simulizi za MalkiaOsam

simulizi za MalkiaOsam

Share

BONYEZA. https://simulizihouse.life KUSOMA VITABU VYANGU

03/08/2026

LUCKY __27

Mwandishi :Malkia Osam

Innocent akatoa midomo yake haraka k**a vile ndiyo kwanza alikuwa anarudi kwenye uhalisia wake ,yaani k**a ni akili basi ndio zilikuwa zinajirudi

Aliyatanua macho kwa mshangao , akarudi hatua moja nyuma haraka, akapitisha mkono wake kwenye nywele hata sijui alikuwa anatafuta nini huko

"Lucky... mimi... A_ah samahani..." akaongea sauti ya chinii ya kujishtukia k**a jitu zima hovyo, sauti yake ilikuwa ya kujutia alicho fanya .

Lucky alibaki amesimama pale pale, macho yake yalikuwa yameganda kumtazama Innocent bila kusema neno .

Uso wake ulikuwa umejaa aibu na mshangao wa wazi kabisa, mapigo ya moyo sasa yalikuwa yanapigana kwa pupa k**a ngoma za mizimu

Mwili wake ulikuwa k**a umepigwa shoti hakujua alie ,akimbie au aseme nini muda huo aibuu ilikuwa kubwa kuliko hata umri wake

"Boss..." Lucky alimuita kwa woga wa mbalii ,huku anamtazama bado

Innocent akafumba macho kwa sekunde chache.
"Sikupaswa kufanya hivyo. Nisamehe Lucky... nilizidiwa na hisia za muda.hata sijui imekuwaje mdogo wangu!!" Innocent bwana et akajikuta kawa na kaka kwa muda huo .

Lucky akameza fundo la mate.

"Hata mimi... sikutarajia kitu k**a hiki kitokee.naamini hakitatokea tena!"

Ukimya mzito ukatawala tena ofisini.
Baada ya dakika chache, Innocent akavuta pumzi ndefu.

"Naamini hivyo pia!! Naomba unisamehe sana kwa hiki nilichofanya Lucky!!" Lucky akainua macho.

"Tunahitaji kusahau kilichotokea muda huu. Tusikubali kuharibu kazi wala maisha yetu."Maneno hayo yaliuchoma moyo wa Innocent, akakumbuka yale maneno kuwa yeye sio mwanaume anaemvutia, lakini akajitahidi kutabasamu

"Nitajaribu."Innocent akachukua funguo za gari mezani.

"Nitakupeleka nyumbani. Ni usiku tayari."

"Hapana Boss, naweza..."

"Hapana. Sitaki urudi peke yako."
Lucky hakubisha tena.

Dakika chache baadaye walikuwa ndani ya gari. Safari yote ilitawaliwa na ukimya. Redio ilikuwa inacheza wimbo wa taratibu, lakini hakuna aliyekuwa na nguvu ya kuusikiliza.

Kila mmoja alikuwa amezama kwenye mawazo yake.
Lucky alikuwa akiitazama taa za barabarani kupitia dirishani huku akijiuliza...Mungu wangu ,hii nini,mbona natetemeka hivi,Innocent amewaza nini,Oooh Munguu ,Huyu kaka ni mume wa mtu jamani ,mbona natamani anikumbatiee aaah !!!..

Naye Innocent aliishika usukani kwa nguvu.
Rose ni mke wangu... lakini kwa nini kila nikimwangalia Lucky moyo wangu unakuwa tofauti? Mbona natamani kuwa nae sasa inamaana Rose alikuwa sawa kwa alichosema Eeh Mungu nipe Nguvu ya kupambania Ndoa yangu....aliwaza huku akivuta pumzi nzito.

Walipofika mbele ya nyumba ya Lucky, Innocent akasimamisha gari.
"Asante kwa kila kitu Boss."
Karibu ashuke, Innocent akamwita.

"Lucky..."Akageuka.

"Kesho uje kazini k**a kawaida. Usiogope."
Lucky akatabasamu kwa mara ya kwanza usiku ule.
"Sawa Boss."

Akafunga mlango wa gari na kuingia ndani.
Innocent alibaki amekaa ndani ya gari kwa dakika kadhaa bila kuwasha injini.

Lucky baada ya kuingia ndani akakumbia Dirishani kumchungulia Innocent k**a ameondoka,Gari ilikuwa bado imesimama pale palee ...

Itaendelea...



HAKIKISHA UNAJIUNGA NA WASP CHANNEL KUPATA MIENDELEZO YA STORY NYINGII

https://whatsapp.com/channel/0029VbD0wn347XeJfcaZpf2b

02/08/2026

LUCKY __26

Mwandishi :Malkia Osam



" Lucki....!!?" Innocent alikurupuka k**a kaona mzimu mbele yake akaushika mkono wa Lucky kwa nguvu

"Hapana.... usiache kazi nakuahidi hili nitaliweka sawa please usiondoke!!" Innocent alishindwa kujizuia zaidi akajikuta anamkumbatia kwa nguvu kidogo.

Alijikuta anapata woga wa ajabu k**a Lucky ataacha kazi ,haijawahi kutokea kabisa yeye kuogopa mfanyakazi yeyote kuacha kazi wala kuhisi baridi kali k**a analohisi kwa Lucky ...

