king kiba new page
Afya ndo mtaji wako
24/10/2022
Habari za uzima wapendwa
nimeandaa group watsap kutoa elimu ya afya pia ushauri na suhulisho la magonjwa mbalimbali
k**a wa elimu karibu sana kwa group
NB; WANAWAKE TU SIO WANAUME
https://chat.whatsapp.com/CEXU6g7P4SqHdzswFqeOM4
Seli shina ni nini?
Mwili wa binadamu una mamia ya seli (chembechembe hai) za aina tofauti zenye umuhimu kiafya. Seli hizi zina jukumu la kuendesha mifumo mbalimbali ya miili yetu, kwa mfano, kuendesha mapigo ya moyo, kuwezesha fikra akilini, usafishaji wa damu kwenye figo, kutengeneza ngozi mpya, na kadhalika. Kazi ya kipekee ya seli shina ni kuwa chimbuko la kuzalisha aina nyingine ya seli. Seli shina pia hufanya shughuli ya ugavi wa seli mpya mwilini. Seli hizi zinapojigawanya huzidisha idadi ya seli shina nyingine au seli nyingine za kawaida. Kwa mfano, seli shina za ngozi zinauwezo wa kuzalisha seli shina zingine zaidi za ngozi au kuzalisha seli tofauti zenye kazi maalumu k**a kutengeneza melanin.
Kwanini seli shina ni muhimu kwa afya yako?
Tunapoumia ama kupata maradhi, seli zetu pia huumia au kufa. Hali hii ikitokea, seli shina huanza kufanya kazi. Seli shina zitaponya majeraha mwilini na pia kujaza nafasi ya seli zinazokufa mara kwa mara. Kwa njia hii, seli shina zinatuweka katika hali ya afya nzuri na kudhibiti mwili kudhoofika mapema. Seli shina ni k**a jeshi la matabibu wanaoonekana kwa hadubini pekee.
Kuna aina ngapi tofauti ya Seli Shina?
Seli shina huwa katika aina au mifumo mbalimbali. Wanasayansi wanaamini kuwa kila kiungo mwilini kina seli shina zake maalumu. Kwa mfano, damu hutengenezwa na seli shina za damu (hematopoietic stem cells). Hata hivyo, seli shina huwepo kuanzia hatua za awali kabisa za uumbaji wa mwanadamu, na pale wanasayansi wanapootesha aina hizi za seli ndipo hufaamika k**a “seli shina za kiinitete”. Sababu inayowafanya wanasayansi kuhusiana karibu na seli shina za kiinitete ni umuhimu wake katika kujenga kila kiungo cha mwilini wetu wakati wa uumbaji. Hii humaanisha ya kuwa seli shina za kiinitete, tofauti na seli shina komavu, zina uwezo wa kubadilika na kuwa seli yoyote kati ya mamia ya seli za binadamu. Kwa mfano, kwakuwa seli shina za damu zinauwezo wa kutengeneza seli za damu tu, seli shina za kiinitete zinauwezo wa kutengeneza seli za damu, mifupa, ubongo, na kadhalika. Pamoja na hayo, seli shina za kiinitete zimepangwa kiasili kujenga seli shina nyingi na hata viungo, wakati seli shina komavu hazina uwezo huu. Hii inamaanisha ya kwamba seli shina za kiinitete zina uwezo asilia mkubwa zaidi kurekebisha viungo majeruhi. Seli shina za kiinitete huzalishwa kupitia mabaki ya viinitete vichanga kwenye vituo vya matibabu ya uzazi, matumizi ambayo ni muhimu la sivyo viinitete hivi hutupwa pasipo ya matumizi yake kwa ajili ya tafiti za tiba.
SSS au Seli Shina Shawishi ni nini?
