Afya yangu

Afya yangu

Share

Tunasaidia watu kuondokana na changamoto za kiafya hususa ni magonjwa yasiyoambukiza.

29/12/2023
Photos from Afya yangu's post 10/12/2023

Vipi ufanye kuongea damu mwilini? 🤏👇👇👇👇👇👇Kwa mawasiliano

0629623538

14/11/2023

⏺️VIASHIRIA VYA UPUNGUFU WA VITAMIN C MWILINI

➡️VIASHIRIA vya upungufu wa vitamini C vinaweza kujumuisha uchovu, michubuko rahisi, na ukak**avu wa ngozi.

➡️Unaweza kuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa na upungufu huu ikiwa una magonjwa fulani, ikiwa ni pamoja na anoreksia.

➡️Vitamini C ni kirutubisho muhimu ambacho kinapaswa kutumiwa mara kwa mara ili kuzuia upungufu huo

▶️Sababu kuu za hatari ya upungufu wa vitamini C ni lishe duni, ulevi, anoreksia, ugonjwa wa akili, uvutaji sigara na usafishaji damu.

▶️⏺️Ingawa dalili za upungufu mkubwa wa vitamini C zinaweza kuchukua miezi kadhaa kusitawi, kuna dalili za hila za kuangalia.

⏺️Ngozi mbaya, iliyo kak**avu

⏺️Vitamini C ina jukumu muhimu katika utengenezaji wa kolajeni, protini ambayo iko kwa wingi katika tishu zinazounganishwa k**a ngozi, nywele, viungo, mifupa na mishipa ya damu.

⏺️Viwango vya vitamini C vinapokuwa chini, hali ya ngozi iliyokak**aa inaweza kutokea nyuma ya mikono, mapaja au matkalio kutokana na mkusanyiko wa protini ya keratini ndani ya vinyweleo.

⏺️▶️Nywele za mwili zilizokunjamana

Upungufu wa vitamini C pia unaweza kusababisha nywele kukua katika umbo lililopinda au lililokunjamana kutokana na kasoro zinazojitokeza katika muundo wa protini wa nywele zinapokua.

Nywele aina hii ni mojawapo ya ishara mahususi za upungufu wa vitamini C lakini huenda zisiwe dhahiri, kwani nywele hizi zilizoharibika zina uwezekano mkubwa wa kukatika.

⏺️Wekundu kwenye vinyweleo

Hali hii husababishwa na mishipa mingi ya damu ambayo hutoa damu na virutubisho kwa eneo hilo.

⏺️Mwili unapokuwa na upungufu wa vitamini C, mishipa hii midogo ya damu inakuwa tete na kukatika kwa urahisi, na hivyo kusababisha madoa madogo yenye rangi nyekundu kutokeza karibu na vinyweleo.

Hii ni ishara ya upungufu wa vitamini C.

⏺️Kuchubuka kwa urahisi

Michubuko hutokea wakati mishipa ya damu chini ya ngozi hupasuka, na kusababisha damu kuvuja katika maeneo kadhaa.Michubuko rahisi ni ishara ya kawaida ya upungufu wa vitamini C kwani uzalishaji duni wa kolajeni husababisha mishipa dhaifu ya damu.

Michubuko inayohusiana na upungufu inaweza kufunika sehemu kubwa za mwili au kuonekana k**a vitone vidogo vya zambarau chini ya ngozi.

⏺️⏹️Majeraha kupona polepole kupindukia

▶️Maumivu ya viungo yanayohusiana na upungufu wa vitamini C, mara nyingi huwa makali ya kutosha kusababisha kuchechemea au ugumu wa kutembea.

⏺️Kutokwa na damu ndani ya viungo kunaweza pia kutokea kwa watu ambao hawana vitamini C, na kusababisha uvimbe na maumivu ya ziada.

▶️Kutokwa na damu kwenye fizi na kupoteza meno

▶️Bila vitamini C ya kutosha, tishu za ufizi hudhoofika na kuvimba na mishipa ya damu huvuja damu kwa urahisi Zaidi.

▶️Kinga duni

▶️Upungufu wa vitamini C unahusishwa na kinga duni na hatari kubwa ya kuambukizwa, pamoja na magonjwa hatari k**a nimonia.

⏺️Anemia ya upungufu wa madini ya chuma unaoendelea

Vitamini C na anemia ya upungufu wa madini mara nyingi hutokea pamoja.