Lucky baada ya kukumbatiwa ,wee!! Aliangua kilio hiko yaani ni k**a vile alikuwa akihitaji hili kumbato kwa muda mrefu sana .

Alilia mpaka mafua mepesii yakaanza kumtoka bila taarifa ,Innocent alikuwa kimyaa kambana vizuri kifuani kwake ,taratibu alikuwa akiupapasa mgongo wake ili kumtuliza ..

"Inno....!!!" Sauti ya Lucky ilikuwa bado ya kulia iliyoambatana na mafua .

"Yes.."

"Naogopa Inno..sitaki kuacha kazi kweli ,lakini haya yanayo endelea yananitisha Inno,kazi ndio kila kitu kwangu nimehangaika sana Inno....mimi....!!!" Sauti ya Lucky ilikuwa imebanwa na kilio

"It's okay Lucky, Hauta acha kazi niamini mimi " Innocent akamkumbatia vizuri zaidi ya mwanzo ..
Vile alivyomkumbatia ajabu Innocent alijikuta anatamani kumkumbatia zaidi na Zaidi yaani hakutamani kabisa kumuachia



Mwili wa Lucky hakuhitaji kumuachia Innocent kabisa. Alitamani akumbatiwe zaidi ya hapo.

Misisimko ya ajabu ilianza kujitokeza kwenye miili yao, kila mmoja akahisi uwepo wa mwenzake kwa namna ambayo hakuwahi kuuelewa hapo awali.

Mkono wa Innocent uliokuwa unampapasa Lucky mgongoni, ulizaa hisia nyingine kabisa kwa Lucky.

Dakika chache zikapita hakuna aliyekuwa tayari kuvunja ule ukimya.
Lucky akafumba macho taratibu, akaegemeza kichwa chake kifuani kwa Innocent.

Kwa mara ya kwanza baada ya siku nyingi, alihisi salama hapo kwenye kifua cha mkaka huyu

Mapigo ya moyo ya Innocent yalikuwa yanagonga kifuani mwake kwa mpangilio mzuri, na kila pigo lilionekana kumpa utulivu ambao alikuwa ameukosa kwa muda mrefu Innocent mwenyewe alijikuta anafumba macho na kupata utulivu hapo

Moyo wake ukajaa hisia nyingi ambazo hata yeye mwenyewe hakuweza kuzitafsiri muda huo .

Luck alijitahidi kupambana na hisia zake ambazo zilikuwa zinapanda wa kila sekunde ya mguso wa Innocent nakumfanya aheme hara haraka .Kila alipojaribu kujisogeza mbali kidogo, moyo wake ulimrudisha karibu tena.

Taratibu inno akainua mkono wake akamfuta machozi yaliyokuwa yamebaki mashavuni mwa Lucky.

"Usilie tena please!!!" Hapo sasa ndio Lucky akashtuka ,yaani kajilegeza kwa Boss wake tena mume wa mtu , akainua uso haraka kumtazama Innocent , wakajikuta wametazamana macho ,Kwa sekunde kadhaa walibaki wanatazamana kimya.

"A-aah Boss... Ahm nataka kwenda nyumba...!!" Innocent alikuwa Anatazama midomo ya Lucky wakati anazungumza akajikuta kiu ya Busu inamgusa mpaka akashindwa kujiuzia akamlamba bonge wa Busu kwenye lips zake

Lucky alihisi tumbo lake likijaa vipepeo wa ajabu.uso wote ukapata Rangi ya Aibu,Moyo wake ukadunda kwa nguvu.

Mtetemo wa ajabu ulitikisa mwili wote wa Lucky kabla hajarudisha akili sawa Innocent alijikuta tena anakutanisha midomo yake na Lucky na hapo sasa lilitembea busu la taratibu kabisa likinogeshwa na ukimya wa hali ya juu wa usiku ...

Lucky alikosa nguvu kabisa ya kusogea nyuma mpaka Innocent alipojishtukia ndio akatoa midomo yake haraka

HAKIKISHA UNAJIUNGA NA WASP CHANNEL KUPATA MIENDELEZO YA STORY NYINGII

https://whatsapp.com/channel/0029VbD0wn347XeJfcaZpf2b

01/08/2026

LUCKY __25

Mwandishi :Malkia Osam



"Kukusamehe kwa kosa gani??"


"Hmm ...Kuwa sababu ya matatizo yako na mke wako.nimekuwa k**a mdudu ndani yenu!"

Innocent alimtazama kwa mshangao.hata akacheka kidogo kwa kusawajisha tu Uso

"Unasema nini Lucky, Lakini hakuna chochote kinachoendelea kati yetu!!"

"Nilisikia kila kitu leo..." Lucky alisema huku sauti yake ikitetemeka na macho yake taratibu yakaanza kujaa machozi

"Nimesikia Rose akiomba talaka kwa sababu yangu. Najua mimi ndiye chanzo cha yote haya."

Chozi moja liliteremka shavuni mwake likapenya mpaka kwenye lips zake ,akameza mate mazito ya uchungu

"Inno..." Lucky aliita kwa ufupi jina la Innocent na kwa sauti ya chini huku anafuta chozi .Innocent akaongeza umakini kumtazama

"Tafadhali usigombane na Rose kwa ajili yangu." Kimya kidogo kikapita ,Innocent alibaki k**a hana neno la kutia

"Nimeamua kuacha kazi." Innocent alishtuka mpaka akasimama.