Wanasayansi na matabibu duniani kote wamepata mategemeo mazuri kuhusu ujio wa Seli Shina Shawishi (SSS). Sababu kuu ni kuwa SSS zina sifa karibu zote za seli shina za kiinitete, ila hazizalishwi kutoka kwa viinitete. Hivyo basi, hakuna pingamizi za kiimadili kuhusu matumizi ya SSS. Zaidi ya haya, SSS hutengenezwa na seli ambazo siyo Seli Shina kutoka kwa mgonjwa mwenyewe, hivyo kuzipa SSS uwezo wa kurudishiwa kwa mgonjwa bila hatari ya kushambuliwa na mfumo wa kinga wa mwili. Jambo hili ni la umuhimu katika tiba yoyote ya upandikizwaji wa Seli Shina.
Kuna mategemeo yapi kuhusiana na Seli Shina na jinsi ambavyo zitaleta mapinduzi katika tiba?
Jukumu la seli shina ni kubadilisha seli zenye majeraha, ugonjwa au seli zilizokufa. Wanasayansi wamepata wazo la kutumia seli shina katika tiba kwa ajili ya wagonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Wazo lao kuu ni kuwapa wagonjwa seli shina au seli komavu zilizozalishwa na seli shina. Kwa namna hii wanatumia nguvu asilia ya Seli Shina kutibu na kumrudisha mgonjwa katika hali ya afya tena. Kwa mfano, k**a mgonjwa amepata shinikizo la moyo, tiba itakayotumika ni kupandikiza seli shina kwa mgonjwa ili kutibu majeraha kwenye moyo. Kwa kawaida idadi ya seli shina tulizonazo mwilini zina uwezo mdogo kurekebisha majeraha. Tukirudi kwenye mfano wa shambulizi wa moyo, seli shina za moyo hazina uwezo wa kutosha wa kuponya majeraha yanayotokana na shinikizo la damu, lakini pale mamilioni ya seli shina za moyo zitakapopandikiwa uwezo wa tiba huongezeka maradufu. Hivyo basi kwa kuwapandikiza wagonjwa kutumia seli shina tunaongeza uwezo wa mwili kuponya zaidi ya uwezo mdogo wa kiasilia. Changamoto chache bado zipo kabla matibabu ya seli shina kuwa tiba ya kidesturi, kwa mfano changamoto za usalama kwasababu ya uwezo wa baadhi ya seli shina kutenegeneza uvimbe wa saratani, na pia changamoto ya mashambulio ya mfumo wa kinga wa mwili. Hata hivyo seli shina huenda zikaleta mageuzi makubwa kwenye matibabu, na pengine baada ya muongo au miongo miwili wengi wetu, pengine hata sisi wenyewe, tutakuwa tunafahamu mtu aliyetibiwa kwa kupandikizwa na seli shina. Seli shina zimeshikilia ahadi ya kuwa na uwezo wa kutibu magonjwa mengi yanayomsibu binadamu k**a saratani, magonjwa ya moyo, ugonjwa wa Parkinson, Uzulufu mwingi, kiharusi, ugonjwa wa Huntington, majeraha ya uti wa mgongo na magonjwa mengine mengi.
Napenda kila mtu aijue hii tiba kwa kuweza kuokoa pesa nyingi na kutibu tatizo moja kwa moja kwa gharama nafuu zaidi
06/08/2022
BAWASIRI,AINA ZAKE,DALILI ZAKE,AINA ZAKE,CHANZO CHAKE NA TIBA ASILI (KUOTA KINYAMA,MIWASHO ,DAMU SEHEMU YA HAJA KUBWA
BAWASIRI NI NINI?
-Bawasiri ni Ugonjwa unaotokana na kuvimba/kupasuka kwa mishipa ya dawa sehemu ya haja kubwa na kupelekea kuota kwa kinyama/Uvimbe ambao ndio huitwa Bawasiri.
Sababu kubwa ya mtu kupata Bawasiri ni Mgandamizo sehemu ya haja kubwa ambapo mgandamizo huo hupelekea kupasuka/kuvimba kwa mishipa midogo midogo ya damu aina ya veins sehemu ya haja kubwa hivyo hupelekea kuota kwa kinyama,miwasho,maumivu makali na kutoa damu
Ugonjwa huu umekuwa ni ugonjwa hatari kutokana na tabia za wagonjwa kuficha kutokana na aibu ya tatizo lenyewe lilipo au kuhofia jamii kumtazama tofauti kwa sababu jamii nyingi hasa za afrika mashariki zinaamini kuwa ugonjwa huu ni mkosi mkubwa.
