HealthRite Tanzania
HealthRite is designed to offer a unique healthcare experience. We focus on convenient access to quality healthcare services.
HealthRite is designed to offer unique healthcare experience.
06/09/2017
22/05/2017
Je unafahamu dalili za awali anazopata mtu mara tu baada ya kuambukizwa virusi vya UKIMWI? Asilimia 70 hadi 80 ya watu hupata dalili k**a Za mtu mwenye Flu, homa, maumivu ya viungo, kichwa kuuma n.k. Hii hutokea kati ya wiki 2 hadi 6 tangu mtu anapopata virusi. Mara nyingi katika mazingira yetu mtu atapima malaria, typhoid na kukuta hana ugonjwa wowote. Baada ya muda dalili hizi hupotea na kurudi katika hali yakawaida bila hata kutumia dawa. Na hapo huwa ndio mwanzo VVU kuendelea kuzaliana kimyakimya. Kutegemeana na nguvu ya Kinga ya mwili kuweza kudhibiti virusi, mtu huweza kukaa muda mrefu hata miaka 5 kabla dalili Za UKIMWI kuanza kujitokeza. Jambo la Maana ni kupima kujua hali yako. Na ukiwa umeambukizwa tumia dawa mara moja. Wasiliana nasi kwa msaada zaidi mfano special arrangement kumuona Daktari baada ya saa Za kazi au weekend n.k. Piga 0744400300 au tembelea www.healthritetz.com
20/05/2017
Je unafahamu dalili za awali anazopata mtu mara tu baada ya kuambukizwa virusi vya UKIMWI? Asilimia 70 hadi 80 ya watu hupata dalili k**a Za mtu mwenye Flu, homa, maumivu ya viungo, kichwa kuuma n.k. Hii hutokea kati ya wiki 2 hadi 6 tangu mtu anapopata virusi. Mara nyingi katika mazingira yetu mtu atapima malaria, typhoid na kukuta hana ugonjwa wowote. Baada ya muda dalili hizi hupotea na kurudi katika hali yakawaida bila hata kutumia dawa. Na hapo huwa ndio mwanzo VVU kuendelea kuzaliana kimyakimya.
13/05/2017
Serikali kupitia wizara ya afya imeanzisha huduma ya kupima idadi ya virusi vya UKIMWI kwenye mzunguko wa damu kitaalamu ikijulikana k**a viral load test. Lengo la kipimo hiki ni kuhakikisha kila mgonjwa anayetumia dawa anafikia kiwango cha kutokuwa na idadi kubwa ya virusi kitaalamu (undetectable viral load). Mgonjwa anapofikia hatua hii, uwezekano wa kuambukiza mtu mwingine unapungua kwa 96%. Matibabu ya VVU ni kwa faida ya mgonjwa na jamii kwa ujumla. Pamoja tushik**ane, huu sio muda wa kunyoosheana vidole. 0744400300/www.healthritetz.com kumwona Daktari muda wowote upendao
12/05/2017
Pengine sio rahisi kubadili mambo yaliyokwisha tokea huko nyuma, lakini mambo yaliyoko leo na yanayokuja yanategemea mtazamo wako kwa sasa. Uamuzi wako wa kupima virusi vya UKIMWI kujua afya yako ni hatua muhimu kwani inakupa fursa ya kuamua hatima ya maisha yako. K**a ugonjwa upo, hauondoki kwa wewe kutopima. Usiogope, kidonge kimoja tu kwa siku kitaokoa maisha yako. Wasiliana nasi kwa 0744400300 au www.healthritetz.com Kumwona Daktari baada ya saa Za kazi au weekend - yaani at your convenience. Tumedhamiria kurahisisha maisha
09/05/2017
Je unafahamu kirusi mmoja anayesababisha UKIMWI anaweza kuzalisha virusi wengine zaidi ya Bilioni moja ndani ya saa 24? Ndio Maana ni muhimu kupima na kujua afya yako mapema ili kupata dawa. Kidonge kimoja tu cha ARV kwa siku kitaokoa maisha yako. Wasiliana nasi utuambie namna unataka upate huduma ya matibabu. Mfano baada ya saa Za kazi, mwisho wa juma (weekend) n.k. Piga 0744400300 au tembelea www.healthritetz.com