"Nani amesema utaacha kazi?"

"Mimi mwenyewe."

"Kwa sababu gani?"

"Kwa sababu sitaki kuwa sababu ya ndoa ya mtu kuvunjika."Innocent akatikisa kichwa kwa nguvu.

"Hapana Lucky. Yaani uache kazi kwa sababu ambazo hazieleweki!!"

Lucky akainua macho kumtazama.

Innocent akaendelea,

"Matatizo yaliyopo kati yangu na Rose hayajaanza leo. Na hayajasababishwa na wewe. Rose ni mke wangu, Wewe matatizo yetu hata hayakuhusu !!"

"Innocent, mimi ni mwanamke. Naelewa alichokuwa anahisi."Kauli hiyo ilimfanya Innocent anyamaze kidogo.

"Labda k**a ningekuwa mbali na maisha yako, haya yote yasingetokea inno,acha tuache haya mambo yapite tuwe tu k**a hatukuwahi kukutana !!" Innocent alivuta hatua moja kumsogelea Luckk."

"Wewe ni mfanyakazi mzuri sana. Hospitali hii inakuhitaji."

Lucky akashusha macho.

"Innocent..."

"Hapana, nisikilize. Hutaondoka kwa sababu ya maneno ya mtu au kwa sababu ya lawama ambazo hata si zako." Lucky alijikuta moyo wake unalegea ,Hii kazi ana ihitaji kuliko chochote lakini anaona ugumu mkubwa mbele yake ...

Moyo wa Lucky ulianza kulegea taratibu. Alitamani sana kubaki kazini alikuwa na kiu ya kuendelea kukaa hapo ofisini alikuwa na Hamu ya kufanya kazi kwenye hii hospitali kubwa yenye hadhi kubwa kuliko yeyee..

Alijikuta analia mpaka kwikwi inamshika bila kitoa sauti ya kilio .... akafungua droo yake taratibu.

Ndani kulikuwa na bahasha ya kahawia.

Aliitoa na kuiweka mezani mbele ya Innocent.

Innocent aliitazama kwa sekunde chache.

"Ni nini hiki?"

Lucky akameza fundo la mate.

"Barua yangu ya kujiuzulu."

Uso wa Innocent ukabadilika ghafla.

"Umeandika lini hii?"

"Tokea mchana."

Macho yao yakagongana.

Na kwa mara ya kwanza, Innocent alihisi hofu ya kumpoteza Lucky kuliko alivyowahi kuhisi hapo kabla.....

Nakujaaaaa

HAKIKISHA UNAJIUNGA NA WASP CHANNEL KUPATA MIENDELEZO YA STORY NYINGII

https://whatsapp.com/channel/0029VbD0wn347XeJfcaZpf2b

31/07/2026

NIMEKOMA ❤️01

SIMULIZI ZA TINNAH

Mimi ni Zabibu mtoto wa uswazi ambae kichwa changu nikibovu mpaka kibovu tena. Nimezaliwa mwaka 1992 mkoa wa lindi wilaya ya masasi. Wazazi wangu ni watu wa kawaida tuu kiuchumi yani sio watu wenye pesa sana wala sio masikini sana, baba yangu ni mfanya biashara ana duka lake la nafaka na mama ni mfanya biashara wa sokoni. Uchumi wetu ni wakati, licha ya kua mimi ni msomi wa chuo kikuu niliyehitimu chuo fulani hapa nchini lakini bwana mie mtu akiniona hawezi nizania kabisa lazima anishushe hadhi kwasababu ya ninavyojiweka aaah bwana maisha mafupi haya kwani shi ngapi!

basi bwana, mwaka 2007 nilipomaliza kidato cha nne nilienda mkoa wa njombe kumsaidia shangazi yangu ambae alikua amejifungua ivyo nilienda kumsaidia masuala ya uzazi, kwanza mpaka naenda haikua kazi ndogo, mama alipambana kwelikweli kunilazimisha niende lakini mwisho wa siku niliamua tuu kwenda mnazani ni kwasababu ya mama! waaala, ni niliingiwa na mawazo ya kubadilisha mazingira ili nipate wanaume wapya ivyo mimi kwenda njombe nilichukulia k**a fursa bwana

kipindi icho nilikua tayari nina umri wa miaka kumi na tano tuu, mimi mwenzenu niliwahi sana kwenda shule kwasababu nilikua na mwili mkubwa ivyo hata kumaliza kidato cha nne nilikua na mwili mkubwa haswaa hata mtu angeniona asingezani nina umri huo wa miaka kumi na tano yaani nilikua bonge la dada afu shangingiii

sio mwili tuu ulikia mkubwa mwenzenu mie nilikua mrembo wa haja yani nilijaaliwa sura na mshepu maashaalah sijisifii ila huo ndio ukweli yani nilikua mzuri alafu mzuri tena,

sura yangu ilikua inavutia yani kwa namna nilivuokua nilikua navutia wanaume kwa wanawake yani nikipita lazima wageuke afu nilivyokua najua kutembea kwa mikogo ndio balaa

basi baada ya kufika njombe nilipokelewa na shangazi ambae alifurahi sana kuniona asijue mwenzie nimekuja kwenye mawindo mie