⏺️Dalili za upungufu wa madini ya chuma ni pamoja na kupauka, uchovu, kupumua kwa shida wakati wa mazoezi, ngozi kavu na nywele na maumivu ya kichwa.

Viwango vya chini vya vitamini C vinaweza kuchangia upungufu wa anemia ya chuma kwa kupunguza ufyonzwaji wa madini ya chuma kutoka kwa vyakula vinavyotokana na mimea na kuathiri vibaya kimetaboliki ya madini ya chuma.

Upungufu wa vitamini C pia huongeza hatari ya kutokwa na damu nyingi, ambayo inaweza kuchangia anemia.

Je lipi suluhisho la tatizo hili
Tumia matunda ambayo yanavirutubisho vya vitamin C ili kuitunza afya yako.

KWAMAWASILIANO .0629623538

Photos from Afya yangu's post 14/11/2023
Photos from Afya yangu's post 14/11/2023

Zingatia kula matunda ili kuukinga mwili n magonjwa pia kuupa mwili nguvu. 0629623538

Photos from Afya yangu's post 21/09/2023

ZIJUE DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kutokuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.

Tatizo hili huwanyima sana watu raha na kupelekea kuwa na mawazo, migogoro katika mahusiano. Watu wenye changamoto hii mara zote wanahitaji dawa zisizo na madhara (virutubisho lishe) vilivyotokana na mimea na matunda na kubadilisha mitindo yao ya kimaisha (lifestyle changes) ili kuweza kurudisha hali zao na kuondoa tatizo.

Dalili Za Upungufu Wa Nguvu Za Kiume:
Zifuatazo ni baadhi ya dalili za upungufu wa nguvu za kiume;

1) Kukosa Hamu Ya Kufanya Tendo La Ndoa.
Tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa mwanaume ni mojawapo ya dalili za upungufu wa nguvu za kiume na linaweza kusababishwa na sababu nyingi sana. Sababu hizo zinaweza kuwa za kimaumbile au kisaikolojia au za mchanganyiko wa sababu za kimaumbile na sababu za kisaikolojia. Baadhi ya sababu za tatizo hili ni pamoja na;

a) Msongo Wa Mawazo (Depression).
Msongo wa mawazo ni ugonjwa wa kisaikolojia unaohusisha hali ya kuwa na mawazo makali kwa muda mrefu yanapelekea kukosa raha kutokana na kujihisi si mtu wa thamani au kukosa starehe katika vitu ulivyozoea kuvifanya na kukufurahisha hapo awali. Mawazo ya namna hii huathiri mwenendo wako wa maisha yako ikiwa ni pamoja na kukosa matamanio ya kimapenzi.

b) Matumizi Ya Madawa Na Pombe.
Matumizi ya baadhi ya madawa na unywaji wa pombe wa kupindukia vinaweza kupelekea tatizo hili la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa. Madawa yanayochangia tatizo hili ni pamoja na; Madawa ya presha ya kupanda (Anti hypertensive drugs), madawa ya kuondoa msongo wa mawazo, madawa yote yanayozuia ufanyaji kazi au uzalishaji wa testosterone kwa mfano cimetidine, finasteride na cyproterone n.k

c) Mawazo Mengi Na Uchovu.
Matatizo ya kikazi na hadhi yako kazini vinaweza kuchangia kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa.K**a unabezwa sana kazini na kujiona hutimizi kazi yako ipasavyo au k**a unachoka sana kazini pia vinaweza kupelekea kukosa hamu ya kufanya mapenzi pindi urudipo nyumbani kwani mahusiano ya kimapenzi yanahitaji yatengewe muda wa kutosha.

d) Kuwa Na Umri Mkubwa.
Kiwango cha homoni ya testosterone inayohusika na hisia za kimapenzi kwa mwanaume hupungua kwa asilimia 1-2 kila mwaka kadri mwanaume anavyozidi kuwa na umri mkubwa. Kiwango cha testosterone kikishuka katika mwili wa mwanaume humfanya asiwe na nguvu, ashindwe kutuliza mawazo kwenye jambo alifanyalo na apoteze hamu ya kufanya mapenzi.

e) Mahusiano Yaliyopo Baina Ya Mwanaume Na Mwanamke.
Matatizo ya kimahusiano kati ya mwanaume na mwanamke yana mchango mkubwa sana katika kusababisha tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa, mfano uwepo wa migogoro kati ya mume na mke, ukosefu wa amani na furaha katika mahusiano huchangia sana mwanaume kukosa hamu ya kufanya mapenzi.