DALILI ZA MTU MWENYE BAWASIRI
1.kupata muwasho mkali katika eneo la juu la haja kubwa
2.kujitokeza kwa kinyama/vinyama eneo la haja kubwa
3.kutokewa na kiuvimbe katika tundu ya haja kubwa
4.kupata kinyesi chenye damu
5.kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia
6. Kupata maumivu ya tumbo/kiuno hasa Bawasiri inapofikia hatua mbaya
AINA ZA BAWASIRI
-Kuna aina 2 za Bawasiri k**a ifuatavyo⤵⤵⤵⤵:
. BAWASIRI YA NJE
Ni kuota kinyama sehemu ya nje ya haja kubwa ambapo kinyama huwa nje hata k**a hujaenda kujisaidia haja kubwa.
.BAWASIRI YA NDANI
Ni kuota kinyama sehemu ya ndani ya haja kubwa mara nyingi huambatana na maumivu makali na damu na kinyama hutoka wakati wa kujisaidia haja kubwa.
Bawasiri ya ndan ina hatua NNE ambazo ni:⤵⤵⤵⤵:
1. HATUA YA KWANZA
Katika hatua hii mtu hujihisi maumivu makali,miwasho pamoja na kutokwa damu wakati wa kujisaidia na kinyama hakionekan wakati wa kujisaidia.
2. HATUA YA PILI
Hii hutokea wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe punde baada ya kujisaidia
3.HATUA YA TATU
Hii hutokea wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kurudisha ndani yeye mwenywe ama inaweza kurud yenyewe baada ya muda
4. HATUA YA NNE
Hii ni bawasiri inayotoka na huwa ngumu kurudi baada ya kujisaidia.
VISABABISHI/MAMBO YANAYOWEZA KUSABABISHA MTU KUPATA BAWASIRI
1. Uzito kupita kiasi(Overweight)
2. Ujauzito
3. Unywaji pombe
4. Kukaa sana sehemu ngumu
5. Kuingiliwa sehemu ya haja kubwa.
6.Kujisaidia Choo Kigumu.Sababu za kujisaidia choo Kigumu ni:
-Vidonda vya TUMBO
-Ngiri/Hernia
-Ulaji duni
-Kuwa na acid mwingi tumboni
7. Kula sana nyama nyekundu
8. Presha ya kupanda
9. Kula sana pilipili
10. Kula udongo(Wajawazito na watoto wadogo)
11. Kujisaidia kwenye vyoo vya kukaa
12. Kuharisha kupita kiasi.
13. Kufanyakaz ngumu/kunyanyua vitu vizito
MADHARA/ATHARI ZA BAWASIRI
1.Upungufu wa damu mwilini
2.Kutokwa na kinyesi bila kujitambua
3.kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa
4.kupungukiwa nguvu za kiume
5.kupungukiwa na uwezo wa kufanya kazi kutokana na maumivu
6.Kupata tatizo la kisaikolojia
7.Kutopata ujauzito
8. Mimba kuharibika
10. Kupata kansa ya utumbo ( Colorectal cancer)
11. Mwili kudhoofika
NJIA ZA KUJIKINGA DHIDI YA BAWASIRI
1.Kula mboga za majani na nafaka zisizo kobolewa kwa wingi
2.kunywa maji mengi lita 2.5 hadi 3 kwa siku
3.Acha kufanya mapenzi kwa kutumia tundu la haja kubwa (kulawitiwa)
4.Punguza kukaa chooni kwa muda mrefu, kunaweza kuongeza shinikizo katika njia ya haja kubwa.
5. Acha kunywa pombe
6.Punguza kula nyama nyekundu
7.Punguza matumizi ya pili pili.