Shangazi yangu hakua mtu mzima sana alikua na miaka k**a thelathini na nane na pia hakua na mume licha ya kua na watoto watatu ambao kila mtu alikua na baba yake


kwa harakaharaka tayari nilijua mauchafu yangu nilirithi kwa shangazi bwana!!!

yaani hizi tabia ambazo kila siku mama alikua ananisimangia na kuniuliza nomerithi wapi nilijipa jibu buana izi tabia ninerithi kwa shangazi sio bure hahaha nacheka k**a mazuri

basi maisha ya kwa shangazi yalianza bwana, mie sio mvivu ivyo nilikua namsaidia sana shangazi kazi za uzazi na kuangalia watoto wake maana alikua amejifungua kwa upasuaji ivyo hakua anaweza kufanya chochote

Shangazi alinipenda sana na alijikuta ananifanya kua shoga ake na akaanza kunieleza maujinga yake hahaha

aliniambia kua eti yeye hawezi kua na mwanaume mmoja na ndio maana ana watoto watatu na baba tofauti tofauti na hiyo ninkwasababu wanaume ni watamu sana ivyo katika umri wake yeye anaona bado sanaaa na ataonja kila ladha ivyo anatarajia kuwa na idadi kubwa sana ya wanaume yaani shangazi hahahaha

mimi nilijua katika maajabu saba ya dunia ajabu la nane ni mimi pekee kumbe kuna na shangazi bwana uwiii sio siri tunafanana sana

sasa baada ya kipindi kirefu kwa shangazi ndio nikaanza kuwajua baba watoto zake maana walikua wanakuja pale nyumbani kwa zamu na kwa kipindi hicho shangazi alikua ameshapona na mtoto alienda miezi tisa ivi hivyo alimuachisha kunyonya na alikua anawapa wanaume wake mapenzi kwani nilishangaa mie na ndio mambo yangu hayo wala aikushangaa

Shangazi alonotambulisha kwa hao wanaume zake kwa kuwaambia mimi ni mtoto wa kakake na nimefanana nae sana ivyo ananopenda sana

Mnazani niliwaacha sasa hawa wame wa shangazi hataa! walinila bwana yaani nilihakikisha nimefanya nao ngono wote bila ya wao kujua k**a nawachanganya na shangazi alikuja kugundua bwana baada ya mtoto wake mkubwa kumwambia maana nilivyo mshenzi nilikua nafanya matusi huko huko ndani ya nyumba ya shangazi qe huogopi

Baada ya shangazi kujua alinitimua kwake kwa kipigo kitakatifu hahaha

Mwenzenu nilitimuliwa k**a mbwa uwiii

yaani iyo siku ndio nilijua shangazi hana masihara kwenye kuingiliwa kwenye tamu zake maana ni alinitwanga mno yaani alinibonda mpaka nililia kwa sauti maana nilikua najikaza kuepusha aibu maana kwa shangazi palikua ni barabarani ivyo watu wangesikia nikilia wangekuja ivyo nilikua nalia kimya kimya ila kipondo kilipokolea uwiii nililia kwa sauti iyooo

yani alikua ananipiga huku ananichana na makucha usoni na kinifinya kila mahala mwenzenu umalaya ulinitokea puani

mimi napigana sana mtaani kutokana na kugombea mabwana na siku nyingine napigwa na mabwana zangu baada ya kuwagonganisha ila kwa kile kipondo cha shangazi nikiri sikuwahi kutana nacho

baada ya kupigwa sana shangazi alinisukumia nje na matusi ya nguoni

yani ni allikua anatukana jamani uwiiii

afu uko nje kulikua na baridi sana si mnajua baridi la iringa yani ni balaa na sikua nimevaa nguo nzito na miguuni nilikua miguu peku jamani

shangazi alinifukuza mpaka barabarani yani alinitimua kabisa karibu na nyumba yake huku ananiambia nikafie mbele huko maana mimi ninmalaya sana alishasikia habari zangu hivyo alikua anajua ivyo ila hakujua ni kwa kiwango kikubwa hivi

basi nilijiokota kwa aibu nikajisogeza barabarani natia huruma utazani nimeaingiziwa kumbe kweli tupu

k**a masihara bwana nililikua nimefukuzwa na ulikua ni usiku wa k**a saa tano hivi

nilichekecha akili yangu na jikafanya maamuzi ya kwenda kwa mangi ambae alikua nimmoja wa mabwana zangu

huyu mangi alikua na duka la chakula pale mtaani ivyo niliona ili nipate malazi na nauli ya kurudi Lindi ebu niende nikamtunuku kitumbua akipigee aaah si ni bwanangu bwana kuliko nibakwe na wakulima huku wakile bure

nilitaka nauli ya kurudi lindi mimi maana ndo kwashangazi nishafukuzwa bora nirudi lindi ambapo nimepazoea bwana


SOMA YOTE KABISA INBOX KWA 1000 TU

LIPIA 0658589666 Salma majala

Kisha njoo inbox 0695786227

JIUNGE NA WASP CHANNEL ILI KUPATA STORY NYINGI ZAIDI BONYEZA LINK TWENDE SAWA

https://whatsapp.com/channel/0029VbD0wn347XeJfcaZpf2b

31/07/2026

LUCKY __24

Mwandishi :Malkia Osam

Roho ilimuuma Lucky kuambiwa hajawahi kumvutia Innocent aah alikaa kimyaa akainamia meza ...