K**a mahusiano yako na mpenzi wako yamekuwa ya miaka mingi sana, unaweza kuwa umemzoea mno mkeo kiasi kwamba ukaanza kukosa hamu ya kufanya naye tendo la ndoa. Hili nalo hutokea mara nyingi.

f) Matatizo Ya Kiafya.
Matatizo ya kiafya ya muda mrefu (chronic diseases) husababisha kupungua kwa hamu ya kufanya tendo la ndoa mfano tatizo la kisukari, tatizo la presha, tatizo la moyo, tatizo la kansa ya muda mrefu, na hali ya kuwa na unene uliozidi kiwango (obesity) n.k

2) Kutokuwa Na Uwezo Wa Kurudia Tendo La Ndoa Zaidi Ya Mara Moja.
Mwanaume mwenye changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume akishakamilisha mshindo mmoja wa tendo la ndoa basi anakua hana uwezo tena wa kurudia mshindo mwingine. Hali hii husababishwa na kutokuwepo na mshukumo wa damu wa kutosha kwenye mishipa ya uume.

3) Kutokuwa Na Uwezo Wa Kusimamisha Uume Kabisa.
Kwa kawaida uume wa mwanaume aliyekamilika (rijali) unaposimama, hutakiwa kuwa imara k**a msumari, lakini kwa mwanaume mwenye changamoto ya upungufu za nguvu za kiume uume wake hata ukisimama hubakia kuwa lege lege na unaweza kusinyaa wakati wowote.

Tatizo hili ni matokeo ya kulegea kwa mishipa ya uume ambayo ndio huufanya uume usimame barabara.

4) Kuwahi Kufika Kileleni.
Kuwahi kufika kileleni ni hali ambayo inampata mwanaume mwenye changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume ambapo hutoa shahawa kabla ya kuanza tendo la ndoa au muda mfupi tu baada ya kuanza tendo la ndoa, bila yeye mwenyewe kukusudia. Kwa kawaida mtu mwenye tatizo la kuwahi kufika kileleni hutoa mbegu zake za kiume hata baada ya maandalizi kidogo sana.

5) Kuchoka Sana Baada Ya Tendo La Ndoa Na Hata Kukinai Kabisa/Hata Kusikia Kichechefu.
Hii ni moja wapo ya dalili za upungufu wa nguvu za kiume. Hali hii huwapata wanaume wenye changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume ambayo wakati mwingine huambatana na usingizi mzito (Kulala fofofo).

6) Kuhisi Maumivu Wakati Wa Tendo La Ndoa/Baada Ya Tendo La Ndoa.
Hii pia ni moja wapo ya dalili za upungufu wa nguvu za kiume, hali hii huweza kuchangiwa na kauthirika kwa tishu za uume ambazo hutokana na upigaji wa punyeto kupita kiasi.

7) Kuchelewa Sana Kufika Kileleni/Kushindwa Kufika Kileleni Kabisa.
Ni ile hali ya mwanaume kuchukua muda mrefu kutoa manii wakati wa kushiriki tendo la ndoa.

Namba yakujikinga na tatizo hili.

1. Kula Lishe Bora.

Chakula unachokula kina mchango mkubwa katika kutibu tatizo la kuwa na kiwango kidogo cha mbegu za kiume(Low s***m count). K**a utarekebisha tu aina ya chakula unachokula kunaweza kupelekea kutibu changamoto ya kuwa na kiwango kidogo cha mbegu za kiume ambapo unashauriwa kupunguza matumizi ya sukari na vyakula vya ngano, badala yake ongeza zaidi matumizi ya matunda, mboga mboga. Hii inaweza kukusaidia kutibu tatizo la kuwa na kiwango kidogo cha mbegu za kiume kwa haraka sana.

Aina za matunda
2. Epuka Matumizi Yaliyokithiri Ya Vyakula/Vinywaji Vyenye Kafeini Kwa Wingi.

K**a unasumbuliwa na tatizo la kuwa na kiwango kidogo cha mbegu za kiume ni vyema ukaepuka matumizi yaliyokithiri ya vyakula au vinywaji vyote vyenye kafeini kwa wingi. Mfano wa vyakula/vinywaji vyenye kafeini kwa wingi ni pamoja na chai ya kahawa, soda nyeusi zote, malta, redbull, chokoleti n.k

chai ya kahawa
3.Tumia Kitunguu Swaumu Kwa Wingi.