8.Jitibie vidonda vya tumbo
9. Jitibie Ngiri
10. Dhibiti uzito wako
11. Jiepushe/punguza kunyanyua vitu vizito mara kwa mara
MATIBABU YA UGONJWA WA BAWASIRI
Kuna matibabu aina mbili katika kutibu ugonjwa wa Bawasiri:
1. MATIBABU YA KISASA
-Matibabu ya kisasa yanahusisha matibabu ya Hospital ambapo tiba kubwa ya Bawasiri kwa hospital ni kufanyiwa upasuaji mdogo ( minor surgery) kwaajili ya kuondoa kinyama. Changamoto kubwa ya matibabu haya ni kwamba asilimia kubwa ya wagonjwa wanaofanya upasuaj wa tatzo hili tatizo hujirudia kwasababu upasuaji huondoa athari ya tatzo na si mzizi wa tatizo yaani ni sawa na kukata mti kisha ukaacha mizizi bila shaka mti huo utachipua na kumea tena.Lakini pia Upasuaji wa Bawasiri huwa na maumivu makali sana na uponaji wa kidonda hufika mpaka miezi miwili,hali hii ya kukaa na kidonda kwa muda mrefu kunaweza kupelekea kupata Kansa ya utumbo ( Colorectal Cancer).
ZIJUE SABABU ZINAZOWAFANYA WAGONJWA WENGI WA BAWASIRI KUTUMIA DAWA NYINGI BILA MAFANIKIO
Kwanza Mgonjwa wa Bawasiri anatakiwa kufahamu ya kwamba,matibabu si dawa pekee.Watu wengi wanaamin kwamba matibabu ni dawa pekee na jambo hili limepelekea wengi kuteseka na matatzo kwa muda mrefu sana bila mafanikio na kupelekea kukata tamaa ya kutafuta tiba na badala yake humuona kila mtoa huduma ni tapeli:
✅Zifuatazo ni sababu zinazowafanya wagonjwa wengi kuteseka na Bawasiri kwa muda mrefu licha ya kutumia dawa mbali mbali:
1.📎 Kutopata dawa sahihi
-Si kila dawa inayotangazwa kutibu Bawasiri inaweza kutibu Bawasiri bali dawa yenye ufanisi wa kutibu ndio inaweza kutibu Bawasiri.
2.📎 Kutofuata ushaur wa daktari.
-Usipofuata yale ambayo daktari anakuelekeza ili kupata suluhisho la Tatzo lako ni ngumu kupona tatzo lako.
3.📎 Kutoziacha sababu zilizopelekea upate Bawasiri. Katika hili wengi wamefeli kwani haiwezekani ukapona Bawasiri ikiwa sababu zilizopelekea upate Bawasiri hutaki kuziacha mfano;
-Pombe
-Uzito mkubwa
-Ulaji mbovu
-Kuingiliwa kinyume
-Kula sana pilipili
-Kukaa sana sehemu ngumu.
-Kunyanyua vitu vizito
-Kutotibu Magonjwa k**a Ngiri na Vidonda vya TUMBO
-Kutokula vyakula vya kulainisha choo k**a vile Mboga za majani & matunda
-Kula udongo(wajawazito)
-Kujisaidia kwenye vyoo vya kukaa.
-Kuharisha mara kwa mara
-Kujisaidia choo Kigumu
✍️Hata utumie dawa zaid ya 100,usipoziacha sababu hizo ni ngumu sana kupona Bawasiri na matokea yake kila mtoa tiba utamuona Tapeli kumbe sababu ni wewe mwenyewe kutofuata miongozo,maelekezo na USHAURI kutoka kwa daktar.
⚫ Ukizingatia hayo utapona Bawasiri kwa muda mfupi sana (wiki mbili hadi nne 4)
japo wapo wanaopona kwa siku 5 licha ya kukaa na Bawasiri kwa miaka kadhaa .
Karibu MKOMBOZI HEALTHY Mkombozi Health Center KWA TIBA YA UHAKIKA
14/03/2022
Afya ndo mtaji wako
Ipende afya yako kuliko kitu longine chchte
king kiba new page Afya ndo mtaji wako
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam
0000