Kichwani picha ya Innocent tangu mara ya kwanza kumuona kulee hospitali walipo kuwa wakigombania Begi lenye pesa, Akawaza Moments zote akajikuta moyo wake una amani na kusahau upuuzi wote wa Rose ..

Lucky alihisi anampenda sana Innocent lakini sio kimapenzi hayupo huko kabisa ila anamkubali tu ..

Gafla tu furaha yake ikapotezwa na kile kilichotokea nje dakike chache zilizo pita , Akajikuta mwili wake wote unaingiwa na baridi ,Maneno makali ya Innocent na vile hakumjali kabisa Rose .

Mmh alijikuta anajisikia vibaya sana k**a mwanamke ,akainuka ili kwenda kuongea na Innocent k**a siku ingine likatoa la hivyo basi anapaswa kuwa upande wa mke wake hata k**a.mkewe ana makosa hatakiwi kumfokea vile tena mbele ya Adui yake ...

Hatua za Lucky ziliishia mlango wa ofisi ya Innocent. kabla hata hajabisha hodi kuingia,Sauti ya Rose ndio ilimfanya akasita kuongeza hatua ingine alikuwa akiongea kwa ukali na sauti ya juu ...

"Sitaki kusikia lolote Innocent Naomba Taraka yangu nataka Taraka yangu Full Stop....!!"

"Rose....yaa.. yani kwa kipi haswa hadi unadai taraka kwanini!!!"

"Kwasababu ya Yule malaya wako ,ulie muona wa maana kuliko mimi !!"

"Rose....!!!"

"Nipe Taraka yangu Innocent, Natoka naenda kumpigia simu baba Tutakutana mahak**ani !!!" Rose alipiga Bonge w U_turn kuondoka bila hata kutazama nyumaa .

Lucky aliona hii ngoma ngumu, hatimae amekuw sababu ya Migogori ya ndoa ya mtu, alipo sikia hatua za Rose kutoka alikimbia akajibana upande mwingine ,Rose alitoka akafata Innocent ambae alikuwa anajitahidi kumtuliza hasira zake ....

Lucky hakuona hata k**a ana stahili kwenda kuongea na Innocent tena alijivuta taratibu ,Wakati anakaribia ofisini kwake alimuona Rose akiondoka kabisa Hapo hospital, Alijikuta mpaka Chozi linamtoka na kujiona ana mkosi mkubwa sana mpaka sasa ...

Alirudi ofisini kwake akili yake imekubali ni bora tu aache kazi hakuna Njia ingine kabisa ...
Alitoa Ma file yoote ya kazi kuweka Taarifa sawa za wagonjwa wote hakutaka kuacha kiporo na alipanga leo ndio iwe siku ya mwisho kuja kazini wacha aendelee kutafuta kazi sehemu ingine k**a atapasa sawa akikosa pia sawa bwana ...

Lucky alifanya kazi hata muda wa kutoka kazini hakutoka kazi zilikuwa bado nyingi kuna taarifa nyingi za wagongwa hakuwa ameziweka kwenye system ,Mikono ilichoka kujaza Kwenye computer lakini hakuwa na jinsi ...

Mpaka wanaingia wenye zamu ya usiku yeye alikuwa bado ana kazi na hakutaka kabisa kusema kuwa anaacha kazi ...

Innocent alikuwa amechoka akili ndani ya ofisini yake mpaka muda huu hakuwa na hamu kabisa ya kurudi kwake badi haelewi mkewe amekubwa na Pepo gani ...


Kwa nafasi kubwa alikuwa akimfikiria Lucky, msichana mpole sana tena mwenye heshima zake. Hakuwahi kuona dalili yoyote ya yeye kutaka kuharibu ndoa yake, lakini mambo yalikuwa yameenda mbali kuliko alivyotarajia.

Alivuta pumzi ndefu na kutazama saa ukutani,alihisi kumuona Lucky kuanzia siku ya kwanza kumuona ,Ukaidi wake wa kung'ang'ania begi ulimfanya acheka kwa nguvu ,Alipo kumbuka alimuacha nje ya mji peke yake bila msaada wowote akajikuta anaumia sana ..



"Aah Mungu wangu..." alinong'ona peke yake huku akichukua simu yake ,Alitafuta jina la lucky akini alisita kidogo kumpigia kuna maneno ya Lucky yalipita kichwani kwake yakalarua moyo wake akajikuta anakosa raha gafla ,akacheka cheko dogo la uchungu

(Mi sio type yangu yule ,Sio kati ya wanaume wanao nivutia yaani k**a unaniwazia huko pole sana....!!!" )

"Soo!!!.... Anapenda aina gani ya wanaume!!! Kumbe naonekana hivyo mbele yake!!??" Akainuka kwenye kiti chake ,Akajikuta anafikirisha akili yake sana kumjenga Boyfriend wa Lucky ,Yaani ni mwanaume wa aina gani huyo yupojee..

Alitamani kumpigia alipo tazama saa ya simu yake ,eh alijikuta anashtuka baada ya kujua ni sa 7 kasoro usiku , yaani hata hajui huo muda umekimbia vipi mpaka kufikia hapo .