Kitunguu swaumu kina ‘Selenium’ na pia kinasaidia kuondoa sumu mwilini, mambo haya mawili muhimu yanasaidia kuongeza spidi ya mbegu za kiume. Pia kitunguu swaumu kina ‘Allicin’ ambayo husaidia kuongeza msukumo wa damu kwenda kwenye uume. Hivyo unashauriwa kuongeza matumizi ya kitunguu swaumu kwenye chakula unachopika. Vile vile unaweza kutafuna punje 2 mpaka 3 za kitunguu swaumu kila unapoenda kulala au unaweza kukatakata (chop) hizo punje 2 au 3 vipande vidogo vidogo kisha unywe na maji.

kitunguu swaumu
4. Ulaji Wa Ndizi.

Ndizi ni chakula kizuri kwa ajili ya afya ya uume wako. Ndizi zina kimeng’enya kimoja kiitwacho ‘Bromelain’ ambacho husaidia kuziweka sawa homoni zinazohusiana na tendo la ndoa (testosterone). Pia ndizi zina Magnesium, vitamini B1 na vitamini C, vitu ambayo ni muhimu sana kwa ajili ya kutengeneza mbegu za kiume.

ndizi
5. Ulaji Wa Mbegu Za Maboga

Mbegu za maboga zina kiasi kingi cha madini ya zinki ambayo ni muhimu katika kutengenezwa kwa mbegu za kiume na homoni ya testosteroni. Pia mbegu za maboga zina vitamini B, C, D, E, na K ambazo zote ni muhimu katika kuongeza idadi ya mbegu za kiume. Vile vile mbegu za maboga zina madini ya kalsiamu, Potasiamu, Phosphorasi na Niacin.

mbegu za maboga
6. Ulaji Wa Mboga Za Majani Kwa Wingi.

Mboga za majani zinapunguza homoni ya ‘estrogen’ na hivyo kufanya homoni ya ‘testosterone’ ipatikane kwa wingi na hivyo kupelekea kuongezeka kwa mbegu za kiume.

spinachi
7. Ulaji Wa Vyakula Vyenye Foliki Asidi Kwa Wingi.

Vyakula vyenye foliki asidi kwa wingi ni pamoja na karoti, Parachichi, Ufuta, maharage, papai, bamia. Hivvyo isipite siku bila kula parachichi walau moja na kutafuna karoti walau moja ikiwa unachangamoto ya kuwa na kiwango kidogo cha mbegu za kiume. Tafiti zinaonesha kuwa wanaume walioongeza ulaji wa vyakula vyenye foliki asidi na zinki waliongeza uwingi wa mbegu zao za kiume kwa zaidi ya asilimia 74 kwa muda wa wiki 2 tu.

8. Kunywa Maji Mengi Kila Siku.
Hili ni suluhisho rahisi lisilohitaji gharama yoyote kwa wale wanaosumbuliwa na changamoto ya kuwa na kiwango kidogo cha mbegu za kiume. Kutokunywa maji ya kutosha kila siku kuna uhusiano wa moja kwa moja na kupungua kwa uwingi wa mbegu za kiume. Hivyo k**a utatekeleza njia zote zilizotajwa hapo juu halafu ukasahau kunywa maji hesabu umekosea sana. Kutegemeana na uzito wako unaweza kunywa maji walau lita 2 mpaka lita 3 kwa siku, hii itakusaidia kwani mbegu za kiume zinatengenezwa kwa maji,

Mazoezi ya kukimbia

KWAMAWASILIANO : 0629623538

Photos from Afya yangu's post 21/09/2023

SARATANI YA TEZI DUME
Tezi dume ni nini?

Tezi dume ni tezi inayopatikana kwa jinsia ya kiume. Tezi hii ina kazi ya kutengezeza majimaji meupe mepesi yenye unato kidogo. Majimaji haya husaidia mbegu za kiume kutembea kwa urahisi.

Ipo wapi?

Tezi dume iko mwishoni mwa kibofu cha mkojo. Pia inauzunguks mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na na mrija wa mkojo wa uume (urethra) na iko mbele kidogo ya utumbo mpana ndani ya fupa la nyonga.

✅ Saratani ya tezi dume ni nini?

