,Maharage
meupe,Mchicha na mboga ya sukuma wiki (Mboga ya Matembele)
MTINDI: Huimarisha kinga ya mwili, hurefusha maisha
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Ubungo Maziwa
Dar Es Salaam
255