"Mungu wangu, Huyu Rose atajielewa kweli huyu mwanamke!!!" Alichukua koti lake haraka kutoka yaani mwenyewe alishangaa huu muda bado awe yupo Ofisini.
Alitembea haraka harakaa ,Kwa bahati mbaya au nzuri alikutana na Ness ambae alishangaa kuona Boss wao mpaka muda huu bado yupo Hospital .

"Leo ajabu ,Mmeamua kufanya kazi Over Time!!!"

"Tumeamua!!?? Na nani!!??" Innocent alipunguza mwendo kidogo akamkazia macho huyo Muuguzi

"Doctor Lucky nae mpaka sasa bado yupo ofisini!!!"

"Mmh!!!" Innocent aliguna kidogo huku akigeuza uso wake kutazama upande ambao Ofisini anayoitumia Lucky ipo

"Anafanya nini.?" Akamtupia swali huyo shost mwingi wa habari .

"Mmmh sijajua ila anakazi !!!"

"Okay!!!" Innocent aligeuza kurudi alipo Lucky tena kwa mwendo wa haraka haraka

"Kwanini huyu bado hajaondoka?" alijiuliza huku akiongeza mwendo kwenda huko ...

Alipofika alikuta mlango ukiwa wazi kidogo.

Lucky alikuwa ameinamia kompyuta, vidole vyake vikitembea taratibu kwenye keyboard. Macho yake yalionekana mekundu kana kwamba alikuwa amelia.

Swala la kuacha kazi sio k**a alilifurahia Ila ilibidi tu akubali kuacha kazi kwa sababu ya haya yanayo endelea , alilia mwenyewe karibu siku nzima huku akimlaumu mungu kwanini hampi kupumua licha ya kusoma kwa bidiii lakini bado elimu yake haithaminiwi kabisa .

Innocent alisimama mlangoni kwa sekunde kadhaa akimtazama bila kusema kitu.

"Mbona bado hujaenda nyumbani?" aliuliza kwa sauti ya upole huku akivuta hatua za Taratibu kumsogelea .

Lucky alishtuka kidogo.

"Aah... Daktari Innocent... nilikuwa namalizia taarifa za wagonjwa."

"Inafika saa ngapi sasa?"

Lucky akatazama saa.

"Nilikuwa sijagundua muda umeenda sana."

Innocent akavuta kiti na kukaa karibu yake.

"Una uhakika ni taarifa za wagonjwa tu zinakufanya ubaki mpaka muda huu?"

Lucky alinyamaza.Kimya kilitanda kwa sekunde kadhaa.

Mwishowe akafunga macho na kuvuta pumzi ndefu.

"Naomba unisamehe Daktari."

"Kukusamehe kwa kosa gani?" Innocent akajiweka vizuri kumtazama kwa makini .....

Lucky kaona bora aachane na hii Kazi kabisa, Je Innocent atamruhusu aache ??

HAKIKISHA UNAJIUNGA NA WASP CHANNEL KUPATA MIENDELEZO YA STORY NYINGII

https://whatsapp.com/channel/0029VbD0wn347XeJfcaZpf2b

30/07/2026

LUCKY __23

Mwandishi :Malkia Osam

Rose aliona k**a kadharauliwa kwa maneno aliyoongea Lucky kwake ilikuwa k**a dharau , Alivuta hatua ndefu nyuma ya Luck akayavuta ma nywele kwa nguvu kumvuta kwa nyumaa

"A_aaah !!!" Lucky alijikuta anapiga kelele huku akirudisha mikono yake nyuma haraka kujisaidia ...

"Mungu wangu.... We Rose!!!??" Hee!! Innocent alishangaa kwa hii movie ya ajabu inayochezwa na mkewe hapa

"Hivi we upojee!!!??" Innocent alishindwa kabisa kuzuia hasira zake , Mwili wote alijikuta unamtetemeka kwa hasira sababu ya huo ujinga anao ufanya Rose .

Alihisi hata mkewe anaweza kuwa na akili ndogo kabisa .. akamsukuma pembeni kwa nguvu ,Rose akaenda kugonga kichwa chake kwenye ukuta .

Nguvu aliyo itumia Innocent kumvuta na kumsukuma Rose ilikuwa kubwa sana

"Vipi Lucky!!!??" Innocent hakuwa na wazo la Rose zaidi alimuwahi Lucky, Kabla Lucky hajajibu aligeuka kumtazama Rose ndipo akakuta Rose anahaha baada ya kushika damu kwenye mkono wake ambazo zilikuwa zinatoka eneo la kichwani .....

Alikuwa anaangalia kwa mshangao yaani haamini kabisa kuwa mume wake huyo alomuita kipenzi ndie kampigiza ukutani halafu mbaya zaidi ,amemkimbilia mwanamke mwingine aisee ,Rose hakuamini

"Haa!!! Innocent mke wako!!!'" Lucky alishtuka sana kuona Rose anatoka Damu yaani aliogopa , Innocent nae akageuka kumtazama Mkewe , kwanza akashusha pumzi za hasira

"Innocent..." Rose akamuita kwa sauti iliyojaa huzuni, innocent hakuitika alishika paji lake la uso kuonesha kachoka na haya mambo ..

Akageuka kumtazama tena Lucky, Akili yake yote ilikuwa kwa Lucky ambaye bado alikuwa ameshika kichwa chake kwa maumivu baada ya kuvutwa nywele kwa nguvu.