Saratani ya tezi dume maana yake ni tezi dume imepata ugonjwa wa saratani..Na hii hutokea pale ambapo chembechembe hai za tezi huasi na kuanza kujigawanya bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili, chembechembe asi hizi mwishowe hutengeneza vivimbe hatari ndani ya tezi dume na hatimaye husambaa mwilini

Visababishi hatarishi kwa saratani ya Tezi dume

Umri Mkubwa kuanzia miaka 50

Nasaba (ukoo wenye historia a saratani hii

Lishe hatarishi-nyama nyekundu kwa wingi, mafuta/samli,maziwa ya krimu

Unene uliokithiri

Ukosefu wa mazoezi

Upungufu wa virutubisho,mfano vit D.

Maambukizi ya mara kwa mara kwenye tezi dume

✅ Dalili zake ni zipi?

↖️Udhaifu katika utoaji wa mkojo, mkojo hauishi.
↖️kwenda kukojoa mara kwa mara.
↖️ Damu ndani ya mkojo.
↖️Kushindwa kukojoa.
↖️Maaumivu ya kiuno na mifupa ya nyonga.
↖️Wagonjwa wengi huanza maumivu ya nyonga k**a ni dalili za awali.
↖️Udhaifu katika utoaji wa mkojo pia kunaweza kutokea kwa kuvimba kwa tezi dume bila ya saratani.
↖️Damu kwenye mkojo nakushindwa kumaliza mkojo ni ishara tosha ya kuwa tezi dume imeathirika.

✅Uchunguzi unafanyika kwa njia zifuatazo

Uchunguzi kwa cancer marker kwa kuchunguza damu (PSA).
Uchunguzi kwa njia ya kipimo cha njia ya haja kubwa (DRE)
Biopsy.
Ultrasound.
X-ray.
Bone scan.

✅ Jinsi ya kutibu saratani ya tezi dume

Upasuaji.
Mionzi
Dawa ya saratani
Homoni.
Matibabu hutegemea

Ngazi na ukali wa ugonjwa.
Je, ugonjwa upo ndani ya tezi dume tu au umesambaa.
Umri na afya ya mgonjwa.
Magonjwa ambatanishi na saratani hiyo, shinikizo la damu, matatizo ya moyo na kisukari.
TIBA

UPASUAJI

Kuondoa tezi dume yote peke yake inaweza ikatosha.
Kuondoa tezi dume na tezi jirani.
Kuondoa tezi dume na kuhasi
Kuondoa tezi dume kidogo kupitia njia ya mkojo na kumpa mgonjwa tiba shufa.
MIONZI.

Sawa na upasuaji inaweza kuondoa ugonjwa iwapo haujasambaa.
Mionzi pia hutolewa k**a tiba shufaa.
DAWA YA SARATANI

Baadhi ya wagonjwa hufaidika na tiba hii, dawa hutolewa kwa muda mfupi na kufuatilia maendeleo ya mgomjwa kwa kufanya PSA,dawa inaweza kuwa moja au mchanganyiko

Suluhisho lakudumu

Tumia virutubisho mbalimbali kujikinga na Saratani za tezi dume

Kwamawasiliano 0629623538
0756 803 312

13/09/2023

Zingatia mlo kamili kwa Afya Bora zaidi

KWA MAWASILIANO . 0629623538

13/09/2023

UGONJWA WA KUUMWA VIUNGO VYA MWILI (ARTHRITIS)

➡️UGONJWA wa maumivu ya viungo huitwa kwa jina lingine yabisikavu. Jina la Kingereza la ugonjwa huo, ‘arthritis, linatokana na maneno ya Kigiriki yanayomaanisha viungo vilivyovimba. Mbali na kuathiri viungo, magonjwa hayo yanaweza kuathiri pia misuli, mifupa, na mishipa inayounganisha misuli na mifupa mbalimbali inayogandamiza viungo.Aina fulani za yabisikavu zinaweza kuathiri ngozi yako, maungo ya ndani ya mwili, na hata macho yako. Tutachunguza hasa magonjwa mawili ya aina ya yabisikavu, yaliyo ya kawaida sana—ugonjwa wa osteoarthritis na baridiyabisi.

➡️Kiungo ni mahali ambapo mifupa miwili imeunganishwa. Mfuko unaonyumbuka hufunika viungo fulani vinavyolainishwa na umajimaji mzito.Mfuko huo huvilinda viungo hivyo na kuvitegandamiza na una utando wa ndani unaotoa umajimaji huo wenye kulainisha.