04/05/2017
Je, unafahamu kuwa unaweza kuishi na Virusi vya UKIMWI (VVU) bila kuwa na UKIMWI (Upungufu wa Kinga Mwilini)? Hii inawezekana endapo utatumia dawa (ARV) kwa usahihi mara tu unapofahamu kuwa una maambukizi ya VVU. Usihofu, matibabu ni rahisi na maisha yataendelea k**a kawaida. Wasiliana nasi utuambie namna unayotaka upatiwe matibabu. Mfano kumwona Daktari baada ya saa Za kazi (usiku), siku Za mwisho wa juma (weekend) n.k. Piga simu 0744 400 300 au tembelea www.healthritetz.com
27/04/2017
POSITIVE LIVING - HealthRite Tanzania Je, unafahamu kuwa zile zama za kusubiri CD4 zishuke ndio uanze dawa (ARV) zimepita? Dawa za kufubaza Virusi vya UKIMWI (VVU) zinatolewa mara tu unapokutwa na maambukizi (Test and Start). Usihofu, matibabu ni rahisi kidonge kimoja tu kwa siku wakati wa kwenda kulala na maisha yanaendelea k**a kawaid...
26/04/2017
- HealthRite Tanzania Je, unafahamu kuwa unaweza kuishi na Virusi vya UKIMWI (VVU) bila kuwa na UKIMWI (Upungufu wa Kinga Mwilini)? Hii inawezekana endapo utatumia dawa (ARV) kwa usahihi mara tu unapofahamu kuwa una maambukizi ya VVU. Usihofu, matibabu ni rahisi na maisha yataendelea k**a kawaida. Wasiliana nasi utuambie...
08/02/2017
SWALI: Je, msichana anaweza kupata mimba k**a mwanaume atajiondoa kabla ya manii/mbegu kutoka (kufika kileleni) wakati wa tendo la ndoa? - HealthRite Tanzania JIBU: Ndio inawezekana kupata ujauzito hata k**a mvulana/mwanaume hakuachilia mbegu ndani ya msichana. Kuna imani potofu kwamba msichana hawezi kupata mimba k**a kijana atachomoa uume wake kabla ya manii/mbegu za kiume kutoka. Ukweli ni kwamba, kumwaga mbegu nje hakutamfanya msichana asipate mimba (...
01/02/2017
Unakula nini wakati wa ujauzito? Lishe wakati wa ujauzito ni muhimu kwa ajili ya afya yako na maendeleo mazuri ya mtoto anayekua tumboni. Zifuatazo ni dondoo za kukuwezesha uwe na lishe nzuri wakati wa ujauzito: Jitahidi upate mlo kamili kila siku kwa kupata vyakula vya wanga, protini, mafuta, vitamini, madini na maji ya kutosha. Fanya nusu ya mlo wako uwe ni mchanganyiko wa matunda na mboga za majani. [ 121 more words ]
http://www.healthritetz.com/368-2/
- HealthRite Tanzania Unakula nini wakati wa ujauzito? Lishe wakati wa ujauzito ni muhimu kwa ajili ya afya yako na maendeleo mazuri ya mtoto anayekua tumboni. Zifuatazo ni dondoo za kukuwezesha uwe na lishe nzuri wakati wa ujauzito: Jitahidi upate mlo kamili kila siku kwa kupata vyakula vya wanga, protini, mafuta, vitam...
28/01/2017
SWALI: Je magonjwa ya zinaa yanaweza kusababisha Ugumba? - HealthRite Tanzania JIBU: Ndiyo, magonjwa ya zinaa yasipotibiwa kwa wakati na kwa usahihi yanaweza kusababisha ugumba hasa kwa wanawake. Ugonjwa wa zinaa ambao haujatibiwa unaweza kusambaa hadi kwenye via/viungo vya ndani vya uzazi vya mwanamke (tumbo la uzazi, mirija ya uzazi, mayai ya uzazi, misuli mbalimbali inayozu...
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
P. O. Box 8828
Dar Es Salaam