"Vipi Lucky, umeumia sana?" Innocent aliuliza kwa wasiwasi.uwiiii Rose alihisi kupasukaa
"Khaa .... innocent!!!???' Yaani aliyatoa macho kwa mshangao hakuamini hakuamini heheh yaani ni k**a kasalitiwa akiwa kwenye nchi yake mwenyewe ..

"Niko sawa baba, usijali..." Lucky akajibu haraka haraka tena kwa woga huku macho yake bado yakimtazama Rose .

Dakika hiyo ukimya mzito ulitawala ,zaidi ya upepo hakuna sauti ilisikia

Rose alihisi moyo wake ukichanika vipande vipande. Hakutarajia hata kidogo kwamba Innocent angemkimbilia Lucky kwanza na kumwacha yeye akiwa anavuja damu.

"Kwa hiyo mimi sina maana tena kwako?" Rose aliuliza kwa sauti ya majonzi.

Innocent akageuka na kumtazama.

"Rose, umefanya nini sasa? Hivi unajielewa kweli?" alisema kwa hasira.

"Nilikuwa namlinda Mume wangu!!!"

"Kumlinda dhidi ya nani? Lucky hajakufanyia chochote! Siwezi kutembea na huyu mwanamke mimi ni mpuuzi gani amekwambia huyu kapata kazi kwa sababu ya kutoa rushwa, Hivi Rose unaakili kweli wewe ,nakuiliza unaakili ... mwanamke mjinga sijawahi kumuona ... Tena nisikie na unielewe saw wewe sina hisia na huyu mwanamke na kamwe siwezi kutembea nae hata k**a ningekuwa sijaoa Elewa nakuheshimu sana ila huna maana SIJAWAHI KUVUTIWA NA HUYU MWANAMKE HATA SIKU MOJA MPUUZI WEWE!!!....." Innocent alitoa zile hasira za ndani kabisa macho yalikuwa makubwa gafla ule uso mzuri wa upole hata sijui ulipotelea wapi alikuwa Innocent mwingine kabisaa hata Lucky hajawahi kumuona ,Alikuwa anaongea huku kamnyooshea kidole Rose tena kwa sisitizo sanaa hakuwa na utani ,Pumbavu mwanamke mjinga huyu wivu wivu tu .

"Unataka kuniambia kila mtu ni adui yako? Kila mtu anayekuzunguka ana makosa isipokuwa wewe? Mwache huyu mwanamke awe na amani na kunzia sasa kuanzia sasa Rose sitaki umsumbue Rose sitakii!!!...."

Rose alibaki kimya.

Kwa mara ya kwanza machozi yakaanza kumtiririka. Hakulia kwa sababu ya jeraha la kichwani, bali kwa sababu alihisi kupoteza nafasi yake ndani ya familia yake mwenyewe.

Rose alimtazama Innocent anaondoka bila hata kujua kaumia Vipi , hili lilimuumiza sana Rose sanaa .

Lucky naye alihisi hali ile inamuumiza. Hakuwahi kutaka kuwa sababu ya ugomvi kati ya wanandoa,Alijisikia vibaya alitamani kumsemesha Rose ajue hata kaumia Vipi lakini hakuona k**a ile ni nafasi yake ..

Nae akaondoka kurudi ofisini kwake , wakamuacha Rose akiwa mwenyewe ..

Lucky alijikuta Ofisini hapakaliki tena Kitu kichungu akabaki kuzunguka kila pembee ,Picha nzima ya lilotokea huko nyuma iligoma kabisa kutoka...

"Kwahiyo innocent ... kasikia kila kitu ndo mana amejua mkewe alisema nimetoa Rushwa au walilijadiri hili zamani....Mungu wangu ooooh ,balaa gani hiliii .......

A_aaah Mungu wangu Mambo yanayonitokea na Jina langu ni tofauti!!" Lucky alijitupa kwenye kiti k**a mzigo ...

(...._SIJAWAHI KUVUTIWA NA HUYU MWANAMKE HATA SIKU MOJA MPUUZI WEWE!!!_....) kati ya maneno yooote aliyoongea Innocent hili neno liligoma kabisa kutoka kichwani kwa Lucky yaani lilikuwa linapasua moyo wake zaidi ya Radi ...

Alijikuta anasogea karibu na kioo akajitazama kwa makini akajikagua akiwa k**a bint .

"Ni kweli nina mkosi kiasi hiki ,sivutii mh!!!"

HAKIKISHA UNAJIUNGA NA WASP CHANNEL KUPATA MIENDELEZO YA STORY NYINGII

https://whatsapp.com/channel/0029VbD0wn347XeJfcaZpf2b

29/07/2026

LUCKY __22

Mwandishi :Malkia Osam

Japo Innocent alikuwa na Uchovu wa siku nzima ilibidi tu ajilazimishe kumpa mkewe haki yake ...

Usiku huo ukawa mtamu zaidi kwa Rose japo Innocent hakwenda mbio za maana ilikuwa ni papapapaa waah yaani alikimbia Mbio fupi k**a mwizi mpya mjini chap tu akanaswa na kuuawa hakuwa na shuhuri tena ...

"Asante mume wangu ,Ujue nime enjoy..." Rose aliongea kwa sauti ya kukoleza nyege huku akipitisha mkono wake kupita kiuononi kwa Innocent ...