➡️Ncha ya mifupa iliyomo ndani ya mfuko huo imefunikwa kwa mfupa mwororo unaoitwa gegedu ambayo inazuia mifupa yako isisuguane. Nayo hulinda viungo vyako kwa kupunguza shinikizo na kwa kufanya mifupa yote ihimili shinikizo kwa usawa. Kwa mfano, unapotembea, kukimbia, au kuruka, shinikizo kwenye viuno na magoti yako linaweza kuwa mara nne hadi mara nane ya shinikizo la uzito wako, gegedu husaidia mifupa yako kuhimili uzito huo inaposhinikizwa.

➡️Mtu anaposhikwa na ugonjwa wa baridi yabisi, mfumo wa kinga wa mwili huanza kushambulia viungo vyake. Kwa sababu isiyojulikana, chembe nyingi za damu, ambazo ni chembe muhimu katika mfumo wa kinga wa mwili huingia ghafla katika vitundu vya kiungo. Jambo hilo husababisha utendaji mwingi wa kemikali ambao hufanya kiungo kifure.

➡️Huenda chembe zinazotokeza umajimaji zianze kuongezeka kwa wingi sana, na kusababisha uvimbe unaoitwa pannus. Kisha uvimbe huo hutokeza vimeng’enya vinavyoharibu gegedu. Sasa kwa sababu mifupa inaweza kugusana, inakuwa vigumu kusogeza kiungo na hiyo husababisha maumivu makali sana. Misuli pia hupoteza nguvu. Hiyo inafanya kiungo kianze kulegea na kuteguka kwa kadiri fulani, na mara nyingi kuharibika umbo.

➡️Kwa kawaida ugonjwa wa baridiyabisi huathiri viwiko, magoti, na miguu kwa wakati mmoja.Asilimia 50 ya wagonjwa wanaougua baridiyabisi hupata pia uvimbe au vinundu chini ya ngozi. Wengine wana upungufu wa damu, na wanaumwa na koo na macho makavu. Uchovu na dalili za mafua, k**a vile homa na maumivu ya misuli, ni dalili nyingine za baridiyabisi.

➡️Si wagonjwa wote wanaougua baridiyabisi walio na dalili zilezile, na hata muda ambao wagonjwa huugua hutofautiana. Huenda mtu mmoja akaanza kuumwa na kukak**aa polepole kwa muda wa majuma kadhaa au hata miaka. Baadhi ya watu huugua baridiyabisi kwa muda wa miezi michache tu kisha wanapona kabisa, wengine wanaugua kwa miaka mingi.

➡️Wanaopatwa na maradhi haya hasa ni wanawake wa makamo. Hata hivyo, mtu yeyote wa umri wowote ule, watoto, na vilevile wanaume, wanaweza kupata ugonjwa huo. Wale walio na watu wa ukoo wenye baridiyabisi, wanakabiliana na hatari ya kuupata kuliko watu wengine

➡️Hata hivyo inaonyesha kwamba kuvuta sigara, kunenepa kupita kiasi, na kutiwa damu mishipani huzidisha hatari ya kupatwa na ugonjwa huo. Ugonjwa wa osteoarthritis hutofautiana na baridiyabisi kwa kuwa hauenei hadi sehemu nyingine za mwili bali huathiri kiungo kimoja tu au viungo vichache. Gegedu inapoharibika hatua kwa hatua, mifupa huanza kusuguana. Wakati huohuo mifupa mipya inayotokeza huanza kukua karibu na kiungo. Uvimbe unaweza kutokea, na mfupa ulio chini ya gegedu huwa mzito na kuharibika umbo.

➡️Dalili nyingine za ugonjwa huo ni, vinundu kwenye viungo vya vidole, sauti ya kusugua katika viungo vilivyoathiriwa, mishtuko ya ghafla ya misuli, na vilevile maumivu, kukak**aa, na kushindwa kusogeza viungo. Zamani ilidhaniwa kwamba ugonjwa huo ulitokea tu kwa sababu ya uzee. Hata hivyo, hakuna uthibitisho wowote kwamba kiungo cha kawaida kinachofanya kazi ya kawaida tu kitaharibika katika kipindi cha maisha.

➡️Wengine wanaoweza kupata ugonjwa huo ni watu ambao wana kasoro fulani katika viungo vyao, au wale wenye misuli dhaifu ya miguu na mapaja, miguu isiyo na urefu sawa, au kasoro katika uti wa mgongo. Wananawake wa makamo na wanawake wazee walio na watu wa ukoo wenye ugonjwa huo wanakabiliwa na hatari ya kuupata.