"Hmmm!!!!...." Innocent hakuwa na neno aliushika ule mkono huku akiupapasa kimahaba bila kuongeza neno ...

asubuhi k**a kawaida Lucky alikuwa anawahi sana kufika kazini ...

Wakati Innocent na mkewe wanaingia Lucky alikuwa akitoka ofisini kwake kuelekea kwenye chumba cha mgonjwa wake.
Macho ya Innocent na Lucky yalipo kutana kila mmoja alijikuta anatabasam bila hata kupanga .

"Habari Boss, Habari Madam!!" Lucky alisalimia huku akiendelea kuchanua Tabasam k**a kawaida Innocent ndie aliejibu kwa bashasha lakini Rose alisonya tu tena kwa sauti ya Juu ...

"Mke wangu!!!" Innocent akabaki kumshangaa Rose wakati huo Luck hata hakujali yeye aliendelea na safari yake.

Baada ya Lucky kufungua mlango na kuingia ndani ya chumba aliufunga na kuegamia mlango , Kwanza alishusha pumzi ndefu ya kuchoka, Sio k**a alikuwa haoni visa vya Rose hapana , Vilimuumiza sana tu ila alichagua kujifanya haoni ukweli moyoni alikuwa anakerekw sana na hiyo tabia ....

"Huyu mwanamke sijui kwanini hanipendi jamani!!!" Akajiuliza moyoni huku akifungua jarada la mgonjwa ...

Baada ya kumalizama na Mgonjwa , aliamua kwenda kuongea na Rose moja kwa moja labda kuna kitu anaweza kurekebisha ..

Rose alikuwa akiendelea na majukumu yake k**a kawaida ,baada ya kumuona Lucky hasimu wake akasimama wima alimtazama k**a anauliza jambo

"Samahani Da rose ,Nilikuwa naomba tuongee kidogo!!!"
Rose hakujibu kitu aliinuka tu japo neno dada lilimkera sanaa Rose ,Yaani huyu Lucky anajikuta mtoto wa afu mbili au?? Mxeuw .

Walisogea pembeni kidogo ya jengo sehemu ambayo hapakuwa na watu.

"Da...."

"Wee!!! Wewee....!!!" Rose alimnyooshea kidole kwanza hilo neno dada yaani Dada lilikuwa likimvurunda akili Rose mpaka kichaa chake kinataka kupanda .

"Da..nyokoo.."akabana pua moja huku akigeza sauti ya Lucky "Komaa we bint mi sio dada yako... haya ongea haraka haraka nina wagonjwa pale !!!"
Lucky akaona hii issue hii ni serous sana aisee, akalazimisha tu tabasam maana alitaka amani na sio vita na hata hajui kwanini anamkasirikia sana Huyu mwanamke ...

Kwa bahati nzuri au mbaya bwana ,Innocent alikuwa akitoka kuelekea upande wa maabara ambapo ndio upande walipo wao ..

Ile anatokeza tu hivi akakutana na kisanga cha Rose kikimwambia Dada ya Nyoko ,Innocent akasikilizia maana hakuelewa hapa kuna nini na kwanini waje nyuma huku ....

Basi Lucky hata hakuonesha makuu bint wa watu , akamtazama Rose bado uso wake ukiwa na Nuru

"Samahani ,Madam nimekuita huku , Nilikuwa naomba unisamehe sana k**a kuna sehemu yeyote niliyokosea ,au nambie wapi nakosea ili nitengeneze maana sio vizuri tunafanya kazi wote kisha tunakuwa na ugomvi ugomvi sio vizuri haileti picha nzuri Madam!!!"

"Hmm!!! Mxeuw!!!" Rose akasonya huku akijitengeneza vizuri kusimama ..

"We Bint ...sikupendi tu yaani ndo imetokea sikupendi ..So k**a unaweza Ungeacha tu kazi my dia!!!"

"Kuacha kazi ni kitu kisicho wezekana ...! Yaani kuacha tu kazi kwa sababu wewe haunipendi sio kweli.... ila k**a kuna kitu naweza kurekebisha nitafanya hivyo... nimetafuta kazi kwa miaka mingi sana...imekuwa k**a bahati kwangu nimepata hata mshahara wa kwanza sijashika unambie niache kazi ili kukuridhisha wewe hapana!!!""

"A__aaah kwahiyo ni kweli ulitoa rushwa ya Ngono ili upate kazi sio!!??"

"Ninii!!!??" Lucky alishangaa kidogo jambo alilolopoka Rose

"Ulilala na Mume wangu ili tu akupe kazi sio ,nakuona unavyomchekea chekea maraya wewe hayawani kuja kutia nuks kwenye ndoa za watu tu .....!!!"

"Khaaa!!! Rosee!!! Itakuwa umekosea mpenzi ,Siwezi kulala na Innocent hata k**a angekuwa hajakuoa ,Mi sio type yule ,Sio kati ya wanaume wanao nivutia yaani k**a unaniwazia huko pole sana....!!!"
Lucky aliona hapa anaongea na kichaa ngoja akaendelee na kazi zake .. Hakufanikiwa kupiga hata hatua mbili alivutwa nywele na Rose nusu aanguke chini ...



HAKIKISHA UNAJIUNGA NA WASP CHANNEL KUPATA MIENDELEZO YA STORY NYINGII

https://whatsapp.com/channel/0029VbD0wn347XeJfcaZpf2b

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salaam