⏺️MATIBABU

➡️Matibabu ya yabisikavu kwa kawaida huhusisha kutumia dawa, mazoezi ya mwili, na kubadili namna ya kuishi. Huenda tabibu wa maungo akaanzisha matibabu ya mazoezi ya mwili. Mazoezi hayo yanaweza kuhusisha mazoezi ya kukaza misuli, mazoezi yanayoboresha mfumo wa kupumua na mzunguko wa damu, k**a vile kutembea au kukimbia, na mazoezi ya misuli ya kuinua vitu vizito. Mazoezi hayo yamesaidia sana kupunguza dalili nyingi k**a vile uvimbe na maumivu ya viungo, unyong’onyevu, uchovu, na kushuka moyo.

➡️Mazoezi yanaweza pia kuzuia kudhoofika kwa mifupa. Kupunguza unene kunaweza kusaidia sana kutuliza maumivu ya viungo yanayosababishwa na yabisikavu.

➡️Chakula kinachoweza kupunguza unene na vilevile maumivu ni mboga, matunda, na samaki wanaoishi katika bahari zenye maji baridi na mafuta mengi inayoitwa omega-3. Chakula kilichotayarishwa katika viwanda na chakula chenye mafuta yenye asidi nyingi kiepukwe. Vyakula vinavyotengenezwa kwa maziwa, ngano, na jamii ya mboga za mtunguja, nyanya, viazi, pilipili, na biringani husaidia kutibu

KWA MAWASILIANO. 0629623538

30/08/2023

Faham madharau ya hormonal imbalance

Kwa mawasiliano 0629623538

Photos from Afya yangu's post 27/08/2023

He unafahamu vyakula gani utumie ili kulinda Afya ya mmeng'enyo was chakula?🤏🤏👇👇👇👇👇👇👇

Kwa mawasiliano 0629623538

27/08/2023

UMENG'ENYAJI WA CHAKULA.

Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula (pia: mwanya wa chakula
1. Ni jumla ya viungo mwilini mwa binadamu na mamalia wengine vinavyofanya kazi ya kuingiza chakula mwilini, kukisagasaga, kukisafirisha ndani ya mwili, kukimeng'enya, kuondoa lishe ya mwili ndani yake, na kutoa mabaki nje ya mwili. Kwa hiyo mfumo wa mmeng'enyo wa chakula ni njia yote kuanzia mdomo hadi mkundu.

Mfumo wa Mmeng'enyo wa Chakula wa Binadamu
Tafsiri: utumbo mwembamba (small intestine), utumbo mpana (large intestine), ini (liver), kongosho (pancrease), ulimi (tongue), tumbo (stomach), tezi za mate (salivary glands), umio (esophagus), puru (re**um), mkundu (a**s)
Magonjwa yake huchunguzwa na elimu ya gastro-enterolojia.

Kwa lugha nyingine unahusika na umeng'enyaji wa chakula mpaka kuwa katika hali inayoweza kusharabiwa na mwili. Ili chakula kiweze kutumika mwilini, ni lazima kivunjwevunjwe kiwe katika hali rahisi ya kuweza kusharabiwa. Kazi hiyo hufanywa na mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula wa mwanadamu hufanana na ule wa sungura, panya au pimbi. Sehemu kuu zinazohusika katika umeng’enyaji huo ni kinywa, umio, mfuko wa tumbo, ini, mfuko wa nyongo, utumbo mwembamba, kongosho, utumbo mpana na puru.

Chakula kinaposafiri katika njia yake hufanyiwa mabadiliko ya kiumbo na ya kikemikali. Kila sehemu ya mfumo wa mmeng’enyo wa chakula ina kazi maalum. Chakula cha mnyama au binadamu huweza kuwa cha kabohaidreti/wanga, protini, mafuta au mchanganyiko wa viambato hivyo. Myeyuko wa makundi hayo ya vyakula hutokea katika sehemu mbalimbali za njia ya chakula kwa njia za kemikali.

Mmeng’enyo kinywani

Mfuko wa tumbo

Utumbo mwembamba

Utumbo mpana

Magonjwa ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula

Kujikinga kutokana na magonjwa ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula

KWAMASILIANO. 0629623538

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Dar es Salaam?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address


Dar Es Salam
Dar Es Salaam
255